mbona huwa anarudia tu kuwa hajakutana na jk barabarani na hasemi walikutana wapi?
Awataki kusema tu, Ila walikutana hall 3 pale Mlimani kwa chumba ya yure dada mig..oo.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mbona huwa anarudia tu kuwa hajakutana na jk barabarani na hasemi walikutana wapi?
sawa mh. wa richmond , lakini mbona hujatuambia kuhusu richmond, na pia kazi wanazofanya vijana wako pale arusha ambao wao wanasema wewe ni wao. hakuna kitu kitakachofanyika katika nchi hii halafu iwe sir, hakuna, kwa vile wewe unajua unachokifanya ktk serikali hii, unafahamu sana. kwa nadhani usijitetee cha msingi acha kuihujumu serikali ya jk, uache wewe pamoja na vijana wako. kwa sababu wewe unaweza kuficha lakini vijana wako hawawezi kuficha wanayasema yote kwa sababu si vijana wote ni wako wengine ni ndumilakuwili nimeamua kukueleza ukweli, yaani unaanza kukataa kuhusu hujuma baada ya kushindwa kuhujumu? ni ajabu. serikali hii imechaguliwa na watanzania unapoihujumu basi unawahujumu watanzania ambao wewe unadai unawaonea huruma. huruma gani mh. wakati ulikuwa tayari kuhakikisha unalazimisha kusaini mikataba gandamizi? na ya kifisadi. vijana gani unawatetea wewe ulipokuwa waziri mkuu hukujua kuwa kuna vijana wasio na kazi, leo hii wakati hupo madarakani unaanza kuona! hapana huu si uungwana huo ni udanganyifu. leo baada ya kuwepo pinda umeanza kuona ajira ya vijana ni tatizo ulikuwa wapi, au ulikuwa busy na mikataba feki sasa ndio unakumbuka. Samahani sana mh. inatosha ,uliowafanyia watz inatosha, kama unadhani ulikuwa mwema ila hatukukuelewa basi ni bahati mbaya, unaweza kudanganya monduli lakini huwezi kudanganya tz nzima. inatosha, ushauri, nakuomba kwa huruma yako usitaafu siasa ili ufanye kazi nyingine , unafahamika una kampuni na fedha, mashamba,majumba mengi ndani na nje ya nchi toka enzi za nyerere tunakuomba utuhurumie sasa watz. inatosha .umwogope mungu na pia fahamu jinsi ulivyo na ukwasi na jinsi hali wa watz wengine walivyo na shida na jinsi wanavyotaabika. ukijiona wewe ulivyo mbali na watz wengune ndio utajua kuwa wewe ni tajiri. pokea ujumbe huu
"I think this is enough for your stomach" watu matumbo yalikuwa yanaunguruma ndiyo maana kamanisha hivyo, cha maana alichoongea ni hicho cha vijana na ajira, ni bomu haswa
Katika hilo la usiri wa serikali hakuna haja ya kusubiri Katiba mpya, Katiba mpya haitakua "kikombe cha babu" kwa kila tatizo.KATIBA mpya ituondolee usiri katika mambo yanayohusu nchi. Kila kitendo cha kiongozi lazima kiwe halali na kihojiwe, taarifa sahihi na za ukweli lazima zipatikane. Inaumiza kama mtu anakataa kujibu maswali yenye umuhimu kwa jamii na hufanya mahojiano mazima yamhusu yeye na nafsi yake tu!
Wengi wetu tuliokaa mkao wa kula toka jana na kudhani kiranja wa Monduli atamwaga ugali baada ya mpangaji wetu wa Magogoni kumwaga mboga miezi kadhaa ilopita tumepigwa na butwaa baada ya EL kuongelea ajira ya vijana hahaha!
Kwa wenye ufahamu hili ni tusi kubwa sana kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano,kwa kuwa kama Rafiki wa karibu wa Rais mbali ya kuwa Kiongozi hawezi kuamka kuita waandishi wa habari na kuwaambia kuwa ''HATA MABAYA YA RAIS KIKWETE SIYAFAMU''kwa kuwa anasisitiza HAKUKUTA NA RAIS KIKWETE MITAANI atambue kuwa Wananchi wataendelea kumbana kusema UKWELI MPAKA PUMZI YA MWISHO.
- Kuna waliofikia kudai eti namhujumu Mhe. Rais. Wengine eti nna mpango wa kumpindua kwenye Halmashauri kuu ijayo. Sina mpango wa hujuma na hata mabaya ya rais Kikwete siyafahamu.
"Gazeti flani linaloniandama lilishafikia hatua ya kusema ndo nahusika na maasi ya vijana wa UVCCM, ni uwongo na wala sihusiki kwa namna yoyote na vijana wa Arusha. Nilikuwa nje kwa matibabu, ningejuaje nini wanapanga vijana?"
.......? Do huu ugonjwa utakuwa hatari sana maana Nigeria, Malasia, Singapore, India, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani???? Nilifikiri viongozi wetu wanatibiwa India??
Tofauti na RA, EL hawezi kutema ugali kabisa kwa sasa. Huyu mheshimiwa ana imani kubwa kutinga magogoni 2015 na kampeni zake ziko wazi, nawashangaa mnapokaa na kumsubiri ateme ugali. Kimsingi mimi namwona anajibu tuhuma nyingi zinazoelekezwa kwake na maadui wa humo humo CCM kwa sasa.
Nadhani kikubwa tunachoweza kukiona hapa ni kwamba vita ndani ya CCM kwenyewe imepamba moto, sina data za ndani lakini kwa sisi watazamaji tunaona wazi na kuna ushahidi wa wazi kwamba mpambano upo na ni mkali kiasi cha kuwafanya wanaopambana kushindwa kuficha kucha zao. Ni ajabu leo hii kusikia kila mmoja ndani ya CCM hii hii yenye kujisifu kwa amani kulalama anataka kutolewa roho na mwana-CCM mwenzake, mikwaruzano ya wazi kwenye vyombo vya habari, matukio ya kijangili na ki-ushirikina ya wazi wazi kabisa ni dalili tosha kabisa kwamba sasa mambo yanaelekea kulazimika kukaa sawa. EL kasema hakuna aliye juu ya sheria, kama ni sheria isiwe kwa mmoja tu... yaani anamaanisha kwanini mnafuata yeye peke yake wakati hajafanya dhambi peke yake? kama ni sheria kwanini msianze huko juu kabisa? na kama hamuwezi kuanza huko juu kabisa basi mwacheni aendelee na mambo yake.