Tetesi: Mabadiliko Baraza la Mawaziri; J. Makamba, Mhagama, Ummy Mwalimu nje; Adadi Rajabu, Bashe watajwa

Tetesi: Mabadiliko Baraza la Mawaziri; J. Makamba, Mhagama, Ummy Mwalimu nje; Adadi Rajabu, Bashe watajwa

Kwa hiyo wapinzani wanashirikiana na makamba kumhujumu Mgufuli? Nchi ya ajabu sana hii..... Hivi hawa wanatetea nini sasa?
 
Muda wowote mabadiliko makubwa yanategemea kutokea katika baraza la mawaziri ambapo mawaziri kadhaa watatemwa kutokana na sababu kadhaa.

1. Jenister Muhagama - Anatuhumiwa kwa kuzunguka mamlaka za teuzi (Rais na Waziri Mkuu) katika sakata la kumteuwa kaimu mkurugenzi wa NSSF... Mhagama alitenda kosa hilo akishirikiana na Balozi Ombeni Sefue ambaye kwa sasa kashatumbuliwa.

2. January Makamba - Maranyingi amesikika na kurekodiwa akimsema vibaya Rais, akimsengenya Rais pamoja na kuratibu mipango mbalimbali ya kumdhoofisha Rais Magufuli. haya anayatenda katika Hotel ya Protea Dar es Salaa., na Dodoma ambapo amekuwa akifanya vikao vya siri usiku wa manane na baadhi ya wabunge wa upinzani, pamoja na wafanyabiashara wakubwa wakiwemo wa sukari

3. Ummy Mwalimu - Inasemekana kasi na uwezo wake mdogo haumrithishi Rais kwa sasa..

Katika mabadiliko hayo Adadi Rajabu, Mbunge wa Muheza inasemekana anaweza kuingia kuchukua nafasi ya Kitwanga, wengine wanaotajwa ni Bashe, mbunge wa Nzega ambaye anaweza kupewa docket ya Mazingira au Maliasili na pia Serukamba amekuwa akitajwa.

Mytake: wananchi kwa umoja wetu tumuunge mkono Rais Magufuli ana dhamira njema kabisa la kuwatumikia watanzania.
Si bure, kuna mtu unampigia debe!
Huna lolote Ila kuna majungu u!edhamiria kuyafanya!
Unatoa wapi tetesi za watu watatu kwa incidences tofauti!
Majungu si mtaji, kwa uroho wenu mnamuharibia raisi!
 
Duuh hii panga pangua hadi hii half time timu haijafunga goli. WB inasema wananchi milioni kumi na mbili ni masikini hoe hae... Ngoja tuendelee kujipa moyo...
Hao maskini milioni 12 wameupata kuanzia lini? unahusishaje na utawala uliyoko madarakani kwa miezi hii 7?
 
Kweli jf ni kiboko, nakumbuka kuna member alikuja humu akasema aliyekuwa naibu katibu mkuu wa UN ,MIGIRO wakati wowote anatangazwa kuwa balozi uingereza,na kweli mda mfupo ikatangazawa hivyo. Yani huko ikulu hakuna siri

Baada ya Magufuli kufagia mabaki ya jk ikulu nilitarajia hakutakua na leaks tena Magogoni!
Kumbe nilijiamimisha bure nyeti kibao zinavuja
 
Tunaendelea kuchochea kuni haramu haiwezi kuwa halali!

Maandiko yanahusika hapa Kesho kwa wale wakristo Utatu Mtakatifu anatuhusu.
 
mvua njooo katarina njooo,najaribu kujikumbusha haka kawimbo ka enzi za utooo tulipokua tukiona wingu limetanda tuliimba hivyoo.japo hatukua tukijua madhara ya mvua katarina
 
Mpaka leo sijaelewa Ummy Mwalimu na Mhagama (as well as Nape) walipataje kuwa mawaziri katika Serikali iliyothubutu kusema baadhi ya Wizara mawaziri "makini" hawajaonekana. Nadhani hii ilitokana na ile dhana ya kila mmoja kwenye top 3 kutakiwa kupendekeza watu wake.
 
Mytake: wananchi
sema wanaccm ,.usiwajumlishe wananchi wote wengine hatumuungi mkono kwakuwa mapendekezo yetu jp hayatumii mfano,.kumteua muhongo huku ni muhusika wa escrow,.mwakyembe nk
so tumia neno wanaccm,.sio wananchi woooote tupongeze na kusifia kama mfanyavyo nyieeee
 
Aliyafanya kikwete haya, alibadilisha mawaziri kila uchao lakini hakupata mavuno yaliyo bora, ccm ni ileile hakuna anae faa huko ndani. Bora angebaki mwenyewe na waziri mkuu makini zaidi. Tena kwenye listi angeongezwa Mwakyembe aliekuwa anacheka kama juha wakati waziri mlevi akitoa majibu ni aibu kubwa kama waziri wa sheria apishe tu na yeye.
mkuu yaani kwa mtu mwenye akili timamu,.ccm siyakushabikia kabisaaaaa
mwakyembe ndo wazr husika wa katiba na sheria za nchi hii,then mtu mlevi mlevi2 anavunja katiba tena mbele ya chombo cha buge,.then anachekelea bila haibu,.hivi hawa viongoz wakoje sijui,....jpm anakaz sana kwa hii system ya kuchekeleana hovyohovyo,.labda aame chama,.ila ndani ya ccm,..hamna atakofanikiwa
 
Back
Top Bottom