Maana ya neno hallelujah Diamond Platnumz amekosea kulitumia?

Maana ya neno hallelujah Diamond Platnumz amekosea kulitumia?

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
1,393
Reaction score
3,237
ac79e673900816a880b7419ebedbf26b.jpg


Zawadi Lupelo

Wanajamvi salamu kwanza!

Nimeusikiliza wimbo mpya wa Diamond Platnumz kwa makini sana. Kitu kilichonitatiza na kuja kunishughulisha hapa jamvini ni neno hallelujah na namna lilivyotumika ni maoni yangu kwamba limetumika kimakosa katika wimbo huo ambao ni wa mapenzi hasa ukizingatia maana ya msingi ya neno ambapo huwa linatumika kwenye ibada katika kumsifu Mungu ni neno linalomaanisha "Mungu apewe sifa".

Ni neno ambalo linaenda sambamba na maneno Bwana asifiwe, tumsifu Yesu Kristo na kadhalika huko makanisani kufikia hatua ya kulitumia hili neno kwenye wimbo wa mapenzi katika muktadha wa Diamond Platnumz ni kufeli kwake katika uteuzi wa maneno.

Haiwezekani umezungukwa na mademu wapo nusu uchi unaimba Hallelujah huku ni kuitweza imani na utukufu wa Mungu.

Ni matumaini yangu wakati mwingine atakuwa makini kwenye kuchagua maneno ya kutumia ili kuhakikisha haleti mkanganyiko wowote.

I rest my case.

Zawadi Lupelo.
 
ac79e673900816a880b7419ebedbf26b.jpg


Zawadi B. Lupelo

Wanajamvi salamu kwanza!

Nimeusikiliza wimbo mpya wa Diamond Platnumz kwa makini sana. Kitu kilichonitatiza na kuja kunishughulisha hapa jamvini ni neno hallelujah na namna lilivyotumika ni maoni yangu kwamba limetumika kimakosa katika wimbo huo ambao ni wa mapenzi hasa ukizingatia maana ya msingi ya neno ambapo huwa linatumika kwenye ibada katika kumsifu Mungu ni neno linalomaanisha "Mungu apewe sifa".

Ni neno ambalo linaenda sambamba na maneno Bwana asifiwe, tumsifu Yesu Kristo na kadhalika huko makanisani kufikia hatua ya kulitumia hili neno kwenye wimbo wa mapenzi katika muktadha wa Diamond Platnumz ni kufeli kwake katika uteuzi wa maneno.

Ni matumaini yangu wakati mwingine atakuwa makini kwenye kuchagua maneno ya kutumia ili kuhakikisha haleti mkanganyiko wowote.

I rest my case.

Zawadi B. Lupelo.
Hebu niusikilize kwa Makin m sijauelewa kabisa na hata mpangilio wake wa maneno ajitahid kutunga mashairi yanayoeleweka jmn
 
Kwanza mkuu unatakiwa utambue kwamba kitu kina sababu,
kwahiyo unaposema Mungu apewe sifa unatakiwa ujiulize "apewe sifa kwaajili gani?"
anhaa maybe kwa kukuzawadia kitu flani,

okay hata kwa diamond, unatakiwa ujiulize amesema Mungu apewe sifa kwaajili gani? ndipo jibu linakuja
'Apewe kwaajili ya kumpatia zawadi ya Mwanamke mzuri ambaye ndiye anayemsifia ndani ya huo wimbo!...'

Vilevile unatakiwa ukumbuke kwamba Mapenzi sio dhambi, na kumshukuru Mungu na kumtukuza kwa zawadi aliyokupatia pia sio dhambi.
Usipomkumbuka Mungu kwa vitu vidogo basi hata kwa vikubwa hautomshukuru..

HALELLUJAH......
No more Explanation tafadhal u said it all.
 
Kuna nyimbo nyingi tuu duniani kote kwa ujumla yanatumika majina ya utukufu ya mungu na contents ya hizo nyimbo ni mapenzi tuu kwa hiyo hili sio la kushangaza hapa.

Kuna wengine humu humu wapenzi wao wanawaita ANGEL sio, malaika pia ni viumbe vya utukufu kwa walio na imani.

Kuna mchezaji mpira manCity anaitwa Jesus Hana hata maadili mkuu muhuni wa kutupwa sijui Kama havuti bangi yule.

Bob Marley, luck dude, Morgan heritage, Sade adu, Drake ana nyimbo inaitwa "6 GOD" hata hawa wataarabu hawa si wanasemaga mule Allhamdulilah au Mashaallah haya pia ni maneno ya kitukufu kwa hiyo sio big deal hapa.

