Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

We umelipwa shilingi ngapi kutoa mawazo yako hapa?

kuna tofauti kubwa sana kati ya maoni na ngonjera na mashairi kijana!sina muda wa kukurudisha shule kuijua tofauti hiyo.....tumia tu akili yako sawasawa utaiona tofauti!
 
Uchungu wa kiume huujui...remember JK is our President..

Pili, hapa Lowassa anataka kujikosha na najua fika kwamba mwaka 1995 JK alimshinda Mkapa, pengine JK alikuwa na mpango wa Mapinduzi 1997 ama kuhama chama... ama hasira na Nyerere. Hivyo taarifa ilipomfikia Mkapa toka kwa Daudi Mwakawago Mungu amrehemu ndio maana kafa maskini kwa uzalendo wake - Mkapa akiwa rais akapuuza. sasa kimbelembele cha Lowassa ni kutaka kumtahadharisha JK wakati huyu ni President, yeye nani?.

Aaaaah samahani nimesahau wewe shabiki sii mchezaji!

Yawezekana yeye ni Jabilil
 
Inaonekana uelewa wako wa siasa za ndani ya CCM ni mdogo sana au haupo kabisa.

Lowassa ataitwa akajieleze kwenye kamati ya maadili, hii kamati haina mamlaka ya kufanya uamuzi wa mwisho wa kujivua gamba. Mamlaka hayo ni ya nec na nec wamekubali kuipa CC. Halafu tujiulize kama lile azimio la kujivua gamba lilitaka ushahidi wa kimahakama au lilitaka nini? ukishapata jibu...GO FIGURE!

Why Lowassa anasakamwa?!... hivi unaishi bongo au unafuatilia siasa za bongo au uko NEPTUNE?

Achana nao hawa vijana wanaoshangilia kisa eti lowassa "alipiga simu".......!ile ngoma bado mbichi na lowassa anajua hivyo ndioa mana bado anahaha kuwatafuta wajumbe wa kamati kuu wamuonee huruma kwa taarifa yako,toka hiyo majuzi amekuwa akiwabembeleza wazee kina mkapa wamnusuru,hawa wapambe wake hapa wanachezeshwa ngoma wasioijua na media alizozinunua!
 
Hapo sasa!...ndio maana inakuwa kazi kwako kufikiria machungu yake. na huwezi...Kama yangekuwa na uzazi wala nisingebishana na wewe.

Sio swala la kumkubali JK kuwa ni kiongozi mzuri bali JK ni rais ambaye anatakiwa kuheshimiwa na sii kutishwa na watu ktk mikutano ya chama ili iweje?... hasa na watu hawa

zlug5.jpg

Naona wameunganisha nguvu kwa 2015, kama Rutto, Musyoka, kibaki na Kenyata kwa ajili 2012.
 
mpira hauko half time! Umemalizika! EL aliipongeza NEC kurudisha hilo swala CC halafu huko watamwita ajieleze, na jambo la pili, mbona Lowasa tu ndiye anajadiliwa sana kwenye hili swala? Akipona itakuwaje? Waliyomhukumu watazungumza nini tena? Tuwe 'neutral.'

Hawezi kupona mzee,lowassa is a dead person kwa suala hili!kupongeza huku unanung'unika maana yake hukufurahishwa na maamuzi ndio maana unasema kabisa,kama huijui kamati kuu muulize mzee malecela 2005 alivyofnyiwa kitu mbaya huko baada ya cc kujua ana nguvu nyingi nec,walienda kumchinjia huko!kule unaambiwa tu tunaona ukae pembeni kwa maslahi ya taifa,harakati zako zitavunja nchi kutokana na taarifa za kiintelijensia tulizopatiwa na TISS full stop!lowasa anajua hilo ndio mana vikao na mboe vimekua haviishi katika siku za hivi karibuni,swali je huko atapokelewa?

mtu kama sumaye anasumbuliwa zaidi ni siasa za arusha za safari hii ni "zamu yetu watu wa arusha" sina hakika na wewe bwana mollel kama pia hii inakusumbua naamini wewe ni great thinker huwezi kuwa na upuuzi huo wa "zamu yetu"
 
unataka kutuaminisha kwa nguvu kwamba sasa hivi hali ya upinzani iko juu kuliko mwaka 1995 mrema na nccr yake walivyokuwa wanaitesa ccm?!!!!!!!mbona upinzani huu ni kama cha mtoto kwa ule wa 1995 ambapo kina Guninita walivuliwa gamba kwa kuwasupport kina kikwete!


