Maamuzi ya Hayati Magufuli yaigharimu Tanzania zaidi ya Bilioni 266

Maamuzi ya Hayati Magufuli yaigharimu Tanzania zaidi ya Bilioni 266

Mh. Tundu Antiphas Lissu aliposhauri namna nzuri ya kuachana na hao watu na hivyo kuepuka mambo kama haya aliitwa msaliti na kuambulia risasi 30 mwilini. Yapo maamuzi ya kijinga na matokeo yake ndio kama haya...mtaikumbuka MIGA na bado!
Hawa jamaa ni wanafiki sana siku hizi siisikii wa kimuita mzee MIGA kwasababu muda unaongea,Lisu anaenda kuwa Rasi wa kwanza kutoka upinzani wananchi tumejigunza mambo mengi kutoka kwake.
 
Hivi karibuni, tumeshuhudia tangazo la Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji, sehemu ya Benki ya Dunia, ambapo usuluhishi dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umefungwa. Tume hiyo imetoa adhabu yake, ikiamuru Tanzania kulipa fidia ya zaidi ya Dola za Marekani Milioni 109.5 sawa na takribani bilioni 266 za kitanzania (ikiwa ni pamoja na riba iliyokusanywa tayari) kwa wadai. Adhabu hii inahusu madai ya uharibifu kutokana na kunyang'anywa kwa mradi wa Nikeli wa Ntaka Hill kwa njia isiyo halali.

Indiana Resources Limited (ASX: IDA), ambayo ni mmiliki mkuu wa kampuni za Ntaka Nickel Holdings Ltd, Nachingwea UK Ltd, na Nachingwea Nickel Ltd, inayojulikana kama "wadai", imetoa sasisho kuhusu tukio hili. Indiana ndiyo meneja wa mradi huo na inawajibika kwa shughuli zote za usuluhishi dhidi ya Tanzania.

Adhabu hiyo imetolewa baada ya kikundi cha usuluhishi kubaini kuwa Tanzania ilinyang'anya mradi huo kinyume cha sheria mnamo tarehe 10 Januari 2018, kukiuka Mkataba wa Uwekezaji wa Kimataifa kati ya Uingereza na Tanzania. Hivyo basi, Tanzania imeamriwa kulipa fidia pamoja na hasara zingine, pamoja na riba inayozidisha kwa kiwango cha 2% juu ya kiwango cha msingi cha Dola za Marekani kuanzia tarehe ya kunyang'anywa hadi tarehe ya malipo.

Ni muhimu kutambua kuwa gharama za usuluhishi, ikiwa ni pamoja na ada na matumizi ya Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji, zinapaswa kubebwa na Tanzania. Aidha, Tanzania imeamriwa kulipa gharama za kisheria na matumizi ya wadai.

Indiana Resources Limited imetoa taarifa ambapo Mwenyekiti Mtendaji, Bronwyn Barnes, ameelezea furaha yake juu ya kupokea maamuzi ya mahakama. Amesisitiza kuwa kiasi cha adhabu kinathibitisha uwekezaji mkubwa ambao umepotea kutokana na kunyang'anywa kwa mradi huo na amewashukuru wanahisa ambao wamemsaidia katika kipindi chote cha usuluhishi.

Indiana sasa inakusudia kuanza mchakato wa kutekeleza adhabu hiyo. Ni muhimu kutambua kuwa Mkataba wa Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji umepitishwa na nchi wanachama 158 wa Benki ya Dunia, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Hii inamaanisha kuwa adhabu yoyote iliyotolewa na tume hiyo inaweza kutekelezwa katika nchi hizo kama uamuzi wa mahakama zao wenyewe.

Kwa upande wake, Bronwyn Barnes ameahidi kuendelea kuwajulisha wanahisa kadri mchakato wa utekelezaji unavyoendelea.

Historia ya madai haya inaanzia tarehe 21 Aprili 2015, ambapo Tanzania ilitoa Leseni ya Kuhifadhi kwa Mradi huo. Hata hivyo, mnamo Julai 2017, Serikali ya Tanzania ilibadilisha Sheria ya Madini ya 2010 na kuondoa daraja la Leseni ya Kuhifadhi bila kutoa mbadala wake.

