Mabadiliko ya Sheria: Rais, Makamu wake, Jaji Mkuu, Waziri Mkuu na Spika wa Bunge kutofunguliwa kesi Mahakamani

Mabadiliko ya Sheria: Rais, Makamu wake, Jaji Mkuu, Waziri Mkuu na Spika wa Bunge kutofunguliwa kesi Mahakamani

Nimeandika nkafuta, nkandika tena nkafuta.

Kweli miaka 60 baada ya uhuru tunawaza kupeleka miswada bungeni ya kuwalinda viongozi kwa makosa yao wanapokuwa madarakani, tena karne ya 21??? Dah![emoji854][emoji6]
 
06 JUNE 2020
Utawala wa Sheria

Uchambuzi wa Mswada Na. 3 wa Mwaka 2020, mtaalamu wa sheria afafanua



Uchambuzi wa Mswada Na. 3 wa Mwaka 2020 Mei 29, 2020, Bunge la Tanzania limekaribisha wadaua na wananchi kutoa maoni yao kuhusu Mswada Na. 3 unaorekebisha sheria mbalimbali ikwemo Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu, 1994 (BRADEA) na Sheria ya Uongozi wa Mahakama namba 4 ya 2011.

Moja ya mambo yanayopendekezwa katika mswada huo wenye lengo la kubadili sheria 13 ni pamoja na kuongezwa kinga ya kisheria kwa Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika wa Bunge, na Jaji Mkuu kutokushitakiwa moja kwa moja na badala yake mashitaka kuelekezwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mapendekezo hayo pia yanapekwenda kuwapa kinga wafanyakazi wa mahakama, ambapo kinga hiyo ikitumika vibaya itapelekea uvunjifu mkubwa wa haki. Tazama uchambuzi huu kisha toa mano yako.

Source : HAKI TV
 
June 9, 2020
Dodoma, Tanzania

MBUNGE ATAKA RAIS ALAZIMISHWE KUONGEZEWA MUDA HATA KAMA HATAKI "ATAKE ASITAKE TUTAONGEZA MUDA-NDUGAI
Spika aunga mkono hoja , ahaidi katiba inaweza kubadilishwa maana Bunge lina mamlaka ya kubadilisha katiba ikiwemo muda wa Rais kukaa madarakani kama pendekezo litawasilishwa Bungeni

 
Mfano kuweka kinga ya kutokushtakiwa kwa viongozi waandamizi.Kwangu hili si tatizo.Hata akishtakiwa,sioni ni jinsi gani hiyo itabadilisha maisha yangu.Mungu atahukumu yeye mwenyewe kwa haki.

Kuongezewa Rais muda wa kuongoza nchi.Naam,waongeze tu.Kama aishivyo Mungu wangu,sielewi hata sekunde chache zijazo nitakuwa hai au mfu.Ni nani ajuaye?Mungu mwenyewe atahukumu kwa haki.Akiruhusu,mimi ni nani nikatae?Akikataa,hata kama mtu atakubali,hakuna anayeweza kushindana naye
 
Ila kweli maana hiyo nafasi yenyewe ni moja tu haiwezekani wote kupata hata tungekuwa tunabadilisha kila mwaka,kuna watu wametumia nguvu muda na mali zao ila hawakupata hiyo nafasi. Tatizo ni kwamba wanaoonekana kung'ang'ania na wanaopinga hilo jambo wote wana tatizo aina moja.
 
Naomba kuuliza mbona cheo cha Makamu wa Rais hakipo kwenye orodha ya viongozi wasioshtakiwa baada ya kustaafu??

Ikumbukwe Bunge la 11 katika shughuli zake imependekeza kufanya mabadiliko ya sheria mbalimbali ikiwemo ya kutoshtakiwa kwa Rais, Jaji Mkuu, Spika, Naibu Spika na Waziri Mkuu, kama katika kutekeleza majukumu yao ikatafsiriwa kutenda kinyume na Katiba ya nchi.
 
