Maamuzi Magumu: Nimeamua kuwa baba wa mtoto wa rafiki yangu

Maamuzi Magumu: Nimeamua kuwa baba wa mtoto wa rafiki yangu

Kumbuka inaelekea ni wewe ndiye uliyonekana kuwa front katika kubeba huo mzigo maana yeye alishakupotezea ukawa unamtafuta..

Dunia haipo kama jinsi uionavyo hizo jitihada za wewe kumtafuta believe me ni nguvu za kukuaribia future yako kupitia huyo mama...

Trust me scenario za hivi huwa zina bitter end.

Kusaidia MTU ni jambo jema tena sana but take extra precaution namna unavyoenda kuhandle hii issue. All the best
Mleta mada yupo sahihi maana kwa sasa anawaza kwa kutumia kichwa cha juu , which is good😁😁, tusubiri akianza kuwaza kwa kutumia kichwa kidogo.atarudi hapa home sweet home Jf kwa ushauri mwingine😁😁😁😁
 
Mleta mada yupo sahihi maana kwa sasa anawaza kwa kutumia kichwa cha juu , which is good[emoji16][emoji16], tusubiri akianza kuwaza kwa kutumia kichwa kidogo.atarudi hapa home sweet home Jf kwa ushauri mwingine[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sijawahi kufikiri kuwa hata wewe mchokozi na mtundu kiaina
 
Haya mambo nchi za wenzetu ni ya kawaida sana tatizo huku shit hole tunaona ya ajabu kwasababu ya roho mbaya.
Usemayo ni kweli, kuna mzee mmoja Danish alioa single parent tena mkurya toka Tz alikuwa masomoni huyo Madanish akamwambia tulee mtoto wako tusizae na hadi leo wanazeeka pamoja
 
Ma single. Maza wengi diniani wanasumbuliwa na nyumbani za kupanga. Mi staki umpe upendo kiviiiile, maana una wengi wa kuwapenda ikiwemo familiya yako na mama yako,na wengine wajao, Hata ukikutana ma Mimi leo huyo mbona utamsahau![emoji16] kabla hilo halijatokea wewe MPE nyumbani tu Mungu atakubariki.

Maisha ya usingle mother ni kama kamali, naona umejitoa hadi raha, lakini nature ya usingle mother unaweza ifunye hiyo furaha ulopanga kutoweka, mtoto akizaliwa huwa ni mtamu, baba yake lazima aanze uchokozi, weekend ukiwa kwa mkeo, huyo Dada akakupigia hupokei,unaogopa kuharibu kwa mkeo, Dada mchepuko anapata upweke na hasira, Mara SMS ya mzazi mwenzie inaingia " najua unanichukia ila mm nakupenda, Mke wangu ndo kikwazo, plz njoo umchukulie mtoto matumizi, plz Niko chini ya figo zako"[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji2]
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Eti???
Nisimpende hivyo???
Kwa kifupi ninayemhurumia ni yule aliyekataliwa.
Sioni nafasi ya upendo wetu kuendelea zaidi ya heshima na urafiki wa kawaida.
Sikusudii kumfanya kuwa karibu yangu zaidi ya kumpa sapoti ndogo ndogo wakati huu mgumu kwake.
Ninajua thamani ya mtu kukukali ngaa kidogo wakati wa mapito yako magumu.
Ni hivyo tu Lucky
 
***********************
Nikasepa zangu mkoani kikazi. Siku napokea simu toka kwa Mama kijacho,alinielezea "Kibuyu hongera umepata mtoto wa kiume." Nilifurah sna si kwa kauli yake ya kunimilikisha mtoto, bali kwa kuwa sehemu ya uhai wa huyo mtoto.
Baada ya saa 24 akaruhusiwa kutoka Amana hospitali.

Mwajuma akawa ananiambia rafiki zake wanataka kujua jina la mtoto, kwahiyo nichague jina nimpe mtoto. Nilimwambia awape nafasi wazazi wampe jina mjukuu wao. Akasema nitoe Mimi baba. Ukatokea mvutano wa kijinga, sikuwa tayar kumpa mtoto jina. Mimi n mkristo wao n waislamu.
Nilikuwa na sababu, daima sipend unafiki. Kwani nilijua lazima mtoto atapewa jina lingine tu. Kuepusha hilo sikutoa jina.

