Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

ngona nilale sasa......hakuna jipya back to square one!!
 
anasema fedha zipo, ziko wapi sasa mbona hatuzioni, wadogo zetu chungu mzima wamekosa mikopo kwa ajili ya elimu na ndio vijana haohao anaoongelea!
Na hivyo viwanda serikari liliyoshindwa kujiendesha itaweza kuendesha viwanda pia!?
TZ tumeishiwa! Another either person/leader/party/institution should rise to rescue this country and tell us the truth
Tatizo la umeme wanashindwa kulitatua mika miaka nenda miaka rudi na ndio kitovu cha mafisadi kujichotea pesa.HIVYO VIWANDA VITAENDESHWAJE???!!!!!!!!!
 
Nadhani kuna kitu kazuiliwa. Alikuwa kishakaa ili aanze kuongea mapema, akaondoka ghafla. Yawezekana alipigiwa simu na kupewa maelekezo tofauti? Matarajio ya wengi yalikuwa aongelee masuala mengi, Richmond/Dowans, hali ya usalama a nchi, afya yake (baada ya kudaiwa kuwa alikuwa nje kwa matibabu) n.k

Alichofanya kimenishangaza, not expected at all

Nimewapata Invisible.. kumbe jamaa alikuwa na meeting ndo maana akapigiwa simu kali.. Ok ok! sasa naskia mheshimiwa alikuwa kapaniki sana, alichokusudia kuongea sicho.. naskia alishajitutumua kwamba liwalo na liwe leo lazima kieleweke.. ile simu imemharibia dili.. Jamaa mwoga sana, siasa za kibongo hazihitaji waoga.. sasa hali yake itakuwa mbaya kwa sababu kuna nyoka mmoja ameniambia kwamba alikwenda kwenye trash ya pc aliyochapa hotuba yake, akairetrive kutoka kwenye pc dust-bin. na amesema ataiprint ili mhe akirudi DSM aikute mezani kwake.. ili kumwonyesha kwamba what he was going to do was already known. sasa tuone faida ya woga wake itakuwaje. na snake wa ukweli anadai ataimwaga hotuba hiyo wazi kwenye vyombo vya habari au gazeti, hotuba yenyewe inahusiana na mambo ya siri kati yake na mzee na si rahisi kuyakana kwamba si yake..
".... unakumbuka kwa uwazi, na wewe ni shahidi wa gharama na maumivu tuliyoyapata kuliokoa Jimbo la igunga, wala muda haujapita hata madonda yetu ndani ya chama hayajapoa..kuna mpuuzi mwingine anataka kutuwekea wakati mgumu tena.. unisikilize, Mimi sitakubaliana na Hilo, wanachama wote.. hawatakubaliana na Hilo, wala Sitaruhusu Chama kifie mikononi mwangu.. Utanisamehe.. kwa nitalotenda.."

hatupendi Kuona Vurugu ndani ya CCM au CHADEMA au chama chochote cha Siasa. ila zaidi hatupendi waoga.. Uoga ni sumu mbaya zaidi.. nakumbuka Mzee Mengi aliwahi sema Mwoga ni zaidi ya mchawi..
 
images
 
I updated the 1st post:

Mwandishi wetu kamsisitizia kuwa watu wamesisitiza wanataka kujua kauli yake juu ya Richmond/Dowans/Symbio na suala la kujivua gamba ndani ya CCM, vinginevyo mkutano huu hautakuwa na maana na watu wanahisi labda umetishwa. Kajibu kuwa masuala haya atayazungumzia lakini leo si wakati muafaka, kuna wakati atayazungumzia.
 
hao sijui kmati kuu wakikutana wamtimue tu
 
huyu jamaa si angejiroaekodi kwny cd kisha angepeleka kwny vyombo vya habari, ni kitugani sasa hiki amefanya.
 
