Elections 2015 Lowassa: Serikali yangu itaangalia jinsi ya kuvunja mkataba wa bandari ya Bagamoyo

Elections 2015 Lowassa: Serikali yangu itaangalia jinsi ya kuvunja mkataba wa bandari ya Bagamoyo

Tatizo unasikiliza maneno ya wanasiasa na kuyaaamini na hapa namaanisha wote wa Ug, Ke na kwetu pia! Hawo wanasiasa wote hakuna kitu wanajua wao wanaongea tu kwa kufuata kile watu kama ninyi mnapenda kusikia na maamuzi wanayoyafanya ndiyo yanayokuja kuzigharimu nchi zetu!
Uganda hawawezi kutumia Bandari ya Tanga kwa ajili ya ku-export mafuta yao ni rahisi kihivyo tu!

Pili Tanzania hatuna fedha ya kuwekeza kwenye Ujenzi wa Reli mpya ya ktk Tanga mpka Uganda pmj na Bandari ili kukidhi soko la Uganda, hayo maneno yote unayosikia ya Bandari ya Bagamoyo hizo siyo fedha zetu ni fedha za ktk Uchina na mtoa fedha ndiyo anaamua ni wapi aweke fedha yake sasa kama wamechagua B'moyo
wana sababu ingawaje sizijui sababu zenyewe!

Tatu kama ukiniuliza mimi Tanzania kwa sasa hatuhitaji reli mpya ya ktk Tanga kwenda Uganda bali tunahitaji kwanza kuzijenga upya Reli zetu tulizonazo ili zifanye kazi kwa full capacity kama Reli ya kati iende sambamba na kufufua Bandari ya Kigoma ambayo ilikuwa inashusha mizigo ktk kwenye treni na kuipakia kwenye Meli kwenda Zambia, Kongo na Burundi, kufufua na kuijenga upya reli ya ktk Dar kupitia Ruvu na nyingine ktk Tanga mpaka Arusha, hivyo tunapaswa kuanzia hapo kwanza kabla ya kufikiria kujenga Reli ambayo haipo kabisa sijui mpka Uganda!

Pesa za kuwalipa fidia wakazi wanaohamishwa kupisha huo ujenzi zimechakachuliwa sana watu wanalipwa pesa Viduchu ulipaji wa fidia ni wa hovyo hovyo hauzingatii ukubwa wa kiwanja na mali zilizopo ndani, walipaji fidia wamefanya ufisadi mkubwa kwa kuwaibia pesa wale wakazi ambao wana uelewa mdogo juu ya haki zao. Bandari ya Bagamoyo si muhimu kwa sasa.
 
kuna harufu ya ufisadi kwenye hiyo bandari ,,, ya DSM c inatosha bora ingeboreshwa bandari ya mtwara na tanga
 
Hizi contract za bagamoyo ni za deal deal tu , jamaa wanasubir big man aondoke ofisin then wapige chini mradi mzima
 
Ingekuwa vyema kama ungesemea kidogo hiyo ya bagamoyo na umuhimu wake. Si lazima mizigo kwenda Uganda tu, tuna viwanda kaskazini mwa Tanzania. Ambako vipuli vya kuviendesha vinahitajika. Kwa swala la mtwara, kuna nchi jirani kama Zambia, mikoa yetu ya mbeya na kwingineko nazo zingefaidi. Iweje bagamoyo? Tafadhali fafanua ndugu, nasi tujue dhana halisi ya hiyo bandari ya Bagamoyo.

Bandari hii imejengwa Kama fadhila kwa china baada ya kutoa pesa zote za kampeni ya ccm pia China wataiendesha hiyo Bandari wenyewe kwa mda wa miaka 50 ndipo irejeshwe mikononi mwa Serikali ya Tanzania, Kuna malalamiko mengi juu ya fidia kwa wakazi wanaohamishwa kupisha huo Ujenzi ( kufa kufaana) kuna wajanja wachache Tatari wamepiga pesa nyingi kupitia humo humo fidia kwa kiasi kikubwa ni za hovyo hovyo wanalipa kulingana na Uelewa wa mtu wakiona wewe ni mjanja unalipwa pesa angalau angalau hata Kama kiwanja chako ni kidogo, lakini wakijua wewe huna uelewa wa haki zako unalipwa pesa kiduchu hata kama unamiliki kiwanja kikubwa na nyumba, Lowasa analielewa hili jambo vizuri ndiyo Maana kasema ataupitia Upiya huo mkataba wa Bandari ya Bagamoyo na kuhakikisha kuwa haki kwa wakazi zimezingatiwa.
 
