Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

Dingswayo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
4,019
Reaction score
2,925
attachment.php

Dodoma/Dar. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.

Alisema hayo jana katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Katika hotuba yake, Lukuvi aliwaeleza waumini waliofurika katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu wa kanisa hilo katika jimbo kuwa waendelee kuliombea Bunge lifanye uamuzi sahihi wa serikali mbili.

Aliwataka Watanzania kuipuuza Rasimu ya Katiba katika suala la Muungano na Serikali tatu kwa madai kuwa kutaka kuwapo mfumo huo ni kutaka Watanzania waingie vitani.

"Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena, angalieni nchi ya Korea Kusini na Korea Kaskazini ambao waligawanyika na sasa ni maadui wakubwa wanaokaa mipakani wamenyoosheana bunduki," alisema na kuongeza:

"Waumini ndugu zangu wapendwa, kwa sasa tupo katika hali mbaya sana hapo bungeni, tunaomba mtuombee kuna watu ambao wanataka madaraka kwa nguvu na wameanza kutafuta jinsi ya kuvunja Muungano na kudai kuwapo kwa Serikali tatu, nawaomba sana wapuuzeni wale wote ambao wanataka serikali tatu."

Alisema watu wa aina hiyo wanaonekana kuwa wana huruma na Watanzania na wanadai kuwapo kwa Serikali ya Tanganyika wakati hiyo Tanganyika wanayoidai ni jina tu ambalo Wajerumani walikaa mezani wakabuni na kutuletea.

Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.

Alisema wanaopiga kelele wana ajenda za siri na nia yao kutaka kufanya fujo na kusababisha machafuko... "Kwani ukiwa na mke mmoja akakushinda unafikiri utatuzi ni kuoa mke mwingine?"

Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.

"Unajua jeshi haliwezi kukaa na bunduki bila fedha. Hiyo Serikali ya tatu ambayo jeshi litakuwa chini yake haina vyanzo vya mapato vya kueleweka, sasa hao wanajeshi watalipwa nini? Wenye mitutu watakubali kuishi bila fedha?"

Alisema hata vyanzo vya mapato ambavyo vimeandikwa katika Rasimu ya Katiba ni lazima visimamiwe na pande mbili za Muungano, akiwa na maana ya Tanganyika na Zanzibar na kwamba kama upande mmoja ukishindwa kuchangia hali itakuwa mbaya.

"Kama tunataka serikali ya tatu ni lazima tuhakikishe kuwa inakuwa na vyanzo vya uhakika vya mapato. Jambo hili siyo ubishi wala ushindani ni suala la kujenga hoja na kujadili kwa kina, ni ngumu sana katika utekelezaji wake," alisema.

Rais Kikwete wakati akizindua Bunge la Katiba mjini Dodoma aligusia suala hilo ambalo Lukuvi alilieleza katika ibada hiyo.

Kwa upande wake, Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano.

Alisema angetamani kumshauri Rais alivunje Bunge la Katiba kutokana na Bunge hilo kukosa mwelekeo na kukosa adabu.

Alipotakiwa kufafanua baadaye kuhusu kauli ya Lukuvi, askofu huyo alisema kuwa Waziri huyo hakutakiwa kutoa kauli nyepesi kama ile ukizingatia yeye ni mtu aliyepo madarakani.

"Kauli ya Lukuvi ilikuwa nyepesi sana kuzungumzia kwamba nchi itaingia kwenye vita. Ilitakiwa aende mbele zaidi kama mtu mwenye madaraka kwa kufafanua zaidi," alisema.

"Mimi nataka serikali mbili kwa sababu tumeshazoea kusali chini ya miti tukiwa na amani na tukiwa na serikali tatu tutasali kwa mtutu. Kama umeshindwa kuwatunza wanawake wawili ulionao je, huyo wa tatu ambaye humjui tabia yake utamtunzaje?" alisema.


