Elections 2015 Lowassa: Tusipopata mabadiliko CCM Wananchi watatafuta nje ya CCM

Elections 2015 Lowassa: Tusipopata mabadiliko CCM Wananchi watatafuta nje ya CCM

Hii taarifa sio ya kuaminika ila kama Chadema wamemkubali Lowasa ni kwa lengo tu la kuipunguza nguvu CCM.

Kama ni kweli CCM haitakua tena ile tunayoijua japo Lowassa naye hatapata Uraisi.

Nakusapot 10000000% kk kiraia!!
 
Last edited by a moderator:
Inabidi Chadema watuambie nini kinataka kutokea ..... hizi habari za Lowasa kwenda Chadema sasa zimeanza kusemwa hata na watu niliokuwa sitegemei kuwa na mawazo kama haya .......

Sasa nimeanza kukumbuka msemo maarufu wa "Chadema tuna matope ya kumpaka Lowasa na tuna sabuni ya kumsafisha" ........
 
hakuna lisilo wezekana chini ya jua, lkn kwa lowasa kujiunga na UKAWA itakuwa amejichimbia kaburi na kujizika mwenyewe.
 
Kama Nilivyokwisha Sema Huko Mwanzo Kuwa Magufuli Atakuwa Ndiyo Chaguo La CCM Kwa Vile Vigezo Nilivyowapeni Sasa Katika Hali Ya Kujiamini Kabisa Nawapeni Taarifa Hii Kuwa Mzee Mtei Amekubali Rasmi Kujitaoa Muhanga Kwa Kumtoa Katika Kinyang'anyiro Dr. Slaa Kuwa Mgombea Wa Urais Kwa Tiketi Ya UKAWA Na Sasa Ni Rasmi Kuwa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa Muda Wowote ANAHAMIA RASMI Kutoka CCM Na Kuhamia CHADEMA Na Hapo Hapo Kupewa Nafasi Ya Kupeperusha Bendera Ya UKAWA Katika Mbio Za Kuelekea IKULU Mwezi October Tarehe 25.

Muda Wowote Kutoka Sasa Walinzi Wake Wakiongozwa Na Bwana Aloyce Tendewa Wanarudi Idarani Kuendelea Na Majukumu Yao Mengine Na Kinachosubiriwa Sasa Upande Wa UKAWA Kumtangaza Ni Kuwa Wanaweka Mambo Sawa Katika Nyanja Zote Na Katika Siku 3 Hizi Lowassa ATATANGAZWA Rasmi Kuwa Ametua CHADEMA Japo Mke Wake Mama Regina Amejitahidi Mno Kumsihi Mumewe Asihame CCM Lakini Lowassa Bado Ana Machungu, Hasira Huku Akishawishiwa Vibaya Na Washauri Wake Wakuu Haswa Haswa Mzee Apson Mwang'onda.

Mliokuwa Mkinidhihaki Kuhusu Magufuli Na Akawa Yeye Sasa Wote Mmepotea Hebu Nidhihikani Na Hili Pia Na Nina Uhakika 100% Wa Hii Breaking News Yangu Kwenu. Lowassa Kuhamia CHADEMA Rasmi Na Kuwa Mpeperusha Bendera Kwa Tiketi Ya UKAWA. Take It From Me! Fumbo Alilolifumba Jana Mbunge James Mbatia Mlilielewa?

Lowassa UMESHAJIPOTEZA Rasmi Kisiasa.


naona CCM hili habari siyo nzuri kwao. Jingine msubirie Lawassa atawaletea Balali.
 
Inabidi Chadema watuambie nini kinataka kutokea ..... hizi habari za Lowasa kwenda Chadema sasa zimeanza kusemwa hata na watu niliokuwa sitegemei kuwa na mawazo kama haya .......

Sasa nimeanza kukumbuka msemo maarufu wa "Chadema tuna matope ya kumpaka Lowasa na tuna sabuni ya kumsafisha" ........

kuiangusha serikali iliyopo madarakani siyo kazi ndogo. Kwenye siasa hakuna rafiki au adui wa kudumu.
 
