Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

Bora tuishi chini ya utawala wa jeshi kuliko huu wa ccm
 
JWTZ ni jeshi la wananchi wa Tanzania hivyo lipo pale kulinda maslahi ya wananchi ambao wao ndio wanaowalipa mishahara. Kama hivi sasa mishahara yao inapatikana kwanini isipatikane tukiwa na serikali TATU? Ikumbukwe kwamba matumizi ya serikali ya muungano yatatokana na bajeti itakayopitishwa na bunge lake likiwa na vyanzo mahususi vya mapato!! Luluvi na wote wanaotumia propaganda ya kuwatisha wananchi kuwa jeshi litachukua/pindua serikali iwapo kutakuwepo serikali TATU wajue kuwa wanawatukana wanajeshi wetu kuwa hawajui wajibu wao na vitendo hivi vya wakina Lukuvi ni vya kihaini!!!

Serikali haiwezi kupinduliwa kwa sababu ya kuwa na serikali TATU bali serikali inaweza kuchukuliwa na wananjeshi kama mtaendeleza tabia yenu nyie magamba ya kuwarithisha uongozi watoto wenu ambao tunajua ni mburula!!
 
JWTZ ni jeshi la wananchi wa Tanzania hivyo lipo pale kulinda maslahi ya wananchi ambao wao ndio wanaowalipa mishahara. Kama hivi sasa mishahara yao inapatikana kwanini isipatikane tukiwa na serikali TATU? Ikumbukwe kwamba matumizi ya serikali ya muungano yatatokana na bajeti itakayopitishwa na bunge lake likiwa na vyanzo mahususi vya mapato!! Luluvi na wote wanaotumia propaganda ya kuwatisha wananchi kuwa jeshi litachukua/pindua serikali iwapo kutakuwepo serikali TATU wajue kuwa wanawatukana wanajeshi wetu kuwa hawajui wajibu wao na vitendo hivi vya wakina Lukuvi ni vya kihaini!!!


Well said Mkuu! Hasa hapo kwenye red. Na ingekuwa kwenye nchi ambayo kila chombo cha serikali kinawajibika independently Mkuu wa majeshi angetoa tamko kupinga kauli hiyo kwani inawadhalilisha wanajeshi.
 
hee? mwa lukuvi mdesi hela! Anza kwanza kwa huu muungano kisheria ni famba! Uhalalisheni kwanza, halafu muone kama bila Tanganyika mtafanikiwa!
 
lukuvi.jpg

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi.PICHA|MAKTABA

Na Habel Chidawali na Fidelis Butahe, Mwananchi

Jumatatu,Aprili14 2014 saa 9:37 AM


Kwa ufupi

Ataka Watanzania kuwaombea ili serikali mbili zipite.



Dodoma/Dar. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.



Alisema hayo jana katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.



Katika hotuba yake, Lukuvi aliwaeleza waumini waliofurika katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu wa kanisa hilo katika jimbo kuwa waendelee kuliombea Bunge lifanye uamuzi sahihi wa serikali mbili.

Aliwataka Watanzania kuipuuza Rasimu ya Katiba katika suala la Muungano na Serikali tatu kwa madai kuwa kutaka kuwapo mfumo huo ni kutaka Watanzania waingie vitani.



“Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena, angalieni nchi ya Korea Kusini na Korea Kaskazini ambao waligawanyika na sasa ni maadui wakubwa wanaokaa mipakani wamenyoosheana bunduki,” alisema na kuongeza:



“Waumini ndugu zangu wapendwa, kwa sasa tupo katika hali mbaya sana hapo bungeni, tunaomba mtuombee kuna watu ambao wanataka madaraka kwa nguvu na wameanza kutafuta jinsi ya kuvunja Muungano na kudai kuwapo kwa Serikali tatu, nawaomba sana wapuuzeni wale wote ambao wanataka serikali tatu.”



Alisema watu wa aina hiyo wanaonekana kuwa wana huruma na Watanzania na wanadai kuwapo kwa Serikali ya Tanganyika wakati hiyo Tanganyika wanayoidai ni jina tu ambalo Wajerumani walikaa mezani wakabuni na kutuletea.

Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.



Alisema wanaopiga kelele wana ajenda za siri na nia yao kutaka kufanya fujo na kusababisha machafuko... “Kwani ukiwa na mke mmoja akakushinda unafikiri utatuzi ni kuoa mke mwingine?”

Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.



“Unajua jeshi haliwezi kukaa na bunduki bila fedha. Hiyo Serikali ya tatu ambayo jeshi litakuwa chini yake haina vyanzo vya mapato vya kueleweka, sasa hao wanajeshi watalipwa nini? Wenye mitutu watakubali kuishi bila fedha?”

