Ndio hapo sasaAtautoa wapi mkuu!
Yeyekafanya research! Yani eti research ni sawa na mkataba,
Sasa unazunguka tu mlemle kama umechanganyikiwa na kupoteza lengo.Nimeweka wazi kuhusu hao patriots!! Wazalendo wa Magufuli, ambao kimsingi, majority hawana uzalendo wowote!! Nyie hamna uzalendo wa kumzidi Mchina lakini bado alifahamu umuhimu kama sio ulazima wa FDI! Wala hawakusema "tuna soko kubwa kwahiyo kama viwanda tutajenga wenyewe"! Wao waliongozwa na commercial mind, na sio ule uzaleno uliopitwa na wakati wa "Madini hayaozi"!
Another misunderstanding!
Kwani Marekani si bonge la tajiri?!
Hapo issue sio nchi hii na ile na zenyewe ni tajiri bali ni nchi ipi ipo tayari ku-offer nini!!! Hao Wahindi kwa sasa tusubiri tu waje kununua mbaazi zetu!!
Kwahiyo hizo nchi zingine ndo zitajali sana maslahi ya Tanzania?!
Nimeyasoma mengi kwenye andiko lako nilikotoa mstari nilio'quote' hapo juu. Nikacheka!us inahangaika sasa kwa sababu master mind wa china ni wamarekani ambao wanalipwa vizuri na china
Sasa kama Tanzania haitajali maslahi yake, wewe unadhani china ndio atayajali?Kwahiyo hizo nchi zingine ndo zitajali sana maslahi ya Tanzania?!
Ingekuwa watu hawajali maslahi mkataba ungesainiwa tangu wakati wa Mkwere! The problem, watu mnachanganya mambo, na kwavile mmemezeshwa propaganda, mnafanya judgement kupitia hizo propaganda!!!Sasa kama Tanzania haitajali maslahi yake, wewe unadhani china ndio atayajali?
Hivi unaelewa unachoandika?
Kama huna access ya inner circle yao huwezi kujua ni sawa na unaona mtu kafanikiwa kweli kwenye Biashara ya Nguo, na wewe unachukua muda wa miaka 2 ukifanya uchunguzi wa hio biashara na unajua A-Z anavyofanya, unafungua hio biashara na wewe unaona haikupi faida, kumbe ana Biashara nyingine ambayo ndio inampa faida. Kwa wafanya Biashara nguli na Viongozi nguli wanajua namna ya kucheza na mifumo ya duniaNimeyasoma mengi kwenye andiko lako nilikotoa mstari nilio'quote' hapo juu. Nikacheka!
Lakini nilipofika kwenye mstari huu, nikashangaa!
Wewe na mimi hatujui kwa nini mkataba haukusainiwa wakati wa Kikwete, na wala usigeuze unachopigania hapa kiwe ndio sababu ya kutugeuzia kibao.Ingekuwa watu hawajali maslahi mkataba ungesainiwa tangu wakati wa Mkwere! The problem, watu mnachanganya mambo, na kwavile mmemezeshwa propaganda, mnafanya judgement kupitia hizo propaganda!!!
Nadhani 2019 Kakoko aliongea na media, na hapo ndipo Merchant Group walijitokeza na kusema Kakoko ni mwongo! Na licha ya Kakoko kuitwa mwongo, akaufyata na hakutoka tena front kuji-defend kwa sababu haiwezekani DG wa taasisi kubwa kabisa uitwe muongo halafu ukae kimya!!
Lakini kubwa zaidi, tafuta clip ya Kakoko usikilize hoja zake...
Mkuu 'Lob', ninakuelewa barabara kwa hayo uliyoandika hapa.Kama huna access ya inner circle yao huwezi kujua ni sawa na unaona mtu kafanikiwa kweli kwenye Biashara ya Nguo, na wewe unachukua muda wa miaka 2 ukifanya uchunguzi wa hio biashara na unajua A-Z anavyofanya, unafungua hio biashara na wewe unaona haikupi faida, kumbe ana Biashara nyingine ambayo ndio inampa faida. Kwa wafanya Biashara nguli na Viongozi nguli wanajua namna ya kucheza na mifumo ya dunia
Naunga mkono hoja!Ndugu yangu Chige niliahidi ntarudi, lakini naomba nizungumzie kidogo kuhusu hili suala la The Belt-Road-Initiative (BRI). Kwanza kabisa, huu mradi ulianza kupangwa kipindi cha Raisi Hu-Juntao na aliweka wazi kabisa kwenye kikao cha halmashauri kuu ya chama cha kikomunisti cha Uchina.
Zaidi ya asilimia hamsini (50% of world merchandise) ya bidhaa za dunia hii zinapitia kwenye mfereji wa Malacca ambao ni muhimu sana kwa uchumi na usalama wa dunia. Hali hii inawafanya Uchina wajihisi kwamba lolote linaweza kutokea endepo ukanda wa Pasifiki utachafuka.
Gideon Rachman wa The Financial Times aliwahi kumnukuu moja wa Majemedari wakubwa kabisa wa Marekani akisema hivi "If the Chinese starts war in the Pasific, we will fucking sail those waters and choke them at the Malacca Strait". Mafuta yote yanayoenda Uchina, Vietnam, Japan na Korea kutoka Ghuba ya Uajemi hupitia mfereji wa Malacca.
Hivyo ukibana pale Uchina lazima atahangaika sana ukizingatia yeye ndiye nchi inayoongoza duniani kwa kuingiza mafuta na gesi kutoka nje (Greatest Importer of Oil and Gas). Pia ndiye msafirishaji mkubwa wa bidhaa duniani (The Greatest Exporter of Merchandise): Hivyo anategemea sana mfereji wa Malacca, lakini bahati mbaya sana Marekani ameshafahamu huu udhaifu ndiyo maana anaweka kambi ya jeshi eneo lile.
