Mkuu, Mabasi yaliyofungiwa ni 14 tu. Dar Express wana mabasi zaidi ya 20. Watu wengine wameshkilia mtazamo wa hujuma dhidi ya Dar express bila kufanya hata kautafiti kadogo tu. Sio siri, kama wewe ni mtumiaji wa mara kwa mara wa mabasi ya Dar Express, utakuwa umegundua kuwa ubora wa huduma ya baadhi ya mabasi hayo imeshuka sana katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Mimi ni mteja mzuri tu wa kampuni hii. Huwa ninapanda Dar Express walau mara mbili kila mwezi( Dar- Arusha, Arusha -Dar). Katika safari zangu mbili zilizopita, safari yetu iliishia njiani - kisa ubovu wa gari. Tumetoka Dar, kufika chalinze gari ikaanza kuvuja oil sana. Jamaa wakapambana nayo ikatulia. Tulipofika mombo( Mkumbara?), bodi ikakatika na kulalia tairi za nyuma. Hapo ikawa mwisho wa safari yetu. Sikukata tamaa, nikaunga unga safari hadi Arusha. Niliopomaliza shughuli zangu nikaamua kurudi Dar kwa kutumia tena . Njiani pancha mara tatu. Tukafika mahali, gari ikienda spidi zaidi ya 80, inayumba sana. haya mambo hayakuwepo siku za nyuma! Isitoshe, kuna baadhi ya madereva wao ni wakorofi mno. mmoja alikuwa akienda kwa kasi sana. Abiria tukapiga kelele. Akapunguza mwendo, akawa anatembea spidi ya kilomota 40 kwa saa- kutoka Segera hadi chalinze!
Ushauri kwangu kwa mzee Mremi: Ajitahidi kudumisha viwango vya ubora alivyoanza navyo; Awalipe madereva wake vizuri na aweke mfumo mzuri wa kufuatilia maoni kutoka kwa wateja wake.