Inaonekana ni miaka zaidi ya 15 imepita toka wakati ule. Upinza wakati ule ulikuwa na nguvu lakini ujanja wa CCM ulikuwa mkubwa zaidi kwa kuwa watu wengi walikuwa wamelala. Hata sasa kuna wengi wamelala lakini kuna kuongezeka kwa wazalendo na wanaopienda Tanzania ndani ya CCM na sehemu nyingine. Na ukiangalia demography ya Tanzania imebadilika sana, ujinga unapungua. Siku zile Mrema alisema hawa wezi watu walibisha, wakasema toa ushahidi wakabananga ushahidi wake, lakini sasa watu wanwapa ushahidi wananchi wenye akili na wanaaona.
 
Watu msihamaki na Lowasa, Ina maana hatukusoma fasihi simulizi? Kwa mujibu wa Lowasa anapotaja huo mkataba (kama ni kweli) anatuambia watanzania "Kikwete uliujua huu mkataba na ulikuwa mkataba wako (wetu), ndio maana nilipotaka kuusimamisha uliniambia acha kuna mbinu nyingine utafanya/tutafanya "
 
Kwa hiyo tunachoambiwa hapa ni kuwa hatufahamu ukweli kuhusu Richmond, yaani Lowassa anatakaa ndani ya Kikao kuwa Richmond si yake lakini hasemi ni ya nani, na anasema rais ndiye aliyemkataza kuvunja mkataba. Na JK anadai kuwa makatobu walimshauri.....bado kuna swali how did we get there, who got us to Richmond na kwanini wahusika hawajaadhibiwa? Kuna uwezekano kweli Rais na Waziri Mkuu wasijui mkataba unaoingiwa na serikali. Fool can't fool me again.
Kweli kabisa mkuu wangu waliokaa huko Dodoma ni wajinga watupu wamekutana. yaani mtu anazungumzia kuvunja mkataba mbele ya kikako wakati ushahidi unaonyesha jinsi Richmond walivyoingia nchini. Report ya Mwakyembe ilionyesha wazi jinsi Tanesco walivyopinga, jinsi mgawanyo wa Mega watts ulivyochambuliwa na hata kulazimishwa kuweka mkataba..Sisi wananchi tumejadili kwa kirefu sakata hili la Richmond hapa JF na hadi leo ninayo nakala ya mada hii na maelezo ya katibu mkuu ambaye sasa hivi yuko ardhi kama sikosei..
Kapigwa vita weee lakini maneno yake yanasimama mbele ya haki na hawawezi kutengua kitu.
 
Mkuu, Mh. Lowasa asiwe na uoga watanzania tumemkubari awe Rais wetu 2015, kama atapendekezwa na Chama chake, ila kama anaona kuna mizengwe basi atoke CCM ajiunge na chama chochote na awe mgombea Urais tutampatia kura zetu hata akitaka kuwa mgombea binafsi tutampatia.

unamdanganya.......!
 
Kweli kabisa mkuu wangu waliokaa huko Dodoma ni wajinga watupu wamekutana. yaani mtu anazungumzia kuvunja mkataba mbele ya kikako wakati ushahidi unaonyesha jinsi Richmond walivyoingia nchini. Report ya Mwakyembe ilionyesha wazi jinsi Tanesco walivyopinga, jinsi mgawanyo wa Mega watts ulivyochambuliwa na hata kulazimishwa kuweka mkataba..Sisi wananchi tumejadili kwa kirefu sakata hili la Richmond hapa JF na hadi leo ninayo nakala ya mada hii na maelezo ya katibu mkuu ambaye sasa hivi yuko ardhi kama sikosei..
Kapigwa vita weee lakini maneno yake yanasimama mbele ya haki na hawawezi kutengua kitu.

Kwa hiyo tatizo liko wapi? mie nafikiri Lowasa alijiudhulu ikwa kutoa nafasi kwa wahusika wamushurikie kama amefanya makosa. tafsri yangu ndo hiyo. Kinyume chake jamaa yuko sahihi.
 
