Maana halisi ya "Luxury Bus" ni nini?

Maana halisi ya "Luxury Bus" ni nini?

Hakuna luxury bus inayobeba abiria zaidi ya 30. Hizo ni busses za nauli ya juu tu kwa vile zina choo na WiFi. Luxury ni pale unapokuwa na maximum comfort wakati wa safari. Mabasi yetu hata hiyo Wi-Fi wameandika tu haipo. Kwenye TV huwezi kuchagua unachotaka kuangalia.... Utaoneshwa mkojani au muvi zilizotafsiriwa njia nzima. Utapewa biscuit na soda moja au maji tena hata soda yenyewe hauchagui unapewa yeyote tu.
Njiani mtaongia hotel moja na kina CHAKITO au Ms. SERENGETI. Wahudumu wa ndani wataongea na nyie kwa kebehi kama wamewapa lift tu.
Tofauti yenu na aliyepanda KING MUSUKUMA ni kuwa nyie hamtachimba dawa njiani.
Basi za mchina hazina comfort kabisa , suspension zao ziko jittery mwanzo mwisho mpaka huwa nashindwa kusoma vitabu nikiwa safarini.
 
Kwani kuna bus gani luxury la kwenda simiyu, mana wasukuma ni karaha kwelikweli, yanaongea kwa nguvu uku yanatafuna maindi ya kuchoma na miwa.
😆😆 ongeza huwa wanaongea kwa sauti kama wapo kwenye mashamba ya mpunga wakifukuza ndege😆
 
wewe ukiskia Luxury unaelewa nini kwani?,hapahapa Tanzania kuna basi zina choo ndani zina free wifi ,2 in 1 seats + VIP seats ,ina tablet kila seat , ndani mnapewa vinywaj na baadhi ya vitu vya kutafuna na zimepewa daraja la luxury, sasa wewe wataka nini tena apo.sema zipo chache mno hata kampuni zenyewe zenye luxury buses unakuta wanazo mbili au tatu tu.
Tanzania bado hakuna luxury bus , hizo features zote hapo umezitaja lakini mabasi hayo yapo kwenye steel suspensions na yote ni engine mbele
Ili basi at least iwe considered luxury bus
Full Air suspensions
Rear mounted engine for quiter cabin
Choo cha haja zote
Sealed windows
Seats with enough leg room
130° plus seat inclination angle

Ukitembea kuanzia zambia kwenda kule juu ndo unakutana na basi hizi , sio kwamba watanzania hawawezi kuzinunua la, sheria za Tanroad zinakinzana na specifications za manufacturers wengi wa luxurious buses, maana ili upate seats 53 zenye inclination angle nzuri lazima basi liwe refu.
Tanroad hawataki basi ndefu
 
Maandazi, maindi ya kuchoma, mayai, biskut, sambusa, soda tatu za aina tofauti afu mtoto kanywa nusunusu kila moja, yani kitumbo kimemvimba ndii anahemea juujuu kama anataka kufa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaaah

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Hakuna luxury bus inayobeba abiria zaidi ya 30. Hizo ni busses za nauli ya juu tu kwa vile zina choo na WiFi. Luxury ni pale unapokuwa na maximum comfort wakati wa safari. Mabasi yetu hata hiyo Wi-Fi wameandika tu haipo. Kwenye TV huwezi kuchagua unachotaka kuangalia.... Utaoneshwa mkojani au muvi zilizotafsiriwa njia nzima. Utapewa biscuit na soda moja au maji tena hata soda yenyewe hauchagui unapewa yeyote tu.
Njiani mtaongia hotel moja na kina CHAKITO au Ms. SERENGETI. Wahudumu wa ndani wataongea na nyie kwa kebehi kama wamewapa lift tu.
Tofauti yenu na aliyepanda KING MUSUKUMA ni kuwa nyie hamtachimba dawa njiani.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Tanzania bado hakuna luxury bus , hizo features zote hapo umezitaja lakini mabasi hayo yapo kwenye steel suspensions na yote ni engine mbele
Ili basi at least iwe considered luxury bus
Full Air suspensions
Rear mounted engine for quiter cabin
Choo cha haja zote
Sealed windows
Seats with enough leg room
130° plus seat inclination angle

Ukitembea kuanzia zambia kwenda kule juu ndo unakutana na basi hizi , sio kwamba watanzania hawawezi kuzinunua la, sheria za Tanroad zinakinzana na specifications za manufacturers wengi wa luxurious buses, maana ili upate seats 53 zenye inclination angle nzuri lazima basi liwe refu.
Tanroad hawataki basi ndefu
sikubishii kwasaabu hiyo ndio tafsiri yako ya luxury bus
 
Maandazi, maindi ya kuchoma, mayai, biskut, sambusa, soda tatu za aina tofauti afu mtoto kanywa nusunusu kila moja, yani kitumbo kimemvimba ndii anahemea juujuu kama anataka kufa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Basi za mchina hazina comfort kabisa , suspension zao ziko jittery mwanzo mwisho mpaka huwa nashindwa kusoma vitabu nikiwa safarini.
Achana na kusoma siku moja nunua kahawa yako ujaribu kunywa gari ikiwa inatembea
 
Achana na kusoma siku moja nunua kahawa yako ujaribu kunywa gari ikiwa inatembea
Hahahah siwezi jaribu,nilipanda intercape bus siku 1 kisha nikapewa kikombe cha kahawa asubuhi nikanywa vizuri kabisa bila shida.
 
Hii mashine acha kabisa!!!. Ikipita jirani yako unasikia kabisa hii kitu ina nguvu.Inakwenda na ratiba bro, hizo gari zenu za kichina route hii ya Arusha-Musoma au Arusha - Tarime haziwezi .
Hiyo naweza kuhiita route dume, maana gari zake ni roho ya paka, springs zake kama jiwe yaani bus hazinepi na likiruka ni jumla jumla.

Nilipanda moja hivi kutoka Mpanda/katavi kuelekea arusha asee, kwanza njia yenyewe sasa na hiyo bus speed yake 😲!!.
 
Niliwahi panda Scandnavia kwenda Mbeya, tukapewa kahawa, chai au maziwa.

Miaka hiyo.
Hiizi ndio gari nilizowahi shuhudia kuhudumu katika level za luxury Tanzania.
Kuanzia
1.wahudumu Na huduma Yao.
2.Sheria za kampuni.
3.Usalama wa abiria na Mali zao.
Sijui zilipoteaje poteaje aiseee



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom