Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

Jiwe alisaga akili za watu wengi hapa nawaza angekuwa hai mpaka amalize muda wake nakujiongezea sijui tungekuwa na Taifa la watu gani

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Na wanasahau ni huyu huyu ndie alituambia serikali wenyewe tuna uwezo wa kujenga copper smelter inayohitajika na Acacia. Na watu tuliposema kwamba hizo ni porojo tu, misukule yake kama kawaida ikaishia kumwaga matusi tu!

Matokeo yake, hadi umauti umemkuta, hata "tofali" moja hawajajenga!
 
Asante sana, Mkuu kwa maelezo yako.

Redbold: Ukosefu huu wa taarifa za ndani ndiyo unasababisha stofahamu kwenye mradi wa Bagamoyo. Kutegemea kuunganisha dots pekee kufanya majumuisho ya jumla ni kunaongeza urefu wa mjadala. Kwa sababu watu wengi wanao uwezo na mbinu za kuunganisha dots ili wafanye majumuhisho wanayoyataka. Nina imani tupo pamoja katika hili.

Jambo rahisi kabisa kupunguza urefu wa mjadala huu ilikuwa ni kuweka makubaliano kwenye suala/mradi hili/huu wazi. Hivi kitu chema kwa nini kifichwefichwe...! Najua itasemwa, kuweka wazi kila kitu kitasababisha 'insecurity of project integrity specifically kwenye techno-economic strategies '.Sisi hatuhitaji technical and economic aspects za mradi tunataka kujua 'legal bound agreement' ya namna gani tutanufaika kama taifa vile vile si vibaya kujua China atanufaikaje. Mbona kwenye madini nchi na Barrick mambo yako wazi kiasi? Huku kuna nini kiasi tunategemea kuunganisha dots badala ya kupata taarifa za ndani?

Mkuu nadhani sasa umeelewa 'wasiwasi' wangu.
 
Wanyonge wanatapatapa walishazoea propaganda.Zama za camera za show off zilishapita
 
Hakuna evidence aliyokupa, soma vizuri amesema kwa taarifa zisizo rasmi... Na amesema siyo rasmi kwa kuwa alishindwa kupata taarifa rasmi. Tumia akili kibaraka wa beberu na Mchina wewe.
Uelewa wako mdogo mno!!!

Kila taasisi ina wasemaje wake!! Kwahiyo taarifa ukipewa na asiye msemaji, hiyo inaitwa taarifa zisizo rasmi! Usidhani taarifa zisizo rasmi za bandari zinatolewa na makuli, au watu wasio kwenye system!!!

Secretary anaweza kukupa taarifa! Wakati mwingine anaweza kukuonesha hata doc, lakini asikuachie kama attachment yako!

Kwavile huwezi kuitumia kama supporting doc, na aliyekupa hana mamlaka ya kufanya hivyo! Hiyo inaitwa taarifa isiyo rasmi, na wala huwezi kutaja source ya taarifa hiyo!!!
 
tunashukuru had
Tunashukuru kwa hadithi yako nzuri tu
Sasa ili mradi wa Bandari ufanikiwe ni lazima I mizigo iwepo ya kutosha, je kwa ilivyo tunayo mizigo kiasi hicho kihalali uwepo wa Bandari ya Bagamoyo wawekezaji ni hapa naona tunataka kuleta hadithi ua yai ns kuku mama alianza
Pili tuna Bandari tatu ya Mtwara Dar na Tanga, je hizo hazitoshi

Tatu kama hizo 4th generation ships haiwezi kuingia Bandari tulizo nazo , kwanini hiyo Bandari ya Bagamoyo tusijenge in phases mfano ghati number moja kwanza n.k
 
Kwavile huwezi kuitumia kama supporting doc, na aliyekupa hana mamlaka ya kufanya hivyo! Hiyo inaitwa taarifa isiyo rasmi, na wala huwezi kutaja source ya taarifa hiyo!!
Labda kwenye counter-intel na mambo mengine kama hayo mbinu hii inaweza kufaa kwa sababu nidhamu ya uaminifu ni kubwa kwa wahusika. Lakini, kwenye 'public hearing' ambapo watu wanataka kushinda 'political trust' kwa wananchi, mbinu hii inaweza kutumika kama kichaka cha kusukuma ajenda ambazo zaweza kuwa na 'ill au healthy motive'. Sasa kuepusha mkanganyiko, mambo yawekwe wazi.

Kumbuka kwa namna yoyote ile sipingi jambo lolote litakalowezesha Tanzania kustawi katika nyanja zote lakini ikiwa imekita mizizi yake katika kujitegemea ki-kweli kweli.
 