Uchina hili analiita The Malacca Dilemma, na Peter Navarro mmoja ya washauri wakubwa wa Raisi Donald Trump ameliandika sana kwenye kitabu chake kiitwacho Death by China: Confronting the Dragon-Global Call to Action , akikiri kwamba huu ni moja ya udhaifu ambao Marekani lazima iutumie katika kupambana na Uchina.
SASA TANZANIA INAINGIAJE KWENYE HILI:
Uchina katika kuhangaika na kukwepa hii kadhia akaamua kuja na BRI, ambapo wangefufua The GREAT SILK-ROAD ambayo itapita nchi kavu na baharini. Kama ulivyosema Bandari ya Bagamoyo ilitakiwa ijengwe Kenya na kwenye mkakati wa BRN inainyesha ni LAMU na siyo BAGAMOYO, lakini Mzee Kikwete na Benard Membe wakashawishi ije kujengwa hapa Tanzania.
Sasa lengo ni kwamba Uchina angejenga reli ndefu (Standard Gauge Railway) kutoka Uchina hadi nchini Pakistani ambapo ingekutana na bandari ya Gwadar (Gwadar Port) ambayo itakuwa na ukubwa kama ule wa bandari ya Bagamoyo. Lengo ni kwamba bandari hii itakuwa inapokea bidhaa zote kutoka Ghuba ya Uajemi na kuzipakia kwenye treni hadi Uchina, hivyo kukwepa kupita mfereji wa Malacca.
Hivyo, Bandari za Bagamoyo na Gwadar ndiyo yangekuwa malango makuu ya kuunganisha Bara la Afrika na Asia. Kwasababu Bagamoyo peke yake ingehudumia nchi nyingi sana za Afrika kwasababu ni Special Economic Zone. Pia kuna uwezekano mkubwa sana kama Bandari ya Bagamoyo ingejengwa basi ingeweza kuunganisha hadi Congo DRC, kufika Port Matada kwa njia ya reli na kufanikisha biashara baina ya Africa na Amerika Kusini.
SASA NINI TATIZO:
Watanzania wengi wanapinga sana huu mradi lakini binafsi Feasibility Study nimeiona. Pia waliohusika na kuandaa hii Study mkataba pia waliusona na nikabahatika kufahamu baadhi ya vitu. Inavyofahamika mkataba ni makubaliano ya pande mbili na huwezi kumlazimisha mtu akubali tu hata pale anapata hasara. Kuna mengi yameongelewa sana kuhusu huu mkataba, mengine yana ukweli na mengine ni propaganda zilizoambatana na ujinga wa kutofahamu mambo.
Lakini kubwa zaidi fahamu kwamba ndani ya nchi kumekuwa na kambi mbili zenye minyukano mikubwa sana. Kuna wale Pro-China na Pro-USA, bahati mbaya kuna baadhi ya watu wakubwa nchini wanahusika moja kwa moja na maslahi za hizi kambi (Hili ni jambo la hatari sana kwa usalama wa nchi). Kama tunaangalia maslahi ya kambi hizi mbili bila kuweka Tanzania mbele basi tutakuja kujuta sana huko mbele.
Kumekuwa na fitna, uzandiki na kuumizana sana, ikafika hadi kipindi tukaaminishwa kwamba Mzee Jakaya alikuwa ni mtu mpumbavu na mjinga kupindukia kiasi cha kutaka kuuza nchi yote hii kwa wakoloni wa Kichina na aliyezuia hili lisifanyike ni Mtanzania Mzalendo na Mwenye Uchungu na Nchi hii kuliko raisi mwingine yoyote kuwahi kutoke, Marehemu Raisi Magufuli. Hili kuna watu waliliamini na kuna wengine tulilitilia shaka kwasababu tulibahatika kufahamu kinachoendelea.
Nifahamuvyo mimi ni kwamba Mkataba ni makubaliono ya pande mbili na kama kuna mambo hayakaa vizuri ni vyema kurudi mezani na kufanya juu chini ili kuyazungumza upya. Alichokifanya Raisi Magufuli ni kutafuta umaarufu na kutaka kubagaza watu. Hivyo katika hili ningependa Raisi aunde tume maalumu ya wataalamu wa mikataba wa ndani ya nje ya nchi ambao watatusaidia kupitia vipengele mbalimbali, lakini pia kuajiri QUANTUM ANALYSTS ambao watafanya makadilio ya faida na hasara za kiuchumi ambazo Tanzania itazipata katika kipindi chote cha mkataba.
HILI LINANIKUMBUSHA JAMBO LILILOWAHI KUTOKEA KIPINDI CHA MZEE NYERERE:
Wakati Mzee Nyerere anataka kujenga TAZARA aliwafuata Wamarekani na wakasema ile reli ingejengwa kwa miaka 20. Kuna wataalamu wetu walipigia sana hili jambo chapuo lakini akaamua kwenda Uchina wakasema wangejenga kwa miaka 5. Mao Zedong na Zhou Enlai walimwambia Mzee Nyerere wewe ni rafiki yetu na sisi wote ni masikini, lakini mahitaji yetu na yenu ni tofauti hivyo tutawasaidia kujenga reli.
Marekani, Urusi, Uingereza na Ujerumani walipinga sana huu mradi kufanywa. Wale wahandisi walifanya uchunguzi ambapo walitembea kwa mguu kwa zaidi ya miezi tisa wakiangalia sehemu ambayo reli ingepita. Waziri Mkuu wa Uingereza bwana Harold Wilson alimwambia Nyerere kwamba mashirika ya ujasisi yamefanya uchunguzi na kufahamu kwamba mawaziri wengi wa Nyerere kama Mohamed Babu, Prof. Ibrahimu Kaduma na wengine ni majasusi wa Uchina na wanalipwa na Uchina ili kuuiza Tanzania.
