Mabasi ya 'Dar Express' yanahujumiwa?

Mabasi ya 'Dar Express' yanahujumiwa?

Mkuu, Mabasi yaliyofungiwa ni 14 tu. Dar Express wana mabasi zaidi ya 20. Watu wengine wameshkilia mtazamo wa hujuma dhidi ya Dar express bila kufanya hata kautafiti kadogo tu. Sio siri, kama wewe ni mtumiaji wa mara kwa mara wa mabasi ya Dar Express, utakuwa umegundua kuwa ubora wa huduma ya baadhi ya mabasi hayo imeshuka sana katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Mimi ni mteja mzuri tu wa kampuni hii. Huwa ninapanda Dar Express walau mara mbili kila mwezi( Dar- Arusha, Arusha -Dar). Katika safari zangu mbili zilizopita, safari yetu iliishia njiani - kisa ubovu wa gari. Tumetoka Dar, kufika chalinze gari ikaanza kuvuja oil sana. Jamaa wakapambana nayo ikatulia. Tulipofika mombo( Mkumbara?), bodi ikakatika na kulalia tairi za nyuma. Hapo ikawa mwisho wa safari yetu. Sikukata tamaa, nikaunga unga safari hadi Arusha. Niliopomaliza shughuli zangu nikaamua kurudi Dar kwa kutumia tena . Njiani pancha mara tatu. Tukafika mahali, gari ikienda spidi zaidi ya 80, inayumba sana. haya mambo hayakuwepo siku za nyuma! Isitoshe, kuna baadhi ya madereva wao ni wakorofi mno. mmoja alikuwa akienda kwa kasi sana. Abiria tukapiga kelele. Akapunguza mwendo, akawa anatembea spidi ya kilomota 40 kwa saa- kutoka Segera hadi chalinze!

Ushauri kwangu kwa mzee Mremi: Ajitahidi kudumisha viwango vya ubora alivyoanza navyo; Awalipe madereva wake vizuri na aweke mfumo mzuri wa kufuatilia maoni kutoka kwa wateja wake.
Mremi.jpg Dar express.jpg dar express1.JPG
 
kwa bwana yesu kila goti litapigwa

VITa vyetu si juu ya damu na nyama bali ju ya falme na mamlaka za pepo wa chafu wa serikali hii ya tanzania...hatimae tutashinda wachaga msiwe na hofu kwa hili ""KWA BWANA YESU KILA GOTI LITAPIGWA"""
 
Ilipofikia ni kama ilivyofikia Scandnavian Express, maana Scandnavia mwishoni mwishoni magari yake yalikuwa mabovu mabovu!
 
Ladba mwanae anataka kuweka magari yake pande hizo kwahiyo anatumia wadhifa wa baba
 
sasa hii ni wewe au?maana umetupa mtihani kidogo....
hii ni mimi mwana wa Umslopogas,nimeshabadili password labda wahack tena..nimeinukuu kwani imeandikwa kwenye kila basi la DE..Ulale unono
 
Kweli Mungu ndiye atakaye mtetea na kumshindia ktk hili
 
Tujuze hizo hujuma kwa sababu wengine kama mimi nimeachwa nja panda
Mweeee mimi hata sijaambulia sijui niko wapi najuta kuingia kwenye hii sridi maana sijui nimeingilia mlango hupi na nitatokea mlango gani nakuomba muanzishaji wa mada hutupe kwa mhutasali japo kiduchu!!
 
Wana JF bwana, Serikali ikifanya kazi mashaka, isifanye kazi mashaka, humu ndani tunalalamika kila siku juu ya ajali za barabarani, serikali imeona kasoro kwenye magari ya Dar Exprss na kuchukua hatua mnaona sio, sababu? Mchaga ndiyo mwenye kumiliki. Mlitaka mpaka roho za watu zitoke ndio mseme mabasi yale yalikuwa yamechoka? Sio kila kitu siasa! Mkiendelea namna hii mtakuwa mnaishusha sana JF na watu makini watapotea hapa na kubaki kuwa kijiwe cha wahuni!
 
VITa vyetu si juu ya damu na nyama bali ju ya falme na mamlaka za pepo wa chafu wa serikali hii ya tanzania...hatimae tutashinda wachaga tusiwe na hofu kwa hili ""KWA BWANA YESU KILA GOTI LITAPIGWA"""NEEMA ZA MUNGU
 
VITa vyetu si juu ya damu na nyama bali ju ya falme na mamlaka za pepo wa chafu wa serikali hii ya tanzania...hatimae tutashinda wachaga tusiwe na hofu kwa hili ""KWA BWANA YESU KILA GOTI LITAPIGWA"""NEEMA ZA MUNGU
 
haya mabasi nayo yaishakuwa ya hovyo na yamezeeka,nlikuwa mteja wao sana,walinitibua wiki 2 zilizopita,nimepanda basi lao la kwanza,ar-dsm saa 1145 lakini tukafika dar saa 1800,hata kilichonifanya niwahi sikufanikiwa,facken!nimehamia kilimanjaro,atleast
 
1. Dar express ana mabasi 47 Jumla. Je kati ya haya ni mangapi mabovu??????
2. Sehemu ya Kula Highway.. Korogwe.. ya huyu Mzee is the CLEANEST in Tz haswa Vyooni.. Wengine inabidi waige.

Ukweli na Uhuwa haviwezi kukaa pamoja!
 
haya mabasi nayo yaishakuwa ya hovyo na yamezeeka,nlikuwa mteja wao sana,walinitibua wiki 2 zilizopita,nimepanda basi lao la kwanza,ar-dsm saa 1145 lakini tukafika dar saa 1800,hata kilichonifanya niwahi sikufanikiwa,facken!nimehamia kilimanjaro,atleast

Naungana na wewe. Exactly same experience twice.
 
Wakuu ni kweli hata mm mwenyewe nimeongea na mtu w karibu na Mr.Mremi ,ni kwamba kuna mabasi yanahitaji kupumzishwa na yamekuwa yakimletea hasara sna,ndani ya mwaka mmoja yemesababisha ajali ndogo ndogo na kufia barabarani.so hamna fitna wala nini.
 
Back
Top Bottom