Elections 2015 Lowassa: Serikali yangu itaangalia jinsi ya kuvunja mkataba wa bandari ya Bagamoyo

Elections 2015 Lowassa: Serikali yangu itaangalia jinsi ya kuvunja mkataba wa bandari ya Bagamoyo

Hai make sense kutumia mabilioni kujenga reli lakini ina make sense kutumia mabilioni kugawana escrow, kulipa wasanii ktk kampeni,kutumia nguvu ya ziada[mabilion au matrilioni ya Tshs.] katika kampeni kwa ajili ya kudhibiti upinzani ambao umepata nguvu kwasababu ya Serikali ya ccm kutotendea watz. haki katika mambo mbalimbali.
 
Nimeipenda hii.Ujenzi wa bandari ya Bagamoyo hauna maaslahi kabisa kwa taifa.Ni ufujaji tu wa resources za nchi yetu unaolenga kwenye maslahi binafsi.

Ngoyai, isingekuwa tatizo la kiafya,ungeipata kura yangu bila kinyongo.Hata hivyo ili nithibitishe hasira yangu dhidi ya CCM,kura yangu nitakupa.
Leo katika taarifa ya habari ya Channel Ten nimemsikia Rais wa awamu ya tano Ngoyai Lowassa akisema kwamba serikali yake itaangalia jinsi ya kuuvunja mkataba wa bandari ya Wachina Bagamoyo.
Amesema haoni mantiki ya kutumia mabilioni kujenga bandari moja Bagamoyo wakati bandari za Tanga na Mtwara ziko ovyo.
Kama kawaida wananchi wa Tanga wamesema kura zao zote ni kwa UKAWA na adui CCM lazima asome namba mwaka huu.....
VIVA UKAWA!
NOTE: Kwa msio fahamu kuna umbali wa kilomita 1200 kutoka Tanga mpaka Kampala (Uganda) ukilinganisha na kilomita 1500 kutoka Mombasa (Kenya) mpaka Kampala. Lakini Waganda wanatumia bandari ya Mombasa sana kwa sababu Tanga hamna kitu!
 
Hapa tunaongelea Bandari ambayo inasafirisha Mizigo in bulk ya Uganda, kuwafanya Waganda waache kutumia Bandari ya Mombasa badala yake watumie yetu ni kama haiwezekani kwa maana hatuwezi kufanya huwo uwekezaji, elewa viwanda vikubwa Uganda viko Mji wa Jinja na hapo katikati ambapo ndipo Uganda Railway ilikopita ikitokea Mombasa na inakwenda mpaka Ziwa Viktoria ambako pia kuna Bandari inayoshusha mizigo na kusafirishwa kwa meli, sasa ili kuwafanya watumie Bandari yetu nilazima tufanye uwekezaji wote huwo, sasa kwa mizigo ipi ya maana ya ambayo Uganda wanayo?

Mkuu maelezo yako yanaeleweka. Nadhani Lowasa asiingie madarakani na kusnza kulipiza visasi.
Kuna mambo mengine sio ya kuyaongelea sasa hivi. Angoje hadi awe rais.mpkaka hapo kura za bagamoyo hajazikosa?
 
It makes alot of sense kudevelop Northern Corridor ya Tanzania (reli na barabara kutoka Tanga mpaka kanda ya ziwa kupitia Moshi-Arusha). Kumbuka kwamba Uganda wamegundua mafuta na wanataka kuyaexport kupitia bandari ya Tanga, hivyo bomba pia litajengwa.
Fanya research kabla ya kuandika. Uganda ni nchi inayoimport goods worth over $4 billion per year, na kuexport $3.2 billion. Hizo ni ndogo kwako?
Na nani alikuambia hiyo corridor itakuwa inatumiwa na Uganda pekee?
Amka ndugu weka uchama pembeni sio kila kitu ni siasa!

Tatizo unasikiliza maneno ya wanasiasa na kuyaaamini na hapa namaanisha wote wa Ug, Ke na kwetu pia! Hawo wanasiasa wote hakuna kitu wanajua wao wanaongea tu kwa kufuata kile watu kama ninyi mnapenda kusikia na maamuzi wanayoyafanya ndiyo yanayokuja kuzigharimu nchi zetu!
Uganda hawawezi kutumia Bandari ya Tanga kwa ajili ya ku-export mafuta yao ni rahisi kihivyo tu!

Pili Tanzania hatuna fedha ya kuwekeza kwenye Ujenzi wa Reli mpya ya ktk Tanga mpka Uganda pmj na Bandari ili kukidhi soko la Uganda, hayo maneno yote unayosikia ya Bandari ya Bagamoyo hizo siyo fedha zetu ni fedha za ktk Uchina na mtoa fedha ndiyo anaamua ni wapi aweke fedha yake sasa kama wamechagua B'moyo
wana sababu ingawaje sizijui sababu zenyewe!

Tatu kama ukiniuliza mimi Tanzania kwa sasa hatuhitaji reli mpya ya ktk Tanga kwenda Uganda bali tunahitaji kwanza kuzijenga upya Reli zetu tulizonazo ili zifanye kazi kwa full capacity kama Reli ya kati iende sambamba na kufufua Bandari ya Kigoma ambayo ilikuwa inashusha mizigo ktk kwenye treni na kuipakia kwenye Meli kwenda Zambia, Kongo na Burundi, kufufua na kuijenga upya reli ya ktk Dar kupitia Ruvu na nyingine ktk Tanga mpaka Arusha, hivyo tunapaswa kuanzia hapo kwanza kabla ya kufikiria kujenga Reli ambayo haipo kabisa sijui mpka Uganda!
 
