Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

Kumbe Lowasa mwoga kiasi hiki, hafai kuwa rais. Alikuwa na jambo kubwa(kumwaga ugali) aliseme leo lakini kapigwa mkwala akabadilika dakika za majeruhi na kuja na upupu huu. Fisadi ni fisadi tu hawezi kuwa jasiri hata siku moja ,siku zote mwenye hatia ni mwoga.
 
Wakuu,

Lowassa kaondoka hapa Monduli muda si mrefu na inasemekana kaitwa Ikulu.

Alichoongea hakikuwa kwenye mpangilio unaoeleweka na imezidi kushangaza kuona anaondoka mida hii. Tunafuatilia tutawafahamisha zaidi
Nimekubali msemo wake kuwa yeye na rais hawakukutana barabarani. Kwa hiyo urafiki mbele au kwanza watanzania na matatizo yao shauri yao
pili kumbe ikulu kunaendeka tu? na kweli hawa wawili wananufaika na matatizo yetu
 
Wakuu,
  • .
  • Kuna waliofikia kudai eti namhujumu Mhe. Rais. Wengine eti nna mpango wa kumpindua kwenye Halmashauri kuu ijayo. Sina mpango wa hujuma na hata mabaya ya rais Kikwete siyafahamu.

teh tih toh jamani naombeni ruhusa ya kucheka.. tih toh.. ha ha haaaa... aa my Lowasa.. Ha he he.. Kuna yule informa wako anayesomasoma vijarida na vihabari na kukupasha yaliyojiri kwenye habari.. akipitia Humu jamvini ataona hapo nilipobold Red.. akurudishie taarifa kwamba kuna mtu mmoja jamvini amecheka sana uliposema hata mabaya ya mzee huyajui.. Mtu mzima kuogopa mtu mzima mwenzako ooooovyo.. unaogopa mpaka kivuli chako.. Pole. we?.. Halafu Ntakuvuruga mimi.. sipendi mtu mzima aongee hovyohovyo mbele ya watanzania. Lazima utuheshimu watanzania yaani sisi tuwe jalala la kudanganywa kila mchao?!. kwanini uongee ujingaujinga wakati ukweli unaujua.. Kuna siku mliwahi hata kutaka kurushiana ngumi na mzee kwenye Korido ya Hoteli kule nairobi.. unadhani cctv camera za hoteli hazijawarekodi??? na sababu yenyewe ya ugomvi wenu ni ya kipuuzi na aibu.. kha.. mnisamehe Mods.. Huyu Mheshimiwa anakera sana sometimes.. wacha niondoke zangu humu jamvini kama kuna mtu kanikera basi Lowasa zaidi.. nijizuie nisijefurisha zaidi.. BYE!!
 
Hivi siku hizi kuna direct flight kutoka Monduli mpaka Dar? Au amekodi Charter?
 
bishop hiluka unakosea kukopi majina yoooote ya cureent users...kama huna cha kupost ka usome coment za wenzako
 
Lowasa amepatwa na msongo mkubwa sana, kuna kitu alitaka kusema inaonekana alizuiwa wakati tayari kaita waandishi. Ningeomba video yake ili tuone (body language) ilikuwaje. Kuna wakati Invisible alisema kakatisha akaingia ndani. Sidhani kama aliwaita waandishi kuwaambia hajawatuma vijana wa Arusha, haiwezekani kuwa aliwaita kuwaambia hajakutana na JK barabarani. Jk kesha mtosa inawezekana swaga la Igunga linawachanganya wavua gamba hivyo wamevuta pumzi. Je simu ilitoka kwa nani ???????? Please invisible come out .............
 
Hapo bana hata akiongea maneno mengi kiasi gani,
Kama tu hakuzungumzia Richmond, Dowans, Kujivua Gamba na uenyekiti wa CCM mwaka 2012 basi mkutano wake huo utakua ni sawa vijiwe vya kahawa tu kwa ajili ya kupitishia muda jua lizame
 
teh tih toh jamani naombeni ruhusa ya kucheka.. tih toh.. ha ha haaaa... aa my Lowasa.. Ha he he.. Kuna yule informa wako anayesomasoma vijarida na vihabari na kukupasha yaliyojiri kwenye habari.. akipitia Humu jamvini ataona hapo nilipobold Red.. akurudishie taarifa kwamba kuna mtu mmoja jamvini amecheka sana uliposema hata mabaya ya mzee huyajui.. Mtu mzima kuogopa mtu mzima mwenzako ooooovyo.. unaogopa mpaka kivuli chako.. Pole. we?.. Halafu Ntakuvuruga mimi.. sipendi mtu mzima aongee hovyohovyo mbele ya watanzania. Lazima utuheshimu watanzania yaani sisi tuwe jalala la kudanganywa kila mchao?!. kwanini uongee ujingaujinga wakati ukweli unaujua.. Kuna siku mliwahi hata kutaka kurushiana ngumi na mzee kwenye Korido ya Hoteli kule nairobi.. unadhani cctv camera za hoteli hazijawarekodi??? na sababu yenyewe ya ugomvi wenu ni ya kipuuzi na aibu.. kha.. mnisamehe Mods.. Huyu Mheshimiwa anakera sana sometimes.. wacha niondoke zangu humu jamvini kama kuna mtu kanikera basi Lowasa zaidi.. nijizuie nisijefurisha zaidi.. BYE!!


salma kwa hili la leo huyu jamaa lazima apakwe matope ..anacheza na akili za watu..aache ujinga kabisa na ajue kuwa kuna watu tunamfaham vizuri tu....na leo ameamua kupindisha ukweli..ameona aibu kuwaambia wandishi wa habari dakika za mwisho kuwa hawezi kuongea nao ila akaona ni heri apoteze mda kwa kuongea ushenzi....nimeomba mwongozo kwa mod bado kimya
 
teh tih toh jamani naombeni ruhusa ya kucheka.. tih toh.. ha ha haaaa... aa my Lowasa.. Ha he he.. Kuna yule informa wako anayesomasoma vijarida na vihabari na kukupasha yaliyojiri kwenye habari.. akipitia Humu jamvini ataona hapo nilipobold Red.. akurudishie taarifa kwamba kuna mtu mmoja jamvini amecheka sana uliposema hata mabaya ya mzee huyajui.. Mtu mzima kuogopa mtu mzima mwenzako ooooovyo.. unaogopa mpaka kivuli chako.. Pole. we?.. Halafu Ntakuvuruga mimi.. sipendi mtu mzima aongee hovyohovyo mbele ya watanzania. Lazima utuheshimu watanzania yaani sisi tuwe jalala la kudanganywa kila mchao?!. kwanini uongee ujingaujinga wakati ukweli unaujua.. Kuna siku mliwahi hata kutaka kurushiana ngumi na mzee kwenye Korido ya Hoteli kule nairobi.. unadhani cctv camera za hoteli hazijawarekodi??? na sababu yenyewe ya ugomvi wenu ni ya kipuuzi na aibu.. kha.. mnisamehe Mods.. Huyu Mheshimiwa anakera sana sometimes.. wacha niondoke zangu humu jamvini kama kuna mtu kanikera basi Lowasa zaidi.. nijizuie nisijefurisha zaidi.. BYE!!

sijui nitumie theory gani za fikizikia kukupata frequency zako ..
usomeki ila unaonekana ni mwanga mkubwa kwenye hili giza totoro kwa sie wenye hamu ya kupata ukweli wa mambo
ila ngoja niendelee kuconnect dot ntafunguka tu.............
 
Uhuru wa vyombo vya habari unakuwa abused.

Sija muelewa,...
unakuwa abused kwa kumuandika sana au unakuwa
abused na magazeti yanayo eneza chuki za kidini?

