Pre GE2025 Luhaga Mpina amshtaki Spika Tulia na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuondolewa Bungeni kinyume na Sheria

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wasi wasi wangu huyu Ngosha watu wa usalama wanaweza kumfanya kitu kibaya sawa na Dr Ulimboka miaka ile ya awamu ya nne.

Ni kama ana chuki dhidi ya SSH ni kama haamini kuwa JPM hayupo tena pale ikulu.
 
Upuuzi umejaa Tanzania hii.
 
Wasi wasi wangu huyu Ngosha watu wa usalama wanaweza kumfanya kitu kibaya sawa na Dr Ulimboka miaka ile ya awamu ya nne.

Ni kama ana chuki dhidi ya SSH ni kama haamini kuwa JPM hayupo tena pale ikulu.
Ni kweli wanaweza kumfanya hivo, ila wajue ipo sehemu tunaelekea, na kwa kufanya hivyo watakuwa wanatusogeza kwa mwendo wa kasi bila ghasi.
 
Ni kweli wanaweza kumfanya hivo, ila wajue ipo sehemu tunaelekea, na kwa kufanya hivyo watakuwa wanatusogeza kwa mwendo wa kasi bila ghasi.
Aliposhughulikiwa yule Dr nini kilifanyika?. Serikali inafanya mengi sana na yanagusa moja kwa moja maisha ya mtu mmoja mmoja.

Uwe na hoja ya kina kuweza kushawishi umma unaotatuliwa matatizo yao kila kukicha.

Uelewa pia ni tatizo la kitaifa, Mpina alipinga sana uwekezaji pale bandarini kwa hoja ndefu akiwa haelewi kwa uhakika nini kinakwenda kufanywa.
 
Kesi ya Mpina ni kuhusu nini?

Kanuni na sheria za Bunge zinapokiukwa hilo ni jambo la Bunge, mwenye mamlaka ya kuzitafsiri ni muhimili wa Bunge, si Mahakama. Mahakama inatafsiri sheria za nchi, si kanuni za Bunge.

Mawakili wanaweza kujazana hata 1,000 kuonesha solidarity na Mpina kwamba kaonewa, au hata kula hela za Mpina, au hata kusikia Mahakama itasemaje, wakijua kwamba kesi haina mashiko Mahakamani na itakataliwa.

Na kwa mawakiki wetu hawa wengine siwezi jushangaa hata wakiamininkwamba wana kesi wanayoweza kushinda, tuangalie mahakama itasemaje.

Mimi natabiri kuwa, kwenye hoja yoyote ya kumshtaki Spika kwa jinsi alivyoliendesha Bunge, mahakama itatupilia mbali shauri hilo, kwa kisema haiwezi kuingilia suala la Spika anavyoendesha Bunge, hilo ni suala la kumalizwa Bungeni.

Hizi kesi nyingine ni za kisiasa za kujenga sympathy kwenye public opinion kuliko kutafuta ushindi Mahakamani.
 
Mkuu kumbuka mchakato wote wa ndani ya Bunge ulishafanyika kwahiyo kwa mujibu wa katiba yetu chombo pekee chenye uwezo wa kutoa haki na chenye uamuzi wa mwisho ni mahakama.

Kwamba Bunge linaweza kumtimua mbunge yeyote na mbunge huyo akaishia kukaa benchi kisa tu ya doctrine of separation of power?

Mahakama yenyewe itakachozingatia ni kwamba all procedures zilifuatwa wakati wa mchakato wa kumsimamisha mbunge ikiwemo 'natural justice' ambayo ni haki ya kusikilizwa kikamilifu.

Sioni kama mahakama itatupilia mbali shauri hili kwa kufanya hivyo manake imeacha jukumu lake la kikatiba la kutoa haki pasipo kujali haki hiyo imevunjwa na nani ama na muhimili gani.
 
HUYU JAMAA ANASHINDA KESI WAPENDWA

MWABUKUSI PART TWO

NIKOKWA WAKALA
 
Haya ndiyo mambo tunatakiwa kubwa busy nayo na story za Simba na Yanga
 
Kwahiyo More than ya mawakili 100 , hawajui Sheria linapokuja suala la Bunge?.

Ila wee chiembe ndio unajua ?

Toa upuuzi wako.
Idadi sio issue, hata wewe nyumbani kwako unaweza kuwa na mbuzi au kondoo 10000, lakini hawawezi kukutisha, hizo kesi zinasaidia academics tu, hakuna namna mahakama itaingilia Bunge
 
Mfano Rais yupo muhimili wa Executive ambapo mwajiriwa aliyefukuzwa kazi na mwajiri wake anaweza kuanzia ngazi za usuluhishi kama CMA akakata rufaa hadi kwa Rais akitka arejeshwe kazini lakini Rais anaweza kushikilia msimamo wa mtu huyo kutorejeshwa kazini.

Mtu huyo akienda mahakamani (Labour division) kudai haki yake ya kurejeshwa kazini haina maana kwamba mahakama itakataa kusikiliza shauri lake kisa tu muhimili mwingine ulishamfukuza kazi.

Shauri litasikilizwa na kama mtu huyo ana haki basi atarejeshwa kazini.

Rejea mamlaka ya kuteua ambayo yapo vested to the President.
Rais anaweza kumteua mtu yeyote kushika madaraka ya ofisi yoyote ya umma lakini kama kuna ukiukwaji uliofanyika kwenye zoezi zima la uteuzi labda mtu huyo kukosa sifa fulani basi mtu yeyote anaweza kwenda mahakamani kupinga uteuzi huo.

Rejea kesi ya Addo Shaibu dhidi ya Rais Magufuli na mwanasheria mkuu wa serikali ambapo Addo Shaibu alipinga uteuzi wa Adelardus Kilangi kuteuliwa kuwa mwanasheria mkuu wa serikali.
 
Idadi sio issue, hata wewe nyumbani kwako unaweza kuwa na mbuzi au kondoo 10000, lakini hawawezi kukutisha, hizo kesi zinasaidia academics tu, hakuna namna mahakama itaingilia Bunge
Kwa nini Watanzania wengi inaonekana hawaelewi hii point ya msingi kabisa?

Hivi watu wetu hawajui basic separation of powers hivi?
 
Mahakama zenyewe zinasikilizia Rais ameamkaje siku hiyo hizo nazo ni Mahakama?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…