Ilipingwa kampeni kubwa ambayo ilifika kipindi wakasema kwamba Tanzania inaenda kuwa koloni la Uchina. Baadhi ya wasomi wa Tanzania wa wakati huo walikubali na kuamini zile propaganda. Tofauti na Mzee Magufuli, Raisi Nyerere alikuwa ni Shrewd Statesman and an Excellent Diplomat with a clear understanding of global politics. Aliamua reli ijengwe na akasema yeye anachotaka ni pesa hajali kama ni Nyekundu kutoka kwa Wakomunisti au Bluu kutoka kwa Mabepari.
KITU AMBACHO WENGI HAWAKIFAHAMU:
Wakati reli inajengwa wamarekani walitumia vyombo vya habari na wataalamu kukashifu na kusema kwamba ile reli haitakuwa na kiwango cha ubora kama reli za Ulaya na Marekani. Wengi waliikashifu TAZARA kwa kuiita reli ya mwanzi (The Bamboo Railway): Yule Muhandisi wa kichina aliyesimamia Ujenzi wa reli na wenzake walishawahi kuvamiwa na majasusi wa Marekani hadi kupigana makonde wakati wa ujenzi wa ile reli.
SHIDA IKO WAPI SASA ???:
Nasema kwa ujasiri na uhakika mkubwa kabisa kwamba wasomi wa kitanzania walioko kwenye vyama vya siasa, jeshi na kwenye idara zetu za ujasusi na upelelezi ni watu ambao hawana uelewe mpana wa mambo. Watanzania wengi hatuna kumbukumbu ya nchi hii imetokea wapi na imefikaje hapa zaidi ya kupeana taarifa za kusimuliana tu. Hatufahamu dunia inaendaje na jinsi gani mwenendo huu wa dunia unaweza kuathiri siasa za nchi changa kama Tanzania. Pia hatufahamu wapi nchi yetu inaenda na hatuna kabisa uhakika wa taswira ya nchi yetu kwa miaka 20 ijayo.
Huwa najiuliza sana kama Mzee Nyerere angekuwa na roho nyepesi na hana uelewa mpana wa mambo sidhani kama leo hii Tanzania ingekuwa na reli ya TAZARA, sidhani. Nilimsikia Bwana Kakoko akisema kwamba Uchina ya leo siyo Uchina ile ya kipindi cha TAZARA na nikapata uhakika wa hicho nilichokisema hapo juu, cha kukosa uelewa wa siasa za dunia. AU Aidha Kakoko alikuwa anafahamu lakini akaamua kupiga Propaganda, lakini yote tisa mimi ambaye nimesoma Political Science and Diplomacy nikaamua kumsamehe kwasababu huenda hana utaalamu na haya mambo.
Ila nachokifahamu ni kwamba UCHINA alijenga TAZARA siyo kwasababu ya kusaidia wajamaa wenzake wa kiafrika peke yake, bali aliangalia maslahi ya kiuchumi ya miaka zaidi ya 40 mbele. Kama watanzania wanaamini kwamba ile reli ilikuwa ni zawadi kutoka kwa mjomba basi nawashauri waache kufikiri huo ujinga kuanzia leo. Uchina na Urusi wote walitoa misaada kwasababu ilifanikisha ajenda zao za kisiasa, kiusalama na kidiplomasia. TAZARA imemsaidia sana Uchina kidiplomasia, kiuchumi na kiusalama kama ambavyo Bagamoyo itamsaidia. Hivyo Uchina wa kipindi kile na Uchina wa leo ni walewale wale na hawajawahi badilika, kama mnadhani duniani kuna FREE-LUNCH basi mnajidanganya.
NINI KIFANYIKE SASA ???:
Katika pilika zangu za kusoma migogoro ya kimataifa, uwekezaji na kuifanyia kazi nimefahamu kitu kimoja cha msingi sana. Ili migogoro itatuliwe vizuri ni lazima kuwe na CONFIDENTIALITY, ili kusaidia Political Passion of Citizens zisivuruge kabisa majadiliano. Naamini hili suala lingekuwa wazi kuishia ngazi za Bunge tu, ambapo kamati za Bunge zingepewa mamlaka kulijadili na siyo kila raia ambaye hana hata ufahamu nalo akalizungumzia.
Sasa ili kukata mzizi wa fitina na kusaidia nchi isonge mbele Raisi angeunda tume huru ya uchunguzi (Commission of Inquiry) ya wataalamu ambayo itahusika na kupitia mkataba wa Bandari ya Bagamoyo. Tena ili kuhakikisha weledi Raisi atafute wasomi nguli hata wa nje ili kusiadia kuifanyia Consultancy hiyo Tume: Lakini pia maadamu watu walioandaa huo mkataba kipindi cha awamu ya Mzee Kikwete bado wapo basi waitwe na hiyo tume wahojiwe na watoe sababu za kwanini wao kukubaliana na ule mkataba.
Pia maadamu timu ya wataalamu wa kipindi cha utawala wa Raisi Magufuli waliomshauri akatae ule mradi kwasababu mkataba ni wa hovyo, kijinga na kifisadi bado wapo nao waitwe na tume na kutoa sababu zao. Mwisho wa siku tume ipimie nani anasema ukweli , wapi tumekwama na watoea mapendekezo ya jinsi mkataba unaweza kutekelezwa kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili (Tanzania na Uchina).