Ila sie Afrika tusifanye miradi kwa sababu mchina kasema hv,au mzungu beberu kasema hv,na sie si tuna akili,tukune bongo,tutumie think tanks wetu ambao hawajawa compromised,maana nchi hii watu wananunuliwa kirahisi kweli,kwa kujengewa vyoo kwenye majimbo yao.
Ila huyu mchina unayemsifia ana tofauti na mchina aliyepo pale Urafiki Textile?
Maana wabongo wanaofanya kazi pale ni kama wapo utumwani,kuna umaskini wa kutisha,na kila spea mpaka fagio za chooni zinatoka China!!
 
And so hauwezi kutupa evidence... Hiyo haina tofauti na stori za vijiweni. Una shida gani kibaraka?
 
Mkuu nadhani haya mambo ameyafafanua. Wachina watakuja kujenga viwanda kwa ajili ya bidhaa zao hapo Bagamoyo....Sina hakika kama mizigo yetu pia itakuwa inapita hapo!
 
Man, haya mambo mnayakuza bure tu, na matokeo yake mnashindwa kuweka productive inputs!!! Hili taifa tayari lina sheria zake!!! Sheria zetu tayari zinataja ni kodi zipi huwa zina msamaha!!

Sihitaji kuona mkataba kutetea hoja kwamba, kodi zinazosemwa kutaka msamaha haziwezi kuwa kodi za uagizaji bidhaa, kama vile VAT on imported goods!!!

VAT always husamehewa kwenye imported capital goods!!

HAIWEZEKANI eti wewe uagize gari, halafu VAT achukue Mchina... hakuna kitu kama hicho!!

Ukiona umeagiza bidhaa, halafu hulipii VAT serikalini basi fahamu bidhaa hiyo tayari ipo kwenye kundi la bidhaa zinazosamehewa VAT!

Ingawaje kwa makusudi tu Kakoko hakusema ni kodi ipi, lakini nina uhakika mkubwa kwamba kodi kubwa kabisa anayoisema ni income tax!!!

Na income tax husamehewa ili kutompungumzia mwekezaji mapato yake anayopata kupitia dividends, cargo and ships handling, warehousing, n.k!

Huko kote Mwekezaji huwa anaingiza pesa ambazo kimsingi zinatakiwa zikatwe income tax!! Lakini Bakhresa kaingiza scania 200, halafu VAT on imported Scanias iende kwa Mchina? Hakuna kitu kama hicho!

Na usisahau, hii ni research iliyoongozwa na mtu mwenye uzoefu na miradi ya China Ulaya, Asia, na Afrika, kwahiyo anaongea kitu alicho na uzoefu nacho!!

Na hata anaposema "taarifa isiyo" rasmi, haina maana kwamba ni taarifa isiyo sahihi!

Aidha, nikipata wasaa, nitatafuta PR ya Mwakilishi wa China Merchant Group, ambae kwa kujiamini kabisa, alisema wazi wazi kwamba Kakoko ni muongo, na wala hakuwepo siku ya majadiliano!!!

Mbona Kakoko hakujitokeza tena mbele kupinga madai ya Mr. Moosa Mao?
Kwa bahati mbaya sana, HILO HALITAKUJA KUTOKEA... anyway, labda kwavile kuna utawala mwingine! Usisahau suala la mikataba kuwekwa wazi kimekuwa ndio kilio cha muda mrefu cha Wabunge, manake hata wenyewe wanashindwa kupewa hii mikataba!!
 
Ni wapi hapo nilipomsifia?! Na kama nimemsifia, hizo sifa ni sifa fake, au?!

Hivi kusema Bandari zinazoendeshwa na Mchina huwa zinafanya vizuri kwa sababu ana advantage ya ku-handle percent kubwa ya shehena inayopita baharini, hiyo ni kumsifia au ndo ukweli wenyewe?!

Au kuna mahali nimesema Mchina ni mtu mzuri kweli kweli?!
 
Ni ujinga kusifia uzuri wa matokeo ya mradi badala ya ubora wa Mkataba!!
 

Spika ni clueless kabisa, haya ni maoni binafsi. Naamini hajui pa kusimamia na ni mtu wa kuendeshwa tu asiyejua uzito wa nafasi yake.

Najiuliza hivi contents za mkataba yeye hana? Kwamba hajui vipengele vya hiyo mikataba hadi kusema walishauriwa vibaya, kwamba baada tu ya JPM kufariki ndio wamepata clue ya nini kilichojiri wakati ule! Ni watu wajinga tu ndio watawaamini watu wa nature ya Ndugai.
 
Ikiwa inajulikana NAGU na JK ndio wenye majibu inakuwaje wadau wanataka mleta mada ndio awaoneshe mkataba at

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
tunashukuru had

Tunashukuru kwa hadithi yako nzuri tu
Unajua nini?

I can understand you guys... thread yangu ni ndefu mno, na wengi wenu mmeshindwa kuisoma yote!!! Maswali uliyouliza nimeshayadili tayari!!!

