Maamuzi ya Hayati Magufuli yaigharimu Tanzania zaidi ya Bilioni 266

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Hivi karibuni, Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji, ambayo ni sehemu ya Benki ya Dunia, imefunga usuluhishi dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tume hiyo imetoa adhabu yake, ikiamuru Tanzania kulipa fidia ya zaidi ya Dola za Marekani Milioni 109.5 sawa na takribani bilioni 266 za kitanzania (ikiwa ni pamoja na limbikizo la riba) kwa wadai. Adhabu hii inahusu madai ya uharibifu kutokana na kunyang'anywa kwa mradi wa Nikeli wa Ntaka Hill kwa njia isiyo halali.

Indiana Resources Limited (ASX: IDA), ambayo ni mmiliki mkuu wa kampuni za Ntaka Nickel Holdings Ltd, Nachingwea UK Ltd, na Nachingwea Nickel Ltd, ambao kwa Pamoja ni "wadai", katika mgogoro huu, imetoa sasisho kuhusu tukio hili. Kwamba Indiana ndiye msimamizi wa miradi tajwa hapo juu ambayo shughuli zake ndio kiini cha mgogoro huu dhidi ya Tanzania.

Adhabu hiyo imetolewa baada ya jopo la usuluhishi kubaini kuwa Tanzania ilinyang'anya mradi huo kinyume cha sheria mnamo tarehe 10 Januari 2018, na hivyo kukiuka Mkataba wa Uwekezaji wa Kimataifa kati ya Uingereza na Tanzania. Hivyo basi, Tanzania imeamriwa kulipa fidia pamoja na hasara zingine, ikiwemo na malimbikizo ya riba kwa kiwango cha 2%. Riba hii ni juu ya kiwango cha msingi cha Dola za Marekani kuanzia tarehe ya kunyang'anywa miradi hadi tarehe ya malipo.

Katika maamuzi yake, Tume hii imeamua kuibebesha Tanzania gharama za usuluhishi, ikiwa ni pamoja na ada na gharama za Tume. Aidha, Tanzania imeamriwa pia kulipa gharama walizoingia wadai katika usuluhishi huo.

Katika taarifa yake kupitia mwenyekiti mtendaji ndugu Bronwyn Barnes, Indiana Resources Limited imeeleza furaha yake juu ya maamuzi haya. Imesisitiza kuwa kiasi cha adhabu kinathibitisha uwekezaji mkubwa ambao umepotea kutokana na kunyang'anywa kwa mradi huo na amewashukuru wanahisa ambao wamemsaidia katika kipindi chote cha usuluhishi.

Indiana sasa inakusudia kuanza mchakato wa kukazia hukumu hiyo. Ni muhimu kutambua kuwa Mkataba wa Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji umepitishwa na nchi wanachama 158 wa Benki ya Dunia, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Hii inamaanisha kuwa adhabu yoyote iliyotolewa na tume hiyo inaweza kutekelezwa katika nchi hizo kama uamuzi wa mahakama zao wenyewe.

Kwa upande wake, Bronwyn Barnes ameahidi kuendelea kuwajulisha wanahisa kadri mchakato wa utekelezaji unavyoendelea.

Historia ya madai haya inaanzia tarehe 21 Aprili 2015, ambapo Tanzania ilitoa Leseni ya Kuhifadhi kwa Mradi huo. Hata hivyo, mnamo Julai 2017, Serikali ya Tanzania ilibadilisha Sheria ya Madini ya 2010 na kuondoa daraja la Leseni ya Kuhifadhi bila kutoa mbadala wake.

Kufikia tarehe 10 Januari 2018, Tanzania ilichapisha kanuni mpya za madini, zilizoweka bayana kuwa leseni za kuhifadhi hazitakuwepo tena na haki zote zilirejeshwa kwa Serikali. Indiana Resources Limited ilishiriki katika majadiliano na Serikali ya Tanzania kuanzia Januari 2018 hadi Desemba 2019, kujaribu kutatua suala la umiliki wa mradi huo. Hata hivyo, jitihada hizo hazikuzaa matunda na Serikali ya Tanzania ilifanya tangazo la mwaliko wa umma kwa zabuni ya pamoja kwa maendeleo ya maeneo yaliyokuwa chini ya leseni za kuhifadhi.

Maamuzi haya ya Tume ya usuluhishi ni muhimu sana sio tu kwa Indiana Resources Limited, bali pia Kwa nchi wanachama wa Tume na wawekezaji Kwa ujumla. Uamuzi huu unakumbusha umuhimu wa kulinda na kuheshimu mikataba ya uwekezaji. Pia inatupa ni fundisho kuhusu jukumu letu la kuhakikisha kuwa haki za wawekezaji zinalindwa na kwamba serikali zinaheshimu mikataba iliyosainiwa.

