Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,892
- 16,476
Luteni Kanali Vladimir Putin: Afisa muandamizi wa KGB Ujerumani Mashariki na mfadhili wa makundi ya kigaidi Middle East (PFLP, Hezbollah, Hamas)
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.
Ndugu zangu watanzania;
Mnaweza mkaanza kwa kuusoma kwanza uzi huu>>> Patrice Lumumba University of Russia: Ngome kuu ya majasusi wa KGB ya kufunza itikadi za Ujamaa kwa wanafunzi kutoka nchi masikini za Dunia ya Tatu
P.F.L.P NA KIONGZI WAO YASSER ARAFAT
====
Wakati comrade Yasser Arafat alipotembelea Moscow mnamo mwaka wa 1968, Moscow ilianza kumuona kama vile ni mtu wao, na mwaka uliofuata Arafat akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa PLO (Palestinian Liberation Organisation). Mahusiano imara baina ya Soviets na watu wa Palestine ndio yakawa yameanzishwa.
Mpaka kufikia mwaka wa 1970, baada ya Soviets kupoteza ushawishi wake kwa Misri, mahusiano na wanamgambo wa kipalestina ulikuwa umeimarishwa zaidi na kuanzia hapo silaha pamoja na mafunzo ya kijeshi kutoka Soviet vilianza kupelekwa kwa makundi hayo ya wapalestine.
Ukweli ni kwamba, KGB ndio waliokuwa wanaamua kundi lipi linapaswa kupokea msaada wa kifedha pamoja na silaha na mpaka kufikia mwaka 1972 Soviets walikuwa wametamka ya kwamba harakati za wapalestina ni nguzo muhimu sana katika ukombozi wa waarab wote pale mashariki ya kati. Ilipofika majira ya kiangazi mwaka 1974 ubalozi wa PLO ukafunguliwa rasmi huko jijini Moscow nchini Russia.
Katika kipindi hiki Yasser Arafat akapewa mpaka nafasi ya kuhutubia Umoja wa Mataifa (UN) na punde tu PLO wakapewa hadhi ya kiti cha uangalizi (observer status) pale UN mnamo mwaka wa 1974.
LIEUTENANT COLONEL VLADMIR PUTIN
====
Vladmir Putin kabla ya kuwa Rais wa Russia alikuwa ndiye boss wa kwanza wa FSB (mbadala wa USSR-KGB) akiwa na cheo cha Lieutenant Colonel na haikuwahi kutokea hapo kabla kwa maana kwa kawaida idara za ujasusi huko jeshini karibia nchi zote zikiongozwa na wanajeshi wa vyeo vya Major General tu.
Baadae akaja akawa assistant station chief wa KGB huko jijini Dresden East German (hapa alikuwa bado na cheo cha MAJOR kabla ya kupanda vyeo viwili juu na kustaafu kama Lieutenant Colonel) akiratibu shughuli (liaison officer) za idara ya usalama ya East German iliyokuwa inaitwa Staatssicherheit (Stasi) pamoja na zile za kwao KGB.
Vladimir Putin akiwa peke yake bila msaada wa maafisa wengine aliwahi kufanikiwa kuzitetea na kuzilinda ofisi za KGB huko Ujerumani Mashariki kutokana na umati wa waandamanaji na waporaji baada ya ukuta wa Berlin kuanguka. Bwana Putin alikuwa akifanya kazi kama afisa mdogo wa cheo cha Major ndani ya KGB huko jijini Dresden mnamo mwaka 1989 wakati ukuta ulipoanguka.
Kulingana na maelezo ya watu mbalimbali, inasemekana kwamba Putin alichomoa pistol/bastola yake kutoka kiunoni na kupiga risasi moja juu ile paaaaaah ili kutawanyisha umati wa ule waandamanaji waliokuwa na hasira waliotaka kuvamia ofisi za shirika hilo la upelelezi na kutaka kuiba mafaili yake.
Watu wengi wanaamini kwamba Putin, ambaye alifanya kazi kama agent wa KGB kwa ushirikiano wa karibu sana na shirika la ujasusi la Stasi huko Ujerumani wakati wa miaka ya 1980, alifanya bidii sana kuharakisha ukuta huo hauanguki.
