Uchaguzi 2020 Maalim Seif anapodai "Mamlaka Kamili" anamaanisha kuvunja Muungano?

Uchaguzi 2020 Maalim Seif anapodai "Mamlaka Kamili" anamaanisha kuvunja Muungano?

KalamuTena

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2018
Posts
13,187
Reaction score
17,167
Maana yake nini?

Kama nchi iko kwenye muungano na nchi nyingine, inaweza kudai kuwa na "mamlaka kamili" bila kuathiri muunganio huo?

Maalim, mgombea urais wa Zanzibar anapodai kuwa na mamlaka kamili, ana maana lengo lake ni kuuvunja muungano?

Akichaguliwa atachukua hatua zipi kuuvunja muungano.

Je, CHADEMA wana maoni gani kuhusu jambo hili? Na huko mbeleni, kama sera yao ya "Majimbo" itakuwa imetekelezwa endapo watapata ushindi, itakuwa halali kwa jimbo fulani kujichukulia "Mamlaka Kamili", kuachana na majimbo mengine?

Ni nini ushiriki wa wananchi katika uamzi wa kuuvunja au kutouvunja muungano, au inatosha tu kwa Maalim kuchaguliwa kwa sera hiyo kuchukua uamzi wa kuuondoa Muungano?

Maalim Seif anaifanya kazi ya Tundu Lissu kuwa ngumu zaidi wakati huu wa kampeni.
 
Majimbo hayawezi kujitangazia uhuru / kujitangaza kuwa dola kwasababu yameundwa kutoka ktk Tanzania Bara / Tanganyika.

Zanzibar inaweza kujitoa ktk muungano kwasababu kabla ya 1964 walikuwa nchi / dola kamili.

Msimamo wa Chadema ni muungano wa serikali 3 kama zilivyopendekezwa ktk rasimu ya Jaji Joseph Sinde Warioba.
 
Seif anawahadaa wapambe wake kwani ili kuvunja muungano inabidi ipatikane theruthi mbili ya bara na mbili ya Zanzibar wakati Zanzibar wagombea wake 15 wameshaenguliwa ni wazi hatazipata.

Wapemba wengi wamewekeza bara ikiwamo na yeye mwenyewe ana nyumba bara hivi unafikiri ni wajinga wamruhusu avunje muungano maana kitakachofuata kila mtu arudi kwao
 
Matatizo ya ujuaji wa viongozi wa ccm , badala ya muungano kuwa wa wananchi wenyewe , wao viongozi ndio wakaungana , sasa walichokipanda si ndio wanachovuna huelewi nini?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Seif anawahadaa wapambe wake kwani ili kuvunja muungano inabidi ipatikane theruthi mbili ya bara na mbili ya Zanzibar wakati Zanzibar wagombea wake 15 wameshaenguliwa ni wazi hatazipata.
Wapemba wengi wamewekeza bara ikiwamo na yeye mwenyewe ana nyumba bara hivi unafikiri ni wajinga wamruhusu avunje muungano maana kitakachofuata kila mtu arudi kwao

..hapo ni kama wakiamua kufuata taratibu.

..wanaweza kulazimisha kuuvunja bila kufuata taratibu.

..hata wakiuvunja siyo rahisi kuwalazimisha Wazanzibari waliohamia Tanganyika warudi kwao.

..hakuna Mtanganyika mwenye akili timamu anaweza kumfukuza Bakhresa.

..lakini pia Watanganyika wamechoka kuwabeba CCM-Znz kila uchaguzi.

..Ni afadhali tuwe na mfumo ambao Watanganyika hatutalazimika, kila miaka mitano, kuwasaidia CCM kuiba uchaguzi.
 
Seif anawahadaa wapambe wake kwani ili kuvunja muungano inabidi ipatikane theruthi mbili ya bara na mbili ya Zanzibar wakati Zanzibar wagombea wake 15 wameshaenguliwa ni wazi hatazipata.
Wapemba wengi wamewekeza bara ikiwamo na yeye mwenyewe ana nyumba bara hivi unafikiri ni wajinga wamruhusu avunje muungano maana kitakachofuata kila mtu arudi kwao
Wakenya wengi /kampuni za kikenya nyingi wamewekeza/zimewekeza Tanzania , kwani tuna muungano nao?
 
Wananchi wa Zanzibar wangepewa nafasi ya kupiga kura za maoni kama wanataka huu muungano ikiwa hawautaki basi na uvunjwe tu.

