Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

So wewe ni mpiga magufuli afu ni mkubali Sera za msoga ama.just declare your interest tukuelewe kabisa.mana inaonekana kabisa una mahaba.
Umemuelezea beberu kuwa alikuja kufanya tafiti lakini tayari alikuwa na majibu yake ya kupinga huo mradi. Na wewe umendika ugoro mwingi Ila ishu kubwa iko kwenye mradi utekelezwe basi Ila wewe umejaza ugoro mwingi ili kupoteza maboya eti unafanya tafiti na wewe.
Kubali kuwa unautaka mradi twende sawa na ukishaweka mind yako ivyo Ina Mana hautoona ubaya hata Kama upo.
Bro wewe ni particle moja within a universe huwezi amulia viumbe wengine.you are just very minor i.e very very very minor kama una maslahi na nchi weka hapa huo mktaba uangaliwe na nchi.huu mradi unapigiwa chapuo na msoga gang
Naomba nikupuuze basi endapo hutajali?!
 
Aisee... hilo suala linauma sana!!! Mtanzania ni mwizi from family to a national level!! Watu wengi wanakwamishwa kwenye biashara na ndugu zao wenyewe!!

Wakati wa vuguvugu la katiba mpya (during JK's time) niliongea sana hili kuhusu ni namna gani jamii ya Kitanzania ilivyo jamii ya hovyo! NI namna jamii yetu ilivyokosa maadili!

INAUMIZA SANA!! Ajabu ya taifa hili, hata wale wachache miongoni mwetu wakiamua kuwa tofauti na wengine na hivyo kuzingatia maadili yao, basi wanakuwa maadui hata wa wafanyakazi wenzao!!
Yes ni jamii ya ovyo nenda ambako hakuna jamii ya ovyo kwani umefungwa miguu.kuna free mobility.kuna mentality hii imejengeka miongoni mwa watu wasiojua asili ya binadamu ama mtu ambaye hajaishi na jamii zingine kuwa ya kwenu ni ovyo.mkuu tafuta nchi uhame hujakatazwa. Hata sayari unahama mbona Elon Musk ongea naye utahamia Mars unadhani Kuna mahala pakatifu duniani
 
Nita so ma tena na tena mpaka nifahamu ulichoandika na ulichokikusudia.....

Barikiwa sana
 
Again, jikite hapa>>> Taja hapa hayo masharti unayosema mabovu, na yamesainiwa lini!!
Mkuu 'Chige', mimi nasoma na kuelewa unachoandika humu. Nimesoma mabandiko yako karibu yote kuhusu mradi huu wa Bagamoyo.

Pia naomba uelewe kwamba mimi sipingi mahali popote, umhimu na mahitaji ya mradi huu kwa taifa letu. Nasisitiza hili ulielewe vizuri sana.

Ukinielewa hivyo, utaanza kuona kwa nini mimi natofautiana na wewe kabisa. Ndiyo maana imenibidi nirudi nyuma na kusoma maandishi yako tena ili nijiridhishe na niliyoyaelewa kutokana na maandiko yako hayo.

Unaposisitiza nitaje hayo masharti mabovu, wewe unayo yasiyokuwa mabovu ambayo una uhakika yamo kwenye mapatano? Kama huna ni kipi kinachokutofautisha mimi na wewe.

Ukiwa ni mtu mwenye fikra, utajaribu kutuliza akili yako na kujiuliza jinsi ulivyowasilisha maandishi yako kwenye mijadala hii. Utaona wazi wewe hupo huru, akili yako imetekwa kuhimiza hayo unayoyataka yatokee, hata kama huna uhakika nayo.

Sasa kama hupiganii tumbo lako na kusahau mahitaji ya nchi yako, ingekupa muda kufikiri na kujihoji kuhusu nilichoandika hapa.
 
Nimesema, nchi za Magharibi, hususani Marekani wanaipinga BRI kwa hofu ya China kusambaza ushawishi wake sehemu mbalimbali duniani!!!

Aidha, meli hazimilikiwi na serikali bali na wafanya biashara!!!

Viwanda havijengwi na serikali bali na wafanyabiashara!

Ni kutokana na ukweli huo ndo maana pamoja na migogoro ya biashara isiyoisha kati ya US na China, bado one of the busiest port in the United States ni Bandari ya Long Beach, California ambao wenyewe wanakuambia shehena kubwa bandarini hapo inatokea China!!

Na hali ipo hivyo hata kwa Bandari ya Los Angeles!!