Alikuwa ni mmoja wa raia wachache wa Soviet ambao walikuwa wa kwanza kukutana ana kwa ana na waandamanaji wa kijerumani wakati umati wa watu ulipogonga kuvamia ofisi ya Stasi kule jijini Dresden na kisha kujiandaa kulibomoa jengo ambalo Putin na wenzie walikuwa wakifanya kazi zao za upelelezi wa niaba ya taifa la Soviet. Putin alifanikiwa kuushawishi umati wa watu wote wakarudi nyuma.
Televisheni za nchini Russia hapo awali ziliwahi kuelezea jinsi Bwana Putin alivyoshika bastola mbele ya umati na kutumia lugha ya kijerumani kwa ufasaha (A level alipata A katika Kijerumani.
Ni mzuri sana kwa lugha) na kuweka wazi kuwa alikuwa tayari kuitumia kama mtu yeyote angeruka ukuta ama kuvunja geti. "Hili ni eneo la Soviet na mmesimama kwenye mpaka wetu," Putin alinukuliwa akisema. "Nipo serious na sina masihara nikisema nitapiga risasi mtu atakayevuta mstari huu." Shuhuda mmoja alinukuliwa akisema kwamba Putin alitoa tishio hilo akiwa yupo serious amekunja sura ya mbuzi.
Wakati wa anguko la ukuta huo wa Berlin, inasemekana kulikuwa na sanduku la mbao lililokuwa na siri za Cold War. West walikuwa wanalitafuta kama Diamond. Putin alishindwa kutoroka nalo, alilichoma moto. Kama West wangelikamata Urusi ingekuwa uchi.
BACK TO THE TOPIC
======
Wakati Vladimir Putin alipofika katika jiji la Dresden huko Ujerumani ya Mashariki kama afisa muandamizi wa cheo ya kati wa KGB (alifika Dresden akiwa na cheo cha MAJOR kama sijakosea ila akaja akapanda vyeo viwili juu akastaafu akiwa Lieutenant Colonel) mnamo mwaka 1985, Ujerumani Mashariki ilikuwa tayari inaishi nyuma sana ya muda.
Katika hatihati ya kufilisika, nchi hiyo ilikuwa ikinusurika na kuishi kwa msaada wa mkopo wa mabilioni ya Deutsche Mark (Hii ni pesa ya zamani ya Ujerumani kabla ya matumizi ya Euro) kutoka Ujerumani Magharibi, wakati sauti za upinzani zilikuwa zikiongezeka na kuanza kupamba moto.
Karibu nchi zote za kambi ya mashariki, hali ya maandamano ilikuwa ikiongezeka huku kukiwa na shida na upungufu wa mikakati ya kiuchumi iliyopangwa pamoja na ukatili wa vyombo vya usimamizi wa sheria (Stasi Secret Police)
Mengi ambayo ndugu Putin alifanya wakati wa miaka yake kadhaa ya kazi jijini Dresden bado hayajawekwa wazi, kwa sababu KGB ilikuwa na ufanisi wa hali ya juu sana katika kuchambua na kuhamisha hati za siri kabla ya kuanguka kwa taifa la ujamaa la Ujerumani Mashariki.
Kuna mzee mmoja, mtafiti katika makumbusho ya Stasi (Polisi wa siri wa Ujerumani Mashariki) huko jijini Dresden, ambaye aliwahi kufanya kazi na KGB katika masuala kadhaa ya shughuli za ujasusi, alipata kusema ya kwamba "Ukifanya kazi na Warusi, unapata shida sana kwa maana hawa watu waliharibu na kuteketeza karibu kila kitu,"
Ni vipande tu ndio vimebaki kwenye mafaili yaliyopatikana kutoka ofisi za Stasi juu ya shughuli za ndugu Putin pale. Faili lake ni jembamba, na limeminywa kweli kweli.
Ushahidi pekee wa shughuli zozote za upelelezi zilizohusishwa na Putin ni barua kutoka kwake kwenda kwa boss mkuu Stasi huko jijini Dresden (ni kama TISS-RSO kwa huku Tanzania), akimuomba msaada wake katika kurejesha mawasiliano ya simu kwa mtoaji habari (Informer) katika jeshi la polisi la Ujerumani ambaye "alikuwa anawaunga mkono KGB."
Barua ile ilikuwa ni fupi sana na haikuwa na maelezo yoyote ya ziada, lakini ukweli wa maombi ya moja kwa moja ya Putin kwa boss wa Stasi unaonekana kama vile kutaka kuonyesha umaarufu wa majukumu yake kabla ya kurejea USSR.