Lowassa ana uzoefu wa kuvunja mikataba feki, hata wa RICHMOND alitaka uvunjwe, KIKWETE akachomoa!
 
Ndio sababu aingie Ikulu Magufuli.ataendeleza kanda zote.sio UKAWA inatazama kanda moja tu.kaskazini sijasikia mkataba utakaovunjwa
 
Wakati mkataba unaingiwa mbona hakufanya chochote kuzuia??? Mnafiki mkubwa huyo....
 
Tanga wameiyuwa kwa makusudi kwa kuwani mji wa kiislam
Mji wa Kiislam? We nawe umepotea. Hakuna watu wanaokaa kikao kushauriana kwamba tuiue sehemu flan kwa sababu ni ya watu wa dini flani.....hizo ni propaganda umelishwa na probably watu wa CCM!
Tanzania ni moja na Watanzania ni wamoja. Udini hauna nafasi Tanzania hii!
 
Bangi za Arusha mbaya sana.... Kuvunja mkataba ulioridhiwa na serikali mbili si sawa na kuvunja yai viza...
Wewe wa ajabu sana, yaani akili zako zinakutuma kua ni sahihi kujenga bandari mpya kabisa Bagamoyo, 60km from dar es salaam badala ya kuzikarabati bandari za Mtwara na Tanga ambazo tayari zipo na zinafanya kazi? Ukiweka ushabiki pembeni ukajiuliza hili swali utajua kama huu mkataba unafaa kuvunjwa au uachwe uendelee
 
Namuomba Mungu Lowassa awe raisi maana hata huu mkataba niliokuwa natamani ufutiliwe mbali amesema hauna mantiki. Cc JokaKuu
 
Last edited by a moderator:
hii bandari ilikua ijengwe tanga eneo la mwambani lakini mkwere akaipeleka kwake
 
Sijui nani anaemkaririsha Lowassa ahadi, atwambie akivunja huo mkataba fidia atatoa mfukoni mwake.?

Naona Lowassa anazidi kujiweka mbali na ikulu.

kama hujaelewa viongozi wa ukawa ni wanafiki sana wanatafuta vijimambk vidogo dogo na kumdanganya mzee kuwa ukisema hivi utapata wafuasi wengi . mfano ili kuwapata waislam wa zanzibar mzee aliambiwa agusie swala la kuwatoa MASHEKH MAGEREZANI litampaa kiki mara tena NTAMTOA BABU SEYA , mara tena NTAMFUFUA BALALI. sasa naona tena la bandari ya bagamoyo yote hayo wanamdanganya mzee wa watu maskini
 
Tatizo unasikiliza maneno ya wanasiasa na kuyaaamini na hapa namaanisha wote wa Ug, Ke na kwetu pia! Hawo wanasiasa wote hakuna kitu wanajua wao wanaongea tu kwa kufuata kile watu kama ninyi mnapenda kusikia na maamuzi wanayoyafanya ndiyo yanayokuja kuzigharimu nchi zetu!
Uganda hawawezi kutumia Bandari ya Tanga kwa ajili ya ku-export mafuta yao ni rahisi kihivyo tu!

Pili Tanzania hatuna fedha ya kuwekeza kwenye Ujenzi wa Reli mpya ya ktk Tanga mpka Uganda pmj na Bandari ili kukidhi soko la Uganda, hayo maneno yote unayosikia ya Bandari ya Bagamoyo hizo siyo fedha zetu ni fedha za ktk Uchina na mtoa fedha ndiyo anaamua ni wapi aweke fedha yake sasa kama wamechagua B'moyo
wana sababu ingawaje sizijui sababu zenyewe!

Tatu kama ukiniuliza mimi Tanzania kwa sasa hatuhitaji reli mpya ya ktk Tanga kwenda Uganda bali tunahitaji kwanza kuzijenga upya Reli zetu tulizonazo ili zifanye kazi kwa full capacity kama Reli ya kati iende sambamba na kufufua Bandari ya Kigoma ambayo ilikuwa inashusha mizigo ktk kwenye treni na kuipakia kwenye Meli kwenda Zambia, Kongo na Burundi, kufufua na kuijenga upya reli ya ktk Dar kupitia Ruvu na nyingine ktk Tanga mpaka Arusha, hivyo tunapaswa kuanzia hapo kwanza kabla ya kufikiria kujenga Reli ambayo haipo kabisa sijui mpka Uganda!
Umepata aisee wana sababu zao ambazo mimi na wewe hatuzijui
Kuhusu hilo bomba la mafuta tungekuwa watu serious kama wakenya ingewezekana tena sana tu.
Reli inaanzia Tanga-Moshi-Arusha-Musoma then from Musoma mizigo inapanda meli kwenda moja kwa moja mpaka Kampala
Huo mpango wa kujenga upya reli ya kati yote kwa mara moja ndio naona haiwezekani. Bora tujenge hizi za Tanga na Mtwara kwanza na hiyo ya kati inaweza kujengwa in phases, phase one ikiwa Dar-Dodoma.
 
Back
Top Bottom