Kufikia tarehe 10 Januari 2018, Tanzania ilichapisha kanuni mpya za madini, zilizofanya wazi kuwa leseni za kuhifadhi hazikuwepo tena na haki zote zilirejeshwa kwa Serikali. Indiana Resources Limited ilishiriki katika majadiliano na Serikali ya Tanzania kuanzia Januari 2018 hadi Desemba 2019, kujaribu kutatua suala la umiliki wa mradi huo. Hata hivyo, jitihada hizo hazikuzaa matunda na Serikali ya Tanzania ilifanya tangazo la mwaliko wa umma kwa zabuni ya pamoja kwa maendeleo ya maeneo yaliyokuwa chini ya leseni za kuhifadhi.

Maamuzi haya ya mahakama ya usuluhishi ni muhimu sana kwa Indiana Resources Limited na wadai wengine, kwani inawakumbusha umuhimu wa kulinda na kuheshimu mikataba ya uwekezaji. Pia inatupa fundisho kuhusu jukumu letu la kuhakikisha kuwa haki za wawekezaji zinalindwa na kwamba serikali zinaheshimu mikataba iliyosainiwa.

Hii pia inatoa fursa kwa nchi yetu, Tanzania, kutathmini upya sera zake za uwekezaji na kuhakikisha kwamba inashirikiana vizuri na wawekezaji ili kukuza ukuaji wa uchumi wetu na kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

Pia soma: Tanzania yashindwa kwenye kesi, yaamuriwa kulipa fidia ya zaidi ya Tsh. Bilioni 260
Hii issue ya bandari imenifungua macho kwanini Serikali inashindwa hizi kesi.
 
Maamuzi ya kijasiri ya Magufuli wacha yaigharimu nchi hayo mapesa, hatuwezi kukaa na mikataba ya hovyo yenye unyonyaji kwa taifa, huku walafi wachache walioingia wakifaidi 10% halafu nije kumlaumu Magufuli aliyeivunja, Never. Wacha tudaiwe lakini heshima yetu iwepo.

Kwangu Magufuli kwenye hili ni genius, naamini iko siku, hata huu wa Samia na DPW yake nao utavunjwa, wakati huo Samia akiwa amelala kaburini na laana.
We kweli mwabudu maiti.
Yaani kwako Magufuli ni kama Mungu wako vile...
 
Hivi karibuni, tumeshuhudia tangazo la Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji, sehemu ya Benki ya Dunia, ambapo usuluhishi dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umefungwa. Tume hiyo imetoa adhabu yake, ikiamuru Tanzania kulipa fidia ya zaidi ya Dola za Marekani Milioni 109.5 sawa na takribani bilioni 266 za kitanzania (ikiwa ni pamoja na riba iliyokusanywa tayari) kwa wadai. Adhabu hii inahusu madai ya uharibifu kutokana na kunyang'anywa kwa mradi wa Nikeli wa Ntaka Hill kwa njia isiyo halali.

Indiana Resources Limited (ASX: IDA), ambayo ni mmiliki mkuu wa kampuni za Ntaka Nickel Holdings Ltd, Nachingwea UK Ltd, na Nachingwea Nickel Ltd, inayojulikana kama "wadai", imetoa sasisho kuhusu tukio hili. Indiana ndiyo meneja wa mradi huo na inawajibika kwa shughuli zote za usuluhishi dhidi ya Tanzania.

Adhabu hiyo imetolewa baada ya kikundi cha usuluhishi kubaini kuwa Tanzania ilinyang'anya mradi huo kinyume cha sheria mnamo tarehe 10 Januari 2018, kukiuka Mkataba wa Uwekezaji wa Kimataifa kati ya Uingereza na Tanzania. Hivyo basi, Tanzania imeamriwa kulipa fidia pamoja na hasara zingine, pamoja na riba inayozidisha kwa kiwango cha 2% juu ya kiwango cha msingi cha Dola za Marekani kuanzia tarehe ya kunyang'anywa hadi tarehe ya malipo.

Ni muhimu kutambua kuwa gharama za usuluhishi, ikiwa ni pamoja na ada na matumizi ya Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji, zinapaswa kubebwa na Tanzania. Aidha, Tanzania imeamriwa kulipa gharama za kisheria na matumizi ya wadai.

