Sasa ni dhahiri kwamba hali ya wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya urais hadi udiwani ni ngumu. Inasemekana huyu ni mgombea ubunge wa CCM jimbo la Lushoto Mjini Bosnia amekataliwa wazi wazi bila chenga na wakazi wa jimbo lake.
======
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shabani Shekilindi "Boznia", juzi alilazimika kukatisha mkutano wake wa kampeni katika Kijiji cha Makanya, Kata ya Makanya tarafa ya Mlola baada ya wananchi Kukataa asifanye mkutano.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Katibu Wa CCM wilaya ya Lushoto, Ramadhani Mahanyu, zinasema tukio hilo limetokea Jumanne wiki hii katika kijiji cha Makanya wilayani humo.
"Nikweli hilo tukio, limetokea na tumekaa kujadili tumeona ni wahuni waliopangwa na baadhi ya wapinzani wetu, lakini hali ilikuwa nzuri baadaye tulifanya mkutano na wananchi wanetuelewa, " alisema.
Boznia ni Mbunge ambaye alichaguliwa mwaka 2015 na kwenye kinyang'anyiro cha kura za maoni aliwashinda watu mbalimbali akiwemo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Henry Shekifu na Profesa Vincent Kihiyo.
======
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shabani Shekilindi "Boznia", juzi alilazimika kukatisha mkutano wake wa kampeni katika Kijiji cha Makanya, Kata ya Makanya tarafa ya Mlola baada ya wananchi Kukataa asifanye mkutano.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Katibu Wa CCM wilaya ya Lushoto, Ramadhani Mahanyu, zinasema tukio hilo limetokea Jumanne wiki hii katika kijiji cha Makanya wilayani humo.
"Nikweli hilo tukio, limetokea na tumekaa kujadili tumeona ni wahuni waliopangwa na baadhi ya wapinzani wetu, lakini hali ilikuwa nzuri baadaye tulifanya mkutano na wananchi wanetuelewa, " alisema.
Boznia ni Mbunge ambaye alichaguliwa mwaka 2015 na kwenye kinyang'anyiro cha kura za maoni aliwashinda watu mbalimbali akiwemo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Henry Shekifu na Profesa Vincent Kihiyo.