Mabadiliko ya Sheria mbalimbali kufanyika Bungeni: Wananchi waalikwa kutoa maoni yao (Pitia mabadiliko hapa)

Mabadiliko ya Sheria mbalimbali kufanyika Bungeni: Wananchi waalikwa kutoa maoni yao (Pitia mabadiliko hapa)

w0rM

Member
Joined
May 3, 2011
Posts
81
Reaction score
192
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria inawaalika wadau kutoa maoni ya wadau kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 7 wa Mwaka 2021 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 7) Act, 2021.

Mkutano wa kupokea na kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) utafanyika siku ya Alhamisi tarehe 03 Februari, 2022 saa 5:00 asubuhi katika Ukumbi Na. 9

Jengo la Utawala, Ofisi ya Bunge, Dodoma. Kamati inawaalika Wananchi wenye maoni kuhusu Muswada huo kufika na kuwasilisha mani yao kabla haujapelekwa katika hatua nyingine.

Aidha, Kamati itapokea maoni kwa njia ya posta au baruapepe kabla ya Jumamosi tarehe 5 Januari 2022 saa 5:00 asubuhi kwa anuani

Katibu wa Bunge
Ofisi ya Bunge,
Mtaa wa Makole,
S. L. P. 941,
41105 DODOMA.

Au baruapepe cna@bunge.go.tz au Kamati@bunge.go.tz

My take:
Muda uliyoweka kwa ajili ya kutolea maoni ni muda mchache sana hasa ukizingatia kwanza madaliko yenyewe ya sheria yameandikwa kwa lugha ya Kiingereza.

Kama kweli Kamati ingelikuwa inataka maoni haya ingeweka muda mrefu na sheria zingekuwa kwa lugha zote mbili ili Wananchi waelewe na kuweka maoni yao.

Hili naona ni bora liende tu na ili kuweka ‘justification’ kuwa mabadiliko haya yalipitiwa na Wadau

Kuona mabadiliko yaliyopendekezwa angalia pdf niliyoambatanisha hapa
 

Attachments

IMG_20220202_213722_595.jpg
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria inawaalika wadau kutoa maoni ya wadau kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 7 wa Mwaka 2021 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 7) Act, 2021.

Mkutano wa kupokea na kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) utafanyika siku ya Alhamisi tarehe 03 Februari, 2022 saa 5:00 asubuhi katika Ukumbi Na. 9

Jengo la Utawala, Ofisi ya Bunge, Dodoma. Kamati inawaalika Wananchi wenye maoni kuhusu Muswada huo kufika na kuwasilisha mani yao kabla haujapelekwa katika hatua nyingine.

Aidha, Kamati itapokea maoni kwa njia ya posta au baruapepe kabla ya Jumamosi tarehe 5 Januari 2022 saa 5:00 asubuhi kwa anuani

Katibu wa Bunge
Ofisi ya Bunge,
Mtaa wa Makole,
S. L. P. 941,
41105 DODOMA.

Au baruapepe cna@bunge.go.tz au Kamati@bunge.go.tz

My take:
Muda uliyoweka kwa ajili ya kutolea maoni ni muda mchache sana hasa ukizingatia kwanza madaliko yenyewe ya sheria yameandikwa kwa lugha ya Kiingereza.

Kama kweli Kamati ingelikuwa inataka maoni haya ingeweka muda mrefu na sheria zingekuwa kwa lugha zote mbili ili Wananchi waelewe na kuweka maoni yao.

Hili naona ni bora liende tu na ili kuweka ‘justification’ kuwa mabadiliko haya yalipitiwa na Wadau

Kuona mabadiliko yaliyopendekezwa angalia pdf niliyoambatanisha hapa
Hatubadilishi Katiba kwamba mda uwe mrefu Sana..

Hongera Samia maana uliwaagiza wabadili sheria zote zilizopitwa na wakati.
 
Hatubadilishi Katiba kwamba mda uwe mrefu Sana..

Hongera Samia maana uliwaagiza wabadili sheria zote zilizopitwa na wakati.
Unadhani sheria zilizofanyiwa mabadiliko hapo kwa muda uliotolewa hapo wa kwenda kesho Dodoma unaweza kuboresha wewe kama Mwananchi?

Je, unadhani mapendekezo ya kutumwa kwa barua pepe yatafanyiwa kazi?
 
Tunataka katiba siyo sheria. Sheria hutokana na katiba.. Katba mbovu=sheria mbovu and the reverse is truw.

Amani ni tunda la haki.
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria inawaalika wadau kutoa maoni ya wadau kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 7 wa Mwaka 2021 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 7) Act, 2021...
Penal code naona wameifanyia amendment kubwa. Wadau wa sheria someni between lines kuona kama kuna substance au ni ku deepen ukandamizaji wa raia kwa manufaa ya watawala madikiteita.
 
Hahahahaha hii nchi inachekesha mbongo aache kujadili maisha ya Wema afungue mswada wa kiingereza ausome na autolee maoni?

Ridiculous [emoji1787]
Ya wema na mondi ? !! Hahahaha!!
 
Hahahahaha hii nchi inachekesha mbongo aache kujadili maisha ya Wema afungue mswada wa kiingereza ausome na autolee maoni?

Ridiculous [emoji1787]
Kumbe umeona shida ilipo eenh. Asilimia 99 wanajadili Wema, Diamond, Zuchu na upuuzi mwingine, then full time kulalamika mambo ya msingi. Hiki kizazi ni bure kabisa
 
Wekeni huo muswada hapa tuuchakate kama kweli wanahitaji maoni yetu!
 
Ile sheria waliyojitungia kuwa wasishtakiwe wakitoka madarakani ifutwe, haina tija kwa nchi!
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria inawaalika wadau kutoa maoni ya wadau kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 7 wa Mwaka 2021 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 7) Act, 2021...
Maigizo tupu
 
Huyu bibi hana lengo zuri na Tanzania bara mpka tushituke itakuwa imeshamalizwa na Zanzibar
 
Huyu naye ameanza kuongea vitu vya ajabu ili aonekane Spika Bora mwambieni tunataka Katiba mpya hayo mengine watafanya wao wenyewe huko bungeni
 
Waache utapeli wa kijinga, hakuna sheria yoyote inatungwa na bunge, sheria zote zinatungwa na serikali, hilo bunge ni rubber stamp tu.
 
Hahahahaha hii nchi inachekesha mbongo aache kujadili maisha ya Wema afungue mswada wa kiingereza ausome na autolee maoni?

Ridiculous [emoji1787]
Yaani mwananchi atoke Katavi, Mtwara, e.t.c afunge safari kwenda Dodoma ukumbi na.9 kutoa maoni ya muswada wa sheria?
 
Back
Top Bottom