Mfano kuweka kinga ya kutokushtakiwa kwa viongozi waandamizi.Kwangu hili si tatizo.Hata akishtakiwa,sioni ni jinsi gani hiyo itabadilisha maisha yangu.Mungu atahukumu yeye mwenyewe kwa haki.

Kuongezewa Rais muda wa kuongoza nchi.Naam,waongeze tu.Kama aishivyo Mungu wangu,sielewi hata sekunde chache zijazo nitakuwa hai au mfu.Ni nani ajuaye?Mungu mwenyewe atahukumu kwa haki.Akiruhusu,mimi ni nani nikatae?Akikataa,hata kama mtu atakubali,hakuna anayeweza kushindana naye

Siku akipatikana Rais akaamua mfano unaishi jirani na makazi yake kuwa nyumba zote ikiwemo za ukoo wenu zivunjwe kwa kuwa anataka kujenga kiwanja 'chake' cha ndege ndipo utajua maana na umuhimu wa sheria ya kuwadhibiti na kuwawajibisha. Hilo ni dogo, viongozi wanaweza wakafanya mambo ya ajabu zaidi ya mfano huo ukisoma historia za watawala ulimwenguni na ktk vitabu vya imani.
 
MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wamepinga muswada wa sheria wa marekebiaho ya sheria mbalimbali nchini namba 3 wa mwaka 2020.

THRDC na LHRC wametoa tamko la kupinga muswada huo leo Alhamisi tarehe 4 Juni 2020 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema katika mswada huo kuna marekebisho ya Sheria ya utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu ya 1994 (BRADEA).

Olengurumwa amesema, marekebisho ya kifungu Kifungu namba 4 cha BRADEA kinarekebishwa na kusomeka kwamba, maombi ya kufungua kesi Mahakama Kuu hayatakubaliwa endapo hayajaambatanishwa na kiapo cha mlalamikaji kuelezea jinsi alivyoathiriwa na uvunjifu wa haki na wajibu katika ibara ya 12 hadi 29 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977.

“Tumekuwa tukipeleka kesi ya kulalamika ukiukwaji wa haki za binadamu uliopo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 12 mpaka 29, sasa kwa mujibu wa mabadiliko ambayo yanakuja sasahivi ni lazima uwe na cheti cha kiapo cha kuonyesha kiasi gani wewe mwenyewe umeathirika na ukiukwaji huo,” amesema.

Amesema, Kifungu namba 7(4), ikiwa malalamiko ya uvunjifu wa haki unaelekezwa kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania au, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika wa Bunge, au Jaji Mkuu wa Tanzania, malalamiko hayo yatafungliwa dhidi ya mwanasheria mkuu wa serikali ikiwa na maana hakutakuwa na uwezekano wa kufungua kesi dhidi ya viongozi hao.

View attachment 1468939

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa (wakwanza kulia), Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga (Wapili kulia).

“Sasa hivi, tuna kesi nyingi tumefungua dhidi ya Spika na kuna kipindi Rais alifunguliwa kesi na akina Fatma Karume na Ado Shaibu hizo zote zitaondolewa maana yake Tanzania hatutaweza kumshtaki mtu kama yeye kwa kukiuka Katiba,” amesema.

Aidha, Olengurumwa amesema sheria nyingine ambayo inaelekea kufanyiwa mabadiliko ni sheria ya uongozi wa Mahakama namba nne ya 2011.

Amesema, kifungu namba 64 (a) cha sheria hiyo kimerekebishwa na kuandikwa kuwa mfanyakazi yoyote wa mahakama hatoshtakiwa kwa jambo lolote atakalolifanya au kutolifanya kwa nia njema atakapikuwa anatekeleza majukumu yake.

“Hii inaweka kinga kwa mtu yoyote alioko mahakamani hata kama si Jaji au Hakimu na madhumuni ya marekebisho hayo ni kuipa mahakama nguvu ya kukataa maombi ambayo hayajakidhi matakwa ya ibara wao ndio wanadai hivyo.”

