Maajabu:baada ya Rasimu ya pili na bunge la katiba kuanzaWASOMI wajadili muundo wa serikali unaofaa

Maajabu:baada ya Rasimu ya pili na bunge la katiba kuanzaWASOMI wajadili muundo wa serikali unaofaa

Niliona Mkenya mmoja msomi nae akisema eti hatutaweza 3. Mbona wao wana Governors nani aliwahutubia.Stupid msomi
 
wasomi wetu wanasubiri kuona wakubwa wana maono gani juu ya mada, ndipo hukurupuka ili kufurahisha wakubwa.
 
Unamanisha nini? una maana kwamba hata wabunge wasiijadili au? je nini maana ya Rasimu?
 
Wale walikuwa ni wapuuzi tu! Makamanda mimi nasema hv, bila serikali 3 ni bora tusiwe na muungano wa kijinga namna hii. Patachimbika

huna hoja zozote za kuitetea serikali tatu,bali kwa kuwa ni sera ya chama chako,wasomi wameona mbele na kusema ili kuudumisha Muungano ni lazima kuwa na serikali 1 tu na si 2 wala 3..haki haiwezi kupatikana kwa kutishia kuchimbika acha kuwa mtumwa wa wanasiasa....kuliko kuwa na mafungu ya serikali yaani 2 au 3 bora kuuvunja Muungano!!tumia ubongo na si kucrush wasomi maana wameona mbali
 
Hao wasomi wamesahau kusema kuwa gharama za serikali moja ndio nafuu kuliko zote.

toa ushahidi,,serikali tatu kwa mantiki gani iwe cheap kuliko moja?huoni serikali tatu zitakuwa mzigo kwa wananchi kwani kila nchi itakuwa na wafanyakazi na viongozi wake achilia mbali serikali ya Muungano!!tatizo ni kukubali mawazo ya wanasiasa yatutawale ambao pengine elimu yao ni ndogo sana ama ni kufoji achilia mbali na wale wenye elimu lakini wanaangalia maslahi yao,,ukimuuliza mtu anakuambia 3 coz chadema wanataka na ni cheap,,ukimuuliza ccm anataka mbili coz ndizi za mwl nyerere
 
Kwa hiyo kwa akili zako zilivyo fupi Warioba anavyo tetea na kufafanua juu ya serikali 3 anasimamia upande wa CDM? Tambua 64% ya watanzania walipendekeza serikali 3 hivyo kwa kauli yako basi CDM ipo na wananchi tafauti na CCM unayoishabikia.

kwanza kubali kuwa idadi ya watanzania waliotoa maoni yao juu ya katiba ni wachache na hata wale waliotoa walishinikizwa na wanasiasa!!wengi hata katiba ya sasa hawajaisoma
 
Hawa ni wana CCM ambao mlikwisha taarifiwa walikaa wakachakachua rasmu ya pili ya Katiba. Wanaongozwa na tumbo. Timu imeundwa na akina Mukandala,Bana na wachumia tumbo wengine kama Malyamkono yule Mganda Kyaka toka Misenyi!

hoja za wasomi zina nguvu kuliko za kina nape,sugu na lema ambao shule kwao ni kitendawili acha nchi iongozwe na wasomi
 
ccm kwa uzoefu hawafanyi mambo kwa jazba. Mfumo bora kwa muungano wa Tanganyika na zanzibar ni serikali mbili na hawayumbi kuhusu hilo. Vyama vingine vina jazba na kuhamasisha wananchi kufuata njia isiyokua na maslahi kwa mstakabali wa taifa. Wasomi sasa wanazinduka usingizini wakati Warioba kashatoa pendekezo kutokana na maoni yaliyotolewa kwa jazba badala ya hekima. Yeye pia inaelekea ana jazba. Ni wajibu wa bunge la katiba kupiga tiktak wazo la serikali tatu na kubakiza mambo yote mema ya tume ya Warioba.

serikali 2 ni bora kuliko 3 ila moja ni bora zaidi kiuchumi na kwa umoja
 
Kiuchumi, kwa nini si serikali moja? Tunataka kuona serikali ya tanganyika huru. No tanganyika, no zanzibar, muungano wa serikali mbili kwa faida ya nani? Kama sio manyang'au!

we unadhani kuwepo kwa serikai ya tanganyika kutakusaidia nini cha ziada?
 
Hata huu Muungano ukivunjwa tanganyika tutakuwa na serikali yetu moja.
Bora muungano huu uvunjwe tu hauba faida yeyote kwa tanganyika na kama ipo naomba nieleweshwe.
 
Tatizo ni ss wabara tunahofia Zanzibar kumezwa na waarabu au uislam wakat ni kweli tunawabana.
 
Sijauona huo mjadara ITV, lakini sitashangaa nikisikia kwenye huo mjadara na Dr. Bana nae alikuwepo!
 
Back
Top Bottom