Lulu akubali kukaa jela, awaambia ndugu zake wasikate rufaa kilichotokea ni mipango ya Mungu

Lulu akubali kukaa jela, awaambia ndugu zake wasikate rufaa kilichotokea ni mipango ya Mungu

sheria ifuate mkondo.. asipewe upendeleo kwa kua ni mtu maarufu kwa hapa Tanzania kuna huo upuuzi, huko majuu celebrities wakubwa i.e Tyson wamekaa magerezani.. sheria ufuate mkondo kama huko majuu
 
Kwa hiyo Mungu alipanga yeye amuue Kanumba,aende jela? Huyo Mungu au taahira.

Ndio maana wengine tunasema Mungu au anaeitwa mungu hayupo. Kama ujinga wote unaotokea duniani ni mipango yake basi huyo atakua taahira.

[emoji28] ^.... kanumba afe ili Lulu aende jela^
 
Ni chizi tu anaeweza kukata rufaa kwa hukumu hiyo, kwani hukumu hiyi ni kama amesamehewa tu.
 
Hujamuelewa, na ni kweli pia mtu kwenda jela ni mapenzi ya Shetani,, sasa Mungu gani anayemshauri mja wake kuua?
Kwani kaua au kaua bila kukusudia?
Unaweza kuwa unamuadhibu mwanao ukamchapa kofi akafa.
Lengo halikuwa kumuua lakini umeua bila kukusudia.
Unaweza mtu mkawa mnabishana ukamsukuma akaanguka, umeua bila kukusudia kwa maneno mengine umeua kwa bahati mbaya tu sawa na kupasua kikombe.
Mungu uwa anafanya tupitie magumu kutupima imani yetu na kutupa mafunzo..
 
Sisi wengine tumekaa jela miaka sita kwenye shule za boarding za serikali! Tukila ugali wa dona na maharge yasiyo na ushirikiano ila mwisho wa siku tulitoka. Tulifanya kazi ngumu ikiwa ni pamoja na kusoma vitabu vigumu vya mzungu kwa lugha isiyoeleweka eti wanaiita kiingereza. Hakuna marefu yasiyo na ncha. Cha muhimu awe strong, miaka miwili sio mingi kivilie!
Alafu kuna watu wako Jela Miaka 8 bila kusomewa hukumu yaooo

Ova
 
Na akirudi atakuwa huru kwelikweli tutamkoma
 
Kashakutana na wajanja jela wamemwambia mvua 2 sio Inshu dogo. Utasumbiliwa kukata rufaa mwaka mzima. Mwisho wa siku miaka 2 inapita unawekwa tena ndani miaka minne. Segedance mbona kiroho safi tu. Pale ni kazi za usafi, kuchota maji then saa kumi na mbili kulala. Week end wakina muna wanampelekea mikuku anakula weeee, akitoka full kunenepa tu.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Angeshauliana na wakili wake kwanza hapo akitoka atabaki na criminal rekodi mbaya. Mbeleni ataijutia hio rekodi hasa akitaka fanya kazi nchi za watu
Wabongo wanachukulia simple simple atakua haendi ulaya
 
Aache ujinga Mungu ndiyo apeleke watu wake jela..?? Tena akome kumsingizia huyo Mungu uzinzi ulioletelezea haya asijue ni kazi na mpango wa shetani eti lawama apelekewe Mungu, mshahara wa dhambi ni mauti na mateso km jela avumilie asitafute huruma ya kijinga.
 
Aache ujinga Mungu ndiyo apeleke watu wake jela..?? Tena akome kumsingizia huyo Mungu uzinzi ulioletelezea haya asijue ni kazi na mpango wa shetani eti lawama apelekewe Mungu, mshahara wa dhambi ni mauti na mateso km jela avumilie asitafute huruma ya kijinga.
Kama wewe ni mkristo kasome habari za Yusufu, jinsi Mungu alivyoruhusu akae jela kule misri!!
So, mwache Lulu aseme huo mpango wa Mungu, haina madhara
 
Kama wewe ni mkristo kasome habari za Yusufu, jinsi Mungu alivyoruhusu akae jela kule misri!!
So, mwache Lulu aseme huo mpango wa Mungu, haina madhara
Ajaribiwi wewe, maandiko yanasema Mungu hamjaribu mtu bali tamaa miili yetu, Mungu hajawahi kumpa mtu jaribu kubwa la kumshinda uwezo wake mtu.
 
ndugu umefikiria sana aisee, yaani boarding za miaka hiyo daah, kazi ngumu, ukija kwenye kula harage lina funza na kama halina funza unakula harage kama unakula karanga, ukija dona limejaa funza na nyuzi nyuzi, aisee yale yalikuwa ni mateso kwa kweli, asubuhi kuamshana mchakamchaka, we acha tu

Jela mbali shule mbali. Mimi hata JKT nilikuwa najongo vijijini na kula maviazi ya kuchoma. Sasa jela utajongo wapi?
 
Sisi wengine tumekaa jela miaka sita kwenye shule za boarding za serikali! Tukila ugali wa dona na maharge yasiyo na ushirikiano ila mwisho wa siku tulitoka. Tulifanya kazi ngumu ikiwa ni pamoja na kusoma vitabu vigumu vya mzungu kwa lugha isiyoeleweka eti wanaiita kiingereza. Hakuna marefu yasiyo na ncha. Cha muhimu awe strong, miaka miwili sio mingi kivilie!

Kunakautofauti mkuu wewe kila miezi sita ulienda nyumbali likizo ya mwezi mmoja lakini yeye huko hana poo....wala likizo
 
Ajaribiwi wewe, maandiko yanasema Mungu hamjaribu mtu bali tamaa miili yetu, Mungu hajawahi kumpa mtu jaribu kubwa la kumshinda uwezo wake mtu.
Sasa yeye limemshinda wapi? Wakati kasema kakubari akakar jera.
Lingemshinda angejiua
 
Mwenyenzi Mungu Mkuu..ndie aliyemtuma akafanye ngono bado mdogo..aende Night club bado mdogo..mwambieni achaa upumbavu mkubwa wakumshirikisha Mwenyenzi Mungu na uchafu wake

Kamsome sauli wa kwenye biblia alikuwa mtenda dhambi asie na kifani kuua yeye kila kitu yeye..Lkn Mungu alimbadlisha akawa mtumishi mkubwa na akabadl Jina akaitwa Paulo.Hata Huyu yaliotokea Ni mipango ya Mungu Mungu ana namna ya kuongoza na kuwaokoa Watu unajuaje yasingemkuta Haya Labda angeendelea Kuwa Na Tabia mbovu?? Msijitie wakamilifu Bhana wote Tuna makosa
 
Back
Top Bottom