Kwa lipi FairPlayer! Haya kapata nafasi kuyasema jana tangu 2006?
- Alimpigia simu JK ili avunje mkataba. JK akamkatalia. Kwa nini asijiuzulu wakati huo?
- Kule kuisafisha kashfa hii kwa kutumia TAKUKURU yetu kulifanywa na nani?
-Alipewa nafasi tele na Sitta tena yenye kinga kamili. Akaiacha. Kaamkia NEC jana!
- Mwambie afunguke zaidi. Anadai katukanwa. Aende hata mahakamani angalau.
-Awaombe radhi kwanza WATANZANIA kwa maamuzi hayo.De'Levis,
Humu JF wengi ni mashabiki. Lowassa ni mchapa kazi wote tunajua, kile kipindi cha CRISIS hata wewe ungeweza kufanya maamuzi yasiyo sahihi. Na hiyo ndo kazi ya kiongozi kutoa maamuzi mazito. Sasa kumbe ilikua ni collective accountability. Akaamua kumwacha Prez akawa muungwana.
Leo kwa sababu za matumbo yetu tunamtukana huyu mtu shujaa wetu. Chenge kakamatwa na hela WAZI kabisaaaaa sijawahi kusikia rafiki yangu HALISI akimsema ni fisadi. Why Lowassa!
MWEMBE WENYE MAEMBE NDO UNARUSHIWA MAWE. LOWASSA ANAFAA NDIO MAANA MNAMPINGA.
Duh!
-Awaombe radhi kwanza WATANZANIA kwa maamuzi hayo.
-Lowasa, mbali ya kuchapa kazi ni mwizi pia. Na wezi wote ni wachapakazi sana.
-Kwa nini ametuficha ukweli wote wa kashfa hii?
-Mwaka 1995 alichukua fomu ya kugombea Urais. Nini kilitokea?
Kama kuna kaukweli hivi!!!
Jibu FairPlayer. Hakuna mtu anayejua kuvitumia vyombo vya habari kama Lowasa. Mjanja sana wewe. Hakuna nilichomezeshwa. Sema tu neno moja na roho yangu itapona.Mkuu ni password yako kweli?. Maana naona unafikiri kama mtu magazeti yanamfikiria. Yaani vitu vinachujwa na kisha unamezeshwa!
Think a little bit basi.
Sijui mnanengeneka na nini na huyu mwizi mkubwa!alijua hayo yote sasa alisaidia nini kama waziri mkuu na mzalendo???hivi mitanzania ina akili gani au amewapa mgao!?Lowassa amekana rasmi kuwa yeye hahusiki na mkataba wa Richmond!
Nanukuu:
Mwisho wa kunukuu
Hii leo si sahihi hata yeye (Lowassa) kuhukumiwa kwa kuzingatia kile kinachodaiwa kuwa ni mtizamo wa umma dhidi yake unaompa sura ya ufisadi, jambo ambalo amedai kwamba siyo la kweli.
Chanzo: Mwananchi
Hapa Lowassa ameamua kuueleza umma kabisa kwamba matatizo ya Tanzania mengi yamesababishwa na Rais Kikwete. Na si hivyo tu bali ametaka umma ujue kwamba Kikwete tokea mwanzo alikuwa na matatizo na ndio maana ametoa point hiyo ya Mzee Mwakawago,Watanzania sasa amua wenyewe. Lowassa kwa mara nyingine amemshinda Kikwete je Bunge letu litaendelea kuchekelea kwa vile wote ni nyani wana mikia?
Haya chini ni maneno mazito aliyomwaga Lowassa akiamua kumwaga mboga baada ya Kikwete kutaka kumwaga ugali.
"Mwenyekiti utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa nakuitwa fisadi kwanini?".
"Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda Serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hili, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na siyo wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,"alinukuliwa akihoji Lowassa.
Kadhalika kada huyo wa CCM alinukuliwa akimkumbusha Rais Kikwete kwamba: "Mwenyekiti nikukumbushe mwaka 1997 kule Zanzibar, kina Mzee Daudi Mwakawago walikuja na mafaili yakiwa na tuhuma dhidi ya mtizamo hasi wa jamii dhidi yako, kwa hiyo wakati ule kama si busara za kina Mzee Mkapa (Benjamin) leo usingekuwa hapo ulipo".
sijui mnanengeneka na nini na huyu mwizi mkubwa!alijua hayo yote sasa alisaidia nini kama waziri mkuu na mzalendo???hivi mitanzania ina akili gani au amewapa mgao!???hili jamaa jizi hata sioni sababu ya kulitetea, mpanga mipango na mtekeleza mipango wote wa atia, then huwezi tekeleza mpango bila malipo sasa mbona hayo hayasemi????jizi kubwa hili acheni umawazo mgando!
ngoma inogile asante mkuu kwa update maana huku kwetu hakuna access ya magazeti..well said lowasa aka kondoo wa kafara naamini lowasa ana mengi zaidi ya hayo..
lowassa kwaheri,kurudisha cc ndio jambo lililokuwa likitakiwa kwa kuwa nec unazo nguvu nyingi,sasa cc kule huna watu mzee,kwa heri
Wameniudhi sana NEC ya CCM. Badala ya kuikabidhi dola watuhumiwa wa ufisadi ili sheria ichukue mkondo wake wao wanalirudisha suala hili kwenye CC yao. Tumefikaje hapa pa kubembeleza wahalifu kiasi hiki? Waachieni akina Mramba basi ah!
De'Levis,
Humu JF wengi ni mashabiki. Lowassa ni mchapa kazi wote tunajua, kile kipindi cha CRISIS hata wewe ungeweza kufanya maamuzi yasiyo sahihi. Na hiyo ndo kazi ya kiongozi kutoa maamuzi mazito. Sasa kumbe ilikua ni collective accountability. Akaamua kumwacha Prez akawa muungwana.
Leo kwa sababu za matumbo yetu tunamtukana huyu mtu shujaa wetu. Chenge kakamatwa na hela WAZI kabisaaaaa sijawahi kusikia rafiki yangu HALISI akimsema ni fisadi. Why Lowassa!
MWEMBE WENYE MAEMBE NDO UNARUSHIWA MAWE. LOWASSA ANAFAA NDIO MAANA MNAMPINGA.
Duh!
Kwa taarifa tu baada ya ripoti hiyo ya mwaka 1997 iliyotolewa na Daud Mwakawago, huyo Daud Mwakawago hatunaye tena, yupo ahera.
hata hao cc hawana jeuri kwani wameambiwa walete ushaidi wa tuhuma zake na ikithibitika siyo kweli waliyomchafua wachukuliwe hatua za kinidhamu.
Hii ni kweli Mkuu???