Pre GE2025 Luhaga Mpina amshtaki Spika Tulia na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuondolewa Bungeni kinyume na Sheria

Pre GE2025 Luhaga Mpina amshtaki Spika Tulia na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuondolewa Bungeni kinyume na Sheria

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mama katoa uhuru. enzi zile hapatoshi
Wananchi hawawezi kuishi kwa kutegemea huruma ya kupewa Uhuru na huyo mama yako, Uhuru wa kweli, Haki na Usawa kwa Wananchi wote unapatikana kutoka kwenye Katiba ya nchi pamoja na Sheria zingine zinazotawala katikà nchi husika. Kamwe, Uhuru au Haki za watu Wala hazipatikani kutokana na huruma ya Rais wa nchi.
 
Mahakama inaweza kutoa hukumu kuhusu uendeshwaji wa mhimili unaojitegemea wa Bunge na Spika?

Hukumu hiyo haitaharibu uhuru wa Bunge kama mhimili unaojitegemea?
Hapana mkuu kwakuwa Bunge lilifuata hatua zote za mchakato wa ndani za kuendesha shauri lake na likafika hadi rufaa kwenye kamati ya bunge basi ni sahihi kufungua kesi ya mapitio mahakamani kwakuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho kutoa haki kwa mujibu wa katiba.

Ndiyo maana kuna Check and Balance ndani ya mihimili mitatu ya serikali. Reasonable interference kutoka muhimili mmoja kwenda mwingine hakuharibu uhuru wa mihimili hii mkuu.
 
Anajisumbua bure tu.

Mwambieni Luhaga Mpina kwamba ajiunge na wa-Tanzania wengine wenye mapenzi mema na nchi hii ambao wanapigania Haki, Demokrasia pamoja na upatikanaji wa Katiba Mpya iliyo nzuri yenye kubeba Maoni, mawazo na fikra za Wananchi walio wengi zaidi kwenye nchi hii.
Suala la upatikanaji wa Katiba Mpya iliyo Bora nchini Tanzania siyo Jambo linalowahusu CHADEMA au Wanasiasa peke yao.
Kosa lake nini sometimes tuache Upumabavu yeye ameona ameonewa kwa hiyo kufutafuta haki ambayo amekosa ndo kujisumbua stupid kabisa
 
Kwa hiyo Spika wa Tanzania yupo juu ya sheria? Anaweza kufanya lolote analotaka kwenye himaya yake na asichukuliwe hatua?
Hili si jambo la Tanzania tu.

Ma Bunge mengi ya Westminster style yana mfumo wa kufuata kitu kinaitwa "separation of powers". Ile mihimili mitatu Judiciary, Legislature and Executive inakuwa inaangaliana kwa mipaka fulani.

Kwa kufuata mipaka hii, Mahakama haina nguvu za kuamua jambo lolote kuhusu Bunge linavyoendeshwa. Muhimili wa Bunge upo chini ya Spika.

Ndiyo maana Mahakama ilishawahi kukataa kusikiliza kesi kwa sababu kesi ilikuwa chini ya muhimili wa Bunge.

Ndiyo maana rais Samia alivyotaka Naibu Waziri wa Mambo ya Nje aondoke kwenye ubunge, nafasi ambayo alimpa yeye mwenyewe rais (mbunge wa kuteuliwa na rais), ilibidi rais amuombe mbunge ajiuzulu ubunge, rais hakuweza kutengua mtu ubunge, hata kama ubunge wenyewe ulikuwa ni wa kuteuliwa na rais.
 
Hapana mkuu kwakuwa Bunge lilifuata hatua zote za mchakato wa ndani za kuendesha shauri lake na likafika hadi rufaa kwenye kamati ya bunge basi ni sahihi kufungua kesi ya mapitio mahakamani kwakuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho kutoa haki kwa mujibu wa katiba.