Siku zote kukiwa na utata wa namna hii njia pekee ni kuunda COMMISSION OF INQUIRY ya wataalamu ili kupima hoja zinazotolewa na pande zote mbili. Kitaalamu kama jambo limetokea na kila pande inasema kitu chake, tume za namna hii huundwa ili kutafuta ukweli ni upi, na mwisho huishia kutoa mapendekezo ya kitaalamu. Sasa nadhani suala nyeti kama hili linaweza kumalizwa na wataalamu siyo wanasiasa wasio na ufahamu wowote kuhusu hili jambo.
Mwisho kabisa Raisi na Bunge wapelekewe hiyo ripoti ya uchunguzi ili wao washauriane na kufanya maamuzi sahihi. Aidha tunaukataa huu mradi au tunaukubali: Hili la kusema eti mradi mzuri ila mkataba mbaya hatuyataki. Tukiendelea kwenda hivi gizani na kutegemea kauli za wanasiasa basi ukweli hatutaufahamu kamwe na hujuma na uzandiki vitaendelea.......
RAI YANGU KWA WASOMI WA KITANZANIA:
Mbali na maslahi ya kiuchumi ya Tanzania kuhusishwa, huu ni mtifuano mkubwa sana wa kimataifa ambao haukuanza leo wala jana. Nadhani kabla ya kukosoa, kukubali au kupinga ni vyema tukawa na taarifa sahihi kwanza. Pia tufahamu kabisa huu mradi ukijengwa au kukataliwa ni faida au hasara kwa haya mataifa mawili makubwa: Hivyo tusichague tuweke nchi yetu mbele kwanza na tupate taarifa sahihi ili kuupa kutumika kisiasa bila kufahamu.
Hii Hoja iko vice versa!!UTANGULIZI
Amini usiamini, wale wale ambao wamekuwa wakijivika uzalendo, linapokuja suala la Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, ndiyo hao hao wanaotumikia Mabeberu bila wao kujijua!
Nitajadili mada hii katika sehemu mbili:-
Kwa bahati, binafsi mwaka 2016 nilikuwa “Mbeba Mikoba” wa Researcher mmoja wa Kimarekani (Beberu?) aliyekuwa anafanya utafiti kuhusu Belt and Road Initiative (BRI).
- Kwanini wale wanaoitwa Mabeberu hawawezi kuwa tayari kuona miradi kama ya Bandari ya Bagamoyo inafanikiwa, na
- Hoja zinazotolewa na Wazalendo Kupinga Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.
Kazi yangu kubwa ilikuwa Literature Review!
Kwa wanaofahamu mambo ya Resech, ukifanya Literature Reviews, hususani ya wasomi kama huyu bwana, basi unapata fursa ya kufahamu mambo mengi zaidi yaliyopata kutokea hapo kabla kwenye eneo husika!
Kwa wasiofahamu, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni matokeo ya (BRI) ambayo, Rais wa China, Xi, anailezea BRI kwamba:
Kwa lugha nyepesi, malengo ya China kupitia BRI ni kuiunganisha nchi hiyo na sehemu zingine duniani, hususani Asia, Afrika, na Ulaya! Uunganishaji huo ni kwa ujenzi wa miundombinu, hususani ya bandari, reli, na viwanja vya ndege.
Ndugu yangu MALCOM LUMUMBA alipata kuchambua kwa undani kabisa suala la Belt and Road Initiative!!
Na hapo sidhani kama mtu anahitaji kuwa na Shahada ya Diplomasia ya Uchumi na Ushikirikiano wa Kimataifa kunusa “threat” ya mpango huo wa China kwa mataifa makubwa, hususani Marekani!
Kutokana na ukweli huo, ndo maana haishangazi mara tu BRI ilipotangazwa, Waandishi na Watafiti mbalimbali kutoka nchi za magharibi wakaanza kulivalia njuga suala hilo.
Makala zikaandikwa, na tafiti zikafanywa kuhusu BRI, lakini makala nyingi kama sio zote zililenga kuyatisha mataifa mengine kuwa makini na BRI!
Watu hawa wakageuka kuwa “Wajomba Zetu” Afrika, huku wakituasa tusije tukaingia kwenye mtego huo hatari wa China!
Ni kupitia hizo tafiti ndipo nami nikajikuta nipo na huyo Mtafiti Msomi kweli kweli wa Kimarekani.
Huyu Bwana case studies zake zilikuwa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, Bandari ya Hambantota (Sri-Lanka), pamoja na Bandari ya Piraeus (Ugiriki).
Ukweli ni kwamba, ilinichukua chini ya dakika 3 kugundua Mtafiti huyu ni kama tayari alishakuwa na “matokeo” ya utafiti wake hata kabla kazi haijaanza! Kwa kifupi, alionesha dalili zote za kutounga mkono Mradi wa Bandari ya Bagamoyo!
Hata "beberu" niliyekuwa namtumikia, nae alikuwa pamoja na "Wazalendo" wetu!!
Binafsi, nilikuwa “in favor of” Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, kwahiyo tukaanzisha kimdaharo kisicho rasmi!
Baada ya kuona hoja zake nyingi nazipangua, akaishia kuuliza ikiwa nadhani ni busara kwa taifa maskini kama Tanzania kuwa na bandari kubwa kama ya Bagamoyo!!
Jibu langu kwake lilikuwa rahisi sana, kwamba: Bandari ya Bagamoyo itakuwa ni kubwa mno kwa Tanzania endapo tu unaamini Tanzania na majirani zake wataendelea kuwa maskini kwa miongo kadhaa ijayo, vinginevyo, huwezi kusema ni “kubwa mno”!
