Mabadiliko TRA: Kamishna wa Forodha Mtanganyika Said Athuman Kiondo aondolewa awekwa Juma Bakari Hassan kutoka Zanzibar

Hao ZRA ni sawa tu na Halmashauri zinavyokusanya kodi Tanzania Bara hata boss wa ZRA Mwenda alikuwa Diwani wa Mikocheni na Meya wa Kinondoni

Majukumu ya TRA Zanzibar yako pale pale!
 
TRA haiko Zanzibar punga wewe?
Kijana kama hujui jambo bora ukae kimya.

TRA iliyopo Zanzibar haina uhusiano na mapato yanayokusanywa na ZRB iliyoizaa na kuwa ZRA, mapato yote ya zanzibar yanabaki huko kwa maendeleo ya wananchi wa nchi hiyo ya Kiislamu.

TRA kwa ninavyofaham inafanya kazi kwa kushugulikia mapato yaliyopo kwenye issue ya muungano tu na siyo mapato ya SMZ mfano Bandari, Airport, Ushuru kwa wafanyabiashara nk.

Kuna issues ukikaa na kuangalia jinsi zinavyokwenda unaweza usielewe kabisa hizi nchi mbili zina uhusiano gani zaidi.

So unatakiwa kukaa kwa kutulia si kuandika kitu kwa kujifanya unajua, maana kumleta mzanzibari kushika ofisi kama hiyo si jambo la kucheka aseee.
 
JUMA BAKAR, KWA JINSI NINAVYOMFAHAMU MCHA MUNGU HUYU, WATU WA MAMBO YA CHINI CHINI MMEKWISHA,JAMAA AMENYOOKA VIBAYA SANA,PIA HANA MARINGO KABISA,HONGERA!
 
Hivi hakuna Tanganyika Revenue Authority?

Hakuna Tanganyika Ports Authority?
 
ukisoma Katina Kuna ma, mambo ya muungano na yasiyo ya muungano hivyo wakienda mahakamani serikali itashindwa mapema.
Mambo ya muungano maana yake yanatuhusu sote (wazanzibari na watanganyika).


Mambo yasiyo ya muungano maana yake wazanzibari wafanye yao kwa faida yao lkn watanganyika wafanye kwa ajili ya wote na faida ya wote.

Mfano.
TRA inakusanya fedha halafu 25 % inapelekwa Zanzibar, lkn ZRB (ZRA) inakusanya fedha kwa ajili ya Zanzibar tu.

Amka ewe mtanganyika
 
Hii nchi ni moja. Yeyote anafiti popote
 
Sasa huyo Kamishna aliyeteuliwa atahudumia Serikali ya Tanganyika au Serikali ya Jamhuri ya Muungano!πŸ˜‚πŸ˜‚

Umeonyesha tu ujinga wako!
 
Ni vizuri kudai Tanganyika kwa nguvu zote, ndio hao wanaoutumika kutuhujumu mapato yetu na kuonekana Tanganyika haifanyi kazi, na baadae utasikia TRA ibinafisishwe aletwe mwarabu ili vitu visomane ikulu
 
Kumbuka wazanzibari ni watanzania pia
Nenda kaombe ajira huko Zanzibar ndio utagundua kuna tatizo kubwa la kikatiba.Mzanzibar akiwa Tanganyika ni Mtanzania kamili mwenye haki zote za kiraia.

Mtanganyika akiwa Tanganyika (Tanzania Bara),Mtanganyika akienda Zanzibar ni Mtanganyika hana haki sawa na mzanzibar.Hana haki ya kumiliki ardhi,hana haki ya kupiga kura,hana haki ya ajira ktk Taasisi za kiserekali kama Mahakama,Wizara mbali mbali.

Mzanzibar ana haki zote huku Tanganyika na huko kwao Zanzibar.
Mtanganyika ana haki zote huku Tanganyika lakini ananyimwa haki nyingi akienda nchi ya Zanzibar.

Kifupi Mwl Nyerere alituachia katiba mbovu kuliko zote duniani.
 
Hii ndiyo nature ya muungano wetu. Cha watanganyika ni cha wote lkn cha wazanzibari ni cha wazanzibari pekee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…