Alisema hata vyanzo vya mapato ambavyo vimeandikwa katika Rasimu ya Katiba ni lazima visimamiwe na pande mbili za Muungano, akiwa na maana ya Tanganyika na Zanzibar na kwamba kama upande mmoja ukishindwa kuchangia hali itakuwa mbaya.


“Kama tunataka serikali ya tatu ni lazima tuhakikishe kuwa inakuwa na vyanzo vya uhakika vya mapato. Jambo hili siyo ubishi wala ushindani ni suala la kujenga hoja na kujadili kwa kina, ni ngumu sana katika utekelezaji wake,” alisema.

Rais Kikwete wakati akizindua Bunge la Katiba mjini Dodoma aligusia suala hilo ambalo Lukuvi alilieleza katika ibada hiyo.



Kwa upande wake, Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano.

Alisema angetamani kumshauri Rais alivunje Bunge la Katiba kutokana na Bunge hilo kukosa mwelekeo na kukosa adabu.



Alipotakiwa kufafanua baadaye kuhusu kauli ya Lukuvi, askofu huyo alisema kuwa Waziri huyo hakutakiwa kutoa kauli nyepesi kama ile ukizingatia yeye ni mtu aliyepo madarakani.

“Kauli ya Lukuvi ilikuwa nyepesi sana kuzungumzia kwamba nchi itaingia kwenye vita. Ilitakiwa aende mbele zaidi kama mtu mwenye madaraka kwa kufafanua zaidi,” alisema.



“Mimi nataka serikali mbili kwa sababu tumeshazoea kusali chini ya miti tukiwa na amani na tukiwa na serikali tatu tutasali kwa mtutu. Kama umeshindwa kuwatunza wanawake wawili ulionao je, huyo wa tatu ambaye humjui tabia yake utamtunzaje?” alisema.




Chanzo Mwananchi
 
Bora tutawaliwe na jeshi kuliko utawala huu usio na direction yoyote.
 
They have lost the argumet, now it is time to sell fear, hoja ya mishahara ni ya kijinga kwanj jeshi lilopo sasa ndio hilo hilo litakuwa la.muungano. That's lame argument has already been debunked long time ago.,huyu amekuwa waziri miaka mingi lakini angalieni uwezo wake WA kujenga hoja ulivyo mdogo sasa hawa ndio unategemea amshauri nini rais. Ccm Kweli wameishiwa
 
Najiuliza mara nyingi, hivi ukiwa ccm lazima uwe na mawazo mgando? Halafu hilo la ZANZIBAR kuwa nchi ya kiislam kwani wakiamua hivyo tatizo nini?WATATUSUMBUA VIPI? NA JE, HUO SI UDINI KUZUNGUMZA MAMBO YA WAISLAM KANISANI?
 
  • Thanks
Reactions: prs
Hilo litawezekanaje wakati CCM na manabii wao wa uwongo walishasema na kutabiri watatawala daima au ndo wameamua kufanya utawala wa nchi hii uwe wa mseto na jeshi?Lukuvi alimsikiliza m/kiti wake na kaja na kauli za saluni za wanawake bila kutafakari asemalo!
 
Du, hii ni kauli ya kiuwendawazimu kabisa kuwahi kutolewa na kiongozi wa serikali. This guy must be lunatic!
 
Poor Lukuvi. Shule kwake ndio tatizo. Ni Tanzania tu waziri kamaliza darasa la saba. Unaweza kuona hata ujengaji wa hoja. Alafu tutegemee tija toka kwa maganda ya ndizi haya!
 
lukuvi.jpg

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi.PICHA|MAKTABA

Na Habel Chidawali na Fidelis Butahe, Mwananchi

Jumatatu,Aprili14 2014 saa 9:37 AM


Kwa ufupi

Ataka Watanzania kuwaombea ili serikali mbili zipite.



Dodoma/Dar. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.



Alisema hayo jana katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.



Katika hotuba yake, Lukuvi aliwaeleza waumini waliofurika katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu wa kanisa hilo katika jimbo kuwa waendelee kuliombea Bunge lifanye uamuzi sahihi wa serikali mbili.

Aliwataka Watanzania kuipuuza Rasimu ya Katiba katika suala la Muungano na Serikali tatu kwa madai kuwa kutaka kuwapo mfumo huo ni kutaka Watanzania waingie vitani.



"Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena, angalieni nchi ya Korea Kusini na Korea Kaskazini ambao waligawanyika na sasa ni maadui wakubwa wanaokaa mipakani wamenyoosheana bunduki," alisema na kuongeza:



"Waumini ndugu zangu wapendwa, kwa sasa tupo katika hali mbaya sana hapo bungeni, tunaomba mtuombee kuna watu ambao wanataka madaraka kwa nguvu na wameanza kutafuta jinsi ya kuvunja Muungano na kudai kuwapo kwa Serikali tatu, nawaomba sana wapuuzeni wale wote ambao wanataka serikali tatu."