Kwa ufupi, Mheshimiwa huyu, kama walivyokuwa wenzake wengine, nyimbo zao zilikuwa ni agenda ya siri ya China kuitumia BRI kama Mtego wa Madeni kwa nchi maskini!
Lilipokuja suala la Bandari ya Hambantota kule Sri-Lanka, propaganda zikasambazwa kwamba China IMEITWAA bandari ya Sri Lanka ili kufidia deni lake!
Wazalendo wetu nao wakazidaka propaganda hizo, na bila kufanya utafiti, wakaanza kutueleza kwamba “tukishindwa kulipa deni, Wachina wataichukua Bandari ya Bagamoyo kama walivyofanya kule Sri-Lanka.”
Kuweka kumbukumbu sawa, habari za Wachina KUITWAA bandari hiyo zilipotoshwa. Nitaeleza hili kinaga ubaga hapo baada kwenye makala hii.
Pamoja na suala la “Debt Trap”, watu hawa tunaowaita Mabeberu ambao kwa hili tunawaona wanajali maslahi yetu, pia wakawa wanatuambia agenda nyingine ya siri ya China ya kuanzisha “military base” kupitia BRI.
Hapa wakawa wanalenga kutuambia, hata mradi kama wa Bandari ya Bagamoyo, lengo lake ni Wachina kutaka kuweka kambi za kijeshi eneo hili la Afrika Mashariki!
Hata hivyo, hawatuambii ukweli kwamba, ni wao wenyewe ndio wanaozihofia hizo “military bases” za China endapo zitawepo!
Kila mfuatiliaji wa mambo duniani, anafahamu Marekani ina kambi za kijeshi sehemu kadhaa duniani, lakini linapokuja suala la China au mataifa mengine kufanya yale yale ambayo yeye keshayafanya kwa miongo kadhaa, hapo inageuka kuwa nongwa!
Waingereza wana msemo “If you can’t beat them, join them.”
Guys, amini usiamini, juzi yule Mtafiti niliyekuwa nae ametoa makala kwenye moja ya majarida maarufu sana duniani! Baada ya kuisoma makala ile, hapo hapo nikajisikia uchungu, na kumhurumia!
Yaani yule yule aliyekuwa anaipinga BRI, kwenye hiyo makala anaulaumu wazi wazi Utawala wa Trump kwa kutumia kete ya Debt Trap kama njia ya kuidhoofisha BRI.
Kwenye makala hiyo, kuna sehemu anahoji “Kama kweli BRI ni kitu kibaya kiasi hicho, ni kwanini basi China inaendelea kutafuta Washirika walio tayari kujiunga na BRI.”
Mwishowe, Mtafiti huyu anaisemanga serikali yake kwamba ”USA haitaweza kumzuia Rais wa China kuwekeza kupitia BRI endapo US haitakuwa na mbadala kwa mataifa yanayoshirikiana na China!
Ufaransa, imeanza kuliona hilo kama ilivyowahi kuripotiwa na France24 kwamba:
Desperation ya Mtafiti huyu bila shaka inatokana na vile anavyoona jinsi ambavyo nchi mbalimbali duniani jzinavyojiunga na BRI, kinyume na matarajio ya USA ambayo ilikuwa ina-lobby nchi zingine, hususani Washirika wake kutojiunga na BRI.
Kwa bahati mbaya sana, si Afrika, si Asia! Hadi baadhi ya nchi za Ulaya na Carribean zinaingia kwenye BRI. Mbaya zaidi, miradi ya BRI inaonekana kufanya vizuri sana!
Kwa mfano, mwaka 2016 Bandari ya Piraeus ilikuwa ndio ya kwanza barani Ulaya kubinafsishwa chini ya BRI. Bandari hii ndiyo bandari kubwa kuliko zote nchini Ugiriki, na ndio langu kuu la bahari linalounganisha nchi za EU na Asia!
Hapo kabla, bandari hii ilikuwa haifanyi vizuri, na ripoti za nyuma zilikuwa zinaiweka bandari hiyo kama bandari ya 17 barani Ulaya!
Baada ya Wachina kuchukua 51% ya hisa za bandari hiyo, na hatimae hisa hizo kufikia 67%; ripoti ya mwaka huu kupitia Port Economics inasema kwa sasa Bandari ya Piraeus ndiyo bandari kubwa zaidi (kwa kiwango cha makontena) kwenye ukanda wa Bahari ya Mediterranean, na ya 5 Barani Ulaya!!
Sasa haya ndo mambo ambayo watu hawakuyataka! Yaani bandari iliyo kwenye ardhi ya Mzungu, 67% imilikiwe na Mchina, na hapo hapo inaanza kutishia ushawishi wa bandari zingine zinazomilikiwa na Wazungu wenyewe!
JokaKuu
Sijui vipi wakati nimekuambia?! Sijui au umeshaji-tune kukiamini kile ulichoambiwa na akina Kakoko, ambao hata hivyo sijawahi kusikia wakisema kwamba mkataba ulishasainiwa!Wewe na mimi hatujui kwa nini mkataba haukusainiwa wakati wa Kikwete, na wala usigeuze unachopigania hapa kiwe ndio sababu ya kutugeuzia kibao.
Hivi mtu anaposema kwa mfano: "Habari kwamba TRA hawatakusanya kodi ni uzushi", hivi hapo unatakiwa tena ufafanuliwe kwamba ukweli ni upi?Unasema "Merchant Group walijitokeza na kusema Kakoko ni mwongo." Huyo mchina alikwambia ukweli gani katika majibu yake. Mbona hujayaeleza hapa?
