Wanabodi,
Hii vita ya Corona Tanzania inakumbana na twists and turns za ajabu ajabu!, kwa vile huu ni mlipuko wa ugonjwa, ilitegemewa madaktari Bingwa ndio wangekuwa wakombozi wa taifa letu kwenye janga hili, lakini kwa Tanzania ni maajabu matupu, badala ya Madaktari Bingwa wa Tiba! kuwa wakombozi wa taifa letu, Mkombozi wa kweli wa taifa letu kwenye hii vita ya Corona ni Bingwa wa Kemia, ndiye ametoa ushauri bora kabisa wa Kikemia wa namna bora ya kuikabiliana na janga hili la Corona ili kushinda vita hii.
Je, bingwa huyu wa Kemia ni nani na ametoa ushauri gani?
Andamana nami.
1. Background, Professionalism
Tangu kuanza kwa janga hili la Corona, mimi kama Mtanzania Mzalendo nimeshiriki kikamilifu katika vita hii kikamilifu katika maeneo 5
- Kama Mtanzania tuu wa kawaida
- Kama Mwana jf
- Kama mwandishi wa habari mzoefu
- Kama mtangazaji wa TV Nguli
- Kama mtu mwenye exposure.
Hivyo kwenye hayo maendeleo 5 nimeshiri kwa kutoa maoni mbalimbali, miongoni mwake ni ule ushauri wangu wa mwanzo kuwa zipo wizara zinaweza kuongozwa na Waziri mwanasiasa yoyote, lakini kuna wizara zinazo deal na technical issues, zinapaswa kuongozwa na ma professionals. Moja ya wizara ya Afya, ilipaswa kuongozwa na daktari bingwa na sio a layman kwenye medical field.
Tulipoanza tuu ile siku Waziri wa Afya akiwa daktari Bingwa kwa jina la Janet akizungumzia kuvaa face mask, daktari huyo akiwa mbele ya Waziri wa Afya alisema face mask zitavaliwa na madaktari tuu wanaohudumia wagonjwa. Nikapandisha bandiko humu na kusema it's not right kwasababu kama inachukua siku 14 kuibaini Corona kwa aliyeambukizwa, how will one knows hivyo to be on a safe side ni watu wote wavae facemasks kama China. Waziri angekuwa daktari pale pale angejua.
Corona inatufundisha Tanzania tuna tatizo kuchanganya siasa na professionalism. Hongera Prof. Janabi kwa elimu uliyotoa, so far you are the best! - JamiiForums
2. Mazungumzo na Naibu Waziri wa Afya
Kuna siku nimezungumza na Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndugulile, kama ilivyo kawaida yangu, mimi huwa nina maswali magumu. Miongoni mwa maswali niliyomuuliza Dr. Ndugulile ni swali la kwa vile Corona haina dawa, jee anaweza kueleza hao wagonjwa kwenye vituo vya matibabu wanafanywa nini au wana hudumiwa huduma gani ili Watanzania wenye uwezo waweze kuwahudumia wagonjwa wao ambao hawajazidiwa ili kuzuia hospitali zisielemewe. Dr. Alinigomea!.
Kisha nikamuuliza kwa vile Corona ni mafua, kwanini Wizara ya Afya isihamasishe alternative medicine ya watu kujitibu ili wengine wamalizane nayo juu kwa juu bila kuisumbua serikali na kupelekwa vituo vya huduma?.
Pia swali hili alinigomea na kusisitiza kila mwenye dalili aripotiwe.
Kwa kutumia uzoefu wangu wa exposure, Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndugulile alikuwa ana majibu yote tena ya kidakitari, lakini kwa vile yeye sio Msemaji rasmi, Msemaji rasmi ni Waziri wake, na Waziri sio daktari, Dr. Ndugulile aliogopa kusema akapishana na Waziri wake, lakini Waziri wa Afya angekuwa ni daktari Bingwa, Dr. Ndugulile angezungumza.
Vita Janga la Corona: Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas, Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndungulile, kesho watakuwa live JLNH-Star TV - JamiiForums
Star TV: Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas na Naibu Wazuri wa Afya Dr. Faustine Ndungulile, Wanazungumzia Corona - JamiiForums
Karibu.
Paskali