Luhaga Mpina: Wanaomsifia Rais Samia ndio hao wanaoongoza kwa kumhujumu na kufanya uovu

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina amesema wanaomsifia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ndio hao wanaoongoza kwa kumhujumu na kufanya uovu.

Mpina ametoa kauli hiyo wakati akiwa ziarani jimboni humo ambapo amebaini ubadhirifu wa fedha za miradi ya ujenzi wa shule ambazo hazionekani kutekeleza miradi, huku kukiwa na udanganyifu katika uidhinishaji wa malipo pamoja na kumsajili mkandarasi hewa, ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ndiye anayedaiwa kuhusika katika hayo.

"Huyu mtu kama ni kukamatwa akamatwe atumie mafungu yake alipe hizi fedha za umma jumla ya shilingi milioni 402 ziletwe."

"Huyu Mama Rais wetu Samia Suluhu Hassan watu wanapenda tu kusema maneno, Rais wetu tunampenda, nani kama Samia huku wanamhujumu usiku na mchana, fedha zinaliwa halafu aliyekula hizo fedha ndio wa kwanza kufanya makongamano eti ya kumpongeza Rais na kumwombea ili kuficha uovu, akizungumza neno moja 'Mama Samia' utadhani ni mwema mno, hawa akina Mpina wanaosema wanageuzwa wao ndio maadui wa Rais," amesema Mpina.

Your browser is not able to display this video.
 
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina amesema wanaomsifia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ndio hao wanaoongoza kwa kumhujumu na kufanya uovu.

Mpina ametoa kauli hiyo wakati akiwa ziarani jimboni humo ambapo amebaini ubadhirifu wa fedha za miradi ya ujenzi wa shule ambazo hazionekani kutekeleza miradi, huku kukiwa na udanganyifu katika uidhinishaji wa malipo pamoja na kumsajili mkandarasi hewa, ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ndiye anayedaiwa kuhusika katika hayo.

"Huyu mtu kama ni kukamatwa akamatwe atumie mafungu yake alipe hizi fedha za umma jumla ya shilingi milioni 402 ziletwe."

"Huyu Mama Rais wetu Samia Suluhu Hassan watu wanapenda tu kusema maneno, Rais wetu tunampenda, nani kama Samia huku wanamhujumu usiku na mchana, fedha zinaliwa halafu aliyekula hizo fedha ndio wa kwanza kufanya makongamano eti ya kumpongeza Rais na kumwombea ili kuficha uovu, akizungumza neno moja 'Mama Samia' utadhani ni mwema mno, hawa akina Mpina wanaosema wanageuzwa wao ndio maadui wa Rais," amesema Mpina.
Your browser is not able to display this video.
 
Kina nani hao au anajihami? Ulitaka wamtukane?
 
Kumbe jamaa yangu unauma na kupuliza
Mbona hawataki hao waliokula Fedha za umma?

Anajikosha tuu hana lolote.

Wanaomsigia Rais wanaonesha hela alizotoa na kioichofanyika Sasa kama yeye ameona hela zimeliwa sehemu ndio awataje Ili nae amsifie Rais Kwa utaratibu huo.
 
Kwa uchache niongezee ninao wafahamu,Tlaatlah,Chiembe,Chocevariable,Hata akina Jo ninamashaka?
 
Mbona hawataki hao waliokula Fedha za umma?

Anajikosha tuu hana lolote.

Wanaomsigia Rais wanaonesha hela alizotoa na kioichofanyika Sasa kama yeye ameona hela zimeliwa sehemu ndio awataje Ili nae amsifie Rais Kwa utaratibu huo.
Nasikia mama anatoa 100 Kisha mnatumia 20 then 80 mnaweka mfukoni mnapiga makofi then mnasema mitano tena kwa mama
 
Nasikia mama anatoa 100 Kisha mnatumia 20 then 80 mnaweka mfukoni mnapiga makofi then mnasema mitano tena kwa mama
Umesahau rukhsa ya "kuleni kwa urefu wa kamba" speech?
 
Mbona hawataki hao waliokula Fedha za umma?

Anajikosha tuu hana lolote.

Wanaomsigia Rais wanaonesha hela alizotoa na kioichofanyika Sasa kama yeye ameona hela zimeliwa sehemu ndio awataje Ili nae amsifie Rais Kwa utaratibu huo.
Waliokula fedha ni Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Meatu, kamtaja mbona?
 
Jamaa kasema ukweli tupu
 
Mbona hawataki hao waliokula Fedha za umma?

Anajikosha tuu hana lolote.

Wanaomsigia Rais wanaonesha hela alizotoa na kioichofanyika Sasa kama yeye ameona hela zimeliwa sehemu ndio awataje Ili nae amsifie Rais Kwa utaratibu huo.
Kweli wewe jamaa punguani kweli amemtaja mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya meatu , au uchawa umehamisha ufikiri wako kutoka kichwani kwenda makalioni ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…