Mimi ni mwana CCM, Lakini kwanini tunabadili sheria kwa kuangalia manufaa ya wachache badala ya manufaa ya Taifa
Kipengele cha Undercover kimeongezwa ghafla kwenye sheria ya Criminal procedure Act Cap 20 section 47 Subsection 47A, Lengo kuwa police waliohusika kwa siri kwenye uchunguzi wa uhalifu wasiwe sehemu ya uharifu huo
Sheria inapasa iangalie mbele na sio kuangalia matukio ya watu wachache
Mapendekezo yanayopelekwa Bungeni tena kwa tangazo la Bunge la ghafla watu wakatoe maoni kwa siku moja Dodoma yanalenga kitu gani?
Someni mabadiliko hayo kwa umakini sana sana, Msije baadae mkaanza kulaumu Serikali.
View attachment 2105978
Serikali imepeleka Bungeni mabadiliko ya sheria mbalimbali, ni muhimu watu mkasome vizuri hizi sheria
Luteni Urio na wenzake baada ya kubanwa mahakamani ilionekana moja kwa moja wao ndio waliotengeneza hiyo picha ya kesi ya Mbowe kwa kuwatafuta Makomandoo ili wakafanye uharifu
Fuatilia vizuri Mahojiano ya Kibatala na Urio utangundua Urio anajitetea yeye kama Undercover
Kwa sheria hii ikipita Urio hiyo kesi haimuhusu anaokoka mapema sana, Ongezeko la neno Undercover kwenye sheria hii moja kwa moja Urio na wenzake hawahusiki na kesi hii ya Mbowe