Maajabu ya Corona Tanzania: Badala ya Madaktari Bingwa wa tiba kuliokoa Taifa, ni Bingwa wa Kemia ndiye analiokoa Taifa kwa ushauri wa kikemia



Daaah kama ni raisi tu tunae.

Magu kila akiibuka hewani lazima achafue hali ya hewa.
 
Hakuna mahala ninapoipinga hutuba ya MAGUFULI, Mheshimiwa raisi yuko sahihi 100%.
Najua mawakala wa ukoloni mamboleo hawataielewa hiyo hutuba

Kuna mambo namuunga mkono JPM na hii hotuba yake alichozungumza yupo sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makosa yalishafanyika tangu mwaka 2015! Kwa sasa tupambane tu na hali zetu. Kumlaumu, kumkosoa, nk haitasaidia chochote maana alishajitapa mara nyingi ya kwamba yeye si mtu wa kushauriwa na si mtu wa kuwaamini wasaidizi wake.

Kinachomjia kichwani mwake, ndiyo hicho hicho. Mpaka ifikie 2025, tutashuhudia mengi.
 
Umesema VEMA ILA UNGEYAANDIKA HAYO MAJIBU YALIYOPATIKANA KUTOKA KWA HUYO BINGWA WA KEMIA ILA NAMI NIJIKINGE MAPEMA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maji yanaanza kugeuka kuwa mvuke kwenye nyuzi joto 100, hivyo ukiona mtu anajifukiza mvuke tambua kuwa joto la huo mvuke ni hilo na kuendelea.
 

Nimeona UK mpaka sasa wamegawa PPE 1bn kwenye hospitali zao yes billion moja
Hizo ni zana za kujikinga na maambukizi na bado wanalalamika kuwa hazitoshi
Wafanyakazi 15 wamekufa mpaka sasa
Lakini wanapambana
Ni mda wa kupiga kelele hospitali zisaidiwe sana hata mortuary ziongezwe sio utani


Sent from my iPhone using Tapatalk
 

Hiki ni kituko, kwa hiyo korona ingekuwa hakuna bingwa wa kemia angekuwa hana faida au?

Hii ni ajabu, hivi umeandika nini hapa ndugu yangu? Kweli tuna matatizo makubwa zaidi ya Korona, heri kuomba tu jaman
 
unachokitafuta utakipata muda siyo mrefu,
tchao..
 
Bingwa wa Kemia ametoa ushauri wa Kikemia kuwa vurusi vimeumbwa cells za protein in nature na kuzungukwa fatty acid hivyo vinayeyushwa au kwa kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka au sanitizers ambazo kikemia ni alcohol ambazo zinawayeyusha kwa kuyasaga mafuta au mvuke wa nyuzi joto kubwa una destroy protein in nature inakuwa destroyed by heat.

Bingwa wa Kemia amewataka Watanzania kuendelea kufuata maelekezo ya kitaalamu ya kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona ila pia na kutumia tiba mbalimbali za asili na tiba mbadala kupambana na Corona kwa kunywa tangawizi, vitunguu swaumu, au hata kujifukiza, vitu ambavyo Watanzania walipaswa kufundishwa na madaktari Bingwa wa tiba, badala yake sasa ni Bingwa wa Kemia ndio amekuwa mkombozi wa taifa letu katika vita hii dhidi ya Corona.

Ushauri huu wa Bingwa wa Kemia ndio ukombozi wa Taifa letu dhidi ya janga la Corona, kwasababu naamini kuna wengi wameugua Corona na wakajitibia kwa njia za asili na tiba mbadala na wakapona, hivyo kama kila Mtanzania akiona tuu dalili kwa mbali akaanza na huduma ya kwanza ya homeopathy treatment kwa kutumia natural remedies na treatments na alternative medicine tunaweza kuliokoa taifa letu zaidi kuliko kuwategemea hawa madaktari Bingwa wetu wa tiba za kisasa mahospitalini ambao ni mabubu huku mabingwa wa Kemia ndio wakilisaidia taifa!.

Mpaka hapa nilipofikia, bado kuna haja ya mimi kumtaja huyu bingwa wa Kemia?
P
 
Mithali 14:4
Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe; Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.
 
Kaka kuna muda unaandika vitu vingine mimi nabaki kuwafikiria wanao kwa maana watakuja kuyasoma maandiko yako baada ya miaka kumi ijayo , sasa sijui baada ya kuyasoma maandishi yako ya aina bado wataendelea kuona ufahari kuitumia sure name yao ama itakuwaje aisee poleni watoto wa P!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal huyu mkemia anatuchanganya sasa, hata sijui nifuate lipi.

Mwanzo alisema ni kaugonjwa kadogo tu, tena ni shetani tumkabidhi Mungu amshughulikie.
Baadaye tena hivi karibuni alitangaza maombi ya siku tatu kwa nchi nzima, ili tumkumbushe Mungu kuwa kale kashetani kadogo corona kanataka kuota mapembe, akashughulikie haraka.Leo pia PM alikuwa na viongozi wa dini kwa lengo hilo hilo.

Sasa hata kabla hatujapata jibu kutoka kwa Mungu mkemia amekuja na tiba ya covid-19.
Kumbe tulikuwa tunamsumbua Mungu bure ashughulikie hako kashetani kadogo corona wakati mkemia anayo dawa!!!
Ni kujifukiza tu, hako kafuta kanayeyuka fasta.
Huyu mkemia wetu naona ana roho mbaya sana.
Yaani amewaacha wazungu wanateketea wakati dawa anayo? Halafu sasa hao hao anawaomba wamfutie madeni? Hiyo siyo fair kabisa.

Halafu eti hiyo fumigation iliyofanyika Dar ndiyo inawezekana imeongeza maambukizi ya covid-19 kwenye jiji letu? Ina maana hata naibu raisi DAB mwenye mkoa wake hakujua? Taratibu mkemia wetu hapo.unatudanganya, hata sisi tusiojua kemia tumeshtuka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma mahali kuwa huko Ujerumani kama sijakosea hivyo virusi vilijaribiwa kwenye joto kali kwenye maabara na havikufa kwa hiyo kuondoa dhana kuwa virusi hivi vinakufa kwenye joto kali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…