Kesho yake jioni mwajuma alinipigia akiniambia mama ake anataka kuongea nami. Nikaona mambo yameanza; nikamwambia kwasasa nipo kwenye kelele anipe dakika kumi ntawapigia. Nikamuuliza mama ulimwambia ukweli kuwa Mimi siye?? Alisema hajamwambia. Sikutaka kukuza mada nikanyamaza tu.

Mama alichoniambia ni kunishukuru kwa kumjali mwenzangu, "ila familia inakuomba ukirudi uje nyumbani tuzungumze. Yaliyopita yamepita mwanangu, kwani tumeshakuwa ndugu. Hongera sana baba kwa kupata mtoto wa kiume mwenye afya!"
Nikaitikia "Asante sana mama, nawe hongera kwa kupata mume."
Akacheka kisha akasema haya ongea na mwenzio. Akampa simu mwajuma.
Tukaongea kidogo tu.

*****************
Mwajuma alinisumbua wiki kuhus jina la mtoto nami nikagoma kutoa jina. Akampa jina Hamadi. Binafsi mpaka hapo sikuwa na wazo kuendelea nae huyo binti; mkataba wetu akishajifungua mwisho.

Ikafika karibia na 40,akaniambia anataka kumfanyia kisomo mtoto kwani anamtoa nje. Nikamuuliza anataka nifanyaje? Akaniambia anahitaji pesa. Nikamwambia afanye budget ndogo anipe. Kesho yake jioni akanipa budget. Nikamtumia pesa. Nikamuomba Shem akanunue nguo na bag la mtoto nikamtumia pesa. Maana Shem wangu tulielewana sana.

40 ikafana kwa kila lililopangwa. Nikapigiwa simu na kupewa shoga zake wote waliokuwepo niongee nao. Shem nae akanipigia akinipongeza kumsaidia mwajuma.

Baada ya kurudi nikaletewa mtoto nimuone. Alikuwa mtoto mzuri mwenye afya njema. Nilifurahi sana hasa mtoto aliponifurahia.
Nikamwambia kesho nakuja kwenu. Akafurahi sana. Ila nikamwambia nitasema ukweli tu. Nikamuona amekuwa kimya.

Kesho yake nikajiandaa kwenda kwa wakwe nikiwa na rafiki zangu wawili na bro na mkewe.

Itaendelea.........
 
Kwanini usiangalie uwezekano wa kumuoa? Unataka apate njemba mwingine amnyanyase kisha nawe uanze tena kukosa raha mama wa mwanao ananyanyasika?
Mkuu kuoana hakuhitaji huruma wala fadhila, ni upendo wa dhati katka hali zote.
 
NI MAAMUZI MAGUMU LAKINI YAMETOKA MOYONI

Wapendwa wana jukwa hili la mahusiano, mapenzi na urafiki ninawasalimu nyote.

Kama habari ya awali inavyosemaka kuwa nimechukua uamuzi mgumu wa kuwa baba mtarajiwa wa mtoto mtarajiwa wa rafiki yangu kwa hiyari na kwa kupenda mwenyewe kwa sababu nitakazo zieleza hapa chini, lakini kabla ya hizo sababu naomba nitoe ufafanuzi wa urafiki wetu.

Kuna dada mmoja tulikutana ofisi flani ya serikali, ni dada flani mpole kiasi na mcheshi kiaina. Kwa muda mfupi sana nilivutiwa naye na ikafikia hatua ya kubadilishana naye namba za simu.

Zoezi la huduma lilienda vyema kwa yeye kufanya koneksheni na mtumishi flani na tukafanikiwa kupata hiyo huduma (pass ya kusafiria kwa haraka)

Baada ya hapo hatukuwasiliana haraka japo nilipanga lazima nimtafute. Ulifika wakati tukaanza kuwasiliana hapa na pale. Na ukafika wakati nikawa nachomekea viutani kuwa ninamhitaji awe rafiki yangu.

