Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Mkuu ebu acheni Ujinga wengine hapa tunatumia akili na sii masaburi... Sasa kama habari hii ni yakweli.. Lowassa alijuaje na kutaka kuuvunja mkataba ikiwa mkataba ulikuwa wa JK rais wake....

Halafu JK kusema tu alikuwa akipata ushauri wa makatibu wake (watendaji wa kiserikali) inaonyesha wazi JK alikuwa akifuata sheria na taratibu za kiserikali laa sivyo asingewahusisha makatibu wakuu kama alivyofanya Lowassa na ushahidi upo akiwaamrisha hao makatibu na waziri wafuate maagizo yake....Tafuta jingine!

Hayo ya 1997 we are interested ni kujikosha na kutafuta huruma za JK...Hata mahakamani mkosa baada ya kupatikana na kmakosa, hupewa muda wa kuomba, kujieleza kabla ya kuhukumiwa kifungo..


Hawana nyimbo hawa wafuasi wa lowasa kawapanga kumsafishia njia ya kwenda kutufisadi haswaaa!
Watamnadi saana but hatapata urais kamwe
 
Wameniudhi sana NEC ya CCM. Badala ya kuikabidhi dola watuhumiwa wa ufisadi ili sheria ichukue mkondo wake wao wanalirudisha suala hili kwenye CC yao. Tumefikaje hapa pa kubembeleza wahalifu kiasi hiki? Waachieni akina Mramba basi ah!
 
Mtajuwa sasa kwanini waliomtuma kazi Mwakyembe ...sasa wanataka AFE ......maana ni wazi kuwa pamoja na lowassa kuonekana mbaya ....issue ya Richmond kina mwakyembe na manyanya stella .....walivuta pesa ili wamtose....kutoka kwa JK ....na rule of mafia ina apply ...

Ukiamua kubeba Siri za mafia ...ujiandae kufa......ni wazi Mwakyembe alitakiwa AFE kabla Lowassa hajafunguka (after all hata Lowassa alikuwa AFE ili asifunguke ..Kama sio kuwahi matibabu Ujerumani).......inawezekana hii nayo imemfanya afunguke ili asife na Siri .........

Kama kuna kaukweli hivi!!!
 
hawa wanajaribu sana kucheza na akili za Watanzania na kwa bahati mbaya huko kwenye mikutano ya CCM wamejaa mbumbumbu watupu. Hawa ndio walikaa kikai cha kwanza wakatutangazia wanataka kujivua Magamba.

Ugonvii mkubwa wakatukana na matusi makubwa makubwa huyo Nape alikuwa mru mdogo tu. Nakumbuka kiongozi mmoja akasimama na kuwataja hadharani kuwa Rostam, Chenge na Lowassa ndio wanakiharibu chama na wakafikia maamuzi ya chama kujivua gamba.

Wakavunja sekretariet na ndio kuchaguliwa akina Malima, Chiligati na Nape leo tena wanawageuka baada ya kuahirisha mikutano mingapi?.. Kila kukicha wanakuja na jipya hivi hawa jamaa wanafikiri sisi wajinga sana au?

Haya miezi sita tu iliypita sii ndiouwa fahari ya chama kujivua magamba! leo tena nyoka kujisafisha ni asili yake imekuwa magamba ya Mamba ndio kinga yake..
 
Vita vya panzi neema kwa kunguru.....Lowasa mwaga vitu waTZ tujue ukweli
 
hawa wanajaribu sana kucheza na akili za Watanzania na kwa bahati mbaya huko kwenye mikutano ya CCM wamejaa mbumbumbu watupu. Hawa ndio walikaa kikai cha kwanza wakatutangazia wanataka kujivua Magamba. Ugonvii mkubwa wakatukana na matusi makubwa makubwa huyo Nape alikuwa mru mdogo tu. Nakumbuka kiongozi mmoja akasimama na kuwataja hadharani kuwa Rostam, Chenge na Lowassa ndio wanakiharibu chama na wakafikia maamuzi ya chama kujivua gamba.

