"Mabeberu" Marekani waanza mbinyo kwa Tanzania. Washawishi Serikali yao na Jumuiya ya Kimataifa kuanza vikwazo na kukata misaada

Naona kama watu wanafurahia hii hali,hii nchi ilipitia changamoto nyingi hasa baada ya vita vya Kagera.Hata hapa tutavuka kwa uweza wa Mungu.Mbona kwenye Corona tumetoboa?Huyu hawezi kupendwa na hao wazungu baada ya kuwaminya kwenye rasili mali,unafikiri hana ripoti kinachoendelea anajua.
 
Usiifananishe Tanzania ya sasa na China, bado hatujawafikia wale watu.

Hao investors ndio wanakuwa frustrated everyday, wanasema tu midomoni wanavutia wawekezaji lakini matendo yao yana suggest tofauti, mfano Dangote.
Wengi hizi siasa za kiafrika hamzielewi na mnazivamia kwa pupa. Expections mnazoweka kwa wababe wa nje ni kubwa kuliko uhalisia. Matokeo yake ni msongo wa mawazo wa kujitakia.
 
Ingekuwa kuwa kweli na sio tafsiri ya "saccos" ingetoka kwenye official web site ya serikali ya USA
 
Ingekuwa kuwa kweli na sio tafsiri ya "saccos" ingetoka kwenye official web site ya serikali ya USA
 
Inaonekana honey moon ya ushindi inaelekea itaishia na huzuni!
Shida ya wamarekani wanataka sana ushoga, sijui walimuonja nani mtanzania mpaka wakagundua kuwa sisi tuna joto zuri, watuache, watafute waliowagongagonga
 
Unafurahia nini sijui we mwenyewe umo humu humu unakaa hapo Kimara
 
hwa wanaanza kidogokidogo then raia wanaanza kusikia ule mbinyo hapo tena haihitaji chama cha siasa kuongea na watu watu wanaongea wenyewe ,imagine leo waminye ARV unajua hali itakuwaje?wangapi wanaweza kumuda 150,000 kwa mwezi ya vidonge?
 
Lissu bwana, hivi Mnyaturu wewe una ishu gani na nchi yetu, mbona una hasira hivyo?
tabia ya kuwa isolate watu waziwazi na kuonyesha upande mmoja kwamba nyie ni takataka tu,ni mbaya sana sana tena saaana haitasaidia lolote zaidi ya kuwafariji walioshika mpini wa sime kwa miaka kadhaa ila damage yake ni kubwa,silaha kubwa hata ya familia maskini ni upendo na umoja otherwise...
 
Mku Professor alishindwaje kuwashawishi UN kwa ripoti mbaya tuyopewa.
Kwa ujumla hatuko vizuri kidiplomasia kwa hiyo tutegemee lolote kwani jeuri ndo mwanzo wa yote haya. Tumwombe Mungu atupe Moyo wa kuyapokea kwa uvumilivu
 
Uelewa wa watu wengine humu ni mdogo sana, unalingana na yule aliyeiba kura,ngoja tuone huko mbeleni jinsi tunavyoenda kusamabaratika kama zimbabwe
 
Usihofu ndugu yangu, sababu zenyewe walizozitoa hao wapinzani na hao watu wa Amnesty International na ma NGOs ni sababu za kipuuzi sana ambazo haziwezi kuifanya serikali ya Marekani, UN au EU kuiwekea Tanzania vikwazo vya kiuchumi.

Kwenye report hii wamezungumzia mambo mengi sana kuhusu malalamiko ya wapinzani na hasa CHADEMA na ACT Wazalendo na kidogo CUF, lakini pia NGOs na watu wa haki za binadam ikiwemi majournalists uchwara.

Ukweli ambao usioweza kupingika ni kwamna hayo yaliyo andikwa humu ni kama maneno ya kijiweni yasiyo kuwa na uzito mkubwa wa kuyaamini. Ninporojo tu za kipashkuna pashkuna.

References zao nyingi ni za kutoka kwenye magazeti uchwara kama ya chama cha TWAWEZA ambacho duniani hakijurikani.