“Madhumuni ya marekebisho haya yanakwenda kuondoa nguvu za mtu mmoja mmoja au taasisi kama zakwetu kufungua kesi kwa sababu ya kulinda haki zozote zinazokiukwa Tanzania na hii ni kinyume na ibara ya 26 ya Katiba ya Tanzania ambayo imemruhusu mtu yoyote kwenda mahakamani kudai haki,” amesema.

Kwa upande wake, Anna Henga, Mkurugenzi Mkuu wa LHRC, amesema mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya utekelezaji wa haki za msingi na wajibu yanapingana na ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Baada ya Tanzania kujitoa kwenye mahakama ya Afrika sasa Azaki hatuwezi kwenda huko sasa hata kwenye mahakama za ndani hatutaweza kwasababu sheria hii inaweza kuzuia haki hiyo,” amesema.

Hata hivyo, Henga amesema marekebisho anayaona kama ni muendelezo wa kutaka kunyima haki kwasababu hata sababu za Tanzania kujitoa katika mahakama ya Afrika hazijajulikana hadi sasa.

“Ni kitu cha ajabu sana kwamba Afrika Mahakama ipo nyumbani kwako kama inakuletea heshima wewe ndo unayeitunza halafu unajitoa kwanini? hata hii, unaweza ukashangaa ni kwanini wazuiwe watu ambao wanataka kutetea haki za watu? Ukitafsiri kikawaida maana yake haki itavunjwa zaidi,” amesema.

THRDC na LHRC wametoa wito kuwa mapendekezo hayo ya mabadiliko ya Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Kimsingi na Wajibu yaondolewe kabisa Bungeni kwakuwa maandalizi ya mapendekezo hayo hayakuhusisha
kabisa wadau mbalimbali wakiwemo wadau wa haki za binadamu tangu mwanzo.

Aidha, wamesisitiza kuwa kifungu cha mapendekezo ya sheria kinachotaka kutoa kinga kwa wafanyakazi wote wa Mahakama kutokushtakiwa kirekebishwe na kinga hiyo iendelee kuwepo kwa Majaji na Mahakimu pekee kwa mujibu wa Katiba.

Muswada huo unaopendekeza mabadiliko makubwa ya sheria mbalimbali ambayo THRDC na LHRC wanalaani wakieleza kuwa yanalenga kuondoa haki ya kufungua kesi za kikatiba kwa niaba ya wananchi, uliwasilishwa bungeni na umepangwa kujadiliwa kwenye mkutano wa 19 wa Bunge (Mkutano wa Bajeti) ambao ulianza tarehe 05 Mei na utamalizika
Juni 19 mwaka 2020.


Wananchi wote tuwe na kinga

These motherfuvkers want to get away with murder...

Wanajipotezea muda tu,....wenyewe wafanye crime tu....tukiingia tunafunga wote wether watake au wasitake....

Upumbavu huu
 
Kwa upande wangu sijaelewa Magufuli kupeleka muswada bungeni wa kutoshitakiwa yeye na viongozi wote wa mihimili ya nchi kwa makosa wanayofanya wakiwa madarakani.

Inakuwaje mtu muadilifu, mcha Mungu, kiongozi wa wanyonge, mtu asiyependa rushwa na ufisadi akawa muoga wa kushitakiwa? Una hofu na uwoga gani unatarajiwa kufanywa au ushafanywa hadi kujiwekea kinga kubwa kiasi hicho?

Bila shaka anatuambia yeye sio msafi hata kidogo kwa sababu ukiwa wewe ni msafi unapata uwoga gani wa kushitakiwa?
 
Kwa upande wangu sijaelewa Magufuli kupeleka muswada bungeni wa kutoshitakiwa yeye na viongozi wote wa mihimili ya nchi kwa makosa wanayofanya wakiwa madarakani.