Hizi contract za bagamoyo ni za deal deal tu , jamaa wanasubir big man aondoke ofisin then wapige chini mradi mzima

Lowasa kaongea na wakazi wa Bagamoyo wamemweleza jinsi wanavyonyanyaswa kwa kulipwa Fidia za hovyo hovyo zisizozingatia ukubwa wa viwanja na nyumba zao. Mkataba huo lazima upitiwe upya kwanza kama kweli utakuwa na umuhimu hao wachina wapelekwe Tanga na Lindi na mtwara wajenge Bandari kubwa huko hapo Bagamoyo wananchi bado fidia zao wamepunjwa kwa kuibiwa kifisadi.
 
Nimeona bora muwekezaji mzungu kuliko mchina.


Niliposikia tu WACHINA, wanajenga BURE, kisha wanatumia miaka 50 bureeeee... chini ya Jeshi la CHINA...!!! NILIJUA TUMEKWISHAAAA...!!! WACHINA wakijenga hiyo bandari na kutumia 50 years free of TAXES... HAKI YA MUNGU... TANZANIA ITABAKI SCRAPERS...!!! Wachina wezi jamani...!!! Hakuna wezi kama wachina... CCM ndio marafiki wa wachina sbb ndio wezi wenzao...!!!

BAGAMOYO PORT is the worst ever contract this Govnt of JK has entered with CHINESE... just like Gas contracts...!!! Mungu tuokoe...!!!
Tanga wangeijenga kubwa sanaaaa.. kwa gharama ya serikali 100%... kisha mizigo yote ya nje ya nchi ipitie Tanga...!!! Hakuna haja ya kujenga Bangamoyo, kwa contract ya HOVYO KABISA DUNIANI...!!!

Lowassa, UKAWA tukomboeni...!!!

Mungu tusaidie jamani...!!! Tumekwishaa..!!!🙆🙆🙆
 
Kujengwa bandari hii ni kufuja hela na kuendelea kwao tuu.
Mtwara na TANGA ndo ziliitaji massive investment kama izi.
Apo kwa kweli big no huo mkataba uvunjwe tuu maana ni Yale Yale ya kutaka kujengwa international airport ARUSHA badala ya Mbeya ili hali KIA iko apo just 50km kwa inchi ambayo such airport hazifiki tatu
 
Leo katika taarifa ya habari ya Channel Ten nimemsikia Rais mtarajiwa wa awamu ya tano Ngoyai Lowassa akisema kwamba Serikali yake itaangalia jinsi ya kuuvunja mkataba wa bandari ya Wachina Bagamoyo.

Amesema haoni mantiki ya kutumia mabilioni kujenga bandari moja Bagamoyo wakati bandari za Tanga na Mtwara ziko ovyo.

Kama kawaida wananchi wa Tanga wamesema kura zao zote ni kwa UKAWA na adui CCM lazima asome namba mwaka huu.

VIVA UKAWA!

NOTE: Kwa msio fahamu kuna umbali wa kilomita 1200 kutoka Tanga mpaka Kampala (Uganda) ukilinganisha na kilomita 1500 kutoka Mombasa (Kenya) mpaka Kampala.

Lakini Waganda wanatumia bandari ya Mombasa sana kwa sababu Tanga hamna kitu.

Lowassa hamuwezi na hata muweza mtoto wa mjini Jakaya Kikwete,wacha ajifurahishe tu,mtoto wa mjini ni wamjini na wa shamba ni washamba tu.Kesha mtangulia milele.
 
Kwakweli hata m sioni kama kuna umuhimu sana kujengwa bandari mpya ya bagamoyo with trillions of money wakat tuna bandari zinazohitaji kuboreshwa tu.
 
Lowassa kweli ni GENIUS...!!! Anaona makosa yote JK anayofanya.. makosa makubwa ya wazi kabisa..!!! Vunja kabisa huu mkataba baba ukiingia tu madarakani... Bagamoyo port ni UFISADI WA KUTISHA...!!! WACHINA WATAMALIZA NCHI HII... huu ni mkataba mbovu kuliko yote Tz...!!

Mungu tusaidie...!!!
 
Lowassa hamuwezi na hata muweza mtoto wa mjini Jakaya Kikwete,wacha ajifurahishe tu,mtoto wa mjini ni wamjini na wa shamba ni washamba tu.Kesha mtangulia milele.