CHanzo:Mwananchi


Na Nuzulack Dausen, Mwanachi
Jumatano,Aprili16 2014
Kwa ufupi


"Rais Kikwete naye alikuwa mwanajeshi, sasa kuna ubaya gani kama mwanajeshi akitawala nchi. Kuna ubaya gani mwanajeshi mwenye akili akitawala nchi yetu. Mbona Komba (Kapteni John Komba), aliwahi kuwa mwanajeshi na sasa ni Mbunge wa Mbinga Magharibi. Jeshi ni la wananchi na hao wanajeshi wanaowasema wengine huwa tunakutana nao klabu za muziki."

Baadhi ya wasomi wasema Waziri Lukuvi hakustahili kutoa kauli hiyo katika eneo la ibada. Dar es Salaam. Siku chache baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi kudai kuwa iwapo mfumo wa serikali tatu utapita, jeshi litachukua nchi, wanazuoni wametafsiri kauli hiyo kuwa ni ya kuwajengea hofu wananchi.
Jumapili Lukuvi, akiwa katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alikokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, alisema muundo huo utasababisha nchi kutawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano haitakuwa na fedha za kulipa mishahara wanajeshi.

Lakini mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Mohammed Bakari amesema kauli hiyo ilitolewa katika jukwaa lisilo sahihi hususan kwa kiongozi kama Lukuvi.

"Kila kauli ina mahala pake. Haikutakiwa kwa mtu mwenye madaraka kama yule kuzungumzia mambo nyeti kama hayo kanisani," alisema Dk Bakari.
"Licha ya kwamba kauli yake si mpya ilishasemwa na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete, lakini ilibidi ayaseme hayo ndani ya vikao vyao na si kanisani."

Alisema pamoja na kwamba kiongozi huyo alitoa maoni yake binafsi, ilitakiwa aangalie kwanza kauli yake kabla ya kuitoa. "Unapokuwa na nafasi ya juu ya uongozi, uhuru wako wa kutoa maoni binafsi unapungua. Kwa hiyo kupitia nafasi hiyo itabidi uzingatie masuala ya kuzungumza ukiwa raia, pia kiongozi," alisema.

Mwanasheria Harold Sungusia alisema watu wanaodai serikali mbili wamepungukiwa na hoja na ndiyo maana wanaanzisha masuala mengine yasiyo na tija. "Nimepitia sheria zote nikagundua kuwa mtu anayetetea hoja ya serikali mbili anakosa hoja za msingi ukizingatia tayari muundo huo wa Muungano umedumu kwa miaka 50."
Hata hivyo, mhadhiri wa Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema Watanzania hawatakiwi kuacha kufuata hoja za msingi na kutishika na propaganda. "Hizo ni propaganda kwa sababu hakuna utafiti uliofanywa na kugundua kuwa serikali tatu zitaleta vurugu."

Mkazi wa Mbagala Mtongani, Isaiah Solomon alisema alichosema Lukuvi kinaweza kuwatisha raia hususan wale walio na uelewa mdogo juu ya masuala ya siasa.

"Si jambo jema kusemea mambo hayo kanisani. Pia alizungumzia kuhusu kugharimia jeshi, sifikiri kama ni wanajeshi pekee wanaoweza kuleta madhara iwapo fedha za kuwalipa zikiwa pungufu; wapo wafanyakazi wengine watakaoleta balaa," alisema Solomon.

Mwenyekiti wa chama cha UDP Mkoa wa Dar es Salaam, Joackim Mwakitinga alisema woga wa wanasiasa wanaotaka serikali mbili ndiyo unaofanya watoe kauli za kuogofya wananchi.

"Naona ni woga tu wa wanasiasa wanaotaka kuleta mambo ambayo hayapo katika hoja za muundo wa Muungano," alisema. Mjumbe wa Bunge la Katiba, Joseph Mbilinyi alisema kauli hiyo inadhihirisha jinsi wanaopigia debe serikali mbili walivyo waongo.

Akichangia mjadala bungeni jana, Mbilinyi alisema: "Rais Kikwete naye alikuwa mwanajeshi, sasa kuna ubaya gani kama mwanajeshi akitawala nchi. Kuna ubaya gani mwanajeshi mwenye akili akitawala nchi yetu.

Mbona Komba (Kapteni John Komba), aliwahi kuwa mwanajeshi na sasa ni mbunge wa Mbinga Magharibi. Jeshi ni la wananchi na hao wanajeshi wanaowasema wengine huwa tunakutana nao klabu za muziki."

Chanzo Mwananchi
 

Attachments

  • lukuvi.png
    lukuvi.png
    169 KB · Views: 13,248
Hahahahaha, this propaganda is too cheap. David Kafulila amewaambia mbinu hii haifai tena wao bado wanaing'ang'ania. Basi kama wanaona serikali tatu haifai kwa sababu hizo, kwanini wasipigie upatu serikali moja? Tanganyika yetu ipo wapi angali Zanzibar ipo na ina mamlaka yake kamili kama nchi?
 
Lukuvi analinda kibarua chake kwa neno lolote.

HUWEZI kuongea upuuzi kama Lukuvi hapo kenya ukiwa na dhamana ya ofisi ya serikali na bado ukaachwa madarakani
 
JWTZ ni jeshi la wananchi wa Tanzania hivyo lipo pale kulinda maslahi ya wananchi ambao wao ndio wanaowalipa mishahara. Kama hivi sasa mishahara yao inapatikana kwanini isipatikane tukiwa na serikali TATU? Ikumbukwe kwamba matumizi ya serikali ya muungano yatatokana na bajeti itakayopitishwa na bunge lake likiwa na vyanzo mahususi vya mapato!! Luluvi na wote wanaotumia propaganda ya kuwatisha wananchi kuwa jeshi litachukua/pindua serikali iwapo kutakuwepo serikali TATU wajue kuwa wanawatukana wanajeshi wetu kuwa hawajui wajibu wao na vitendo hivi vya wakina Lukuvi ni vya kihaini!!!
 
Hata hivyo mbona hata hivi sasa Jeshi ndilo linatuongoza? Maana viongozi wajuu wengi waliopo CCM walishakuwa Jeshini tena kwa vyeo vya juu. Mfano: Coln.(rtd) Kikwete J.K., Coln. (rtd) Kinana etc. Vilevile wakuu wa mikoa na wailaya walioteuliwa na mh. Rais, wengi walikuwa wanajeshi wa vyeo vya juu pia.

Propaganda hii inatutia mashaka na kuona ya kuwa, watawala wetu hawa wanataka waje waipindue nchi na kuitawala kijeshi pindi wananchi watakapopitisha kura za maoni za kudai serikali tatu? Watafute hoja nyingine zenye mshiko na siyo kututishia nyau kama walivyozoea.
 
[h=2]If you do not tell the truth about yourself you cannot tell it about other people.[/h]
The smallest minority on earth is the individual. Those who deny individual rights cannot claim to be defenders of minorities.

Tanganyika+Zanzibar​
 
Zaidi ya jwtz sioni nani atahakikisha tanzania inabaki kuwa nchi moja. Wanayofanya kule bungeni ni uhaini. Wanaiua tanzania hivi hivi.
 
kama ana busara basi angesema ili tuwe na umoja amani na mshikamano wa kweli,basi tuwe na nchi moja na serikali moja!
 
Hata hivyo mbona hata hivi sasa Jeshi ndilo linatuongoza? Maana viongozi wajuu wengi waliopo CCM walishakuwa Jeshini tena kwa vyeo vya juu. Mfano: Coln.(rtd) Kikwete J.K., Coln. (rtd) Kinana etc. Vilevile wakuu wa mikoa na wailaya walioteuliwa na mh. Rais, wengi walikuwa wanajeshi wa vyeo vya juu pia.

