Lusinde amvaa Amunike kweupe

Tukiwafunga waganda mwakani haya maneno ya Lusinde yatapoteza maana. Hili ndilo tatizo la Tanzania, kila mtu anajua kila kitu.

Madhara yake mambo yanaharibiwa tena kijinga tu. Vita haijaisha, halafu akumbuke kuwa ile kadi ya pili aliyopewa Samatta haoa Dar imetibua uchezaji mzima wa timu.
 
Lusinde ana utalaam gani ktk soka?..huko jimboni kwake kuna timu gani ya soka aliyoiongoza ikawa hata bingwa wa mkoa?

Wakati tunamfunga cape verde hapa taifa mbona hawakusema kocha afukuzwe
Huo ndio ujinga wa halaiki ambao ni ugonjwa mwingine ambao mtanzania wa kawaida anauugua. Kujua kila kinachoongelewa hata kama ni masuala ya kitaalam.

Hans Poppe alimkandia kocha mmoja kutoka Serbia. Yule kocha akajibu mapigo kwa kumwambia kuwa yeye katumia miaka zaidi ya 10 akiisoma mpira na mifumo yake, hivyo hastahili kubishana na Poppe.

Aina hii ya ujuaji ndio ambayo inazisumbua vilabu vyetu.
 
hatuna soccer academy hata moja halafu unategemea miujiza kwenye soka
hivi tuna mpira gani hadi tuwafunge lesotho kwao!!!
acheni bange
...una uhakika ? Maana Alliance pekee ni sports academy, na mpaka imepanda Premier
 
Huyu kweli kibajaji jina hili linasadifu akili yake ilivyo
 
W
Walipo shinda na cape Verde last game mbn hakutoa ushauri huo?au hakuangalia Mpira?
 
Hata mimi sioni sababu ya kucheza na Uganda Kocha huyu akiwa bado yupo...
 
1. Hiki ni kichekesho, Lusinde badala ya kupambana na TFF inayosababisha soka letu kushuka kwa kujikita katika mambo ya kijinga na kuacha Mambo muhimu yeye anamsakama Amunike. Mfano hai kwa ujinga wa TFF ni hiki kituko cha kupambana ili Manji asiwepo Yanga bila kujali tunahitaji kuwekeza nguvu kwenye Timu ya Taifa.

2. Kitu kingine huyu Lusinde atuambie Serikali imewekeza nini ili kuhakikisha timu inafanya vizuri? au anafikiri zile Mil. 50 ndio kigezo cha timu kushinda? ebu tumweleze Lusinde Samatta kule Genk anapokea 83,000,000/= kwa mwezi.huku wenyewe wanatoa 50,000,000/= eti ili timu ishinde.
 
Huyo zero brain anafikiri kila Kitu nikuropka tu kama Mjengoni Lazima kocha aachwe afanye Kazi kwa uhuru na Aache kuwavunja moyo wachezaji wetu
 
Lusinde kageuka "Mtaalamu Wa Soka" zaidi ya Amunike tangu lini mpaka awe na jeuri ya kutaka kumfukuza?
 
Shida siyo kocha tu hata wachezaji wetu hawajitambui kabisa
 
Nadhani Matokeo ya Jumamosi ya kule Uganda yalimchangacha Kocha Amunike.Pangepatikana paparazi wajanja wakawahoji wachezaji kuhusu mpango wa kocha (game plan) watakuambia mpango wa kocha kabla ya Jumamosi jioni kocha Amunike alikuwa na mpango tofauti kabla ya kupata matokeo ya kule Uganda.Nadhani kama kocha alibadili Game plan Jumamosi usiku YAMKINI basi hata huo mpango mpya walioutumia walikuwa hawajaufanyia mazoezi kikamilifu au hata wachezaji husika yamkini walikuwa hawajaandaliwa.[Haya ni mawazo yangu na niko tayari kukosolewa]. Ahsante
 
...una uhakika ? Maana Alliance pekee ni sports academy, na mpaka imepanda Premier
point yangu ni simple,timu ya taifa inaandaliwa tokea chini/tokea wadogo
sisi tunaokoteza watu wazima ambao wametoka mchangani na kusajiliwa na simba au yanga
 
Jeshi likabidhiwe Timu ikiwezekana kocha awe mwanajeshi mwenye cheo kikubwa. Au timu ikabidhiwe CCM ili tuwe tuashīnda bila kupingwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…