Wakavunja sekretariet na ndio kuchaguliwa akina Malima, Chiligati na Nape leo tena wanawageuka baada ya kuahirisha mikutano mingapi?.. Kila kukicha wanakuja na jipya hivi hawa jamaa wanafikiri sisi wajinga sana au? Haya miezi sita tu iliypita sii ndiouwa fahari ya chama kujivua magamba! leo tena nyoka kujisafisha ni asili yake imekuwa magamba ya Mamba ndio kinga yake..
Mkandara,
Sekretarieti iliyopo sasa ya akina Mukama, Chiligati, Nape, January na Mwigulu itaondoka mapema kabla ya 2012 kama hawana "guts" za kujiondoa wenyewe. Hawana "support" ya yeyote mle ndani ya CCM. Wamezingirwa. Dhambi ya kumtelekeza Mpendazoe inawatafuna baadhi yao.
 
Nape ameambiwa apeleke ushahidi wa kumtuhumu lowassa ni fasadi na akishindwa achukuliwe hatua za kinidhamu ambazo kwa vyovyote vile ni kuachichwa cheo cha katibu mwenezi.
Atautoa wapi ushahidi wakati bunge na hansad zinamsafisha EL hii maana yake ni kwamba hana cheo ni sawa na kuambiwa na mganga upeleke miguu ya nyoka ili mgojwa apone.
 
Atautoa wapi ushahidi wakati bunge na hansad zinamsafisha EL hii maana yake ni kwamba hana cheo ni sawa na kuambiwa na mganga upeleke miguu ya nyoka ili mgojwa apone.

ha haaaa haaaaa

nimekusoma mkuu
 
Nawezaje kuipata ripoti hio ya 1997 ya huyo Mzee? Ilihusu nini hasa? Content yake je? Mkapa alisaidiaje? Kwa nini alimsaidia? Ilikua na athari gani? Kwa hio si kweli kwamba JK ndio kiongozi mwenye mvuto? wala sio chaguo la Mungu? Mmmmh
Kwa taarifa tu baada ya ripoti hiyo ya mwaka 1997 iliyotolewa na Daud Mwakawago, huyo Daud Mwakawago hatunaye tena, yupo ahera.
 
Atautoa wapi ushahidi wakati bunge na hansad zinamsafisha EL hii maana yake ni kwamba hana cheo ni sawa na kuambiwa na mganga upeleke miguu ya nyoka ili mgojwa apone.
Watu waendelee tu na maovu yao nchi hii. Ipo siku. Nani alijua Hosni Mubarak wa Misri atafikishwa mahakamani akiwa kwenye machela? Nguvu zote alizokuwa nazo Gadafi na familia yake ziko wapi sasa?

Wao wawachezee WATANZANIA tu. Kutoka NEC warudi CC, kutoka CC warudi kamati ya "MAADILI", kutoka huko waende sekretarieti, kutoka sekretariet warudi CC, safari ianze upya.
HAKUNAGA kama LOWASA nchi hii!
 
Muheshimiwa hapo kwenye RED mimi nakukatalia 100% siyo kweli kuwa Mzee ruksa alikuwa chaguo la Mwalimu la hasha...Kulikuwa na zengwe kubwa ndani yake...lakini kulikuwa hakuna jinsi ni lazima ionekane kuwa pendekezo la kwanza ni mzee ruksa....

Chaguo la mwalimu wakati ule alikuwa Waziri mkuu wa wakati ule Salim Ahmed Salimu..Lakini kwa busara zao waliona isingependeza kumpendekeza mgombea wa kwanza awe waziri mkuu badala ya makamo wa raisi na raisi wa Zanzibar kwa wakati ule amabaye alikuwa Mzee ruksa....ndipo alipoitwa mzee ruksa na kuombwa akubaili hilo ombi ...lakini akaambiwa wakati wa mkutano mkuu wa CCM pale Chimwaga atakapo tangazwa kuwa yeye ndio Mgombea uraisi ajaye......baadae yeye ashukuru kwa kumpendekeza lakini atoe udhuru kuwa nafasi hii yeye ahiwezi ni kubwa sana kwake....

