Lugha ya makondakta na madereva daladala inatia hasira, abiria tuwe wakali kukemea mmomonyoko wa maadili

Lugha ya makondakta na madereva daladala inatia hasira, abiria tuwe wakali kukemea mmomonyoko wa maadili

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Mwaramutse nshuti,

Mimi sina magari matatu kama ndugu yangu Makamura hivyo hulazimika kutumia usafiri wa umma kama daladala na bajaji kwenda kusaka mkate.

Adha kubwa ambazo nimekuwa nikikutana nazo kwenye usafiri huo ni maneno machafu, yasiyo na staha ya makonda na madereva. Imekuwa kama mtindo kwao, yaani kutamka hadharani maneno yanayohusisha sehemu za siri za kike imekuwa suala la kawaida sana kwao.

Hawajali jinsia, rika, hadhi ya waliopanda kwenye vyombo vyao vya usafiri, wao wanatukana tu bila aibu na kujiona wajanja. Mungu awasamehe.

Kuna siku nipo na kijana wangu ana miaka 7 tumeenda kupanda bajaji. Dereva bajaj kazinguana kidogo na mwenzake kisa abiria, aisee aliporomosha matusi hayo tena akitaja sehemu za siri za kike. Kiustaarabu nikamwambia bro hayo matusi yako naomba usitishe, huoni kuna mtoto? Eeeh si nakageuziwa kibao mimi nikatukanwa mbele ya mwanangu.

Jana mishale ya saa tatu nimekwea daladala ya Segerea, sasa ukishavuka Barakuda kuna foleni matata kutokana na ujenzi unaondelea Segerea Magereza. Dereva kachomekeana na kishandu mmoja, dereva kaanza kuporomosha matusi, sikupendezwa ikabidi kiustaarabu nimuulize, Bro tokea nipande hii gari pale Mwenge wewe ni matusi ya nguoni, hivi huna mama, dada, watoto wa kike? Nikaishia kutukanwa kuwa nina sura mbaya kama uchi wa mwanamke. Abiria wengine wakaishia kucheka. Kiustaarabu nikashuka na kukwea pikipiki nikaendelea na safari.

Hii ni mifano michache kati ya mingi ambayo nimeshuhudia. Hali ni mbaya sana, pamoja na vijana kuvurugwa lakini isiwe sababu ya kuondokewa na utu. Siyo kila mtu anapendezwa na lugha hizo, wengine tunataka kizazi kilichostaharabika.

Murakoze cyane.
 
Mwaramutse nshuti,

Mimi sina magari matatu kama ndugu yangu Makamura hivyo hulazimika kutumia usafiri wa umma kama daladala na bajaji kwenda kusaka mkate.

Adha kubwa ambazo nimekuwa nikikutana nazo kwenye usafiri huo ni maneno machafu, yasiyo na staha ya makonda na madereva. Imekuwa kama mtindo kwao, yaani kutamka hadharani maneno yanayohusisha sehemu za siri za kike imekuwa suala la kawaida sana kwao.

Hawajali jinsia, rika, hadhi ya waliopanda kwenye vyombo vyao vya usafiri, wao wanatukana tu bila aibu na kujiona wajanja. Mungu awasamehe.

Kuna siku nipo na kijana wangu ana miaka 7 tumeenda kupanda bajaji. Dereva bajaj kazinguana kidogo na mwenzake kisa abiria, aisee aliporomosha matusi hayo tena akitaja sehemu za siri za kike. Kiustaarabu nikamwambia bro hayo matusi yako naomba usitishe, huoni kuna mtoto? Eeeh si nakageuziwa kibao mimi nikatukanwa mbele ya mwanangu.

Jana mishale ya saa tatu nimekwea daladala ya Segerea, sasa ukishavuka Barakuda kuna foleni matata kutokana na ujenzi unaondelea Segerea Magereza. Dereva kachomekeana na kishandu mmoja, dereva kaanza kuporomosha matusi, sikupendezwa ikabidi kiustaarabu nimuulize, Bro tokea nipande hii gari pale Mwenge wewe ni matusi ya nguoni, hivi huna mama, dada, watoto wa kike? Nikaishia kutukanwa kuwa nina sura mbaya kama uchi wa mwanamke. Abiria wengine wakaishia kucheka. Kiustaarabu nikashuka na kukwea pikipiki nikaendelea na safari.