Baada ya muda mrefu tulifanikiwa kuwa marafiki hatimaye tukaanza kushirikiana....hapa wakubwa mmeelewa. Jambo nililompenda zaidi ni mwelewa na mwenye misimamo yake mizuri. Tuliwekana wazi kuhusu mahusiano yetu, kwake yeye mpenzi wake alikuwa ni raia wa kigeni na anaishi huko kwao huja mara chache hivyo alikuwa anajiandaa kwenda kumtembelea na walikuwa wamepanga kuoana.

Nini kilitokea kati yao?

Uliwadia wakati wa kusafiri alinijulisha nami nilimpa nafasi ya kuwa mbali naye kimawasiliano ili ajiweke sawa na akili yake iwaze juu ya mpenzi wake. Alifanikiwa kwenda na kurudi. Baada ya kurudi mawasiliano yetu yalikuwa hafifu kwani nilikuwa tight sana na kazi.


Baada ya miezi kama mitatu na nusu, tuliwasiliana na kupiga stori nyingi na mwishowe akanijulisha ni mjamzito. Nikampa hongera zake. Lakini mawasiliano yakazidi kuwa hafifu zaidi. Ukafika wakati nikamuuliza maendeleo na mipango ya ndoa na kama wamepanga lini wataanza kuishi pamoja?

JIBU LAKE NDILO HASA LILINIGUSA NA KUAMUA HAYA
Rafiki yangu huyu alinishtua aliponieleza kuwa walitengana na yule mchumba kwani walipokutana ughaibuni alimfanyia visa vingi vibaya mno..sitavitaja

Na alipotua nchini alimtumia ujumbe kuwa asimtafute tena. Akiwa katika hali ya kutafakari yaliyompata na jinsi gani atasonga mbele...ndipo alianza mahusiano na jamaa flani aliyeanza kumnyemelea kitambo na muda mfupi akapata ujauzito.

Baada ya kupata ujauzito alimjulisha mhusika lakini hakuwa tayari kuukubali bali alimwambia autoe kwani yeye anafamilia lakini aligoma kuutoa na akajiapiza ataulea na kwa vile jamaa ameukataa hata jina litakuwa la upande wa familia yake yaani ubini wa baba.

Habari hii iliniumiza sana na niliwaza haya yafuatayo;
1. Kuwa huyu dada ataishi kwa sonono kubwa wakati wa ujauzito na atamwathiri mtoto akiwa tumboni wazazi wanajua hili

2. Huyu atakayezaliwa hatakuwa na upendo katika jamii na anaweza kuja kuwa na tabia ya ajabu

MAAMUZI YANGU
1. Nikamwomba kama naweza kuwa baba wa wa hiyari na apewe ubini wa jina langu kama baba alikubali hili kwa mshangao mkubwa sana (Haya[emoji116]sijamshirikisha)

2. Nitamhudumia kipindi chote cha ujauzito

3. Nitamfanya mwenye furaha ili kulinda afya mama na ya mtoto atakaye zaliwa

4. Baada ya mtoto kukua yeye yuko huru kuwa na maisha yake bila mimi kumwingilia uhuru wake

5. Nitampa mtoto kiwanja na kumjengea kadri Mungu atakaponiweka hai na kunibariki, ili apate malazi na malezi bora.

Uamuzi huu nimeufanya mwenyewe japo sipangi kuishi na mtoto isipokuwa kumsapoti kimalezi tu.

Baada ya kukubaliana naye hasa kuhusu mtoto kuitwa kwa jina langu kama baba, alifurahi sana kiasi cha kulia machozi na nikamwahidi kuwa siku chache zijazo atakuja mkoa nilipo apate mapumziko ya muda mfupi sio nyumbani kwangu lakini. Amemweleza mama yake mzazi na hajaamini kuwa kuna mtu anaweza kufanya maamuzi magumu kiasi hiki.

Pamoja na hayo sijamweleza kwa undani namna nilivyojipanga kumsapoti mtoto hasa kumpa eneo na kumjengea, hili nimebaki nalo nikiomba Mungu aniwezeshe kulitimiza.