Umemsikia akisema nini kuhusu:-Clip ya Kakoko nimekwishaisikilza mara nyingi humu JF. Kama anasema uongo hilo sijui na wala siwezi kumtetea; lakini bado sijasikia lolote toka kwa mchina ambalo linakanusha uongo huo. Kusema tu "hiyo ni 'FEKI'", sio kueleza ukweli ni upi.
Yaani nikuwekee Research hapa?! Na sio mkataba tena?! Btw, mimi ni muongo, unaweza kumtaja huyo mkweli? Kakoko, au?Ndio hapo sasa
Aweke hapa hiyo research !
Mwongo mkubwa huyu mtu.
Sijui alidhani sote humu ni majuha ???
Kama ambavyo bunge with their naked King Ndugai wanavyotuchukulia wananchi ?
Elezea basi hiyo vice versing.Hii Hoja iko vice versa!!
Mimi kama mtaalamu wa kodi naku zoom tu. Nahitaji kusoma andiko lako zaidi.Braza shikamoo, ila wewe jamaa una akili nyingi mnoo.
Hapa nipo na nitarudi baadaye,........
=========================================================================
Ndugu yangu Chige niliahidi ntarudi, lakini naomba nizungumzie kidogo kuhusu hili suala la The Belt-Road-Initiative (BRI). Kwanza kabisa, huu mradi ulianza kupangwa kipindi cha Raisi Hu-Juntao na aliweka wazi kabisa kwenye kikao cha halmashauri kuu ya chama cha kikomunisti cha Uchina.
Zaidi ya asilimia hamsini (50% of world merchandise) ya bidhaa za dunia hii zinapitia kwenye mfereji wa Malacca ambao ni muhimu sana kwa uchumi na usalama wa dunia. Hali hii inawafanya Uchina wajihisi kwamba lolote linaweza kutokea endepo ukanda wa Pasifiki utachafuka.
Gideon Rachman wa The Financial Times aliwahi kumnukuu moja wa Majemedari wakubwa kabisa wa Marekani akisema hivi "If the Chinese starts war in the Pasific, we will fucking sail those waters and choke them at the Malacca Strait". Mafuta yote yanayoenda Uchina, Vietnam, Japan na Korea kutoka Ghuba ya Uajemi hupitia mfereji wa Malacca.
Hivyo ukibana pale Uchina lazima atahangaika sana ukizingatia yeye ndiye nchi inayoongoza duniani kwa kuingiza mafuta na gesi kutoka nje (Greatest Importer of Oil and Gas). Pia ndiye msafirishaji mkubwa wa bidhaa duniani (The Greatest Exporter of Merchandise): Hivyo anategemea sana mfereji wa Malacca, lakini bahati mbaya sana Marekani ameshafahamu huu udhaifu ndiyo maana anaweka kambi ya jeshi eneo lile.
Uchina hili analiita The Malacca Dilemma, na Peter Navarro mmoja ya washauri wakubwa wa Raisi Donald Trump ameliandika sana kwenye kitabu chake kiitwacho Death by China: Confronting the Dragon-Global Call to Action , akikiri kwamba huu ni moja ya udhaifu ambao Marekani lazima iutumie katika kupambana na Uchina.
SASA TANZANIA INAINGIAJE KWENYE HILI:
Uchina katika kuhangaika na kukwepa hii kadhia akaamua kuja na BRI, ambapo wangefufua The GREAT SILK-ROAD ambayo itapita nchi kavu na baharini. Kama ulivyosema Bandari ya Bagamoyo ilitakiwa ijengwe Kenya na kwenye mkakati wa BRN inainyesha ni LAMU na siyo BAGAMOYO, lakini Mzee Kikwete na Benard Membe wakashawishi ije kujengwa hapa Tanzania.
Sasa lengo ni kwamba Uchina angejenga reli ndefu (Standard Gauge Railway) kutoka Uchina hadi nchini Pakistani ambapo ingekutana na bandari ya Gwadar (Gwadar Port) ambayo itakuwa na ukubwa kama ule wa bandari ya Bagamoyo. Lengo ni kwamba bandari hii itakuwa inapokea bidhaa zote kutoka Ghuba ya Uajemi na kuzipakia kwenye treni hadi Uchina, hivyo kukwepa kupita mfereji wa Malacca.
Hivyo, Bandari za Bagamoyo na Gwadar ndiyo yangekuwa malango makuu ya kuunganisha Bara la Afrika na Asia. Kwasababu Bagamoyo peke yake ingehudumia nchi nyingi sana za Afrika kwasababu ni Special Economic Zone. Pia kuna uwezekano mkubwa sana kama Bandari ya Bagamoyo ingejengwa basi ingeweza kuunganisha hadi Congo DRC, kufika Port Matada kwa njia ya reli na kufanikisha biashara baina ya Africa na Amerika Kusini.
SASA NINI TATIZO:
Watanzania wengi wanapinga sana huu mradi lakini binafsi Feasibility Study nimeiona. Pia waliohusika na kuandaa hii Study mkataba pia waliusona na nikabahatika kufahamu baadhi ya vitu. Inavyofahamika mkataba ni makubaliano ya pande mbili na huwezi kumlazimisha mtu akubali tu hata pale anapata hasara. Kuna mengi yameongelewa sana kuhusu huu mkataba, mengine yana ukweli na mengine ni propaganda zilizoambatana na ujinga wa kutofahamu mambo.
Lakini kubwa zaidi fahamu kwamba ndani ya nchi kumekuwa na kambi mbili zenye minyukano mikubwa sana. Kuna wale Pro-China na Pro-USA, bahati mbaya kuna baadhi ya watu wakubwa nchini wanahusika moja kwa moja na maslahi za hizi kambi (Hili ni jambo la hatari sana kwa usalama wa nchi). Kama tunaangalia maslahi ya kambi hizi mbili bila kuweka Tanzania mbele basi tutakuja kujuta sana huko mbele.
