Maajabu ya Tanzania, siasa halali za vyama vya upinzani kuhesabika kama uhalifu wa makosa ya jinai!

Maajabu ya Tanzania, siasa halali za vyama vya upinzani kuhesabika kama uhalifu wa makosa ya jinai!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) inasomeka hivi " Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakuwa nchi ya kidemokrasia na ya mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu

Katika mazingira hayo vyama vya upinzani vinapaswa kutoa "constructive criticism" ambavyo ndivyo vifanyavyo vyama hivyo, hususani chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema na kwa mujibu wa Katiba ya nchi, tulitegemea chama tawala cha CCM kijibu hoja hizo kwenye majukwaa ya kisiasa

Hali ni tofauti sana, hususani kwenye utawala huu wa awamu ya tano chini ya Rais Magufuli, ambapo wanachukulia wao kuwa "constructive criticism" kuwa ni makosa ya jinai, ambapo Jeshi la Polisi nchini "linaagizwa" liwakamate na kuwafungulia mashitaka ya uchochezi, kukosa uzalendo, usaliti na kutumiwa na mabeberu!

Kwa mazingira ya sasa, Jeshi la Polisi nchini linafanya kazi kwa "maagizo" ya watawala wa CCM na hivyo kufanya Jeshi hilo kuwa kama kitengo cha CCM!

Niwakumbushe wosia muhimu sana uliowahi tolewa na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete, kwenye mkutano mkuu wa CCM, mwaka 2012, huko Dodoma, alipowatahadharisha wanaccm wenzake, kuwa ni makosa makubwa sana kulitegemea Jeshi la Polisi nchini, kuwalinda na kuwabakiza madarakani, kwa kuwa chama cha siasa kama CCM wajibu wake mkubwa ni kuzijibu hoja zinazotolewa na wapinzani kwenye majukwaa ya kisiasa

Niwaambie tu wanaccm, kwa kuwa mmepuuza wosia huo muhimu sana uliotolewa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete, basi niwatabirie kuwa anguko lenu litakuwa kubwa na lenye kishindo kikubwa sana!
 
Watawala wanataka nchi hii yote tujiunge na "Praise and worship team for Magufuli"

Kinyume cha Katiba ya nchi ambayo inaruhusu uwepo wa vyama vingi, ambapo kufanya "constructive criticism" ni wajibu wa vyama vya upinzani
 
Anglau mzee mkuchika anajaribu kuwakumbusha polisi wajibu wao, amesema polisi wakipewa maagizo ambayo ni unlawful waombe kuandikiwa na hao wakuu wa wilaya au mikoa wakitaja sababu ili siku likibuma wao wawe wamejisafisha. Polisi wakifuata maagizo ya waziri wa utawala bora tutaenda vizuri anglau. Kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria nchini mpaka inataia kinyaa.
 
Kwa sasa CCM ina survive kwa nguvu ya polis na TISS. Sijui polis wanafaidika nini . ila kwa TISS wanafaidika sana na mfumo uliopo
 
Kwa sasa CCM ina survive kwa nguvu ya polis na TISS. Sijui polis wanafaidika nini . ila kwa TISS wanafaidika sana na mfumo uliopo
Police department Ni wajinga na wengi wao Ni watu wenye ufaulu hafifu au waliofeli au waliosoma kwa kuungaunga. Sasa mtu Kama huyo unategemea atafanya nini. Bora mgambo wanajitambua kuliko police

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye serikali hii ukiwa upinzani wewe unaaonekana ni zaidi ya shetani lucifer
 
Back
Top Bottom