Hii pia inatoa fursa kwa nchi yetu, Tanzania, kutathmini upya sera zake za uwekezaji na kuhakikisha kwamba inashirikiana vizuri na wawekezaji ili kuleta maendeleo endelevu ya uchumi wetu na kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

Pia soma: Tanzania yashindwa kwenye kesi, yaamuriwa kulipa fidia ya zaidi ya Tsh. Bilioni 260
 
Maamuzi ya kijasiri ya Magufuli wacha yaigharimu nchi hayo mapesa, hatuwezi kukaa na mikataba ya hovyo yenye unyonyaji kwa taifa, huku walafi wachache walioingia wakifaidi 10% halafu nije kumlaumu Magufuli aliyeivunja, Never.

Wacha tudaiwe lakini heshima yetu iwepo, mbona deni la taifa lenyewe kila siku linaongezeka, tumeshazoea kuishi kwa madeni, wacha ibaki hivyo.

Kwangu Magufuli kwenye hili ni genius, naamini iko siku, hata huu wa Samia na DPW yake nao utavunjwa, wakati huo Samia akiwa amelala kaburini na laana.
 


Kawaida ya ccm
 
Huna akili
 
Wakulaumiwa ni Kikwete aliyeingia mikataba ya kipuuzi. Kama ambavyo tutamlaumu Samia kwa mikataba yake ya Dubai.

Magufuli alifanya kilichotakiwa kufanyika ili kuinusuru nchi. Akaleta na sheria mpya ya kulinda rasilimali zetu, tuanze upya, UPUMBAVU wa zamani usijirudie.

Inaumiza SANA SANA leo kuona upumbavu umerudi tena, na sheria inakwenda kubadilishwa ili kuhalalisha UPUMBAVU.

Wanaoitwa usalama wa taifa wapo wanashangaa shangaa tu, kiongozi wa nchi anadanganywa na kundi la wahuni. Hayo maslahi ya nchi mnayoyalinda ni yapi hayo???
 
Mh. Tundu Antiphas Lissu aliposhauri namna nzuri ya kuachana na hao watu na hivyo kuepuka mambo kama haya aliitwa msaliti na kuambulia risasi 30 mwilini. Yapo maamuzi ya kijinga na matokeo yake ndio kama haya...mtaikumbuka MIGA na bado!
 
Mtu mwenye kuipenda nchi yake lazima avunje mikataba yote ya kitumwa kama huu wa DP World akija Rais anayeipenda nchi yake lazima auvunje tu mkataba wa DP World.

Nafikiri sasa tuwetunavunja hii mikataba na tunawashughulikia wote walioingia mikataba hiyo mibovu hapo ndio tutakomesha ujinga wa kusaini mikataba mibovu.
 
VIONGOZI WA AJABU KUPATA KUTOKEA ETI WANAJIITA WAZALENDO
 
Huu mkata hadi magu anauvunja ulisahiniwa na chadema?Nani aliinga mkataba huu?Hii pesa inalipwa kutoka fungu lipi? Kwanini ccm msikubali na kujiuzulu badala ya hizi drama,hii pesa ilipwe na ccm kwasababu mlichukua 10% mkaanguka sahihi wenyewe Kisha mka kuvunja wenyewe sisi inatuhusu nini?
 
Mh. Tundu Antiphas Lissu aliposhauri namna nzuri ya kuachana na hao watu na hivyo kuepuka mambo kama haya aliitwa msaliti na kuambulia risasi 30 mwilini. Yapo maamuzi ya kijinga na matokeo yake ndio kama haya...mtaikumbuka MIGA na bado!
Achakuchanganya mambo Lissu wakati anazungumzia MIGA ilikuwa tunapambana kuhusiana na mkataba ya madini ya Accacia na tuliuvunja na kuanzisha Kampuni ya Twiga na inaendelea vizuri tu mpaka leo.

Kama unaona mikataba ni ya kitumwa na bora kuivunja tu hakuna jinsi ni kama huu wa DP World akija kiongozi anayejitambua lazima auvunje tu.
 
Umeandika utopolo mzito
 
Bila kusahau chama kinachoongoza serekali pia kiwajibishwe.
 
Elimu! Elimu, Elimu!

Mawakili wa serikali ni vilaza mara zote huiingiza serikali katika migogoro ya mikataba mibovu. Hii imesababishwa na uduni na kutoelewa lugha ya kiingereza na sheria za mikataba ya kimataifa kwa wana sheria wa serikali.

Sasa tusubiri kuilipa DPW kwa sababu mpaka sasa serikali ya Samia imeshupaza shingo haitaki kusikia cho chote kutoka kwa wananchi wanaotoa tahadhari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…