Lakini kwavile I usually respect anayetoa hoja, tofauti na wale wengine wanaokuja hapa na kuanza matusi, bila kuzungumzia hoja yoyote, wacha niseme kwa uchache!
Sasa ili mradi wa Bandari ufanikiwe ni lazima I mizigo iwepo ya kutosha, je kwa ilivyo tunayo mizigo kiasi hicho kihalali uwepo wa Bandari ya Bagamoyo wawekezaji ni hapa naona tunataka kuleta hadithi ua yai ns kuku mama alianza
Nimeshasema plan ilikuwa kuifanya bandari kuwa transshipment port, na pili, ku-handle cargo itakayotokana na Industrial Complex.

We all know kwamba bidhaa za China ndizo zimesambaa kila kona Afrika kama sio duniani. Sasa kwa mfano, ukiona meli inatoka US kufuata mzigo China, usidhani zote zinafika China bali zinaishia Singapore ambayo ndiyo largest transshipment port!

Kinachotokea ni kwamba, mega ships kutoka Mashariki ya Mbali zinapakia mzigo China, Korea Kusini na Japan hadi Singapore ambako mzigo utapakuliwa na kuingizwa kwenye meli zingine kutoka sehemu mbalimbali duniani!!

Lengo la Bagamoyo, ilikuwa ndio hilo! Kwamba, badala ya meli kutoka SA, Mozambique, Kenya na sehemu zingine Afrika kwenda hadi Singapore au China, meli hizo zitafuta mzigo Bagamoyo unaoshushwa na meli kubwa kutoka Uchina!!

Lakini hata suala la transshipment lisipoanza mapema, bado tukumbuke bidhaa nyingi zinazoingia Afrika Mashariki na Kati, pamoja na Ukanda wa Maziwa Makuu zinatoka China!

Ni kutokana na hilo ndo maana mradi wa bandari ulikuwa uende sambasamba na ujenzi wa SGR ambao ingeiunganisha Bagamoyo, na zingine! Which means, mizigo ya China inayotoka China kuingia ukanda wetu, yote ingeshushwa Bagamoyo, na kutokea hapo ingesambazwa kwa njia ya reli kwenda nchi mbalimbali!

Lakini kwa upande mwingine, mradi pia ilikuwa uende sambasamba na ujenzi wa industrial complex kubwa sana. Kama plan ingeenda kama ilivyotarajiwa, ile complex ingezalisha bidhaa nyingi sana ambazo zingine zingesafirishwa kwa meli for export!
Pili tuna Bandari tatu ya Mtwara Dar na Tanga, je hizo hazitoshi
Nimeshasema, Mtwara ipo reserved for gas tankers, Tanga kuna miradi miwili. Je, HAZITOSHI?

Kwavile nimeshataja Tanga na Mtwara, swali liwe je, Dar haitoshi?!

Ngoja nikuulize: Tanzania ni maskini! Malawi ni Maskini! Rwanda, Burundi na Uganda ni maskini! In short, nchi zote zinazotumia bandari ya Dar es salaam ni maskini!

Pamoja na umaskini wetu huo, lakini bado bandari ya Dar wakati mwingine huelemewa! Sasa jiulize, endapo uchumi wa nchi unafikia angalau kama tu ule wa South Africa ambayo na yenyewe ni maskini; je unaamini Bandari ya Dar itaweza ku-handle uchumi kama huo?

REMEMBER... uchumi wa nchi hizi ukikua, utachochea more imports and exports! That being said, kama tunataka kuangalia miaka 50 ijayo, au angalau 25, I can confidently say HAZITOSHI!
Tatu kama hizo 4th generation ships haiwezi kuingia Bandari tulizo nazo , kwanini hiyo Bandari ya Bagamoyo tusijenge in phases mfano ghati number moja kwanza n.k
Sijakuelewa! Halafu tukishajenga in phase ndo inakuaje?! Kwamba ili tuijenge wenyewe, au?! Kama ndiyo, rudia swali lako la kwanza, kwamba, je, tutaweza kui-utilize?

Kumbuka, Mchina tayari ana mzigo unaosubiri kwenda sehemu mbalimbali duniani!! So, kama nasi tutakuwa na assurance ya mzigo, kujenga wenyewe itakuwa ni jambo bora lakini Sri Lanka walishindwa kui-utilize bandari yao, na hata Piraeus ya Ugiriki ilianza kupata mzigo wa kutosha baada ya kuingia Mchina!
 
Hakuna evidence aliyokupa, soma vizuri amesema kwa taarifa zisizo rasmi... Na amesema siyo rasmi kwa kuwa alishindwa kupata taarifa rasmi. Tumia akili kibaraka wa beberu na Mchina wewe.
Kwa comment hii tu ndio imeua Hoja ya jamaa asee watz nani kawaroga? hebu tuwekee hapa Mkataba wa Uwanja wa Chato ununuzi wa ndege

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…