Wapendwa wana jf, inaweza kuonekana kuwa uamuzi wangu ni wa kijinga sana lakini kwangu mimi nitaona fahari kubwa kama hili litafaniniwa kwani;

Sisi wanaume tunapaswa kuwa chemichemi ya furaha ya wake zetu, mama, watoto na dada zetu lakini kinyume chake tumekuwa ni chanzo cha machozi.

Tujitahidi sana kuwafanya watu kuwa na furaha badala ya machozi. Muwe na wakati mwema wote.
We jamaa una akili sana, na una upendo sana, Mungu akubariki sana kwa utashi huo, mimi naamini ukifanya hivyo Mungu atakupa zaidi, cha kukusisitiza usimshirikishe kila kitu, hivyo ambavyo vipo moyoni viweke moyoni sio lazima kila kitu umwambie, msome tabia huyo mdada, all in all hongera sana.
 
We jamaa una akili sana, na una upendo sana, Mungu akubariki sana kwa utashi huo, mimi naamini ukifanya hivyo Mungu atakupa zaidi, cha kukusisitiza usimshirikishe kila kitu, hivyo ambavyo vipo moyoni viweke moyoni sio lazima kila kitu umwambie, msome tabia huyo mdada, all in all hongera sana.
Naogopa sana kuahidi kwani mimi ni binadamu.
Kitu ambacho kipo tayari ni kiwanja nacho sitamwambia hadi kila kitu kimekaa sawa na nitafanya kisheria.
Asante
 
Wazazi wako unawasaidia kweli? Una matatizo sio bure.
Tusilinganishe hizi hoja na kuwalinganisha wazazi wako na wachumba tunaokutana nao,

Wazazi wako ni watu muhimu sana hapa duniani sio wakulinganishwa tu unavyojisikia, wana heshima yao aiku zote za maisha yetu mpaka kifo
 
Mkuu sijawahi kuwaza ku fake jambo nyeti kama hili.
Hii ni habari ya kweli na maamuzi haya yana siku 3.
Najua ni magumu hadi najishangaa lakini sitarudi nyuma kwani nilifanya kwa msukumo wa ndani ya moyo

Pamoja na unafanya kitu cha kiungwana sana, na moyo wako umerizia basi we fanya na jitoww kwa moyo mmoja, ila sasa pia usifanye kwa matakwa ya mapenzi ya mwanadada, baadae ukaja jutia sana, nenda taratibu na kwa umakini sana, wanawake wana siri kubwa sana huwezi juwa yeye anakuwazia nini?
 
Pamoja na unafanya kitu cha kiungwana sana, na moyo wako umerizia basi we fanya na jitoww kwa moyo mmoja, ila sasa pia usifanye kwa matakwa ya mapenzi ya mwanadada, baadae ukaja jutia sana, nenda taratibu na kwa umakini sana, wanawake wana siri kubwa sana huwezi juwa yeye anakuwazia nini?
Nitazingatia jirani, asante
 
Umefanya jambo jema lakini fahamu mtoto akikua na kupata ufahamu atamtafuta baba yake halisi!
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Eti???
Nisimpende hivyo???
Kwa kifupi ninayemhurumia ni yule aliyekataliwa.
Sioni nafasi ya upendo wetu kuendelea zaidi ya heshima na urafiki wa kawaida.
Sikusudii kumfanya kuwa karibu yangu zaidi ya kumpa sapoti ndogo ndogo wakati huu mgumu kwake.
Ninajua thamani ya mtu kukukali ngaa kidogo wakati wa mapito yako magumu.
Ni hivyo tu Lucky
Tukipata mwingine aliyekataliwa tukujulishe au wametosha mkuu
 
Itakuwa vizuri amtafute babake lakini alishapata malezi bora
Jirani watu hawana utu tena ndiyo maana wanashanga mbona unawezaje hili, ila mimi natambua unaweza kwa kuwa unalifanya kutoka moyoni, na nina uhakika unafanya kwa mapenzi ya dhati kabisa ya mtoto na maa yake, mambo ya a good Samaritan hayo..
 
Back
Top Bottom