Kwa jinsi alivo sema kwamba ata shitaki magazeti yanayo mfuata fuata
ina maanisha kwamba angekua raisi huyu waandishi wa habari wote
angesha biga "kimya" kwa style yoyote ile.
Possibly it will be the end of JF akiwa raisi,...hell never.
Next time when you get sick,don't come back.
I wish it will be soon before 2014.

He doesn't have the qualifications to be a president.
Ni dikteta asiye na manufaa,( udikteta mwingine mzuri lakini).
 
Ama kweli Lowassa kiboko. Masaa mawili na nusu tu tangu thread ianze Replies 227 and Views 4,365 ? Je hiyo siku muafaka ukifika itakuaje?!
 
Shukrani mkuu je tunaruhusiwa kuuliza maswali pia au hakuna maswali na majibu? Maana tuna lundo la maswali moja wapo ni ile nyumba kule London atuambie hela hiyo imetoka wapi???

Kuwa na nyumba London sio utajiri ni rahisi sana, kule nyumba zinauzwa kama magari na thamani ya nyumba iliyotumika ni ndogo sana, mahesabu huwa yanapigwa kutokea nyumba ilipojengwa. Kutokana na muda ambao amefanya kazi EL hata kama ni wewe kama ungekuwa na akili za maendeleo ungeweza kuwa na zaidi ya hata alivyonavyo EL pamoja na kuwa mengi ni maneno wala sio kweli. Ukiulizwa nyumba iko London mtaa gani na ni plot namba ngapi huwezi kujibu.
 
There are currently 838 users browsing this thread. (219 members and 619 guests)

Kweli siasa imeshika hatamu!
 
Wakuu,

Muda si mrefu tutaweza kwenda Live kutokea Monduli ambapo Mhe. Lowassa (Waziri Mkuu aliyejiuzulu) atakapoongea na vyombo vya habari. Tumefanikiwa kupenyeza mtu hivyo tutaweza kuwaletea alichoongea. Nita-update 1st post kulingana na atakavyokuwa anaongea.