Naye mzee Ruksa akapata washauri wakamwambia mzee usiwe mjinga wewe lini tena utakuja kuwa raisi...ndipo yeye alipo simama baada ya kutangazwa kuwa ndio mgombea..badala ya kutoa udhuru yeye alikubali moja kwa moja.....na ndio hapo ilipochipuka uhasama wa chini chini kati ya Mzee ruksa na Mwl...na migongano ya hapa na pale...mwanzoni wa utawala wa mzee ruksa...sasa wewe unatumabia Mzee ruksa alikuwa chaguo la mwalimu hii sio kweli...kama unampigia chapuo Mr Lowasa mpigie tuu lakini sio kwa kisingizio hiki

Hapa Jamii forums tupo watu wa viwango tofauti. Kuna wanaochangia mada kwa ushabiki na kuna wachambuzi makini. Mada yangu ya hapo chini hata kama haijaeleweka kuhusu Mzee ruksa lakini ina akisi kitu fulani kinachoendana na Lowasa kwamba Ruksa alijiuzuru uwaziri na Lowasa hali kadhalika.

Tufanye uchambuzi kwa kuchunguza sarafu p[ande zote, si upande mmoja tu na kutolea hitimisho ni mtazamo finyu mno. Hata unayemwona mbaya wako akifanya mazuri mpongeze huo ndio ustarabu kwani mazuri anayofanya au atakayofanya ni kwa manufaa yetu sote.

quote_icon.png
By Candid Scope
Leo asubuhi katika moja ya thread inayomhusu Lowasa, niliandika kwamba Lowasa ni shujaa na mfano wa kuigwa kwa wenye upembuzi yakinifu. Amejitahidi kuvumilia hadi leo na katika uvumilivu kama binadamu kuna kikomo.

Masuala ya uongozi wa serikali si jambo la mtu moja, ila mmoja ndiye mwenye kubeba lawama. Tatizo la Umeme lilikuwa la nchi nzima na sote tulikuwa na matarajio ya kampuni iliyopata dhamani kufua umeme ingetupunguzia matatizo ya giza badala yake ndo mambo yakaharibika zaidi.

Kwa vyo vyote Mkuu wa nchi anahusika moja kwa moja kwa vile ndiye kichwa cha nchi na ndiye mwajibikaji number one. Kwa vile kinga ya urais kwa mfumo wa nchi yetu inavyohusudiwa kama ufalme, mwandamizi wake katika masuala ya serikali ambaye ndiye waziri mkuu alibeba lawama.

Lowasa alitumia busara na uamuzi mgumu kujiuzuru uwaziri mkuu kwa kulinda heshima yake, serikali yake na chama chake kama alivyosema, lakini uamuzi wake umetafsiriwa vibaya na wabaya wake wamepata hoja ya kusimamia. Mzee Ruksa kipindi cha Nyerere akiwa waziri wa mambo ya ndani alipata msukosuko kama huo hadi kujiuzuru na kwa heshima yake hiyo alifaulu kutetea heshima yake hadi baadaye kuwa Rais wa nchi, na kumbuka Nyerere ndiye aliyempendekeza awe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Tanzania wakati aliboronga katika moja ya wizara aliyomkabidhi. Kuna wengi walioborongo kipindi cha Nyerere lakini katu hawakuinuka tena, hii ilitokana na namna kosa lilivyofanyika na mhusika alivyopokea na kutambua kosa lake.

Makosa mengi mabaya kuliko aliyofanya Lowasa katika utumishi wake yametokea na hakuna hata mmoja aliyewajibika au kuwajibishwa, na jinsi anavyonyooshewa vidole na akina Nape si uungawana kabisa, wakati hao wanaomnyooshea vidole kichama ni wahaini kwa kuanzisha CCJ ndani ya CCM wakati hawajajivua UCCM.

Leo Lowasa ameanza kufunua baadhi tu ya yaliyofichika, na kama wasingetuliza vichwa mengi angeyatapika. Na hakuna uthibitisho wa ufisadi wa Lowasa, ila ni tuhuma ambazo hazina uthibitisha na hata kama alikosea basi si ufisadi ila uwajibikaji katika utendaji wake, na alitambua hilo na kwa hiari kutokana na msongo toka bungeni aliamua kuachia ngapi ili wengine wajipange upya.

