Maajabu ya Corona Tanzania: Badala ya Madaktari Bingwa wa tiba kuliokoa Taifa, ni Bingwa wa Kemia ndiye analiokoa Taifa kwa ushauri wa kikemia

Miye nashauru hii mbinu ya kufukiza iende tumika kwa wagonjwa waliopo kwenye matibabu tuone tukiona ina matokeo chanya basis tuanze hamasishana uko majumbani iwe ni mwendo wa kupigana chungu tu mpaka wazungu wajue kweli Africa tunaweza
 
Bingwa wa kemia badala angehutubia mabingwa wa afya na wizara yote yeye anaenda kuhutubia wizara ya ulinzi na wakuu wake.
Ni ishara kwamba sasa Coronavirus anaenda kukabiliwa na wazee wa medani. Unadhani huyo Covid-19 atahimili muziki wa AK47, vifaru, mabomu ya mkono, mbwa wenye mafunzo, na karate za wale makomandoo wanaovunja matofali kwa vichwa?

Hii awamu ni zaidi ya Futuhi aiseee 😁😂😂!
 
Very disappointing! tutakimbilia wapi, sijui kitokee nini maambukizi yasizidi na vifo visiongezeke, sijui kama Rais wenu anajua madhara ya kauli zake kwa sisi ambao hatujaenda hata la pili B. Nadhani hata HIV mwanzo iliua wengi kwa sababu kama hizi, kutokufuata ushauri wa kitaalamu badala yake tunategemea kubet kwa sangatiti, ikitokea mtu akapona sote tunasema oyeeeee!

Nimewaonea huruma sana wataalamu na wahudumu wote wa sekta ya afya, Kiongozi wenu hawajali na huu ndio ukweli.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa sijui kama kweli ana washauri, na kama anao inabidi watupwe selo fasta maana kazi imewashinda!
 
Hayo maswali mawili magumu niliyo muuliza Naibu Waziri wa Afya Dr. Faustine Ndugulile ambayo yalitakiwa kujibiwa na madaktari Bingwa wa tiba, leo yamepatiwa majibu badala ya kupatiwa majibu na madaktari Bingwa wa tiba, kitu cha ajabu sana kuhusu mapambano dhidi ya janga la Corona nchini Tanzania, maswali hayo yamepatiwa majibu na Bingwa wa Kemia.

Tanzania tulizoea viongozi wetu wakuu wa kisiasa huwa ni wanasiasa, hivyo ulipo tokea Bingwa wa Kemia alipoutaka urais, kiukweli kuna watu humu tulimshangaa!, tangu lini Bingwa wa Kemia akawa kiongozi wa siasa kuwa mkuu wa nchi?.
Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli - JamiiForums

Lakini kwa mara ya kwanza katika urais wa Tanzania, leo ndio tumeona umuhimu wa kiongozi wa nchi anapokuwa ni Bingwa wa Kemia kuutumia ubingwa wake wa kemia kulisaidia taifa lake kwa ushauri wa Kikemia wa jinsi ya kutumia Kemia kupambana na janga la Corona.

P
 
Vichaa karibu wote hudhani kuwa wanajua kila kitu na wana akili kuliko wenye akili zao
 
ina maana magufuli hamuoni tu pasco, au anajifanyisha?.....haiwezekeni. akuteue tu aisee.
 
Emb pandisha hii pale juu. Nchi hii tumeukwaa mkenge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…