Na ndo maana, hata serikali ya US wenyewe wanakuambia:-

Kwamba, kumbe pamoja na migogoro yao ya kibiashara isiyoisha bado US wanaagiza zaidi bidhaa kutoka China, na kwahiyo bado US-China Shipping Lane ipo busy!!!
Mimi ninazungumzia kwa minajili ya dhana yako ya hiyo BRI na hali ya Tanzania na points ulizoelezea za nchi za magharibi kupinga hiyo BRI .
 
Kwanza kabisa wala sio kwamba Mchina anatupenda!!!

Mchina atupende kwani alianza kuzaliwa nani, akaja nani, akafuatia nani hadi akafikia Mao Zedong na Nyerere, kabla ya JK, Xi, na JPM?!

It's STRICTLY business, and one's own interest, kwahiyo suala la kutujengea ndugu zake halipo lakini anaweza kutukopesha kama anavyowakopesha wengine wote!!

Kwamba, kwani ni "lazima bandari ijengwe na Mchina"? Jibu, SIO LAZIMA... tunaweza kujenga hata sisi wenyewe, ama kwa pesa zetu za ndani, mikopo au financing plan ya aina yoyote ile!!

Hata hivyo, hoja hapa sio uwezo wa kujenga bandari bali uwezo wa kuiendesha bandari kibiashara na hatimae kutengeneza faida!! Hoja hapa ni uwezo wa kuvutia meli nyingi zaidi kutumia bandari yetu na sio bandari nyingine yoyote kwenye ukanda huu!!!

Hoja hapa ni kufahamu comparative and competitive advantages tulizonazo kulinganisha na washindani wetu waliopo na wale watakaokuja!

Kama nimekuelewa vizuri tunamuwezesha mchina asogelee soko lake kwa ukaribu hizo comparative na competitive advantage hazituhusu sisi maana hatuzalishi wao ndio wazalishaji na sisi tunabaki kuwa watazamaji wa movie ya macranes ya kichina yanavyopakua mizigo katika ardhi yetu tutakachoambulia labda service charge kwa dawasco ya maji taka au sijakusoma vizuri mkuu
 
Nashindwa kutia neno kwa sababu umeshasema mapema kwamba hujasoma, manake ingekuwa umesoma, mengi uliyosema nimeshayajadili!
Kamtuhumu Kakoko kuwa anapindisha Ukweli lakini Kakoko huyohuyo katika ufafanuzi wake alimalizia kuwa waliwaandikia barua Wachina kutaka marekebisho sehemu ambazo wanaona hazijakaa sawa ili waje waweke mambo sawa ila hawakuwa wamejibu mpaka mda uo! Hatujui kwanini wachina kwao waliamua kupuuzia mapendekezo ya serikali!
 
Kamtuhumu Kakoko kuwa anapindisha Ukweli lakini Kakoko huyohuyo katika ufafanuzi wake alimalizia kuwa waliwaandikia barua Wachina kutaka marekebisho sehemu ambazo wanaona hazijakaa sawa ili waje waweke mambo sawa ila hawakuwa wamejibu mpaka mda uo! Hatujui kwanini wachina kwao waliamua kupuuzia mapendekezo ya serikali!
Mkuu,mimi nilishaacha kuamini hawa "wataalamu - wanasiasa" wetu miaka 30 iliyopita. Kakoko haaminiki.
 
Mkuu,mimi nilishaacha kuamini hawa "wataalamu - wanasiasa" wetu miaka 30 iliyopita. Kakoko haaminiki.
Changamoto inakuja tumuamini nani? Maana Kakoko, Mkinga na Magufuli wote tunaamini waliona hiyo MOU na wote waliongea kitu kimoja, Wawili hawapo Duniani aliyebaki ni mmoja tu ambaye nae si muongeaji kwakweli Kakoko!!

Issue inakuja ata kipindi wanasaini IPTL, RICHMOND, DOWANCE, SYMBION ao wataalamu wa JK na JKhuyohuyo akiwepo sasa tumuamini nani?
 
Mada yako imeegemea upande mmoja.

Unataka tusiiamini selikali ambayo ndio yenye mkataba, ila unataka tukuamini wewe unae watetea wachina ambae huna mkataba na umeandika kwa kudhani.

Sasa ili mada yako ionekane ya maana weka mkataba hapa.
Mkuu na wewe upo biased; Serikali ni nani ? Serikali ni Magufuli pekee ambaye sio mara moja amedanganya on Camera ?, Au Serikali ni Samia, Ndugai, JK na wengine wengi ambao kwa sasa wanasema Mradi ni mzuri na uendelee?