Matokea mtoto wa Mkulima hana uwezo kabisa wa kuchukua uamuzi mzito. Kwa sasa imethibitika kwamba
bora lawama kuliko fedheha. Mtoto wa mkulima ni fedheha tupu ndani ya serikali kuliko lawama za Lowasa.
 
niliwaeleza kuwa Lowasa hakukurupuka kufanya maamuzi magumu,na alisha wahi kuliongelea hili juu ya kwanini haufunja mkataba,ila kwa kuwa Kijana Nape anafanya kazi kwa kulipiza kisasi alitaka kumuumbua Lowasa pasipo kuelewa msingi mzima wa tatizo la kampuni tata,safi Lowasa

Bado sijaona waziri mwenye maamuzi magumu kama wewe tukiachana na marehem Sokoine
 
Duh!

Ama kweli watanzania tu wavivu wa kufikiri na mbilikimo wa mawazo.

Pamoja na Lowassa kuongea kwa uwazi bado mnadai ni fisadi!. Tena ni maswali hayo hayo mlikuwa mnauliza, mkishajibiwa mnageuka.
Huo sio uspin doctor bali ni upuuzi na kuwa na uwezo mdogo wa kufikiria.
 
Yaani mmeumbuka kweli kweli.

WAPI WAPI HALISI?? lol

Halisi mkuu njoo basi tumvue Lowassa Gamba maana ni Fisadi fisadi fisadi.

Sometimes wakuu wengi humu nashindwa kuwaelewa, nahisi hata JF wengi wetu tunatumia matumbo kufikiri. Baada ya Lowassa kuongea ndo nimeanza kuwaelewa baadhi yenu.

Anyway Mungu atawalipa hapa duniani.
 
Niceeeeee............!!!!! veriiiiiiiii gudiiiiiii, let me add this ujue Lowassa is free from magamba,...

JK kasemaaaaaaa....MWENYE USHAHIDI KUHUSU TUHUMA ZA LOWASSA AZILETE, LA SIVYO WAPAYUKAJI WAKINA NAPE & CHILLI. WATACHUKULIWA HATUA ZA KINIDHAMU, eeeehh bana JK kamaliza kazi, SUMAYE KAPIGILIA MSUMARI WA MOTO, yaani NGUVU YA SUMAYE + LOWASSA ni nomaaaa,

EL FOR PRESIDENT 2015, u hve ma vote, sisikii, sielewiii, sioniii, tunataka Kiongozi mchapa kazi, hata YESU ALICHUKIWA NA KUUAWA, sembuse Lowassa, go buddy....i am done, period..!!!

siku zote mi nilidhani weye ni CDM kumbe ni CCM ... btw! Lowasa anajaribu kujikosha... ili JK aonekane ni mbaya!

kama kweli kosa halikuwa lake .. kwanini alijiuzulu... ile sababu aliyotoa ati "chanzo ni uwaziri mkuu ni danganya toto"




 
Yaani mmeumbuka kweli kweli.

WAPI WAPI HALISI?? lol

Halisi mkuu njoo basi tumvue Lowassa Gamba maana ni Fisadi fisadi fisadi.

Sometimes wakuu wengi humu nashindwa kuwaelewa, nahisi hata JF wengi wetu tunatumia matumbo kufikiri. Baada ya Lowassa kuongea ndo nimeanza kuwaelewa baadhi yenu.

Anyway Mungu atawalipa hapa duniani.


mkuu wewe kama mimi......juzi niliandika tena kwa herufi kubwa kuwa LOWASA HANG'OKI CCM...Mheshimiwa halisi alkaniambia kaka safari hii huyu bwana kakalia kuti kavu atang'oka.lakini ndo hivyo mzee mzima anapeta...kuhusu kikwete sina la kuongeza maana singanture yangu inaongea yote....
 
Lowassa = Sokoine
Kwa lipi FairPlayer! Haya kapata nafasi kuyasema jana tangu 2006?
- Alimpigia simu JK ili avunje mkataba. JK akamkatalia. Kwa nini asijiuzulu wakati huo?
- Kule kuisafisha kashfa hii kwa kutumia TAKUKURU yetu kulifanywa na nani?
-Alipewa nafasi tele na Sitta tena yenye kinga kamili. Akaiacha. Kaamkia NEC jana!
- Mwambie afunguke zaidi. Anadai katukanwa. Aende hata mahakamani angalau.
 
Back
Top Bottom