Mwizi hapendi kuitwa mwizi,na pia hata ukimuuliza kuwa eti umeiba?,hawezi kukubali mpaka pawepo na task force.
 
Kwa hiyo tunachoambiwa hapa ni kuwa hatufahamu ukweli kuhusu Richmond, yaani Lowassa anatakaa ndani ya Kikao kuwa Richmond si yake lakini hasemi ni ya nani, na anasema rais ndiye aliyemkataza kuvunja mkataba. Na JK anadai kuwa makatobu walimshauri.....bado kuna swali how did we get there, who got us to Richmond na kwanini wahusika hawajaadhibiwa? Kuna uwezekano kweli Rais na Waziri Mkuu wasijui mkataba unaoingiwa na serikali. Fool can't fool me again.
Unaweza kuta ni za kwao wote,ama mmoja wao,especially JK hadi sasa sana sana inaonekana ndo mwenye zigo la RICHMOND,yote hii kwasababu alishindwa kumlinda swahiba wake ambaye alipokea maagizo yote...Alisahau makubaliano kwamba yeye ndo next president ama alimgeuka.

Maana michezo ya JK imenichosha,huyu alitakiwa awe msanii wa movies tu basi.

Maana hizi ni zile za ki Hollywood ama Bollywood?
 
Inaonekana ni miaka zaidi ya 15 imepita toka wakati ule. Upinza wakati ule ulikuwa na nguvu lakini ujanja wa CCM ulikuwa mkubwa zaidi kwa kuwa watu wengi walikuwa wamelala. Hata sasa kuna wengi wamelala lakini kuna kuongezeka kwa wazalendo na wanaopienda Tanzania ndani ya CCM na sehemu nyingine. Na ukiangalia demography ya Tanzania imebadilika sana, ujinga unapungua. Siku zile Mrema alisema hawa wezi watu walibisha, wakasema toa ushahidi wakabananga ushahidi wake, lakini sasa watu wanwapa ushahidi wananchi wenye akili na wanaaona.


unasema sasa hivi watu wameamka wakati mpaka sasa wapinzani wote kwa ujumla hawajaweza kuvunja rekodi ya kura alizopata mreme na nccr yake,hata nusu ya kura za hawajazifikia kwa taarifa yako,tatizo watu mkija humu jamii forum mkaona sisi wachache wenye access na mtandao huu tunavyoigonga serikali mnaichulia kama sampling nzuri kuonyesha kuimarika kwa upinzani tanzania!!sisi humu ni sehemu ndogo sana hatutoshi hata kwa kumuwezesha mbunge wa jimbo moja kuingia bungeni,hili ndio linalosababisha chadema ambao kiukweli ndio wengi humu kudhani kila wakati baada ya uchaguzi fulani kuisha kuhisi wameibiwa ama kuonewa,kwa kuwa mtu kila akiingia humu kusoma comment anaona nyingi ziko in favor of cdm sasa matokeo huko site yakitoka tofauti hawezi kuelewa ataamini kuibiwa tu!jamani jamii forum haiwakilishi mawazo ya watanzania wote,wengine hata habari hawana kama kuna kitu kama hiki!
 
unasema sasa hivi watu wameamka wakati mpaka sasa wapinzani wote kwa ujumla hawajaweza kuvunja rekodi ya kura alizopata mreme na nccr yake,hata nusu ya kura za hawajazifikia kwa taarifa yako,tatizo watu mkija humu jamii forum mkaona sisi wachache wenye access na mtandao huu tunavyoigonga serikali mnaichulia kama sampling nzuri kuonyesha kuimarika kwa upinzani tanzania!!sisi humu ni sehemu ndogo sana hatutoshi hata kwa kumuwezesha mbunge wa jimbo moja kuingia bungeni,hili ndio linalosababisha chadema ambao kiukweli ndio wengi humu kudhani kila wakati baada ya uchaguzi fulani kuisha kuhisi wameibiwa ama kuonewa,kwa kuwa mtu kila akiingia humu kusoma comment anaona nyingi ziko in favor of cdm sasa matokeo huko site yakitoka tofauti hawezi kuelewa ataamini kuibiwa tu!jamani jamii forum haiwakilishi mawazo ya watanzania wote,wengine hata habari hawana kama kuna kitu kama hiki!
Mkuu hapo kwenye bold ni kweli hiyo?
 
