Luhaga Mpina, mmoja wa Wana CCM waliochukizwa Samia kuwa Rais, awaita Mawaziri awamu ya 6 matapeli

Tujifunze kukubaliana na mawazo ya wengine hiyo ndio Demikrasia.

Haiwezekani Nchi nzima tukawaza na kupenda jambo moja.

Lazima tofauti iwepo.

Sasa nyie watoto wa mjini mnashangaza sana mnapoogopa kukosolewa na kukimbilia kudai eti mnachukiwa.
Afadhali umeliona hili hata sisi wakati wa marehemu ndio masuala kama haya tulikua tunayapigania lakini bahati mbaya sana wewe nawe ulikua hukubali ule utawala ukosolewe. Nadhani umepata funzo kubwa bwana Stroke
 
Nafkiri kutoa tuhuma kwa Luhaga kuhusu hilo si sawa, yeye ameleta hoja kuwa taratibu za kotoa tozo hiyo zilikiukwa navni kinyume na sheria,kwani bajeti ya serikali ikishapitishwa huruhusiwi kupunguza au kuongeza mapato bila idhini ya bunge.sasa ilitakiwa wizara ijibu je walifuata taratibu? na huo ndio uwajibikaji kwa wananchi maana bunge ni wananchi.Na hilo kwamba utaratibu ulikosewa si Mama mwenyewe ndio alisema tena kwa kufoka na kuamuru irejeshwe maana bunge ndio lilipitisha. Hivyo ushauri ni kuwa hoja ijibiwe kwa hoja tusitafute huruma nyingine zisizohusika.
 

kuna kukosoa, kutoa maoni na ushauri na kuna nongwa..... Hizo namna mbili mtu anakuwa huru nyakati zote kusema na kukosoa ila hapo kwenye NONGWA ni mhusika kusema na kukosoa baada ya kukosa maslahi fulani au kutokuwa sehemu ya wanufaikaji...

Kuna mahala Luhaga tulitegemea kama yuko huru kiakili aweze kusema lakini hakusema ila alisifia lakini wakati yeye anasifia wapo waliokosoa kwa vitu vilivyoonekana kabisa..Ila yeye alikakaa kimya kwa maana ya alikuwa mnufaika....kwangu naamini hana Moral authority ya kutoa comment....Ila watu wenye moral authority ya kutoa coment maana kwa nyakati zote panapoharibika wanasema.....mfano hapo juu umempa kubwa bwana Stroke....kwa kukaa kimya nyakati fulani japo yalikuwepo ya kuongea..
 
Ukweli upi? Wewe tuambie basi ukweli unaoufahamu.
 
Huyu atakuwa ni Sukuma Gang, mbona kakazia sana la umeme!? Ana chuki binafsi na February
 
Duh kazi ipo wengine wanamponda makamba na wengine mpina.Wanatwangana wao kwa wao
 
Kushambulia!!??
ama kuhoji
 
fiiisiiiiiemuuuuu woyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee, mbere kwa mbereeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Mkiambiwaga ukweli mnajificha kwenye kivuli cha Rais mbona mnashindwa kujisimamia nyie mapopoma ya ccm?
 
Acha uzwazwa wewe, Samia ashughulike naye kivipi? amuue au unamaanisha nini? Huyo Samia wenu kwani hakosolewi yeye nani?
 
Sifia kwanza.. "anaupiga mwing"
 
Nani mwenye uwezo wa kuwashughulikia masalia wa mwendazake? Zaidi mtawatoa tu kimya kimya kwenye mfumo, kama mlivyofanya kwa Dr. Bashiru Ali, Polepole, nk.

Ila kuwashughulikia direct, hamuwezi.
Wewe unaijua siasa ya Tz, ulichokisema ni ukweli mtupu.
 
Acha watu waongee, ata Samia alisema waachwe watoe ya moyoni. Sasa wewe unaye zuia tukueleweje?
Wanakimbilia kwa mama kama watoto yatima mara wanaposhindwa kujibu hoja zao!! Jibuni mapigo kama wanaume mtabebwa mpaka lini? Mwisho mbeleko itapasuka.
Msitegemee kusifiwa pale mnapokosea halafu mnajitia eti ooh hawa hawakupenda Samia awe Rais!! Huko ni kujitetea kipuuzi.
 
Tabia ya mtu kutoa maoni, halafu mtu anashughulikiwa, nailaani sana, na walaaniwe wanaoshawishi, na alaaniwe atakaetekelza, lincha ya wengi kumuunga mkono mama, akianza kushughulikia watu bila kujali, sitampenda kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…