Kumekuwa na fitna, uzandiki na kuumizana sana, ikafika hadi kipindi tukaaminishwa kwamba Mzee Jakaya alikuwa ni mtu mpumbavu na mjinga kupindukia kiasi cha kutaka kuuza nchi yote hii kwa wakoloni wa Kichina na aliyezuia hili lisifanyike ni Mtanzania Mzalendo na Mwenye Uchungu na Nchi hii kuliko raisi mwingine yoyote kuwahi kutoke, Marehemu Raisi Magufuli. Hili kuna watu waliliamini na kuna wengine tulilitilia shaka kwasababu tulibahatika kufahamu kinachoendelea.
Nifahamuvyo mimi ni kwamba Mkataba ni makubaliono ya pande mbili na kama kuna mambo hayakaa vizuri ni vyema kurudi mezani na kufanya juu chini ili kuyazungumza upya. Alichokifanya Raisi Magufuli ni kutafuta umaarufu na kutaka kubagaza watu. Hivyo katika hili ningependa Raisi aunde tume maalumu ya wataalamu wa mikataba wa ndani ya nje ya nchi ambao watatusaidia kupitia vipengele mbalimbali, lakini pia kuajiri QUANTUM ANALYSTS ambao watafanya makadilio ya faida na hasara za kiuchumi ambazo Tanzania itazipata katika kipindi chote cha mkataba.
HILI LINANIKUMBUSHA JAMBO LILILOWAHI KUTOKEA KIPINDI CHA MZEE NYERERE:
Wakati Mzee Nyerere anataka kujenga TAZARA aliwafuata Wamarekani na wakasema ile reli ingejengwa kwa miaka 20. Kuna wataalamu wetu walipigia sana hili jambo chapuo lakini akaamua kwenda Uchina wakasema wangejenga kwa miaka 5. Mao Zedong na Zhou Enlai walimwambia Mzee Nyerere wewe ni rafiki yetu na sisi wote ni masikini, lakini mahitaji yetu na yenu ni tofauti hivyo tutawasaidia kujenga reli.
Marekani, Urusi, Uingereza na Ujerumani walipinga sana huu mradi kufanywa. Wale wahandisi walifanya uchunguzi ambapo walitembea kwa mguu kwa zaidi ya miezi tisa wakiangalia sehemu ambayo reli ingepita. Waziri Mkuu wa Uingereza bwana Harold Wilson alimwambia Nyerere kwamba mashirika ya ujasisi yamefanya uchunguzi na kufahamu kwamba mawaziri wengi wa Nyerere kama Mohamed Babu, Prof. Ibrahimu Kaduma na wengine ni majasusi wa Uchina na wanalipwa na Uchina ili kuuiza Tanzania.
Ilipingwa kampeni kubwa ambayo ilifika kipindi wakasema kwamba Tanzania inaenda kuwa koloni la Uchina. Baadhi ya wasomi wa Tanzania wa wakati huo walikubali na kuamini zile propaganda. Tofauti na Mzee Magufuli, Raisi Nyerere alikuwa ni Shrewd Statesman and an Excellent Diplomat with a clear understanding of global politics. Aliamua reli ijengwe na akasema yeye anachotaka ni pesa hajali kama ni Nyekundu kutoka kwa Wakomunisti au Bluu kutoka kwa Mabepari.
KITU AMBACHO WENGI HAWAKIFAHAMU:
Wakati reli inajengwa wamarekani walitumia vyombo vya habari na wataalamu kukashifu na kusema kwamba ile reli haitakuwa na kiwango cha ubora kama reli za Ulaya na Marekani. Wengi waliikashifu TAZARA kwa kuiita reli ya mwanzi (The Bamboo Railway): Yule Muhandisi wa kichina aliyesimamia Ujenzi wa reli na wenzake walishawahi kuvamiwa na majasusi wa Marekani hadi kupigana makonde wakati wa ujenzi wa ile reli.
SHIDA IKO WAPI SASA ???:
Nasema kwa ujasiri na uhakika mkubwa kabisa kwamba wasomi wa kitanzania walioko kwenye vyama vya siasa, jeshi na kwenye idara zetu za ujasusi na upelelezi ni watu ambao hawana uelewe mpana wa mambo. Watanzania wengi hatuna kumbukumbu ya nchi hii imetokea wapi na imefikaje hapa zaidi ya kupeana taarifa za kusimuliana tu. Hatufahamu dunia inaendaje na jinsi gani mwenendo huu wa dunia unaweza kuathiri siasa za nchi changa kama Tanzania. Pia hatufahamu wapi nchi yetu inaenda na hatuna kabisa uhakika wa taswira ya nchi yetu kwa miaka 20 ijayo.
Huwa najiuliza sana kama Mzee Nyerere angekuwa na roho nyepesi na hana uelewa mpana wa mambo sidhani kama leo hii Tanzania ingekuwa na reli ya TAZARA, sidhani. Nilimsikia Bwana Kakoko akisema kwamba Uchina ya leo siyo Uchina ile ya kipindi cha TAZARA na nikapata uhakika wa hicho nilichokisema hapo juu, cha kukosa uelewa wa siasa za dunia. AU Aidha Kakoko alikuwa anafahamu lakini akaamua kupiga Propaganda, lakini yote tisa mimi ambaye nimesoma Political Science and Diplomacy nikaamua kumsamehe kwasababu huenda hana utaalamu na haya mambo.
