Maamuzi Magumu: Nimeamua kuwa baba wa mtoto wa rafiki yangu

Maamuzi Magumu: Nimeamua kuwa baba wa mtoto wa rafiki yangu

***********************
Nikasepa zangu mkoani kikazi. Siku napokea simu toka kwa Mama kijacho,alinielezea "Kibuyu hongera umepata mtoto wa kiume." Nilifurah sna si kwa kauli yake ya kunimilikisha mtoto, bali kwa kuwa sehemu ya uhai wa huyo mtoto.
Baada ya saa 24 akaruhusiwa kutoka Amana hospitali.

Mwajuma akawa ananiambia rafiki zake wanataka kujua jina la mtoto, kwahiyo nichague jina nimpe mtoto. Nilimwambia awape nafasi wazazi wampe jina mjukuu wao. Akasema nitoe Mimi baba. Ukatokea mvutano wa kijinga, sikuwa tayar kumpa mtoto jina. Mimi n mkristo wao n waislamu.
Nilikuwa na sababu, daima sipend unafiki. Kwani nilijua lazima mtoto atapewa jina lingine tu. Kuepusha hilo sikutoa jina.

Kesho yake jioni mwajuma alinipigia akiniambia mama ake anataka kuongea nami. Nikaona mambo yameanza; nikamwambia kwasasa nipo kwenye kelele anipe dakika kumi ntawapigia. Nikamuuliza mama ulimwambia ukweli kuwa Mimi siye?? Alisema hajamwambia. Sikutaka kukuza mada nikanyamaza tu.

Mama alichoniambia ni kunishukuru kwa kumjali mwenzangu, "ila familia inakuomba ukirudi uje nyumbani tuzungumze. Yaliyopita yamepita mwanangu, kwani tumeshakuwa ndugu. Hongera sana baba kwa kupata mtoto wa kiume mwenye afya!"
Nikaitikia "Asante sana mama, nawe hongera kwa kupata mume."
Akacheka kisha akasema haya ongea na mwenzio. Akampa simu mwajuma.
Tukaongea kidogo tu.

*****************
Mwajuma alinisumbua wiki kuhus jina la mtoto nami nikagoma kutoa jina. Akampa jina Hamadi. Binafsi mpaka hapo sikuwa na wazo kuendelea nae huyo binti; mkataba wetu akishajifungua mwisho.

Ikafika karibia na 40,akaniambia anataka kumfanyia kisomo mtoto kwani anamtoa nje. Nikamuuliza anataka nifanyaje? Akaniambia anahitaji pesa. Nikamwambia afanye budget ndogo anipe. Kesho yake jioni akanipa budget. Nikamtumia pesa. Nikamuomba Shem akanunue nguo na bag la mtoto nikamtumia pesa. Maana Shem wangu tulielewana sana.

40 ikafana kwa kila lililopangwa. Nikapigiwa simu na kupewa shoga zake wote waliokuwepo niongee nao. Shem nae akanipigia akinipongeza kumsaidia mwajuma.

Baada ya kurudi nikaletewa mtoto nimuone. Alikuwa mtoto mzuri mwenye afya njema. Nilifurahi sana hasa mtoto aliponifurahia.
Nikamwambia kesho nakuja kwenu. Akafurahi sana. Ila nikamwambia nitasema ukweli tu. Nikamuona amekuwa kimya.

Kesho yake nikajiandaa kwenda kwa wakwe nikiwa na rafiki zangu wawili na bro na mkewe.

Itaendelea.........
Inaendelea lini chief
kibuyu180
 
Anakuja kuwa mke wa pili? Au una mwanamke na weye kakuboa sana?

Natumaini uneishajenga pia kabla ya kumjengea mtoto
 
Huwezi kujimilikisha damu ya mtu mwingine kirahisi hivyo. Provided alishamtaarifu mzazi mwenzie kuhusu mimba basi wewe hauna chako hapo. Mtoto akizaliwa jamaa lazima aje amuone mtoto wake na pia kama ni damu yake ataclaim mtoto wake kama baba hapo baadae.

Umefikiria kirahisi sana kwa kuomba tu jina la mtoto apewe la kwako ila hiyo sio tiketi ya wewe kuwa baba kwa hali yoyote. Mie nadhani labda ungemuoa huyo dada ili uwe at least baba wa kambo laikini si kwa style uliyotumia.

Njia za kuasili mtoto kwa nchi yetu ni ngumu sana sio mizaha mizaha kama hii unayoifanya.
Hivi kwa nini binadamu tunakuwa wagumu sana kuelewa?
 
Back
Top Bottom