Kambota nakushukuru, kwani umevua gamba,
Kumbuka umekufuru, matapishi utaramba,
Siku kweli ikizuru, utajiona mshamba,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.

Kwa wachumiao tumbo, Lowassa mtu shujaa,
Wafikirio kwa matumbo, Lowassa tiba ya njaa,
Watapigana vikumbo, kwenda kwake ganga njaa,
Shairi lako la hovyo, kwani wasifu fisadi.

Hebu rudi darasani, jifunze misamiati,
Udhaifu tabaini, uijue tofauti,
Kamanda na marhuni, vina kubwa tofauti,
Shairi lako la hovyo, wamsifia fisadi.

Kama Lowassa Kamanda, basi ni wa mafisadi,
Kwa hili sitamponda, kulhali ni fisadi,
Kwake nilichokipenda, kukubali yu fisadi,
Kamueleza Kikwete, kuwa sote mafisadi.

Kambota nakushangaa, sijaona kicho chako,
Tafuta dawa ya njaa, si kuvua nguo zako,
Kesho kaka ni balaa, mafisadi si wenzako,
watakutumia sana, utatupwa ja nepi.

Kambota umenikuna, kufichua sura yako,
Ila la maana huna, kwa huo mradi wako,
Wamtumikia ngwena, kitoweo mwisho wako,
Uliza waliowini, kihalali si jinai.

Uchangu kimaadili, umegeuka mradi,
Wachovu waona dili, kutumiwa na fisadi,
Watupia senti mbili, kusafisha mafisadi,
Mwisho wa siku walia, warambapo matapishi.

Kaditamati kituo, mbele sitaendelea,
Onyo wapiga chapuo, fisadi kunyenyekea,
Ipo siku mlo huo, puani utatokea,
Kambota u mmojawapo,wapi utaficha sura?
 
Kwa hiyo tatizo liko wapi? mie nafikiri Lowasa alijiudhulu ikwa kutoa nafasi kwa wahusika wamushurikie kama amefanya makosa. tafsri yangu ndo hiyo. Kinyume chake jamaa yuko sahihi.

Alifanya kosa kukubali kuwa ana kosa, na kutuaminisha kuwa ana kosa. kama si yeye ndiye Richmond kwanini alijiuzulu, alijiuzulu kumlinda nani na kwa maslahi ya nani? It is inconceivable kusema kuwa ulijiuzulu kulinda uchafu ndani ya Serikali. Si rahisi kuamini kuwa alikuwa analinda serikali chafu, si rahisi kuamini kuwa alikuwa analainda uchafu ndani ya chama. Unless aseme alikuwa analinda nini. lakini hatuwezi kudanganyika kuwa alikuwa analinda chama na serikali. As PM alitakiwa kusafisha serikali sio kuondoka kuacha uchafu na kuwazuga watanzania. Alipojiuzulu alituaminisha kuwa yeye ndiye Richmod, haingii akilini Lowassa kukubali kusulubiwa kwa kosa ambalo si lake. Lowassa si yesu na wala hamkaribii yesu wala malaika, kwa hiyo hatutaki kuamini kuwa he was playing Jesus. Unless he was promised something for saving the one he claims to have saved.

Lowassa najua utakuwa unasoma hapa, ukweli ni kwamba YOU ARE GUILTY UNTIL YOU PROVE WITHOUT ANY REASONABLE DOUBT THAT YOU ARE INNOCENT, the reason why you are guilty is because you made us believe so, if you are claiming that you were a scapegoat and you are being punished for saving someone who did(someone who you know), then it is better that you publicly prove otherwise. Ulitufanya tuamini hivyo, na tunaendelea kufanya hivyo, kama kweli wewe si Richmond, ni vema ukatwambia ni nani maana wanaweza kukukolimba tukaendelea kuamini kuwa ni wewe kumbe Richmond ni mwingine.

Ni utoto kusema "mkinifukuza NEC nitasema Richmond ni nani". That is the lowest point of your political career, for sure you can do better than that. Unajua wazi nchi yetu ilivyo, so for your own sake, and for the sake of Tanzania please let us know who is Richmond.
 
Back
Top Bottom