Hawa maaskofu mbona wanatoa hitimisho la kipuuzi namna hii?
Kesi ya Mbowe imeshafikishwa mahakamani, sasa wanawashwa na nini tena kuanza kusema eti inachafua taswira ya nchi!??
Kwani kuna ambae yupo juu ya sheria, au kuwa Mwenyekiti wa chama cha siasa inakupa kinga ya kutokushitakiwa kwa jambo lolote lihusulo uvunjaji wa sheria?
Pia, tunapohubiri kuheshimu misingi ya demokrasia, utawala bora na haki za binadamu,,, sasa kwann kwa Sabaya iwe ni sawa kwamba Serikali inatenda na kufuata utawala bora ila kwa Mbowe imekuwa sio tena kutenda haki bali uonevu? Double standard
Mbowe huyu huyu alikataza watu wasije msiba wa Kaka yake kisa kuepusha maambukizi kwa Jamii yake, ila baada ya mazishi akakimbilia Mwanza kufanya mkusanyiko bila kujali kuwa huko kutapelekea kueneza maambukizi. Kwahyo akaona Jamii ya wana Mwanza wacha wafe tu ilimradi mrengo wake kisiasa utimie. Ila nyie Maaskofu uchwara mkakaa kimya
Kwa double standard hizi, ni wazi nyie maaskofu uchwara mnatumikia upande mmoja na sio kutumikia wananchi wote
Watanzania wenzangu tuweni makini na hawa kina kibweteres' type waliopo Tanzania.