Ndiyo maana kuna Check and Balance ndani ya mihimili mitatu ya serikali. Reasonable interference kutoka muhimili mmoja kwenda mwingine hakuharibu uhuru wa mihimili hii mkuu.
Je, unakumbuka Uamuzi (Hukumu) ya Mahakama ya Rufani juu ya Kesi ya kuruhusiwa Mgombea Binafsi au Wagombea Binafsi kwenye Chaguzi za Siasa hapa Tanzania ambayo iliwasilishwa na Hayati Mch.Dkt. Christopher Mtikila??? Unakumbuka Mahakama ya Rufani iliamua Nini???
 
Hiyo kesi haina mashiko, proceeding za Bunge zina kinga chini ya sheria na katiba, atapigwa kama ngoma
Hapana mkuu kinga ya bunge ipo ndani ya mambo yanayoongelewa ndani ya bunge na wabunge.

Lakini ukija kwenye suala la kutafuta haki pale mchakato wa ndani wa kibunge utakapokamilika na uamuzi wa mwisho kutolewa na bunge basi hapo mbunge ana haki ya kutafuta haki yake kwenye muhimili wa mahakama ambao ndio wenye final say / decision kwenye utoaji wa haki.

Hapo aliyeshtakiwa ni Spika pamoja na AG na ndio watakaohitajika kwenda kujitetea kwa maamuzi waliyoyatoa ambayo kwa mujibu wa mlalamikaji hayakuwa maamuzi halali.
 
Nchi haipoi. Jana Kinana, leo Mpina. Kesho utashangaa unasikia Gen Z wanaulizana connection.
 
Hiyo kesi imeshaisha, inasubiri hukumu tu. Nawashangaa hao Mawakili wake kwa kushindwa kumshauri mtrja wao.
Kitu pekee cha bunge ambacho Mahakama ina mamlaka ya kusikiliza kama kitapelekwa kwenda kuwa challenged Mahakamani ni sheria zilizotungwa na bunge, lakini maamuzi ya bunge. Bunge hata lingeamua kumnyonga Mpina, hakina chombo ambacho kina legal power ya kuhoji maamuzi yake.
Kwahiyo unataka kusema bunge liko juu zaidi ya katiba ya Jamuhuri hata kama ikitokea ukiukwaji wa katiba
 
Hapana mkuu kwakuwa Bunge lilifuata hatua zote za mchakato wa ndani za kuendesha shauri lake na likafika hadi rufaa kwenye kamati ya bunge basi ni sahihi kufungua kesi ya mapitio mahakamani kwakuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho kutoa haki kwa mujibu wa katiba.

Ndiyo maana kuna Check and Balance ndani ya mihimili mitatu ya serikali. Reasonable interference kutoka muhimili mmoja kwenda mwingine hakuharibu uhuru wa mihimili hii mkuu.
Inawezekana ni sahihi kufungua kesi mahakamani, hilo si swali langu, na wala sijapinga hilo.

Nilichouliza ni kwamba, Mahakama inaweza kusikiliza kesi na kutoa hukumu ya kuhusu shauri la Bunge lilivyojiendesha lenyewe, kwa kuzingatia kuwa Mahakama haitakiwi kuingilia shauri la Bunge linavyojiendesha, kwa sababu kusikiliza na kuhukumu mashauri ya hivyo kutakuwa ni kuingilia uhuru wa Bunge kujiendesha lenyewe?

Huoni kwamba hii kesi itatupiliwa mbali na Mahakama, na Mahakama itasema "Hili ni jambo lenu la Bungeni, mna utaratibu wenu wa kumaliza mashauri yenu ya Bungeni, sisi Mahakama hatutakiwi kuingilia mashauri yenu ya jinsi mnavyoendesha Bunge kwa sababu kufanya hivyo kutaingilia uhuru wa Bunge na kuharibu kanuni za separation of powers"?

Huoni kuwa kesi itatupiliwa mbali kwa mantiki hii?
 