Pata tuu burudani mkuu.
 
Kwanza mkuu unatakiwa utambue kwamba kitu kina sababu,
kwahiyo unaposema Mungu apewe sifa unatakiwa ujiulize "apewe sifa kwaajili gani?"
anhaa maybe kwa kukuzawadia kitu flani,

okay hata kwa diamond, unatakiwa ujiulize amesema Mungu apewe sifa kwaajili gani? ndipo jibu linakuja
'Apewe kwaajili ya kumpatia zawadi ya Mwanamke mzuri ambaye ndiye anayemsifia ndani ya huo wimbo!...'

Vilevile unatakiwa ukumbuke kwamba Mapenzi sio dhambi, na kumshukuru Mungu na kumtukuza kwa zawadi aliyokupatia pia sio dhambi.
Usipomkumbuka Mungu kwa vitu vidogo basi hata kwa vikubwa hautomshukuru..

HALELLUJAH......
Ni neno maalumu kwa ajili ya kuworship hiyo ndiyo asili ya neno huwezi kutumia kila sehemu
 
Kweli kabisa hilo neno haleluya ni kwa kwa ajili ya kumsifu Mungu muumba wetu. Sasa haipendezi mademu wapo nusu uchi et haleluya kweli haipendezi bora angetumia neno lingine sio haleluya so sad!
 
Kweli kabisa hilo neno haleluya ni kwa kwa ajili ya kumsifu Mungu muumba wetu. Sasa haipendezi mademu wapo nusu uchi et haleluya kweli haipendezi bora angetumia neno lingine sio haleluya so sad!
Kwa kweli inasikitisha
 
Kwanza mkuu unatakiwa utambue kwamba kila kitu kina sababu,
kwahiyo unaposema Mungu apewe sifa unatakiwa ujiulize "apewe sifa kwaajili gani?"
anhaa maybe kwa kukuzawadia kitu flani,

okay hata kwa diamond, unatakiwa ujiulize amesema Mungu apewe sifa kwaajili gani? ndipo jibu linakuja
'Apewe kwaajili ya kumpatia zawadi ya Mwanamke mzuri ambaye ndiye anayemsifia ndani ya huo wimbo!...'

Vilevile unatakiwa ukumbuke kwamba Mapenzi sio dhambi, na kumshukuru Mungu na kumtukuza kwa zawadi aliyokupatia pia sio dhambi.
Usipomkumbuka Mungu kwa vitu vidogo basi hata kwa vikubwa hautomshukuru..

HALELLUJAH......
Hoja hapa kaka ni maana ya msingi ya neno na muktadha, tuliosoma matumizi ya lugha tunajua kitu kinaitwa muktadha huwezi kuchukua neno la kanisani ukalipeleka baa. Muktadha na uchaguzi wa maneno ni kitu muhimu kwa msanii kuna maneno mengi sana yangefaa hapo
 
kuna watu huwa mnajidai mna midomo mirefu sana ya kukosoa....ndio ashalitumia sasa na views zipo laki 5 in less tha 10 hours....
 
Babu weeee Kuna nyimbo nyingi tuu duniani kote kwa ujumla yanatumika majina ya utukufu ya mungu na contents ya hizo nyimbo ni mapenzi tuu kwa hiyo hili sio la kushangaza hapa.

Kuna wengine humu humu wapenzi wao wanawaita ANGEL sio, malaika pia ni viumbe vya utukufu kwa walio na imani.

Kuna mchezaji mpira manCity anaitwa Jesus Hana hata maadili mkuu muhuni wa kutupwa sijui Kama havuti bangi yule.

Bob Marley, luck dude, Morgan heritage, Sade adu, Drake ana nyimbo inaitwa "6 GOD" hata hawa wataarabu hawa si wanasemaga mule Allhamdulilah au Mashaallah haya pia ni maneno ya kitukufu kwa hiyo sio big deal hapa.

Pata tuu burudani mkuu.
MAN OF STEEL...kutumia "babu weee" mh
 
Wimbo ili ufike mbali lazima ujadilie haijalishi kwa Mazuri au Mabaya., hivyo kwa hilo amefanikiwa!!!
nazani hichi ndicho alicholenga huyu mfanyabiashara mashuhuri wa mziki pendwa bongoland,alijua lazima kuna watu watatoka povu na kuanza uchambuzi wao yakinifu...huku yeye anagain popularity!
 
Back
Top Bottom