Alisema watu wa aina hiyo wanaonekana kuwa wana huruma na Watanzania na wanadai kuwapo kwa Serikali ya Tanganyika wakati hiyo Tanganyika wanayoidai ni jina tu ambalo Wajerumani walikaa mezani wakabuni na kutuletea.

Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.



Alisema wanaopiga kelele wana ajenda za siri na nia yao kutaka kufanya fujo na kusababisha machafuko... "Kwani ukiwa na mke mmoja akakushinda unafikiri utatuzi ni kuoa mke mwingine?"

Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.



"Unajua jeshi haliwezi kukaa na bunduki bila fedha. Hiyo Serikali ya tatu ambayo jeshi litakuwa chini yake haina vyanzo vya mapato vya kueleweka, sasa hao wanajeshi watalipwa nini? Wenye mitutu watakubali kuishi bila fedha?"

Alisema hata vyanzo vya mapato ambavyo vimeandikwa katika Rasimu ya Katiba ni lazima visimamiwe na pande mbili za Muungano, akiwa na maana ya Tanganyika na Zanzibar na kwamba kama upande mmoja ukishindwa kuchangia hali itakuwa mbaya.


"Kama tunataka serikali ya tatu ni lazima tuhakikishe kuwa inakuwa na vyanzo vya uhakika vya mapato. Jambo hili siyo ubishi wala ushindani ni suala la kujenga hoja na kujadili kwa kina, ni ngumu sana katika utekelezaji wake," alisema.

Rais Kikwete wakati akizindua Bunge la Katiba mjini Dodoma aligusia suala hilo ambalo Lukuvi alilieleza katika ibada hiyo.



Kwa upande wake, Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano.

Alisema angetamani kumshauri Rais alivunje Bunge la Katiba kutokana na Bunge hilo kukosa mwelekeo na kukosa adabu.



Alipotakiwa kufafanua baadaye kuhusu kauli ya Lukuvi, askofu huyo alisema kuwa Waziri huyo hakutakiwa kutoa kauli nyepesi kama ile ukizingatia yeye ni mtu aliyepo madarakani.

"Kauli ya Lukuvi ilikuwa nyepesi sana kuzungumzia kwamba nchi itaingia kwenye vita. Ilitakiwa aende mbele zaidi kama mtu mwenye madaraka kwa kufafanua zaidi," alisema.



"Mimi nataka serikali mbili kwa sababu tumeshazoea kusali chini ya miti tukiwa na amani na tukiwa na serikali tatu tutasali kwa mtutu. Kama umeshindwa kuwatunza wanawake wawili ulionao je, huyo wa tatu ambaye humjui tabia yake utamtunzaje?" alisema.




Chanzo Mwananchi

Shame on him. Amekosa maono. Nchi itatawaliwa na jeshi kama wanachi watasema itawaliwe na jeshi. Hii siyo nchi ya jeshi. Ni ya watanzania wote. Na wote kwa umoja wao wana haki ya kuamua hatima yao.

Kudai Serikali ya muungano itashindwa kuwalipa mishara wanajeshi ni kukosa akili za kawaida za kufikiri, na ni kukosa aibu. Kwani kuna hela ngapi zinapotelea mifukono mwao kila siku na hawaonekani kukerwa? Ni ngapi zimepota kwenye misamaha ya kodi isiyostahili, ngapi kwenye mikataba hewa na ngapi kwenye mikataba mibovu?

Nani kasema tunahitaji serikali kubwa kama ya sasa yenye ufanisi mbovu? nani kasema kuna haja ya kuwa na Mkuu wa wilaya, mkurugenzi wa wilaya na Katibu mtendaji hapohapo? Nani kasema kuna haja ya kusafiri kila uchao na msururu wa viongozi wakati mambo hayo yanaweza kuamuliwa hata na mabalozi?

Nadhani kunatatizo kubwa la kuendekeza njaa na hivyo tunalazimika kujipendekeza kwa waliotupa nafasi. Kwa mwanasiasa mkongwe kama yeye, na kwa mtu mzima wa umri wake ni aibu kuwa na mawazo finyu kiasi hicho, ni aibu kupeleka siasa kanisani na ni aibu kuwatisha na kuwadanganya wananchi!
 
Huyu ni zaidi ya klaza wa zama hizi kwani akili umkichwa ni haba hana jipya huyu na hata walio mwalika wana lao jambo.
 
Wasaliti wakubwa wa nchi yetu tanganyika ni wabunge wa ccm kutoka tanzania bara, lukuvi pia yumo katika kundi hilo! Hivi anaposema watanzania waombe mungu serikali mbili zipite, kwani kwa sasa zilizopo ni serikali ngapi? Kweli nimeamini, waliozoea kuishi kwa uwongo hawawezi kujifunza katika kweli!
 
Back
Top Bottom