Shukrani

=================
  • Mwandishi wetu kamsisitizia kuwa watu wamesisitiza wanataka kujua kauli yake juu ya Richmond/Dowans/Symbio na suala la kujivua gamba ndani ya CCM, vinginevyo mkutano huu hautakuwa na maana na watu wanahisi labda umetishwa. Kajibu kuwa masuala haya atayazungumzia lakini leo si wakati muafaka, kuna wakati atayazungumzia.
  • Mwandishi kamwuliza kama ametishwa, maana anaonekana kila la muhimu hataki kuongelea, kajibu kirahisi tu "SINTOJIBU MASWALI HAYO"
  • Mwandishi wetu pia kamwuliza juu ya 'Uvuaji Gamba', nalo kakataa katakata kuongelea, kasema si wakati muafaka.
  • Pamoja na mwandishi wetu kumweleza umuhimu wa yeye kuongelea suala la DOWANS/Richmond kakataa katakata na kusema ataliongelea wakati muafaka na si leo.
  • Wakuu... Kamaliza! Ila kamalizia na "I think this is enough for your stomach" sasa sijaelewa anamaanisha alichoongea au ......?
  • Juu ya DOWANS: Kaulizwa itakuwaje asihusishwe kwenye mjadala huo ilhali kuna watu ndani ya CCM wameshasema waliojiuzulu ndo walipe? Kasema SINA MUDA WA KUJIBU SWALI HILO!
  • Juu ya urais 2015: Hata mimi nashangaa, miaka bado sana, kwanini tuanze kuongelea urais wa 2015? Waandishi acheni propaganda, msipoandika chokochoko hizi hakuna atakayehangaika nazo.
  • Mitikisiko ndani ya CCM ni ya muda tu, tutapita katika hali hii.
  • MAJIBU: Si kama napuuza jitihada za serikali juu ya suala la ajira kwa vijana, lakini hali ni mbaya sana. Nashauri tuvunje kanuni, serikali ikope fedha na ijenge viwanda tuweze kuwaajiri watanzania wengi. Fedha zipo!
  • Moses Mashalo kauliza juu ya mustakabali wa CCM kwa siku zijazo kufuatia hali inayoendelea kwa sasa ndani ya CCM.
  • KAMALIZA... Maswali yanafuata
  • Uchumi wa dunia upo taabani, taifa letu linakabiliwa na hali mbaya. Shilingi yetu inazidi kuporomoka vibaya. Inflation inazidi kuelekea kubaya zaidi. Kuna tatizo kubwa la ajira kwa vijana, kubwa sana. Vijana wakiishi katika hali hii tutakuwa tumekalia bomu la muda na itapelekea kuvunjika kwa amani. Ni vyema tukatafuta suluhu ya mambo haya.
  • Naomba vyombo vya habari tusaidie nchi yetu. Tunapoandika propaganda za chuki kwa nia ya 'kulipuana' tujue tunalipeleka taifa kubaya.
  • Sasa niseme rasmi, IMETOSHA. Sintoendelea kuvumilia kuchafuliwa na vyombo vya habari. Nitachukua hatua kali dhidi ya magazeti yatakayonichafua na vyombo vya habari vyote vinavyonichafua. Ukinichafua nitakupeleka kwenye vyombo husika na niseme uhuru usio na nidhami ni fujo. Uhuru wa vyombo vya habari umekuwa 'abused' sana.
  • Vijana mara nyingi ni radical, wasibezwe na wasilaumiwe kwa wanachofanya bali waelekezwe. Anayekiuka sheria asifumbiwe macho.
  • Vijana wa UVCCM tusiwaingilie, ni taasisi muhimu kwa ajili ya chama chochote cha siasa.
  • Sheria ni sheria, hakuna aliye juu ya sheria. Kama kuna sheria inavunjwa hakuna anayetakiwa kuangaliwa tu.
  • Gazeti flani linaloniandama lilishafikia hatua ya kusema ndo nahusika na maasi ya vijana wa UVCCM, ni uwongo na wala sihusiki kwa namna yoyote na vijana wa Arusha. Nilikuwa nje kwa matibabu, ningejuaje nini wanapanga vijana?
  • Sijakutana na rais Kikwete barabarani, waache kunichonganisha naye na waache kunichafua mbele za watanzania. Walishasema eti nagombea urais mwaka 2010. Naamini hata rais Kikwete anajua kuwa huu ni uzushi tu.
  • Masuala ya Chama huwa yanaishia kwenye vikao, hii ya kubomoana nje ya vikao hayana maana. Siwezi kukihujumu chama changu mwenyewe.
  • Kuna waliofikia kudai eti namhujumu Mhe. Rais. Wengine eti nna mpango wa kumpindua kwenye Halmashauri kuu ijayo. Sina mpango wa hujuma na hata mabaya ya rais Kikwete siyafahamu.
  • Toka nilipojiuzulu uwaziri mkuu nilikaa kimya, kimya ni hekima toka kwa Mwenyezi Mungu
  • Anaomba kutoulizwa maswali ambayo ni nje ya hoja anayoongelea.
  • Anaanza kuongea sasa...
  • Alishakaa ili aanze kuongea, kaondoka na inaelekea kama kuna jambo anaenda kuliweka sawa kwanza.
  • Ilitarajiwa angeanza saa 4 kamili lakini inaelekea ataanza saa 4 unusu, waandishi wapo wengi. Atajivua gamba?

Inaonekana umeandika kiushabiki shabiki kitu ambacho si kizuri kwa mwaandishi. Ilitakiwa utoe vile alivyojibu na vile alivyoulizwa pasi na kuingiza ushabiki na kuacha suala kwa wasikilizaji au wasomaji watoe uamuzi.

Ok lakini thanks kwa taarifa.
 
Back
Top Bottom