Propaganda hii inatutia mashaka na kuona ya kuwa, watawala wetu hawa wanataka waje waipindue nchi na kuitawala kijeshi pindi wananchi watakapopitisha kura za maoni za kudai serikali tatu? Watafute hoja nyingine zenye mshiko na siyo kututishia nyau kama walivyozoea.
Asante kwa mfano wako mkuu
 
Hivi ni Lukuvi yupi huyu anayeongelewa? au ni yule aliyenyang'anya mke wa mtu kule Mpwapwa?
 
Hivi kauli kama ya Lukuvi haitoshi kufunguliwa kesi ya uhaini (treason)? Watu kama hawa hawafai hata kupewa uongozi kwenye serikali ya mitaa, na leo ndio wamo kwenye serikali hii dhaifu ya JK. Lakini acha waendelee kuropoka, tunakaribia kuuona mwisho wao. Labda wahame nchi!
 
Zaidi ya jwtz sioni nani atahakikisha tanzania inabaki kuwa nchi moja. Wanayofanya kule bungeni ni uhaini. Wanaiua tanzania hivi hivi.
Hawa ndio waandishi wetu Tanzania, tunataka serikali tatu na si kuvunja muungano.

By the way kuvunja muungano ni uhaini? ni nini maana ya referundum?
 
Alisema wanaopiga kelele wana ajenda za siri na nia yao kutaka kufanya fujo na kusababisha machafuko... "Kwani ukiwa na mke mmoja akakushinda unafikiri utatuzi ni kuoa mke mwingine?"

Hivi hii kauli kuwa ukiwa na sijui mke mmoja ama wake wawili inatumiwa sana na watawala ndani ya CCM wakati wanazungumzia masuala ya muungano. Ni vyema wakaweka wazi kwenye huo muungano nani mume na mke ni yupi kati ya TANGANYIKA na ZANZIBAR vinginevyo huu ni upotoshaji na zaidi utakuwa ni udhalilishaji wa nchi hizi mbili zinazounda muungano uliojaa utata.
 
ni lazima atafutwe mkuu wa jeshi athibitishe hili, kama kweli wananchi wakiamua serikali 3 watafanya mapinuzi ya kijeshi
 
Nadhani hamjamuelewa Lukuvi. Anachosema ni kwamba serikali ya CCM wameshaamua kama serikali 3 zitapita basi wao (wakubwa wa CCM) watafanya mapinduzi ya kijeshi.

Na hii inadhihirisha hoja ya siku nyingi kuwa chanzo cha machafuko kwenye nchi nyingi hasa nchi za kiafrika na viongozi walioko madarakani.

"Huwezi kuandika Katiba mpya kama huna crisis" WAKO.
 
1. Hivi huyu Lukuvi huwa anaongea vitu gani huyu? Hivi huwa anafiria Kweli?

2. Nimependa hiyo......Mkuu wa Majeshi aje atoe ufafanuzi hapa. Waandishi mfateni Mwamunyange muelezeeni anatuhumiwa kupindua nchi.

ni lazima atafutwe mkuu wa jeshi athibitishe hili, kama kweli wananchi wakiamua serikali 3 watafanya mapinuzi ya kijeshi
 
Huyu kilaza kweli kwani hata kwa mfumo wa sasa jeshi likiamua kutwaa utawala wa nchi litashindwa?
 
Huwezi kujua kama ni shibe iliyopitiliza au ni upofu! Waziri kutoa kauli kama hii huku akijua wazi Rasimu iliyotengenezwa na tume iliyoundwa na bosi wake JK ndio imekuja na maoni ya wananchi yanayosema 'serikali tatu'!
Lililo wazi ni kuwa kuendelea materially na kifikra kwa nchi hii kutachukua muda.
 
Back
Top Bottom