Fuatilia mchakato wote na utendaji wake mie sijaona sehemu ambayo Lowassa katajwa kama fisadi hata Richmond.

Wakati wa mjadala wa Richmond mlengwa hakuwa Lowassa bali serikali nzima na utendaji mbovu wa Rais wetu Kikwete.

Lakini pia ilionekana kuwa Lowassa aliafanyakazi kiasi cha kufanya Kikwete asijulokane kama yupo na ndiyo kisa cha baadhi kutompenda.

Kujiuzulu kwake kuliendana na uwajibikaji wa kisiasa na kuokoa serikali ya Kikwete isianguke kabisa.

Ni bahati mbaya sana kuwa wasomi, usalama wa Taifa na hata wanasiasa wengi pamoja na Rais wetu Kikwete wanajua hivyo.

Leo mtu aliyewasaidia wamemgeuka na kumuona mbaya hii haiwezi kukubalika.

Hatuwezi kuwa na Taifa la watu waongo na wanafiki na wasiojifunza kusema ukweli kuanzia mdogo hadi mkubwa.

Ni bahati mbaya sana kuwa ukweli kama huu hufanya baadhi yetu ama kwa kutoelewa au kwa makusudi kutuporomoshea matusi.

Namshukuru sana aliyenijibu kuwa mie mjinga just kwa kutoa mawazo yangu.

Wenye akili endeleeni kuutafakari huo ijumbe mtaelewa!!
 
Hivi ule utabiri wa sheikh Yahya Jr wa mgombea wa ccm kuwa na majina mchanganyiko wa kikristo na kiislam umeishia wapi?

Au ndo John Pombe?
 
Lowassa ajiunge na Chadema. Chadema kupitia UKAWA wamkubalie awe mgombea kwa
 
Fuatilia mchakato wote na utendaji wake mie sijaona sehemu ambayo Lowassa katajwa kama fisadi hata Richmond.

Wakati wa mjadala wa Richmond mlengwa hakuwa Lowassa bali serikali nzima na utendaji mbovu wa Rais wetu Kikwete.

Lakini pia ilionekana kuwa Lowassa aliafanyakazi kiasi cha kufanya Kikwete asijulokane kama yupo na ndiyo kisa cha baadhi kutompenda.

Kujiuzulu kwake kuliendana na uwajibikaji wa kisiasa na kuokoa serikali ya Kikwete isianguke kabisa.

Ni bahati mbaya sana kuwa wasomi, usalama wa Taifa na hata wanasiasa wengi pamoja na Rais wetu Kikwete wanajua hivyo.

Leo mtu aliyewasaidia wamemgeuka na kumuona mbaya hii haiwezi kukubalika.

Hatuwezi kuwa na Taifa la watu waongo na wanafiki na wasiojifunza kusema ukweli kuanzia mdogo hadi mkubwa.

Ni bahati mbaya sana kuwa ukweli kama huu hufanya baadhi yetu ama kwa kutoelewa au kwa makusudi kutuporomoshea matusi.

Namshukuru sana aliyenijibu kuwa mie mjinga just kwa kutoa mawazo yangu.

Wenye akili endeleeni kuutafakari huo ijumbe mtaelewa!!

Mkuu ni kweli lowasa aje ukawa atatoboa
 
Inabidi Chadema watuambie nini kinataka kutokea ..... hizi habari za Lowasa kwenda Chadema sasa zimeanza kusemwa hata na watu niliokuwa sitegemei kuwa na mawazo kama haya .......

Sasa nimeanza kukumbuka msemo maarufu wa "Chadema tuna matope ya kumpaka Lowasa na tuna sabuni ya kumsafisha" ........

Kuwa mvumilivu tu!Bado kidogo na Emma atakuja hapa ndo ukubwa huo.
 
Tuwaombe ccm warudie tena mchakato wa kutafuta mgombea wa urais na tuombe wampitishe lowassa kwani ni kipenzi cha baadhi ya wananchi.
 
Cdm walimuorodhesha kwenye list of shame (mafisadi) Leo awe mgombea wao. Kwa hiyo mgombea wa ukawa awe fisadi
 
Back
Top Bottom