Hii ni mifano michache kati ya mingi ambayo nimeshuhudia. Hali ni mbaya sana, pamoja na vijana kuvurugwa lakini isiwe sababu ya kuondokewa na utu. Siyo kila mtu anapendezwa na lugha hizo, wengine tunataka kizazi kilichostaharabika.

Murakoze cyane.
We mwandishi umeshindwa kuandika Makondakta??.
Utakuja kuua watu kwa presha bure.
 
Kutajwa kwa tendo la ngono kama lilivyo na kuzitaja sehemu za siri hadharani siku hizi imekuwa ni kawaida.
 
Daslm iliwahi tokea jamaa alitukanwa akiwa na familia yake matusi kama hayo yule jamaa alishuka akawapeleka familia yake nyumbani akarudi bara barani kumsubiri yule Konda baadae kidogo gari hilo jamaa hakuuliza akamshushia kipondo yule Konda abiria hata walikua hawajui imekuaje jamaa kasimamisha kama abiria baadae anamvuta konda na kumpa kichapo yule Konda alifia pale pale sikufatilia tena kama ile kesi iliishaje ingawaje jamaa alikamatwa kwa kosa la kuua....
Arusha pana konda mmoja ana majibu kama anayo mfukoni kuna siku moja alipigwa ngumi ya uso damu zilichuruzika kama bomba la Serikali baada ya kupigwa alikua mpole kama sio yeye maana aliempiga alimjibu vibaya harafu walikua karibu...
 
Daslm iliwahi tokea jamaa alitukanwa akiwa na familia yake matusi kama hayo yule jamaa alishuka akawapeleka familia yake nyumbani akarudi bara barani kumsubiri yule Konda baadae kidogo gari hilo jamaa hakuuliza akamshushia kipondo yule Konda abiria hata walikua hawajui imekuaje jamaa kasimamisha kama abiria baadae anamvuta konda na kumpa kichapo yule Konda alifia pale pale sikufatilia tena kama ile kesi iliishaje ingawaje jamaa alikamatwa kwa kosa la kuua....
Arusha pana konda mmoja ana majibu kama anayo mfukoni kuna siku moja alipigwa ngumi ya uso damu zilichuruzika kama bomba la Serikali baada ya kupigwa alikua mpole kama sio yeye maana aliempiga alimjibu vibaya harafu walikua karibu...
Hawa jamaa wanakupa fezea mbele za watu, na kama si mbabe unaonekana boya. Kinachouma zaidi abiria wanaona jambo la kawaida.
 
Kutajwa kwa tendo la ngono kama lilivyo na kuzitaja sehemu za siri hadharani siku hizi imekuwa ni kawaida.
Sana aisee, vijana tumekuwa wa ovyo. Huwa najiepusha sana kutumia hayo maneno. Hata nikiwa kitaa na wana, akiwepo mmoja anayetukana ovyo huwa nasepa.
 
Hawa jamaa wanakupa fezea mbele za watu, na kama si mbabe unaonekana boya. Kinachouma zaidi abiria wanaona jambo la kawaida.
Magari ya maji ya Chai wamechapwa sana hawana ujinga huo kama maeneo mengine ya Arusha huko Moshono au kwa Mromboo ni balaa...
 
Tutafute hela
Tutafute Pesa
Tutafute chapaa
Tutafute shilling
Tutafute fedhaa
Tutafute maokoto
 
Makondakta na madereva wa daladala, madereva wa bajaj, bodaboda, hawa watu wana matusi balaa.

Na wanafanya makusudi kukera na kuudhi abiria, wao ndo wanajisikia raha, sasa kunae huyo alijichanganya kwangu, mbona nilimfurahishaaa. Na hatokaa anisahau mbwa yulee.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mtu anae jielewa hawezi kaa asumbuane na konda akili zao kisoda tena uanze kuhangaika nao.
 
Karibuni nimeshuhudia konda kijana ana muharasi kwa kauli za hovyo mdada kisa amevaa gauni fupi!
 
Back
Top Bottom