Indiana Resources Limited imetoa taarifa ambapo Mwenyekiti Mtendaji, Bronwyn Barnes, ameelezea furaha yake juu ya kupokea maamuzi ya mahakama. Amesisitiza kuwa kiasi cha adhabu kinathibitisha uwekezaji mkubwa ambao umepotea kutokana na kunyang'anywa kwa mradi huo na amewashukuru wanahisa ambao wamemsaidia katika kipindi chote cha usuluhishi.

Indiana sasa inakusudia kuanza mchakato wa kutekeleza adhabu hiyo. Ni muhimu kutambua kuwa Mkataba wa Tume ya Kimataifa ya Kusuluhisha Migogoro ya Uwekezaji umepitishwa na nchi wanachama 158 wa Benki ya Dunia, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Hii inamaanisha kuwa adhabu yoyote iliyotolewa na tume hiyo inaweza kutekelezwa katika nchi hizo kama uamuzi wa mahakama zao wenyewe.

Kwa upande wake, Bronwyn Barnes ameahidi kuendelea kuwajulisha wanahisa kadri mchakato wa utekelezaji unavyoendelea.

Historia ya madai haya inaanzia tarehe 21 Aprili 2015, ambapo Tanzania ilitoa Leseni ya Kuhifadhi kwa Mradi huo. Hata hivyo, mnamo Julai 2017, Serikali ya Tanzania ilibadilisha Sheria ya Madini ya 2010 na kuondoa daraja la Leseni ya Kuhifadhi bila kutoa mbadala wake.

Kufikia tarehe 10 Januari 2018, Tanzania ilichapisha kanuni mpya za madini, zilizofanya wazi kuwa leseni za kuhifadhi hazikuwepo tena na haki zote zilirejeshwa kwa Serikali. Indiana Resources Limited ilishiriki katika majadiliano na Serikali ya Tanzania kuanzia Januari 2018 hadi Desemba 2019, kujaribu kutatua suala la umiliki wa mradi huo. Hata hivyo, jitihada hizo hazikuzaa matunda na Serikali ya Tanzania ilifanya tangazo la mwaliko wa umma kwa zabuni ya pamoja kwa maendeleo ya maeneo yaliyokuwa chini ya leseni za kuhifadhi.

Maamuzi haya ya mahakama ya usuluhishi ni muhimu sana kwa Indiana Resources Limited na wadai wengine, kwani inawakumbusha umuhimu wa kulinda na kuheshimu mikataba ya uwekezaji. Pia inatupa fundisho kuhusu jukumu letu la kuhakikisha kuwa haki za wawekezaji zinalindwa na kwamba serikali zinaheshimu mikataba iliyosainiwa.

Hii pia inatoa fursa kwa nchi yetu, Tanzania, kutathmini upya sera zake za uwekezaji na kuhakikisha kwamba inashirikiana vizuri na wawekezaji ili kukuza ukuaji wa uchumi wetu na kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

Pia soma: Tanzania yashindwa kwenye kesi, yaamuriwa kulipa fidia ya zaidi ya Tsh. Bilioni 260
Tatizo Lako hufikirii inje ya box. . Magufuli ndiye aliyeingia Mkataba wa kifala Hivyo.?

Bora tulipe hizo pesa kuliko kuendelea kukamuliwa. Hata Bandari mkisaini kuna Mzalendo atatokea ataufyekelea mbali
 
Mh. Tundu Antiphas Lissu aliposhauri namna nzuri ya kuachana na hao watu na hivyo kuepuka mambo kama haya aliitwa msaliti na kuambulia risasi 30 mwilini. Yapo maamuzi ya kijinga na matokeo yake ndio kama haya...mtaikumbuka MIGA na bado!
Namna nzuri ipi ya kuachana na mkataba mbovu ambao tayari ulishasainiwa?

Kuna namna gani ya kukwepa kulipa fidia unapovunja mkataba uliosainiwa, ili kukwepa gharama ambayo Lissu alimshauri Magufuli?

Mkiona jina Magufuli huwa akili zenu zinaganda kufikiri!.

Kama kwako afadhali tuendelee kuishi kwenye mikataba ya kinyonyaji inayotudhalilisha kama taifa, kwangu afadhali ivunjwe ili kulinda heshima yetu hata kama tutadaiwa na dunia yote.
 
