Maajabu ya tairi mbovu na utajiri uliojificha ndani yake

Maajabu ya tairi mbovu na utajiri uliojificha ndani yake

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Zingatia hapa tairi mbovu yaani ilishatumika, ikachakaa ama ikaharibika hivyo haifai kutumika tena kwenye magari

Hii ni fursa ambayo itawafaa sana vijana wetu wa JF wanaosaka ajira

Tairi moja mbovu ya gari kubwa ya mizigo unaweza kuinunua kwa kati ya shilingi 2000 mpaka 5000 kulingana na ubora . Zikiwa tairi 18 mpaka 20 zinatengeneza tani moja

Sasa tuchukulie kwa makisio ya juu.. Utainunua kwa shilingi 5000, lakini atakuja mchunaji ataichuna kwa ndani na kupata mipira kati ya 20 na 25 ..

Mipira ile ya kufungia mizigo kwenye baiskeli na bodaboda

Kila mpira utauza shilingi 500 Kwa jumla. Weka wastani wa mipira 24 kwa tairi sawa na elfu 12,000.. Toa 2000 ya mchunaji unabaki na elfu 10, toa elfu 5 ya manunuzi unabaki na elfu 5 kwa tairi. Zidisha mara 20 unapata laki 1 ffaida

Ukitoka hapo unapeleka tairi zako kiwanda ni na kwenda kuuza kwa kilo.. Tairi 20 zinazotengeneza tani moja utauza kwa bei ya chini kabisa Shilingi laki 2, kumbuka kule ulishapata laki 1 ya mipira na hiyo laki mbili ni yako yote usafiri ni malipo mengine

Sasa tairi 20 ulizonunua kwa laki 1
Zimekuletea faifa ya laki 1 kwenye kuchuna mipira na faida ya laki 2 kiwandani . jumla laki 3.. Hapo faida inaweza kuongezeka ukipata tairi kwa chini ya elfu 5 na ukauza zaidi ya laki 2
Hapo kwa wapambanaji ni fursa yenye kipato cha kueleweka
Sasa twende huko viwandani ushuhudie maajabu
 
Sehemu ya pili..
Maajabu ya tairi mbovu na utajiri uliojificha ndani yake

Kiwanda kitanunua tani moja ya tairi kwa shilingi laki mbili bei ya sasa.. Ataichoma mchomo mmoja unaochukua tani nane kwenye boiler kupitia mchakato uitwao pyrolisis (kama kupika gongo tu)
Tani 8 sawa na shilingi milion 1.6
Zitakuletea wastani wao
.Mafuta ya I.D.O (industrial diesel oil) lita 3000 sawa na tani 3..
. Vumbi (black carbon) wastani wa tani 4
.Waya wastani wao tani 2
Gesi wastani wa nusu tani
Lita moja ya I.D.O kwa sasa ni Tsh 2000 zidisha mara 3000 ni Tsh 6,000,000
Vumbi (carbon black) kwasasa tani moja ni kama elfu 70 zidisha mada 4 ni Tsh 280,000
Waya kwasasa tani ni kama shilingi laki 8 zidisha mara 2 ni Tsh. 1,600,000
Gesi sijapiga hesabu
Kwahiyo mzigo wao shilingi 1.6M unakuletea wastani wa shilingi 7, 880,000/=
Ukitoa gharama zote za uendeshaji bado hukosi faida ya Tsh. 5,000,000/= tasilimu
Kwa wasiojua matumizi ya hizi bidhaa
1. Mafuta ya IDO ni kama nishati mbadala viwandani badala ya diesel, kuni, gas au umeme
2. Vumbi ni malighafi kwenye viwanda vya saruji
3. Waya zipo ngumu na Iaini.. Ngumu zinatumika kama binding wire kwenye ujenzi unaohusisha nondo, laini kama carbon catalyst kwenye viwanda vya nondo.. Si mnajua nondo bila carbon ukiipinda inakatika?
4. Gesi kwa matumizi ya kupikia nk

Hayo ndio maajabu na utajiri uliojificha kwenye tairi mbovu


Good morning Tanganyika
 
Sehemu ya pili.. Maajabu ya tairi mbovu na utajiri uliojificha ndani yake
Kiwanda kitanunua tani moja ya tairi kwa shilingi laki mbili bei ya sasa.. Ataichoma mchomo mmoja unaochukua tani nane kwenye boiler kupitia mchakato uitwao pyrolisis (kama kupika gongo tu)
Tani 8 sawa na shilingi milion 1.6
Zitakuletea wastani wao
.Mafuta ya I.D.O (industrial diesel oil) lita 3000 sawa na tani 3..
. Vumbi (black carbon) wastani wa tani 4
.Waya wastani wao tani 2
Gesi wastani wa nusu tani
Lita moja ya I.D.O kwa sasa ni Tsh 2000 zidisha mara 3000 ni Tsh 6,000,000
Vumbi (carbon black) kwasasa tani moja ni kama elfu 70 zidisha mada 4 ni Tsh 280,000
Waya kwasasa tani ni kama shilingi laki 8 zidisha mara 2 ni Tsh. 1,600,000
Gesi sijapiga hesabu
Kwahiyo mzigo wao shilingi 1.6M unakuletea wastani wa shilingi 7, 880,000/=
Ukitoa gharama zote za uendeshaji bado hukosi faida ya Tsh. 5,000,000/= tasilimu
Kwa wasiojua matumizi ya hizi bidhaa
1. Mafuta ya IDO ni kama nishati mbadala viwandani badala ya diesel, kuni, gas au umeme
2. Vumbi ni malighafi kwenye viwanda vya saruji
3. Waya zipo ngumu na Iaini.. Ngumu zinatumika kama binding wire kwenye ujenzi unaohusisha nondo, laini kama carbon catalyst kwenye viwanda vya nondo.. Si mnajua nondo bila carbon ukiipinda inakatika?
4. Gesi kwa matumizi ya kupikia nk

Hayo ndio maajabu na utajiri uliojificha kwenye tairi mbovu


Good morning Tanganyika
Mkuu hapa naona sheria ya mass balance haizingatiwi!
Inakuwaje input ya tani moja izalishe lots of tani mbele yake without additional of other materials?
 
Mkuu hapa naona sheria ya mass balance haizingatiwi!
Inakuwaje input ya tani moja izalishe lots of tani mbele yake without additional of other materials?
Ziko compressed na hapo sio tani MOJA ni tani 8 jaribu kugawanya na sijaweka actual bali makisio na wakati wa uchomaji kuna vipande vya tairi ndogondogo unajazia
 
Tani moja ya tairi mbovu haiwezi hiyohiyo kua tani moja ya nyaya, carbon na fuel.

Pia haiwezi tumika kuzalisha gesi ya kupikia.
Model C Waste Tyre Pyrolysis Plant
Capacity model: 1Ton-15Ton
Raw materials: Waste Tyre/rubber
Average out-put oil rate: 45% fuel oil, 30% carbon black, 10% steel wire, 10%-15% syngas
 
Tani moja ya tairi mbovu haiwezi hiyohiyo kua tani moja ya nyaya, carbon na fuel.

Pia haiwezi tumika kuzalisha gesi ya kupikia.
056142e39fa8eb5b6a4abba73b2c62b0.jpg
 
Sehemu ya pili.. Maajabu ya tairi mbovu na utajiri uliojificha ndani yake
Kiwanda kitanunua tani moja ya tairi kwa shilingi laki mbili bei ya sasa.. Ataichoma mchomo mmoja unaochukua tani nane kwenye boiler kupitia mchakato uitwao pyrolisis (kama kupika gongo tu)
Tani 8 sawa na shilingi milion 1.6
Zitakuletea wastani wao
.Mafuta ya I.D.O (industrial diesel oil) lita 3000 sawa na tani 3..
. Vumbi (black carbon) wastani wa tani 4
.Waya wastani wao tani 2
Gesi wastani wa nusu tani
Lita moja ya I.D.O kwa sasa ni Tsh 2000 zidisha mara 3000 ni Tsh 6,000,000
Vumbi (carbon black) kwasasa tani moja ni kama elfu 70 zidisha mada 4 ni Tsh 280,000
Waya kwasasa tani ni kama shilingi laki 8 zidisha mara 2 ni Tsh. 1,600,000
Gesi sijapiga hesabu
Kwahiyo mzigo wao shilingi 1.6M unakuletea wastani wa shilingi 7, 880,000/=
Ukitoa gharama zote za uendeshaji bado hukosi faida ya Tsh. 5,000,000/= tasilimu
Kwa wasiojua matumizi ya hizi bidhaa
1. Mafuta ya IDO ni kama nishati mbadala viwandani badala ya diesel, kuni, gas au umeme
2. Vumbi ni malighafi kwenye viwanda vya saruji
3. Waya zipo ngumu na Iaini.. Ngumu zinatumika kama binding wire kwenye ujenzi unaohusisha nondo, laini kama carbon catalyst kwenye viwanda vya nondo.. Si mnajua nondo bila carbon ukiipinda inakatika?
4. Gesi kwa matumizi ya kupikia nk

Hayo ndio maajabu na utajiri uliojificha kwenye tairi mbovu


Good morning Tanganyika
Kuna hesabu haijakaa sawa au maelezo hayajitoshelezi.

Umepigia hesabu ya msingi ambayo ni tani moja ya matairi chakavu, sasa inakuwaje kila kipengele cha production inayozalishwa kwenye separation iwe na uzito wa tani?

Yaani tani moja ya malighafi ya matairi chakavu izalishe takribani tani tano za reproduction?
 
Kuna hesabu haijakaa sawa au maelezo hayajitoshelezi.

Umepigia hesabu ya msingi ambayo ni tani moja ya matairi chakavu, sasa inakuwaje kila kipengele cha production inayozalishwa kwenye separation iwe na uzito wa tani?

Yaani tani moja ya malighafi ya matairi chakavu izalishe takribani tani tano za reproduction?
Soma tena kwa makini.. Kamwe tani moja haiwezi kutoa tani nane
 
Ukitoka hapo unapeleka tairi zako kiwanda ni na kwenda kuuza kwa kilo.. Tairi 20 zinazotengeneza tani moja utauza kwa bei ya chini kabisa Shilingi laki 2, kumbuka kule ulishapata laki 1 ya mipira na hiyo laki mbili ni yako yote usafiri ni malipo mengine
Tairi moja ina uzito wa kilo 50?
 
Back
Top Bottom