Kwahio mkuu sababu hatuna mkataba yet, hivyo hatuwezi kujua.., ila kukosa kwetu mkataba sio kwamba tunakosa logic ya kuona kwamba some things do not add up... Na wala hatuwezi kuamini kauli tu za mtu/watu ambayo kudanganya kwao ni desturi (wanasiasa)
 
Mimi ninazungumzia kwa minajili ya dhana yako ya hiyo BRI na hali ya Tanzania na points ulizoelezea za nchi za magharibi kupinga hiyo BRI .
Nahisi nashindwa kukuelewa kwa sababu swali lako hufafanui vizuri!! Na kama ni kwa mazingira ya Tanzania, nchi za Magharibi, hususani US wamekuwa wakii-discredit BRI kwa kutumia hoja zifuatazo:-

1. BRI ni Debt Trap... kwamba, Mchina anataka kutumia mipesa yake kuzikopesha nchi mbalimbali duniani ili zikishindwa kulipa, Mchina azi-own hizo nchi; ikiwa ni pamoja na kutaka kuhodhi raslimali za nchi husika ili kufidia deni lao!

Ni kutokana na hilo, ndo maana Sri Lanka waliposhindwa kuiendesha Hambantota Port commercially, na hivyo kulazimika kuuza 70% ya hisa za Hambantota, kilichofuata hapo kutoka kwa nchi za magharibi ilikuwa "...si mnaona! Tuliwaambia"

Sasa kwa mazingira ya Tanzania kama unavyosema, unaweza kuhusisha mfano wa Hambantota Port na Bagamoyo Port endapo Bagamoyo Port itajengwa kwa mkopo, na kuiendesha sisi wenyewe!!

Sasa kama tutashindwa kuiendesha bandari kibiashara na hivyo kushindwa kulipa, si tunaweza kulazimika kumtafuta mwekezaji anayeweza kuiendesha profitably?! Hapo ndipo anapoweza kuingia Mchina, na kuamua kuiendesha Bagamoyo Port!

2. Military Bases... hii ndo hoja nyingine inayotumia na USA kwamba, lengo la Mchina kuwekeza kwenye bandari, na kuita hatua hiyo ni strictly business ni janja janja tu ya Mchina lakini lengo lake hasa ni kuweka military bases kwenye nchi husika at security risk!!

Kwa maana nyingine, anatuambia Mchina akijenga bandari pale Bagamoyo, halafu akawa anaiendesha yeye, hiyo ni one step ahead toward establishing military bases!!!

Sasa basi, kwangu hizo naziita propaganda tu kwa sababu, kimsingi wanachohofia US ni Mchina kusambaza ushawishi wake duniani! Ni kichekesho kusema Mchina anataka kuweka military bases wakati US wenyewe ndo wanaongoza kwa kuwa na military bases outside the United States!!

Si kwamba Mchina HANA nia ya kuweka hizo military bases... HELL NO!! Pale Djboouti kaweka military base pua na mdomo na military bases za US na France... sasa hiki ndicho wasichokitaka US na Washirika wake!!

Sasa njia pekee wanayoitumia US ni kutumia lugha itakayopendeza masikioni mwetu.... lugha kama "...hiyo mikopo ni debt trap" au "be careful, hiyo mikopo itahatarisha usalama wa nchi zenu" wakati US hao hao ndio wanaoongoza kudukua mawasiliano ya mataifa mengine, including mataifa ambayo ni washirika wake!

HOWEVER, hivi sasa ukifuatilia tayari wamegundua "threat card" imeshindwa kusaidia kwa sababu mataifa mengi zaidi yanaingia kwenye BRI. Ni kutokana na hilo, ndo maana nchi kama Ufaransa imeamua kutaka kurudisha mpira kwa kipa kama ilivyoandikwa kwenye website ya TV Station inayomilikiwa na serikali, yaani France24 kwamba:-

We’re fighting China in a battle for influence – and a battle over what system of government countries should see as their model,” French Foreign Minister Jean-Yves Le Drian told France Inter radio last month.

China’s increasing involvement in Africa threatens to “end up being negative over the medium to long term”, Macron warned at a press conference in Djibouti on his 2019 African tour.

“I wouldn’t want a new generation of international investments to encroach on our historical partners’ sovereignty or weaken their economies,” he added.

France’s aid reform bill now goes to the Senate and is expected to become law this summer.

Hiyo ni kauli ya serikali, iliyoandikwa na media ya serikali husika; serikali hiyo hiyo "inayotutetea" dhidi ya Mchina!!!

Sasa, ni kweli wanatutahadhalisha dhidi ya China, au wanatutahadhalisha ili tutekeleze ajenda yao ya kupambana na na influence ya Mchina?

What about the United States?

