Elections 2015 Lowassa: Tusipopata mabadiliko CCM Wananchi watatafuta nje ya CCM

Ikiwa ni kweli nitarudisha kadi yangu na nitakuwa msitari wa mbele kumkampenia Magufuli.
 
Nimemsikia john mnyika hizo porojo zenu peleka ccm yenu iliyooza
 
Iwapo CDM itampitisha Elowassa huo ndio utakuwa mwisho wake.Na iwapo Mbowe anafanya jambo hilo basi ajue rasmi anajimaliza kisiasa yeye mwenyewe na chama chake.

Kwani ni mara yake ya kwanza? Mbona alikula hela ya Mkono na hamkujua mpaka pale Zitto alipomuumbua. Isitoshe kama mwenye chama baba mkwe kaamua, DJ atafanya nini zaidi ya kukubaliana na matakwa ya baba mkwe?
 
CHADEMA haiwezi kumkaribisha Lowassa hata kuwa mwanachama wa kawaida tu kwani ananuka ufisadi na tabia ya kutaka madaraka kwa mapesa. Huyo aende ACT ndiko watakakoelewana.

Na akienda ACT hawezi kubeba nchi...
Maana kwanza ACT ni chama cha waasi na pia isitoshe kuna watu wapo kule ila ni ukawa
 
Nina hakika Lowasa akienda CDM basi CCM bye bye
 
Sioni taabu ya nini kwa Slaa kukataa wakati Mkakati ni Kushika dola... alikuwa tayari kumchukua Sitta Enzi zile atashindwa nini kumchukua Lowasa mwenye mtaji Mkubwa wa watu wa ndani ya CCM ?

Uchafu wa Lowassa hauvumiliki. CHADEMA itanuka wakimpokea Lowassa. Hata kama Sitta alikuwa na matatizo wakati wakiwa tayari kumpokea hapo mwanzo lakini alikuwa hajanuka kama Lowassa
 
Hizi post ndio zinashusha heshima ya JF.Mods mnaachaje huu puuzi?Upotoshwaji wa.kiwango kikuu.
CC
Moderators
 
Mmmmh!! Haya wacha muvi iendelee... Me nabadilisha mikao tu
 
Uchafu wa Lowassa hauvumiliki. CHADEMA itanuka wakimpokea Lowassa. Hata kama Sitta alikuwa na matatizo wakati wakiwa tayari kumpokea hapo mwanzo lakini alikuwa hajanuka kama Lowassa

Kwa nini asipokelewe we unataka wachaga tuendelee kunyanyaswa nchi yetu sote hii we kama ni muha hama chama nenda kokote kule ----- wewe
 
Hahaha mnanichekesha, watu humu ndani wanakua km wageni wa siasa, usimwamini mwanasiasa hata mara moja, hata akiwa upinzani alafu mmesahau kwenye siasa hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu
 

Uongo mwingine uwd unaupika kulingana na mazingira. Labda nikukumbushe tu kuwa chadema sahiv haiwez kuamua mgombea uraisi kwasababu iko ndan ya ukawa, pili kwa hatua walio fikia hawa ukawa n vigumu kurud nyuma kunza kumjadili lowasa. Labda ungenambia Lowasa kaenda ACT ningefikiria kuamin
 
Huyu jamaa kweli ni mapengo maana anachoandika utadhani ni mtunza siri wa CDM... just saying
 
We we we halafu we dereee! Mbowe achana na mpango wako huo kama ni kweli hili, hata Mrema mwaka 1995 alifanya hivyohivyo kwa chama cha NCCR na NCCR ikafa hadi leo hii imepoteza hadhi. Lowassa na Zitto ni ndugu ya CCM wana masilahi mapana ndani ya CCM kuliko CDM, msije mkafanya kosa la kiufundi kama hili. Naunga mkono Lowassa kujiunga na CDM lakini sio kuwa mgombea urais.
 
Uzi wao huu, hatudanganyiiiiiki, chezea hengine hetu hagumu
 

Rangi ya uzushi huu ni kijani na njano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…