Wakulaumiwa ni Kikwete aliyeingia mikataba ya kipuuzi. Kama ambavyo tutamlaumu Samia owa mikataba yake ya Dubai.

Magufuli alifanya kilichotakiwa kufanyika ili kuinusuru nchi. Akaleta na sheria mpya ya kulinda rasilimali zetu, tuanze upya, UPUMBAVU wa zamani usijirudie.

Inaumiza SANA SANA leo kuona upumbavu umerudi tena, na sheria inakwenda kubadilishwa ili kuhalalisha UPUMBAVU.

Wanaoitwa usalama wa taifa wapo wanashangaa shangaa tu, kiongozi wa nchi anadanhanywa na kundi la wahuni. Hayo maslahi ya nchi mnayoyalinda ni yapi hayo???
Magufuli alipora uchaguzi akajaza wabunge wa CCM kwa kisingizio kuwa ni wazalendo. Mbona hatuoni hao wazalendo wakifanya uzalendo wao? Kibaya zaidi ndio hao wanapelekewa bill ya kubadili hizo sheria walizotunga wenyewe.
 
Namna nzuri ipi ya kuachana na mkataba mbovu ambao tayari ulishasainiwa?

Kuna namna gani ya kukwepa kulipa fidia unapovunja mkataba uliosaini ambayo Lissu alimshauri Magufuli?

Kama kwako afadhali tuendelee kuishi kwenye mikataba ya kinyonyaji inayotudhalilisha kama taifa, kwangu afadhali ivunjwe ili kulinda heshima yetu hata kama tutadaiwa na dunia yote.
Sawa mkuu hizi pesa mkalipe ccm au tuuze mali zenu tulipe madeni.
 
Elimu! Elimu, Elimu!

Mawakili wa serikali ni vilaza mara zote huiingiza serikali katika migogoro ya mikataba mibovu. Hii imesababishwa na uduni na kutoelewa lugha ya kiingereza na sheria za mikataba ya kimataifa kwa wana sheria wa serikali.

Sasa tusubiri kuilipa DPW kwa sababu mpaka sasa serikali ya Samia imeshupaza shingo haitaki kusikia cho chote kutoka kwa wananchi wanaotoa tahadhari.

Mawakili wa serikali wamelemazwa na mahakama dhaifu za humu ndani, ambapo mahakama zinapewa maelekezo ya namna ya kuamua kesi.
 
Achakuchanganya mambo Lissu wakati anazungumzia MIGA ilikuwa tunapambana kuhusiana na mkataba ya madini ya Accacia na tuliuvunja na kuanzisha Kampuni ya Twiga na inaendelea vizuri tu mpaka leo.

Kama unaona mikataba ni ya kitumwa na bora kuivunja tu hakuna jinsi ni kama huu wa DP World akija kiongozi anayejitambua lazima auvunje tu.
Wengi wao wakiona jina Magufuli huwa akili zao zinaganda, hazifanyi kazi tena.
 
Maamuzi ya kijasiri ya Magufuli wacha yaigharimu nchi hayo mapesa, hatuwezi kukaa na mikataba ya hovyo yenye unyonyaji kwa taifa, huku walafi wachache walioingia wakifaidi 10% halafu nije kumlaumu Magufuli aliyeivunja, Never. Wacha tudaiwe lakini heshima yetu iwepo.

Kwangu Magufuli kwenye hili ni genius, naamini iko siku, hata huu wa Samia na DPW yake nao utavunjwa, wakati huo Samia akiwa amelala kaburini na laana.
Heshima ya kipumbavu hiyo
 
Tabia za mawakili wa serikali kushindwa kesi kwa makusudi zimeanza tena...hizi kesi ndo zilizompa utajiri Nimrodi...
 
Nani CCM wewe, tembea na hoja tu...
Hakuna hoja zaidi ya gharama hii pesa ya kulipa wawekezaji kwamaamuzi mabovu ya kuingia mikataba na kuchukua 10% baada ya muda ccm wenyewe mkavunja ili kutafuta muwekezaji mpya ili mpige 10% mpya kwa huu dalali tuambie hii kwa huu ujinga hii pesa inatoka chama gani chadema Chauma au ccm.
 
Back
Top Bottom