Inakuwaje mtu muadilifu, mcha Mungu, kiongozi wa wanyonge, mtu asiyependa rushwa na ufisadi akawa muoga wa kushitakiwa? Una hofu na uwoga gani unatarajiwa kufanywa au ushafanywa hadi kujiwekea kinga kubwa kiasi hicho?

Bila shaka anatuambia yeye sio msafi hata kidogo kwa sababu ukiwa wewe ni msafi unapata uwoga gani wa kushitakiwa?
Nyerere hakutaka hakuogopa japo kuna watu waliumia wakati wa vijiji vya ujamaa
 
Basi mimi nlijua rais ata akitoka madarakani hawezi kushtakiwa apa kwetu. Kumbe waliopita tunaweza kuwashtaki?
 
Kwa upande wangu sijaelewa Magufuli kupeleka muswada bungeni wa kutoshitakiwa yeye na viongozi wote wa mihimili ya nchi kwa makosa wanayofanya wakiwa madarakani.

Inakuwaje mtu muadilifu, mcha Mungu, kiongozi wa wanyonge, mtu asiyependa rushwa na ufisadi akawa muoga wa kushitakiwa? Una hofu na uwoga gani unatarajiwa kufanywa au ushafanywa hadi kujiwekea kinga kubwa kiasi hicho?

Bila shaka anatuambia yeye sio msafi hata kidogo kwa sababu ukiwa wewe ni msafi unapata uwoga gani wa kushitakiwa?
Acha mzuka we, Magu hajaiweka yeye, ameikuta ipo tangu na tangu! Huo mzuka peleka ufipa!
 
Kwa upande wangu sijaelewa Magufuli kupeleka muswada bungeni wa kutoshitakiwa yeye na viongozi wote wa mihimili ya nchi kwa makosa wanayofanya wakiwa madarakani.

Inakuwaje mtu muadilifu, mcha Mungu, kiongozi wa wanyonge, mtu asiyependa rushwa na ufisadi akawa muoga wa kushitakiwa? Una hofu na uwoga gani unatarajiwa kufanywa au ushafanywa hadi kujiwekea kinga kubwa kiasi hicho?

Bila shaka anatuambia yeye sio msafi hata kidogo kwa sababu ukiwa wewe ni msafi unapata uwoga gani wa kushitakiwa?
Kwani shida ipo wapi mkuu. Si yeye mwenyewe amekwishaonyesha mifano kadhaa?

Kwani sheria inapotungwa haiwezi tunguliwa?

Labda useme huyo anayetakiwa kuhakikisha na kuona haki zikitendeka naye awe bwege!

Sioni tatizo kwa hizi sheria mbovu kutunguliwa kama anayeheshimu haki anaamua kuzitupilia mbali na kuwawajibisha waliojitungia sheria ziwalinde kwa kufanya maovu.
 
Inashangaza sana..
Raisi pendwa wa dunia, muadilifu, mnyenyekevu, mpenda wanyonge, mzalendo, msomi, anayechukia wapiga dili..........

Everyday is Saturday.......................... 😎
 
Kwa upande wangu sijaelewa Magufuli kupeleka muswada bungeni wa kutoshitakiwa yeye na viongozi wote wa mihimili ya nchi kwa makosa wanayofanya wakiwa madarakani.

Inakuwaje mtu muadilifu, mcha Mungu, kiongozi wa wanyonge, mtu asiyependa rushwa na ufisadi akawa muoga wa kushitakiwa? Una hofu na uwoga gani unatarajiwa kufanywa au ushafanywa hadi kujiwekea kinga kubwa kiasi hicho?

Bila shaka anatuambia yeye sio msafi hata kidogo kwa sababu ukiwa wewe ni msafi unapata uwoga gani wa kushitakiwa?
Swali la msingi kabisa hili na wangekupata wangekuvunja shingo.
 
Back
Top Bottom