Kwa kifupi serikali ya Marekani haioni sababu yoyote ya kimsingi ya kuiwekea Tanzania vikwazo vya uchumi. Watanzania kwa ujumla wanaishi vizuri na hakuna mtu ananyanyasika au kunyanyaswa na serikali yake.

Magufuli anafanya kazi nzuri ya kuwaletea wananchi wake maendeleo. Sisi hatukuwanyang'anya mashamba watu wao kama Zimbabwe ilivyo fanya na wala serikali yetu haiwasulubu watu wake kwa hiyo ni porojo tu za vilabuni ambavyo havina mantik.

Off course NGOs na taasisi za kimataifa kama Amnesty International ambavyo vilitarajia kusikia su kuona vurugu zetu zijitokea, hazita jisikia vizuri kwa sababu hawawezi ku operate Tanzania kwa faida. Kama kujilisha tuna jilisha sisi wenyewe na hatutegemei sana misaada ya nje kwa vyakula.

Mahusiano ya kibiashara na nchi za nje yanaendelea kama kawaida na mikopo kutoka World Bank na IMF tutaendelea kupata vile vile tukiihitaji.

Kwa report hii mimi naona wapinzani ambao ni radicals, wanaharakati kama akina Maria Sarungi, Fatma Karume na wengineo ambao walitegemea sisi tuwekewe vikwazo vya uchumi wameshindwa vibaya sana na hawana hamu tena ya maisha. Ningewaomba watafute sttategy nyingine lakini sio ya haki za binadam.

Wao wanafikiri ulimwengu hauoni mambo yanayotendeka Tanzania. Ulimwengu unajua kila kitu kinachofanywa na serika ya magufuli. Kama magufuli angekuwa anafanya vitu vibaya wananchi wake vyombo vyao vya habari kama CNN International, BBC International na Al Jazeera wangekuwa wanareport kila siku mambo yanayo tokea huku. Lakini mambo ya kikekike na ya kishogashoga ya akina Zuhura Yunus, Salim Kikeke na Mary Mgawe wa VOA kwa kiswahili mnafikiri nani anayasikiriza, ni sisi tu na majiranibzetu wakenya wakongo na uganda kidogo.

Watu wakubwa wanao tuchafulia nje ni hawa Amnesty International walioko Kenya wakishirikiana na wapinzani wetu hasa CHADEMA, ACT na CUF.
na NGOs wachwara wa Europe hasa wa ujerumani.
 
hwa wanaanza kidogokidogo then raia wanaanza kusikia ule mbinyo hapo tena haihitaji chama cha siasa kuongea na watu watu wanaongea wenyewe ,imagine leo waminye ARV unajua hali itakuwaje?wangapi wanaweza kumuda 150,000 kwa mwezi ya vidonge?
Kuna post nimesema hivi vikwazo vitatuumiza zaidi sisi familia maskini na siyo Raisi Magufuli au Lissu na wenzie.
Raisi hadi kufa kwake yeye na mkewe watapata huduma bora kwa fedha zetu.
Lissu na wenzie na familia zao wataenda Ulaya na Marekani, watapewa fedha za ufadhili kujikimu na kufanya harakati, watasomeshwa watoto wao nje lakini tusio wanasiasa na ndugu zetu maskini huko vijijini ndiyo tutapata adha itokanayo na vikwazo.

Hata akiondoka Raisi Magufuli madarakani bado athari za vikwazo zitatutesa miaka mingi ijayo. Mfano Zimbabwe Morgan Tshovingirai na Bob Mugabe wameshakufa lakini vikwazo bado vinaitesa Zimbabwe.

Tutafute namna nyingine ya kudai haki au mabadiliko. Hii ya Sasa ya kuichafua nchi na kutaka vikwazo siyo nzuri kwa yeyote zaidi ya kufurahisha watu binafsi mmoja mmoja walipa visasi.

Nafikiri ndiyo maana watu hawaja andamana wameona mbali..
Watanzania siyo wajinga kiasi hicho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…