Ila nachokifahamu ni kwamba UCHINA alijenga TAZARA siyo kwasababu ya kusaidia wajamaa wenzake wa kiafrika peke yake, bali aliangalia maslahi ya kiuchumi ya miaka zaidi ya 40 mbele. Kama watanzania wanaamini kwamba ile reli ilikuwa ni zawadi kutoka kwa mjomba basi nawashauri waache kufikiri huo ujinga kuanzia leo. Uchina na Urusi wote walitoa misaada kwasababu ilifanikisha ajenda zao za kisiasa, kiusalama na kidiplomasia. TAZARA imemsaidia sana Uchina kidiplomasia, kiuchumi na kiusalama kama ambavyo Bagamoyo itamsaidia. Hivyo Uchina wa kipindi kile na Uchina wa leo ni walewale wale na hawajawahi badilika, kama mnadhani duniani kuna FREE-LUNCH basi mnajidanganya.
NINI KIFANYIKE SASA ???:
Katika pilika zangu za kusoma migogoro ya kimataifa, uwekezaji na kuifanyia kazi nimefahamu kitu kimoja cha msingi sana. Ili migogoro itatuliwe vizuri ni lazima kuwe na CONFIDENTIALITY, ili kusaidia Political Passion of Citizens zisivuruge kabisa majadiliano. Naamini hili suala lingekuwa wazi kuishia ngazi za Bunge tu, ambapo kamati za Bunge zingepewa mamlaka kulijadili na siyo kila raia ambaye hana hata ufahamu nalo akalizungumzia.
Sasa ili kukata mzizi wa fitina na kusaidia nchi isonge mbele Raisi angeunda tume huru ya uchunguzi (Commission of Inquiry) ya wataalamu ambayo itahusika na kupitia mkataba wa Bandari ya Bagamoyo. Tena ili kuhakikisha weledi Raisi atafute wasomi nguli hata wa nje ili kusiadia kuifanyia Consultancy hiyo Tume: Lakini pia maadamu watu walioandaa huo mkataba kipindi cha awamu ya Mzee Kikwete bado wapo basi waitwe na hiyo tume wahojiwe na watoe sababu za kwanini wao kukubaliana na ule mkataba.
Pia maadamu timu ya wataalamu wa kipindi cha utawala wa Raisi Magufuli waliomshauri akatae ule mradi kwasababu mkataba ni wa hovyo, kijinga na kifisadi bado wapo nao waitwe na tume na kutoa sababu zao. Mwisho wa siku tume ipimie nani anasema ukweli , wapi tumekwama na watoea mapendekezo ya jinsi mkataba unaweza kutekelezwa kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili (Tanzania na Uchina).
Siku zote kukiwa na utata wa namna hii njia pekee ni kuunda COMMISSION OF INQUIRY ya wataalamu ili kupima hoja zinazotolewa na pande zote mbili. Kitaalamu kama jambo limetokea na kila pande inasema kitu chake, tume za namna hii huundwa ili kutafuta ukweli ni upi, na mwisho huishia kutoa mapendekezo ya kitaalamu. Sasa nadhani suala nyeti kama hili linaweza kumalizwa na wataalamu siyo wanasiasa wasio na ufahamu wowote kuhusu hili jambo.
Mwisho kabisa Raisi na Bunge wapelekewe hiyo ripoti ya uchunguzi ili wao washauriane na kufanya maamuzi sahihi. Aidha tunaukataa huu mradi au tunaukubali: Hili la kusema eti mradi mzuri ila mkataba mbaya hatuyataki. Tukiendelea kwenda hivi gizani na kutegemea kauli za wanasiasa basi ukweli hatutaufahamu kamwe na hujuma na uzandiki vitaendelea.......
RAI YANGU KWA WASOMI WA KITANZANIA:
Mbali na maslahi ya kiuchumi ya Tanzania kuhusishwa, huu ni mtifuano mkubwa sana wa kimataifa ambao haukuanza leo wala jana. Nadhani kabla ya kukosoa, kukubali au kupinga ni vyema tukawa na taarifa sahihi kwanza. Pia tufahamu kabisa huu mradi ukijengwa au kukataliwa ni faida au hasara kwa haya mataifa mawili makubwa: Hivyo tusichague tuweke nchi yetu mbele kwanza na tupate taarifa sahihi ili kuepuka kutumika kisiasa bila kufahamu.
Wakati huu tunaganga yaliyopo. Hili kwa sasa ni kiporo au lilikwishachacha.Sijui vipi wakati nimekuambia?! Sijui au umeshaji-tune kukiamini kile ulichoambiwa na akina Kakoko, ambao hata hivyo sijawahi kusikia wakisema kwamba mkataba ulishasainiwa!
Okay, mimi na wewe hatujui... ina maana unashindwa hata kutumia common sense?!
Ni kauli ipi kati ya hizi umewahi kuisikia kati ya:-
1. "...majadiliano bado yanaendelea, kwa sababu kuna mambo hatujakubaliana" na,
2. "... tumevunja mkataba wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo"
Hivi mtu anaposema kwa mfano: "Habari kwamba TRA hawatakusanya kodi ni uzushi", hivi hapo unatakiwa tena ufafanuliwe kwamba ukweli ni upi?
Umemsikia akisema nini kuhusu:-
1. Kodi,
2. Uendelezaji wa Bandari zingine, na
3. Muda ambao Mchina ata-operate bandari?
AMEEEEEEEEEEEEN!!Hallelujah....................................
Nimesoma bandiko lako lenuvizuri sana...mmeeleza vizuri sana kiasi kwamba nimeafiki hiliAMEEEEEEEEEEEEN!!
AMEEEEEEEEN!!!
AMEEEEEEN!!!
[emoji1317]AMEEEEEEEEEEEEN!!
AMEEEEEEEEN!!!
AMEEEEEEN!!!