I updated the 1st post:

Mwandishi wetu kamsisitizia kuwa watu wamesisitiza wanataka kujua kauli yake juu ya Richmond/Dowans/Symbio na suala la kujivua gamba ndani ya CCM, vinginevyo mkutano huu hautakuwa na maana na watu wanahisi labda umetishwa. Kajibu kuwa masuala haya atayazungumzia lakini leo si wakati muafaka, kuna wakati atayazungumzia.


aende zake huko....huyo alikuwa amekuja mazima kumwaga kila kitu ila nahisi alivyoondoka gafla kwa dakika kadhaa amepigwa mkwara huyo ndio maana kaongea bila mpangilio
 
aende zake huko....huyo alikuwa amekuja mazima kumwaga kila kitu ila nahisi alivyoondoka gafla kwa dakika kadhaa amepigwa mkwara huyo ndio maana kaongea bila mpangilio
Penye bold panahusika...

Jamaa ameonekana ghafla kama hakujipanga ilhali ilishaandaliwa muda mrefu. He was not settled at all.
 
".... unakumbuka kwa uwazi, na wewe ni shahidi wa gharama na maumivu tuliyoyapata kuliokoa Jimbo la igunga, wala muda haujapita hata madonda yetu ndani ya chama hayajapoa..kuna mpuuzi mwingine anataka kutuwekea wakati mgumu tena.. unisikilize, Mimi sitakubaliana na Hilo, wanachama wote.. hawatakubaliana na Hilo, wala Sitaruhusu Chama kifie mikononi mwangu.. Utanisamehe.. kwa nitalotenda.."

.

Hebu tuambie haya maneno kaandika nani? Hujaeleweka Salma.
 
".... unakumbuka kwa uwazi, na wewe ni shahidi wa gharama na maumivu tuliyoyapata kuliokoa Jimbo la igunga, wala muda haujapita hata madonda yetu ndani ya chama hayajapoa..kuna mpuuzi mwingine anataka kutuwekea wakati mgumu tena.. unisikilize, Mimi sitakubaliana na Hilo, wanachama wote.. hawatakubaliana na Hilo, wala Sitaruhusu Chama kifie mikononi mwangu.. Utanisamehe.. kwa nitalotenda.."


 
Naanza kupoteza imani yangu kwake 2015

Kwa level ya Lowassa hakupaswa kabisa kuitisha press conference ya kuongelea vitu vidogo kama hivyo, nadhani leo atakuwa amewanyong'onyeza sana wapenzi wake na kuwapa kicheko adui zake...
 
Wakuu,

Muda si mrefu tutaweza kwenda Live kutokea Monduli ambapo Mhe. Lowassa (Waziri Mkuu aliyejiuzulu) atakapoongea na vyombo vya habari. Tumefanikiwa kupenyeza mtu hivyo tutaweza kuwaletea alichoongea. Nita-update 1st post kulingana na atakavyokuwa anaongea.