Hakuna sababu ya kuwa na ndoa ambayo mwenzako haoni sababu.
 
..hapo ni kama wakiamua kufuata taratibu.

..wanaweza kulazimisha kuuvunja bila kufuata taratibu.

..hata wakiuvunja siyo rahisi kuwalazimisha Wazanzibari waliohamia Tanganyika warudi kwao.

..hakuna Mtanganyika mwenye akili timamu anaweza kumfukuza Bakhresa.

..lakini pia Watanganyika wamechoka kuwabeba CCM-Znz kila uchaguzi.

..Ni afadhali tuwe na mfumo ambao Watanganyika hatutalazimika, kila miaka mitano, kuwasaidia CCM kuiba uchaguzi.
Bila muungano mzanzibari ataishi Tanganyika kwa vibali sawa na wageni wengine toka mataifa ya nje. Natamani sana hilo litokee.
 
..hapo ni kama wakiamua kufuata taratibu.

..wanaweza kulazimisha kuuvunja bila kufuata taratibu.

..hata wakiuvunja siyo rahisi kuwalazimisha Wazanzibari waliohamia Tanganyika warudi kwao.

..hakuna Mtanganyika mwenye akili timamu anaweza kumfukuza Bakhresa.

..lakini pia Watanganyika wamechoka kuwabeba CCM-Znz kila uchaguzi.

..Ni afadhali tuwe na mfumo ambao Watanganyika hatutalazimika, kila miaka mitano, kuwasaidia CCM kuiba uchaguzi.
Akilazimisha anafunguliwa kesi ya uhaini hata yeye anajua.
Muungano ukivunjika na faida zake zinavunjika bakhresa atabaki kama mwekezaji, wapemba aliowaajili watapunguzwa na wanaobaki itabidi walipiwe work permit na resident permit atakosa faida nyingi sana ndio utambue nani anafaidika na muungano
 
Maana yake nini?

Kama nchi iko kwenye muungano na nchi nyingine, inaweza kudai kuwa na "mamlaka kamili" bila kuathiri muunganio huo?

Maalim, mgombea urais wa Zanzibar anapodai kuwa na mamlaka kamili, ana maana lengo lake ni kuuvunja muungano?

Akichaguliwa atachukua hatua zipi kuuvunja muungano.

Je, CHADEMA wana maoni gani kuhusu jambo hili? Na huko mbeleni, kama sera yao ya "Majimbo" itakuwa imetekelezwa endapo watapata ushindi, itakuwa halali kwa jimbo fulani kujichukulia "Mamlaka Kamili", kuachana na majimbo mengine?

Ni nini ushiriki wa wananchi katika uamzi wa kuuvunja au kutouvunja muungano, au inatosha tu kwa Maalim kuchaguliwa kwa sera hiyo kuchukua uamzi wa kuuondoa Muungano?

Maalim Seif anaifanya kazi ya Tundu Lissu kuwa ngumu zaidi wakati huu wa kampeni.
Chadema na maalim seif wote wanasema
Muungano ni jambo la hiari wananchi Ndio waamue muungano gani wanaoutaka
 
Na si CHADEMA na Maalim tu, hata huyo Mwasisi wa Muungano alishawahi kusema " Muungano ni kama koti, likikubana unalivua"
 
Tunataka Zanzibar huru yenye mamlaka kamili. Zanzibar ni nchi yenye watu wake, mipaka yake na sheria zake kabla hata huu muungano haujatengenezwa.

Muungano ni koti tu, tukilichoka tunaweza kulivua. Tusilazimishwe kile ambacho hatukitaki.
 
Seif anawahadaa wapambe wake kwani ili kuvunja muungano inabidi ipatikane theruthi mbili ya bara na mbili ya Zanzibar wakati Zanzibar wagombea wake 15 wameshaenguliwa ni wazi hatazipata.
Wapemba wengi wamewekeza bara ikiwamo na yeye mwenyewe ana nyumba bara hivi unafikiri ni wajinga wamruhusu avunje muungano maana kitakachofuata kila mtu arudi kwao

Bakhresa ana viwanda Kenya , Uganda , Zimbabwe na nchi nyengine za kiafrika mbona hatusikii kuhusu mambo ya Muungano ??

Kuwa na mali nchi nyengine sio kigezo cha kulazimisha watu waungane.

Huu muungano wetu si muungano ni Uvamizi wa Laanatullahi Nyerere aliouita muungano.
 
Back
Top Bottom