Hili si jambo la Tanzania tu.

Ma Bunge mengi ya Westminster style yana mfumo wa kufuata kitu kinaitwa "separation of powers". Ile mihimili mitatu Judiciary, Legislature and Executive inakuwa inaangaliana kwa mipaka fulani.

Kwa kufuata mipaka hii, Mahakama haina nguvu za kuamua jambo lolote kuhusu Bunge linavyoendeshwa. Muhimili wa Bunge upo chini ya Spika.

Ndiyo maana Mahakama ilishawahi kukataa kusikiliza kesi kwa sababu kesi ilikuwa chini ya muhimili wa Bunge.

Ndiyo maana rais Samia alivyotaka Naibu Waziri wa Mambo ya Nje aondoke kwenye ubunge, nafasi ambayo alimpa yeye mwenyewe rais (mbunge wa kuteuliwa na rais), ilibidi rais amuombe mbunge ajiuzulu ubunge, rais hakuweza kutengua mtu ubunge, hata kama ubunge wenyewe ulikuwa ni wa kuteuliwa na rais.
Kazi ya bunge ni kutunga sheria kazi ya mahakama ni kutafsiri hizo sheria ambazo bunge limezitunga na kwenda mbali zaidi kuangalia kama hazikiuki katika.
Hapo kinacho enda kuangaliwa ni kanuni zilizotumika kumhukumu mpina zimefuatwa hiyo sio kuingilia mhimili.
Ndio maana kuna sheria bunge linaweza kutunga lakini zikapingwa mahakamani
 
Inawezekana ni sahihi kufungua kesi mahakamani, hilo si swali langu, na wala sijapinga hilo.

Nilichouliza ni kwamba, Mahakama inaweza kusikiliza kesi na kutoa hukumu ya kuhusu shauri la Bunge lilivyojiendesha lenyewe, kwa kuzingatia kuwa Mahakama haitakiwi kuingilia shauri la Bunge linavyojiendesha, kwa sababu kusikiliza na kuhukumu mashauri ya hivyo kutakuwa ni kuingilia uhuru wa Bunge kujiendesha lenyewe?

Huoni kwamba hii kesi itatupiliwa mbali na Mahakama, na Mahakama itasema "Hili ni jambo lenu la Bungeni, mna utaratibu wenu wa kumaliza mashauri yenu ya Bungeni, sisi Mahakama hatutakiwi kuingilia mashauri yenu ya jinsi mnavyoendesha Bunge kwa sababu kufanya hivyo kutaingilia uhuru wa Bunge na kuharibu kanuni za separation of powers"?

Huoni kuwa kesi itatupiliwa mbali kwa mantiki hii?
Mahakama kazi yake ni kutoa tafsiri ya sheria, Bunge kutunga sheria na mambo mengine

Hivyo hakuna tatizo hapo... mahakama itaangalia kama taratibu zikifatwa kwa mujibu wa sheria, ndio kazi yake
 
Hili si jambo la Tanzania tu.

Ma Bunge mengi ya Westminster style yana mfumo wa kufuata kitu kinaitwa "separation of powers". Ile mihimili mitatu Judiciary, Legislature and Executive inakuwa inaangaliana kwa mipaka fulani.

Kwa kufuata mipaka hii, Mahakama haina nguvu za kuamua jambo lolote kuhusu Bunge linavyoendeshwa. Muhimili wa Bunge upo chini ya Spika.

Ndiyo maana Mahakama ilishawahi kukataa kusikiliza kesi kwa sababu kesi ilikuwa chini ya muhimili wa Bunge.

Ndiyo maana rais Samia alivyotaka Naibu Waziri wa Mambo ya Nje aondoke kwenye ubunge, nafasi ambayo alimpa yeye mwenyewe rais (mbunge wa kuteuliwa na rais), ilibidi rais amuombe mbunge ajiuzulu ubunge, rais hakuweza kutengua mtu ubunge, hata kama ubunge wenyewe ulikuwa ni wa kuteuliwa na rais.
Na kingine kaenda kumshitaki spika na sio bunge
 
Kesi ya ngedere imepelekwa kwa nyani alafu anategemea kushinda 🙄
 
Kosa lake nini sometimes tuache Upumabavu yeye ameona ameonewa kwa hiyo kufutafuta haki ambayo amekosa ndo kujisumbua stupid kabisa
Hii kesi ni ya kuhusu Bunge linavyojiendesha, Mahakama haiwezi kutoa hukumu kuhusu shauri la uendeshwaji wa Bunge, kwa sababu ya kanuni ya separation of powers.

Mahakama itamuambia Mpina arudishe suala hili Bungeni.
 
Kazi ya bunge ni kutunga sheria kazi ya mahakama ni kutafsiri hizo sheria ambazo bunge limezitunga na kwenda mbali zaidi kuangalia kama hazikiuki katika.
Hapo kinacho enda kuangaliwa ni kanuni zilizotumika kumhukumu mpina zimefuatwa hiyo sio kuingilia mhimili.
Ndio maana kuna sheria bunge linaweza kutunga lakini zikapingwa mahakamani
Hakika mfano ole ngurumo kama sijakosea jina lake ameshinda kesi kuhusu mambo haya ya sheria kinzani zilizotungwa na Bunge
 
Mahakama kazi yake ni kutoa tafsiri ya sheria, Bunge kutunga sheria na mambo mengine

Hivyo hakuna tatizo hapo... mahakama itaangalia kama taratibu zikifatwa kwa mujibu wa sheria, ndio kazi yake
Mahakama haiwezi kutoa hukumu kuhusu suala la uendeshwaji wa Bunge zaidi ya kusema kuwa hili ni suala la Bunge na shauri hilo halitakiwi kusikilizwa na Mahakama, lirudishwe Bungeni.

Kwa sababu kati ya Mahakama na Bunge kuna seoaration of powers.

Mahakama haimwambii Spika jinsi gani ya kuendesha Bunge, na Spika/ Bubge hailiambii Mahakama jinsi gani ya kutafsiri sheria.
 
Wameshindwa kesi kabla haijaanza.

Wakili wa kwanza anasema "Wanashitaki viwanda vya sukari kupata hasara" wakati anayeshitaki hana kiwanda cha sukari.

halafu wakati huohuo kesi ya boiashara unaofanya ya kikatiba.

Ujuha huo.

Hawa wanaisumbuwa mahakama, walipe ghatrama za kesi na wawalipe wanaowachafuwa majina.,3

Kesi hii itaishia Mpina kufilisiwa siyo tu na aliowashitaki bali na wenye viwanda pia.

Hivi Mwenye kiwanda kipi cha sukari Tanzania anauwezo wa kusimama na kuipinga serikali?

Huyo wa kwanza, macho yake yameanza kulia kabla hajalizwa.
 
Mawakili wa Luhaga Mpina wanazungumza na waandishi wa habari muda huu.

Pamoja na nambo mengine, mawakili hao wamesema mojawapo ya kesi zilizofunguliwa ni ile anayomshtaki Spika wa Bunge na Mwanasheria mkuu wa Serikali kwa kunyang'anywa na kunyimwa haki ya kuwakilisha wananchi wa kisesa na watanzania wote kwa vikao 15 Bungeni ambapo msingi wa kesi yake anaamini ameonewa kwa kuondolewa kinyume cha Sheria.

Aidha, Mpina anaamini hatua za kuchukuliwa dhidi yake zilikuwa zimepangwa hata kabla ya yeye kusikilizwa.

Hadi sasa, zaidi ya Mawakili 100 wamejitolea kumsaidia Mpina kwenye kesi hii.

Pia soma

Safi sana mpina pigania haki utashinda!
 
Back
Top Bottom