Shukrani

=================
  • Mwandishi wetu kamsisitizia kuwa watu wamesisitiza wanataka kujua kauli yake juu ya Richmond/Dowans/Symbio na suala la kujivua gamba ndani ya CCM, vinginevyo mkutano huu hautakuwa na maana na watu wanahisi labda umetishwa. Kajibu kuwa masuala haya atayazungumzia lakini leo si wakati muafaka, kuna wakati atayazungumzia.
  • Mwandishi kamwuliza kama ametishwa, maana anaonekana kila la muhimu hataki kuongelea, kajibu kirahisi tu "SINTOJIBU MASWALI HAYO"
  • Mwandishi wetu pia kamwuliza juu ya 'Uvuaji Gamba', nalo kakataa katakata kuongelea, kasema si wakati muafaka.
  • Pamoja na mwandishi wetu kumweleza umuhimu wa yeye kuongelea suala la DOWANS/Richmond kakataa katakata na kusema ataliongelea wakati muafaka na si leo.
  • Wakuu... Kamaliza! Ila kamalizia na "I think this is enough for your stomach" sasa sijaelewa anamaanisha alichoongea au ......?
  • Juu ya DOWANS: Kaulizwa itakuwaje asihusishwe kwenye mjadala huo ilhali kuna watu ndani ya CCM wameshasema waliojiuzulu ndo walipe? Kasema SINA MUDA WA KUJIBU SWALI HILO!
  • Juu ya urais 2015: Hata mimi nashangaa, miaka bado sana, kwanini tuanze kuongelea urais wa 2015? Waandishi acheni propaganda, msipoandika chokochoko hizi hakuna atakayehangaika nazo.
  • Mitikisiko ndani ya CCM ni ya muda tu, tutapita katika hali hii.
  • MAJIBU: Si kama napuuza jitihada za serikali juu ya suala la ajira kwa vijana, lakini hali ni mbaya sana. Nashauri tuvunje kanuni, serikali ikope fedha na ijenge viwanda tuweze kuwaajiri watanzania wengi. Fedha zipo!
  • Moses Mashalo kauliza juu ya mustakabali wa CCM kwa siku zijazo kufuatia hali inayoendelea kwa sasa ndani ya CCM.
  • KAMALIZA... Maswali yanafuata
  • Uchumi wa dunia upo taabani, taifa letu linakabiliwa na hali mbaya. Shilingi yetu inazidi kuporomoka vibaya. Inflation inazidi kuelekea kubaya zaidi. Kuna tatizo kubwa la ajira kwa vijana, kubwa sana. Vijana wakiishi katika hali hii tutakuwa tumekalia bomu la muda na itapelekea kuvunjika kwa amani. Ni vyema tukatafuta suluhu ya mambo haya.
  • Naomba vyombo vya habari tusaidie nchi yetu. Tunapoandika propaganda za chuki kwa nia ya 'kulipuana' tujue tunalipeleka taifa kubaya.
  • Sasa niseme rasmi, IMETOSHA. Sintoendelea kuvumilia kuchafuliwa na vyombo vya habari. Nitachukua hatua kali dhidi ya magazeti yatakayonichafua na vyombo vya habari vyote vinavyonichafua. Ukinichafua nitakupeleka kwenye vyombo husika na niseme uhuru usio na nidhami ni fujo. Uhuru wa vyombo vya habari umekuwa 'abused' sana.
  • Vijana mara nyingi ni radical, wasibezwe na wasilaumiwe kwa wanachofanya bali waelekezwe. Anayekiuka sheria asifumbiwe macho.
  • Vijana wa UVCCM tusiwaingilie, ni taasisi muhimu kwa ajili ya chama chochote cha siasa.
  • Sheria ni sheria, hakuna aliye juu ya sheria. Kama kuna sheria inavunjwa hakuna anayetakiwa kuangaliwa tu.
  • Gazeti flani linaloniandama lilishafikia hatua ya kusema ndo nahusika na maasi ya vijana wa UVCCM, ni uwongo na wala sihusiki kwa namna yoyote na vijana wa Arusha. Nilikuwa nje kwa matibabu, ningejuaje nini wanapanga vijana?
  • Sijakutana na rais Kikwete barabarani, waache kunichonganisha naye na waache kunichafua mbele za watanzania. Walishasema eti nagombea urais mwaka 2010. Naamini hata rais Kikwete anajua kuwa huu ni uzushi tu.
  • Masuala ya Chama huwa yanaishia kwenye vikao, hii ya kubomoana nje ya vikao hayana maana. Siwezi kukihujumu chama changu mwenyewe.
  • Kuna waliofikia kudai eti namhujumu Mhe. Rais. Wengine eti nna mpango wa kumpindua kwenye Halmashauri kuu ijayo. Sina mpango wa hujuma na hata mabaya ya rais Kikwete siyafahamu.
  • Toka nilipojiuzulu uwaziri mkuu nilikaa kimya, kimya ni hekima toka kwa Mwenyezi Mungu
  • Anaomba kutoulizwa maswali ambayo ni nje ya hoja anayoongelea.
  • Anaanza kuongea sasa...
  • Alishakaa ili aanze kuongea, kaondoka na inaelekea kama kuna jambo anaenda kuliweka sawa kwanza.
  • Ilitarajiwa angeanza saa 4 kamili lakini inaelekea ataanza saa 4 unusu, waandishi wapo wengi. Atajivua gamba?

Mkuu angekuwa amesoma hii thread..........yangekuwa mengine leo hii!!!!!!!

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...e-can-never-be-misquoted-a-true-friend-2.html
 
Back
Top Bottom