Wee kweli...🐗🐗

Kwanini unaishi..? Hasara tupu wewe.."!😨😨
 
Ndugu inabidi kwanza uelewe Historia ya haya mambo kabla ya kuandika tu kwa ushabiki wa kisiasa! Sababu ya nchi ya Uganda kutumia Bandari Mombasa haina uhusiano wowote ule na Tanga, TanZania!

Uganda wanatumia Bandari ya Mombasa kwa sababu za Kihistoria, Wazungu walijenga Reli ya kutoka Mombasa mpaka Uganda kupitia Industrial area ya Uganda, Jinja mpaka Z.Viktoria na ndio maana inaitwa Uganda Railway hivyo kuwafanya Waganda waache kutumia Bandari ya Mombasa na kutumia ya kwetu siyo rahisi na kujenga Bandari ya Tanga tu peke yake haitoshi ni lazima pia tujenge Reli mpya ya kuunganisha Tanga na Uganda mpaka Jinja sasa hiyo siyo kazi rahisi kwani hai make economic sense yaani kutumia mabilioni ya Dola za Kimarekani kwa ajili tu ya soko la Uganda? usisahau pia kujenga Bandri mpya Ziwa Victoria n.k sasa uwekezaji wote huu kwa mizigo gani ya gani Uganda inayo import na kuexport?
Import Volume ya Uganda ni kiasi gani mpaka iweze kutufanya kufanya uwekezaji mkubwa kiasi hicho?

Jaribuni kujishuhghulisha kidogo kabla ya kulaumu kila kitu, hauwezi kuwafanya waganda waache kutumia Bandari ya Mombasa na kutumia ya kwetu kwani hakulipi kiuchumi!

Kwa hiyo pale Bagamoyo hiyo bandari inatakiwa kuserve nini cha ziada anbacho hakiwezekani kufanywa na bandari za Mtwara, Dar na Tanga zikiwekwa vema.
 
Hapa tunaongelea Bandari ambayo inasafirisha Mizigo in bulk ya Uganda, kuwafanya Waganda waache kutumia Bandari ya Mombasa badala yake watumie yetu ni kama haiwezekani kwa maana hatuwezi kufanya huwo uwekezaji, elewa viwanda vikubwa Uganda viko Mji wa Jinja na hapo katikati ambapo ndipo Uganda Railway ilikopita ikitokea Mombasa na inakwenda mpaka Ziwa Viktoria ambako pia kuna Bandari inayoshusha mizigo na kusafirishwa kwa meli, sasa ili kuwafanya watumie Bandari yetu nilazima tufanye uwekezaji wote huwo, sasa kwa mizigo ipi ya maana ya ambayo Uganda wanayo?

Barbarosa tatizo lipo iv.bandari ya dar inatumika hadi kwa mizigo ya kaskazin yaani ni kama bandari ya tanga imekufa.vivo ivyo na ya mtwara kwa kusin wanatumia bandari ya dar.sasa matokeo take tunagawana watumiaji wa kaskazin mwa Tanzania Mombasa na dar kitu ambacho ni kosa.kumbuka kaskazin kuna uwekezaji mikubwa tuu na kuna miji mikubwa.na ukiwa arusha bandari ya Mombasa ni karibu kuliko dar na bagamoyo.sasa kwanini tusiendelee kuboresha tanga kwa ajili ya kaskazin mwa Tanzania na mtwara kusin mwa Tanzania? maana faida ni nyingi kuliko hasara.moja umbali mfupi pili garama ya ujenz mpya wa bandari unakuwa hamna.
 
Ukishaanza kuona nchi inaingia mikataba ovyo ovyo ujue chama tawala kimeishiwa pumzi,kila kitu misaada ndo matokeo yake tunaweka nchi rehani,gesi ndo hivo,madini ndo hivo,misitu ndo hivo,baada ya jumapili watupishe bana,
 
ahadi zingine hizi,
bao la mkono,kutakuwa na jina la mgombea ukawa au kila chama na mgombea wake?
CCM Hao ikulu tena
 
It makes a lot of sense.... hawa kabla ya kuita wenzao wapumbafu na malofa walitakiwa wajipime kwanza sababu haihitaji akili za form 4 mwenye division 6 kujua hii kitu !!

Lakini matunda ya bakuli na dili za tembo, sasa hata kesho utasikia tumezindua mradi wa kujenga vyoo ufadhili china !!!
 
Back
Top Bottom