Luhanga Mpina apewa siku 10 na Spika kuleta ushahidi wa Bashe kulidanganya Bunge

Luhanga Mpina apewa siku 10 na Spika kuleta ushahidi wa Bashe kulidanganya Bunge

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
luhaga-mpinaa-jpg.3017557

Pichani ni Luhaga Mpina
Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson amempa siku 10 Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwasilisha uthibitisho kwamba Waziri wa Kilimo, Hussen Bashe amelidanganya Bunge.

Dk Tulia ametoa maelekezo hayo wakati akiahirisha Bunge leo Jumanne ya Juni 4, 2024 baada ya mbunge huyo kudai, “Waziri Bashe amesema uongo na amevunja sheria.”

Wakati wa mabishano ya hoja kati ya Bashe na Mpina kuhusu uingizaji wa sukari ya nje, Dk Ackson amemuliza Mpina kwa kutumia kanuni ya 70 kwamba ana hakika waziri anasema uongo. Mpina amejibu “anasema uongo na kuvunja sheria.”

Kufuatia hali hiyo amesema kwa mujibu wa kanuni ya Bunge ya 70 anayesema mbunge au waziri amesema uongo ndiye anatakiwa kuleta uthibitisho.

“Naomba ieleweke siyo kwamba namuweka Mpina kwenye kona,” amesema Spika. Mpina anatakiwa kuwasilisha ushahidi wake Juni 14, 2024.

Hoja iliyosababisha Mpina kutakiwa kuwasilisha uthibitisho inahusu kiwango cha uagizaji wa sukari ya ziada nje ya nchi katika kipindi ambacho viwanda vinakuwa vimesimamisha uzalishaji.

Mpina amedai kwa mujibu wa sheria uagizaji wa sukari nje ya nchi kwa ajili ya kuziba pengo unatakiwa uwe takriban tani 150, 000 na zabuni itangazwe.

UPDATES
 
Hata kabla ya kuleta ushahidi, ujumbe wa Mpina umeshafika.

Mhe. Mpina siku zote analia na upigaji kwenye vibali vya uagizaji commodities, anamwambia waziri fuata utaratibu unaopangwa na Bodi ya Sukari, sio utashi wako.

Leo Waziri Bashe kakiri kwamba ni kweli uagizaji sukari haunaga zabuni.


Kwa hiyo Waziri anaweza akajiamulia akampigia simu let's say Pascal Mayalla akamwambia Mayalla jiandae nakuletea kibali cha kuagiza sukari. Jiandae means kama huna hela kachukue mkopo kwa kutumia kibali hiki, hela lazima irudi, nchi nzima itakula sukari yako wewe miezi sita, bei utapanga wewe, business plan ya biashara ni takwimu za commodity deficit za bodi ya sukari, nani atakunyima mkopo?

Ila cha juu lazima urudishe kwa Waziri. Ndio mchoro wa Quid Pro Quo corruption ya uagizaji sukari.
 
Hata iweje, Luhaga Mpina amekwisha jipambanua kuwa yeye ni tofauti na wabunge wengine ndani ya CCM.

Lililobaki ni kwa wananchi kutambuautofauti kati yake na wabunge wengine wa CCM, na kumpa shukrani anazozistahili.
 
Analeta na hawaufatilii
Pale pale Bashe alimjibu Spika kwamba NFRA haitakiwi kuagiza sukari. Na alimsaidia spika kwa kusema Mpina yuko sahihi, kwamba NFRA walibadili kanuni ili wadanganyika tusikose sukari.

Lakini ni kwamba Luhaga Mpina yuko sahihi, na hatohitajika kupeleka ushahidi kwasababu Bashe aliisha kiri kwa Spika kwamba Mpina yuko sahihi, wao NFRA ndio walipindisha/kubadilisha kanuni.

Kwa sababu ili sukari iagizwe yani Gape Sugar lazima bodi ya sukari itoe mapendekezo, na wao walitoa mapendekezo ya tani laki 120, yeye Base alisema laki 4.
 
Kapeleka ushahidi mara nyingi sana, na kapelekwa kwenye kamati ya maadili mara nyingi na anawashinda.
Sio kweli, alidai Trillion 30 zilifanyiwa ufisadi wakati bajeti ni Trillion 40+. Akaulizwa kivipi 70% ya bajeti iliwe na mishahara ilipwe? Niambie unathibitishaje uongo kama huu?

Aliambiwa athibitishe tu kuhusu kupuuzwa kwa katazo la Waziri Mkuu kukamata ngombe za wafugaji!! Ila eti masuala ya data hajawahi itwa? Coz angeumbuka tu
 
Ngosha habaatishi, na anatambua kwamba wanamtafuta wamuweke "kwenye kona" kama maiki ilivyo jikosha..teh😜
Yule mpotoshaji sana ni wajinga tu msiojua mambo ndio mnamshabikia. Mfano alisema miamala shuku pekee ni Trillion 120 kwa mwaka, kwamba Tanzania ina miamala zaidi ya Trillion 1000 kwa mwaka? Jamaa ni kilaza tu sema amewadaka vilaz
 
Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson amempa siku 10 Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwasilisha uthibitisho kwamba Waziri wa Kilimo, Hussen Bashe amelidanganya Bunge...
Waziri Bashe pia atueleze hao wenye viwanda waliopata vibali vya kuagiza sukari nje, wakakaidi kuagiza na wananchi kuendelea kuteseka, aliwachukulia hatua gani za kisheria na hiyo ndiyo point kuliko hizo blah blah za kumsakama Mpina.

Maana kipande cha hotuba yake nimeiangalia You Tube, naona ni sifa tu na majingambo mengii wakati raia tushasota sana na 'deficit' ya sukari wakati uwezo wa kuzuia hayo yasitokee alikuwa nao!

Maisha ya raia wa Tz kwa sasa hayana mtetezi yeyote, awe Rais ama Waziri, hakuna.

Tukisema wanakula na matajiri tutakuwa tunakosea?
 
Acha uongo, mbona alishindwa thibitisha kivipi Trillion 30 zimefisadiwa kwa mujibu wa ripoti ya CAG
Muongo wewe, na sijui unatoa wapi taarifa zako, njoo bungeni upate ukweli. Kinachoongelewa hapa ni hoja ya NFRA na Sugar Gape kama ilivyo wasilishwa na Bashe.

Na Mpina alivyo mpinga Bashe alijibu pale pale akamwambia Spika kwamba Mpina yuko sahihi, NFRA ndio walibadilisha kanuni, lakini Bodi ya sukari ndiyo iliyokuwa inatoa mapendekezo ya kisi cha kununua nje siyo NFRA.

Wewe umetoka kilabuni sijui unadakia tu kisa umeona jina la Mpina na humpendi.
 
Back
Top Bottom