Itaendelea siku nyingine. Nipo busy kidogo na biashara za hapa mjini........!!!!!!!
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.
Ndugu zangu watanzania;
Mnaweza mkaanza kwa kuusoma kwanza uzi huu>>> Patrice Lumumba University of Russia: Ngome kuu ya majasusi wa KGB ya kufunza itikadi za Ujamaa kwa wanafunzi kutoka nchi masikini za Dunia ya Tatu
P.F.L.P NA KIONGZI WAO YASSER ARAFAT
====
Wakati comrade Yasser Arafat alipotembelea Moscow mnamo mwaka wa 1968, Moscow ilianza kumuona kama vile ni mtu wao, na mwaka uliofuata Arafat akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa PLO (Palestinian Liberation Organisation). Mahusiano imara baina ya Soviets na watu wa Palestine ndio yakawa yameanzishwa.
Mpaka kufikia mwaka wa 1970, baada ya Soviets kupoteza ushawishi wake kwa Misri, mahusiano na wanamgambo wa kipalestina ulikuwa umeimarishwa zaidi na kuanzia hapo silaha pamoja na mafunzo ya kijeshi kutoka Soviet vilianza kupelekwa kwa makundi hayo ya wapalestine.
Ukweli ni kwamba, KGB ndio waliokuwa wanaamua kundi lipi linapaswa kupokea msaada wa kifedha pamoja na silaha na mpaka kufikia mwaka 1972 Soviets walikuwa wametamka ya kwamba harakati za wapalestina ni nguzo muhimu sana katika ukombozi wa waarab wote pale mashariki ya kati. Ilipofika majira ya kiangazi mwaka 1974 ubalozi wa PLO ukafunguliwa rasmi huko jijini Moscow nchini Russia.
Katika kipindi hiki Yasser Arafat akapewa mpaka nafasi ya kuhutubia Umoja wa Mataifa (UN) na punde tu PLO wakapewa hadhi ya kiti cha uangalizi (observer status) pale UN mnamo mwaka wa 1974.
LIEUTENANT COLONEL VLADMIR PUTIN
====
Vladmir Putin kabla ya kuwa Rais wa Russia alikuwa ndiye boss wa kwanza wa FSB (mbadala wa USSR-KGB) akiwa na cheo cha Lieutenant Colonel na haikuwahi kutokea hapo kabla kwa maana kwa kawaida idara za ujasusi huko jeshini karibia nchi zote zikiongozwa na wanajeshi wa vyeo vya Major General tu.
Baadae akaja akawa assistant station chief wa KGB huko jijini Dresden East German (hapa alikuwa bado na cheo cha MAJOR kabla ya kupanda vyeo viwili juu na kustaafu kama Lieutenant Colonel) akiratibu shughuli (liaison officer) za idara ya usalama ya East German iliyokuwa inaitwa Staatssicherheit (Stasi) pamoja na zile za kwao KGB.
Vladimir Putin akiwa peke yake bila msaada wa maafisa wengine aliwahi kufanikiwa kuzitetea na kuzilinda ofisi za KGB huko Ujerumani Mashariki kutokana na umati wa waandamanaji na waporaji baada ya ukuta wa Berlin kuanguka. Bwana Putin alikuwa akifanya kazi kama afisa mdogo wa cheo cha Major ndani ya KGB huko jijini Dresden mnamo mwaka 1989 wakati ukuta ulipoanguka.
Kulingana na maelezo ya watu mbalimbali, inasemekana kwamba Putin alichomoa pistol/bastola yake kutoka kiunoni na kupiga risasi moja juu ile paaaaaah ili kutawanyisha umati wa ule waandamanaji waliokuwa na hasira waliotaka kuvamia ofisi za shirika hilo la upelelezi na kutaka kuiba mafaili yake.
Watu wengi wanaamini kwamba Putin, ambaye alifanya kazi kama agent wa KGB kwa ushirikiano wa karibu sana na shirika la ujasusi la Stasi huko Ujerumani wakati wa miaka ya 1980, alifanya bidii sana kuharakisha ukuta huo hauanguki.
Alikuwa ni mmoja wa raia wachache wa Soviet ambao walikuwa wa kwanza kukutana ana kwa ana na waandamanaji wa kijerumani wakati umati wa watu ulipogonga kuvamia ofisi ya Stasi kule jijini Dresden na kisha kujiandaa kulibomoa jengo ambalo Putin na wenzie walikuwa wakifanya kazi zao za upelelezi wa niaba ya taifa la Soviet. Putin alifanikiwa kuushawishi umati wa watu wote wakarudi nyuma.
