Mabadiliko ya Sheria: Rais, Makamu wake, Jaji Mkuu, Waziri Mkuu na Spika wa Bunge kutofunguliwa kesi Mahakamani

We kilaza kaa kimya. Kwanza Rais akiwa madarakani hashitakiwi kwa jinai yoyote. Pili mwanasheria mkuu atawasimamia hao viongozi kwa ishu ambazo watakuwa wanmeshitakiwa wakifanya kazi zao. Na imeruhusiwa kuwashitaki ila mashitaka yanapelekwa kwa Ag. Hata mpaka sasa Ag ndio huwa ana wakilisha viongozi wakishitakiwa kwa kazi wanazozifanya.
 
Wapinzani wasingesusia bunge la katiba huenda tungekuwa na katiba mpya!
Lakini akidi ilikuwa inatosha kupitisha katiba mpya baada ya wapinzani kutoka na bunge la katiba.Na nadhani ilishapitishwa inasubiri kuzinduliwa tu
 
Nyerere angekuwa hai angekuwa anatawala tena kwani angeisha kuwa ametoka BUTIAMA zamani!!! Hivi huko ccm hakuna wanaume wanaoweza kuthibiti udikteta huu wa Jiwe?
 
Huu uchaguzi wa 2020 inaelekea damu zitamwagika. Hali si nzuri Kuna wanaopigana kwa meno na kucha ili wabaki madarakani.
Hivi na wewe bado una damu ya kumwagwa?? [emoji12]
 
Mtu mwovu kwanza ni mwoga, na hutafuta namna ya kukwepa mkono wa sheria siku zote kutokana na maovu anayofanya. Tupaze sauti zetu kwa nguvu kupinga haya!
 
Ukiua kwa upanga sharti ufe kwa upanga. Say no kwa uvunjifu wa katiba na haki za raia.
 
Wapinzani wasingesusia bunge la katiba huenda tungekuwa na katiba mpya!

Usilaumu aliyesusia bila kutaja ambaye alibaki katika nafasi ya maamuzi. Kwani kuna jambo liliwahi kuachwa kuamuliwa kwa sababu ya mbunge kujitoa Bungeni??? Kuna uchaguzi uliwahi kusimama eti kwa sababu baadhi ya washiriki kukataa kushiriki?

Demokrasia tulionayo inawapa nguvu ya maamuzi wengi. Na wengi ndio walibaki. Swali la msingi ni walipobaki walifanya nini.

Hujui kuwa walikuja na rasimu mbadala? Nini kimeendelea kuhusu hiyp rasimu. Kuwa na dhamira safi moyoni wakati ukilaumu aliyejitoa bila kujali aliyebaki alifanya nini.
 
Nadhani pengine Bashite anaandaliwa mazingira ya kupewa uwaziri mkuu ili hiyo sheria ije imkinge.
 
Hata waweke katiba ya kutokufa,yote ni bure tu zaidi inategemea na ajae Kama ataamua kulipiza kisasi hawana pa kuchomokea.Mfumo ukishakutupa huna chako waweza fanywa chochote
 
Watu wamefanya ukatili kisha wanajitungia sheria ili kulinda uharamia wao. Kibaya zaidi wanatunga sheria za kujilinda, lakini hawataki katiba ya wananchi! Hapa ndio vyama vya upinzani wanapaswa kupiga kelele za kutosha.
Pia ikipita watatutesa sana kuliko awamu iliyopita
 
Halafu bado kuna mtu na akili zake timamu atakuja hapa kupongeza CCM na mwenyekiti wake.

Sasa wakipitisha hiyo sheria kama watakavyo, kutakuwa na tofauti gani kati ya Viongozi wa serikali ya sasa na ile ya kikoloni?!
 
Watu wamefanya ukatili kisha wanajitungia sheria ili kulinda uharamia wao. Kibaya zaidi wanatunga sheria za kujilinda, lakini hawataki katiba ya wananchi! Hapa ndio vyama vya upinzani wanapaswa kupiga kelele za kutosha.
Watanzania tunawabeza sana wapinzani,Mimi nawashauri wapinzani nyamazeni kimyaaaaaa,msiseme lolote kuhusu hili,wacheni wapitishe mambo yao,wapeleke na muswada mwingine wa kuwaabudu wao Watanzania tuko tayari tutawaabudu tu.
 
Halafu bado kuna mtu na akili zake timamu atakuja hapa kupongeza CCM na mwenyekiti wake.

Sasa wakipitisha hiyo sheria kama watakavyo, kutakuwa na tofauti gani kati ya Viongozi wa serikali ya sasa na ile ya kikoloni?!
Kinga ya kutoshtakiwa si Kinga ya kutolipwa kulingana na matendo yako.
Ukiwatendea mabaya wenzio jiandae tu kulipwa mabaya yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…