M-BET: Mdhamini pekee wa timu katika NBC PL mwenye furaha kuliko wote

ninosi

Senior Member
Joined
Jun 30, 2022
Posts
151
Reaction score
333
Kwa hali ilivyo sasa kama mdhamini katika NBCPL anataka kupata return ya haraka kwa hela aliyowekeza, Simba SC ni sehemu sahihi. Hili limejidhihirisha msimu huu (2022/23) ambapo M-BET anapata marejesho lukuki.

Katika msimu huu (2022/23);
1. M-BET imemwaga bilioni 1 Simba Queen. Kwa sasa Simba Queen yupo nusu fainali ya CAFCL.
2. M-BET imemwaga zaidi ya bilioni 16 Simba SC. Kwa sasa Simba SC anasubiri 16/11/2022 kupangiwa timu katika hatua ya makundi ya CAFCL.

Mafanikio ambayo timu hizo mbili zimepata katika msimu huu, zimeipa M-BET fursa kubwa ya kuweza kujitangaza duniani. Na hiii inaenda kumuongezea faida maradufu.

ANGALIZO:
Makampuni mnapotaka kujitangaza katika NBCPL, jaribuni kufanya upembuzi makini ni wapi muweke mzigo na siyo kuendeshwa na 'mahaba' kama yule 'jamaa wa Kinondoni' ambaye kwa sasa anajuta kutoa bilioni 12 kwa timu ambayo kila kukicha inalifedhehesha taifa.


 

Mkuu uko sahihi.. Kwa timu ambazo Simba SC atapangwiwa katika michuano migumu ya CAFCL zitabidi zitafute video za mechi za awali (CAF Preliminary Rounds) ili kuona nguvu ya Simba SC msimu huu. Hapa sasa ndiyo M-BET atazidi kuchanja mbuga.
 
Kweli Lage hakukosea kuwaweka katika group la ma Mbumbumbu, apa NBC Simba ubingwa wasahau kabisa katika miaka ya hivi karibuni kule CAF timu zikianza hatua za Makundi M-bet hausiki.
Muwe mnafuatilia mambo Ili muwe na ufahamu wa kutosha, u mbumbumbu si ugonjwa[emoji1][emoji1]
 
Ugomjwa [emoji777]
Ugonjwa [emoji3581]

Najua unapitia magumu,jikaze
 

Mkuu ushapata mihogo kweli, mana naona umekurupuka. Unachokiongea nimekijibu post #6 hapo juu.

Olo ini Olo wahi kwa Ashura Cheupe hapa kuna mihogo yako ushalipiwa.
 
Timu iko nyumbani afu mashabiki wanagoma jaza uwanja
Kwa takwimu za Tff Yanga ndio timu inayoongoza Kwa kuingiza mashabiki uwanjani iwe ugenini au Nyumbani, Hivi karibuni Msemaji wa Mbumbumbu fc alilalamika Simba ikicheza mashabiki hawajui uwanjani Kwa wingi kiasikwamba inaingiza milioni 14 kwenye Mechi ya Nyumbani.
Sasa msifananishe timu ya mpira wa miguu (Yanga) na kikundi Cha mbumbumbu (Simba) kinacho jaribu kucheza mpira.
 
Sasa mihogo na mnyama nani ana uzoefu kwenye haya mashindano ya wanaume?

Mnyama hana sababu ya kufuatilia maana ni mshiriki. Mihogo ndio inapaswa kufuatilia

BTW.... Visit Tanzania.....
 
Mihogo imepanda bei maana walaji ni wengi....

Wengine wanashangilia mafanikio uwanjani wengine wanaringa kuwa na mashabiki wengi uwanjani

Kama ni kujaza mashabiki basi kashindaneni na kina TOT taarab
 
Mihogo imepanda bei maana walaji ni wengi....

Wengine wanashangilia mafanikio uwanjani wengine wanaringa kuwa na mashabiki wengi uwanjani

Kama ni kujaza mashabiki basi kashindaneni na kina TOT taarab
Yanga ndio timu yenye mafanikio kuliko klabu yoyote ya mpira wa miguu Kwa maana ya Mataji apa Tanzania.
 
Kwa takwimu za CAF simba ndio inaongoza kwa kujaza mashabiki wengi uwanjani, endelea na takwimu zako za anibiteni
 
Kwa takwimu za CAF simba ndio inaongoza kwa kujaza mashabiki wengi uwanjani, endelea na takwimu zako za anibiteni
Uko sahihi Mkuu.. Mfano mechi ya juzi dhidi ya Club Africain, pamoja na UNICEF Tanzania kununua tiketi 10,000 ili wazigawe kwa mashabiki wa Uto in tiketi 293 pekee ndizo mashabiki walzôpata. Tiketi 9707 zilidoda na hivyo UNICEF Tanzania kupata hasara.
 
Kwa takwimu za CAF simba ndio inaongoza kwa kujaza mashabiki wengi uwanjani, endelea na takwimu zako za anibiteni
We kweli Mbumbumbu, Caf takwimu za Simba viwanjani wanazitoa wapi wakati FA ya Tanzania ndio inayo itaja Yanga kama timu inayoingiza mashabiki wengi viwanjani uku Msemaji wa Simba alilalamika mashabiki kiduchu wanao kwenda uwanjani na kusababisha timu kupata milioni 14 Kwa gemu Moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…