Televisheni za nchini Russia hapo awali ziliwahi kuelezea jinsi Bwana Putin alivyoshika bastola mbele ya umati na kutumia lugha ya kijerumani kwa ufasaha (A level alipata A katika Kijerumani.
Ni mzuri sana kwa lugha) na kuweka wazi kuwa alikuwa tayari kuitumia kama mtu yeyote angeruka ukuta ama kuvunja geti. "Hili ni eneo la Soviet na mmesimama kwenye mpaka wetu," Putin alinukuliwa akisema. "Nipo serious na sina masihara nikisema nitapiga risasi mtu atakayevuta mstari huu." Shuhuda mmoja alinukuliwa akisema kwamba Putin alitoa tishio hilo akiwa yupo serious amekunja sura ya mbuzi.
Wakati wa anguko la ukuta huo wa Berlin, inasemekana kulikuwa na sanduku la mbao lililokuwa na siri za Cold War. West walikuwa wanalitafuta kama Diamond. Putin alishindwa kutoroka nalo, alilichoma moto. Kama West wangelikamata Urusi ingekuwa uchi.
BACK TO THE TOPIC
======
Wakati Vladimir Putin alipofika katika jiji la Dresden huko Ujerumani ya Mashariki kama afisa muandamizi wa cheo ya kati wa KGB (alifika Dresden akiwa na cheo cha MAJOR kama sijakosea ila akaja akapanda vyeo viwili juu akastaafu akiwa Lieutenant Colonel) mnamo mwaka 1985, Ujerumani Mashariki ilikuwa tayari inaishi nyuma sana ya muda.
Katika hatihati ya kufilisika, nchi hiyo ilikuwa ikinusurika na kuishi kwa msaada wa mkopo wa mabilioni ya Deutsche Mark (Hii ni pesa ya zamani ya Ujerumani kabla ya matumizi ya Euro) kutoka Ujerumani Magharibi, wakati sauti za upinzani zilikuwa zikiongezeka na kuanza kupamba moto.
Karibu nchi zote za kambi ya mashariki, hali ya maandamano ilikuwa ikiongezeka huku kukiwa na shida na upungufu wa mikakati ya kiuchumi iliyopangwa pamoja na ukatili wa vyombo vya usimamizi wa sheria (Stasi Secret Police)
Mengi ambayo ndugu Putin alifanya wakati wa miaka yake kadhaa ya kazi jijini Dresden bado hayajawekwa wazi, kwa sababu KGB ilikuwa na ufanisi wa hali ya juu sana katika kuchambua na kuhamisha hati za siri kabla ya kuanguka kwa taifa la ujamaa la Ujerumani Mashariki.
Kuna mzee mmoja, mtafiti katika makumbusho ya Stasi (Polisi wa siri wa Ujerumani Mashariki) huko jijini Dresden, ambaye aliwahi kufanya kazi na KGB katika masuala kadhaa ya shughuli za ujasusi, alipata kusema ya kwamba "Ukifanya kazi na Warusi, unapata shida sana kwa maana hawa watu waliharibu na kuteketeza karibu kila kitu,"
Ni vipande tu ndio vimebaki kwenye mafaili yaliyopatikana kutoka ofisi za Stasi juu ya shughuli za ndugu Putin pale. Faili lake ni jembamba, na limeminywa kweli kweli.
Ushahidi pekee wa shughuli zozote za upelelezi zilizohusishwa na Putin ni barua kutoka kwake kwenda kwa boss mkuu Stasi huko jijini Dresden (ni kama TISS-RSO kwa huku Tanzania), akimuomba msaada wake katika kurejesha mawasiliano ya simu kwa mtoaji habari (Informer) katika jeshi la polisi la Ujerumani ambaye "alikuwa anawaunga mkono KGB."
Barua ile ilikuwa ni fupi sana na haikuwa na maelezo yoyote ya ziada, lakini ukweli wa maombi ya moja kwa moja ya Putin kwa boss wa Stasi unaonekana kama vile kutaka kuonyesha umaarufu wa majukumu yake kabla ya kurejea USSR.
Itaendelea siku nyingine. Nipo busy kidogo na biashara za hapa mjini........!!!!!!!
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.