Mchambuzi mmoja wa Kimarekani anaandika kwenye Jarida la Fortune kwamba:-

The U.S. can’t keep waiting for China’s Belt and Road Initiative to fail​

Kisha anaendelea:-

Chinese President Xi Jinping has gambled his legacy on One Belt One Road (OBOR), a sweeping campaign to “rejuvenate” China’s lost greatness through foreign investments and diplomatic partnerships. The U.S. has responded with a combination of fascination, denial, and contempt. The Trump administration spent four years trying to sully OBOR, also known as the Belt and Road Initiative, or BRI—calling it “predatory,” promoting unsubstantiated rumors that it is an exercise in “debt trap diplomacy,” and pressuring allies and partners not to join.
Nimemfuatilia huyo Mchambuzi, ana makala kwenye magazeti yote makubwa ya ughaibuni unayoyafahamu, lakini hapo kwenye RED anazungumza wazi ni namna gani Trump Administration imetumia miaka 4 kututahadhalisha ni namna BRI ilivyo Zimwi kwenye ngozi ya kondoo... na hapo ametumia neno SULLY!

Mchambuzi huyo anaendelea:-
That strategy has failed because the debt diplomacy trope doesn’t capture what is actually happening on the ground with most Chinese investments. If OBOR is really so dangerous and predatory, why does China keep finding so many willing partners? The U.S. cannot stop the inexorable expansion of Xi’s massive project without making a better counteroffer to countries considering alignment with China. In other words, America needs to stop criticizing and start competing.
Kisha anakumbusha kauli mbalimbali za viongozi wa Marekani katika kampeni yao ya ku-discredit BRI, kwamba:-
It wasn’t for lack of trying. The Trump administration’s foreign policy team mounted a whole-of-government, sustained effort to undermine the world’s confidence in OBOR. The 2018 National Defense Strategy accused China of practicing “predatory economics.” Beijing is trying to build a “treasury-run empire,” Secretary of State Mike Pompeo said, and “we intend to oppose them at every turn.” Mike Pence gave numerous speeches making similar statements. When Italy joined OBOR in March 2019, the U.S. National Security Council tweeted, “Endorsing BRI lends legitimacy to China’s predatory approach to investment and will bring no benefits to the Italian people.”
Nadhani jana niligusia suala la mataifa ya magharibi kuanza kuisaliti US kwenye kampeni zake dhidi ya BRI, na hapo juu Italy unaiona!! And it's a matter of time kabla washirika wake wengine hawajamsaliti kwa sababu ukweli mchungu ni kwamba, katika dunia ya leo unaweza kumkwepa Mmarekani lakini sio Mchina!!

Hapa chini jamaa anapigilia msumari:-
The strategy flopped. Between 2017 and 2019, more than a dozen Latin American countries joined OBOR. Ten Caribbean nations have joined, and many are still actively soliciting Chinese investment. Nearly all NATO member states in Eastern and Southern Europe have associated with OBOR.
Sasa unaweza kuhoji tena in relation to Bandari ya Bagamoyo!!! Jibu la hilo lipo kwenye ufunguzi wa thread yangu kwamba:-
Amini usiamini, wale wale ambao wamekuwa wakijivika uzalendo, linapokuja suala la Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, ndiyo hao hao wanaotumikia Mabeberu bila wao kujijua!
Kwamba, kwavile USA wanaiona BRI Threat kwa upande wao, basi tutarajie mengi mabaya yatasemwa yatakayotokana na miradi ya BRI!! Mengine ni ya kweli na mengine ni proganda!!

Wapiga propaganda wa magharibi wataandika hili na lile, na kisha miongoni mwetu tutayadaka bila kuyafanyia uchunguzi na kudadisi undani wake!!!

Na ukweli mchungu ni kwamba, ukaribu wa Tanzania na Uchina unaweza kuitisha zaidi US pengine kuliko possible investment ya nchi yoyote!!!

So, the question is: Kama kuna wapuuzi wanaosema watu aina yangu tumenunuliwa na Mchina, au tuna maslahu binafsi; what kama ni wao wenyewe ndio wamenunuliwa na hao Mabeberu ili kutishia watu wauogope mradi?!

And REMEMBER... hapa wala simaanishi kwamba ile framework agreement (sio MKATABA, ingawaje watu wanazugumzia mkataba) ni bora... LA HASHA, na ndo maana kwenye thread yangu nimeacha sehemu kwa ajili ya RECOMMENDATION!!

Binafsi, nina mengi ya kueleza kwenye financial aspects ya mradi kama vile jinsi ya ku-handle masuala ya kodi, na mambo mengine yenye maslahi kwetu, including muda wa ku-operate (from Build Operate Transfer Scheme)!!!

Hivi sasa naifanyia personal research Islamic Build Operate Transfer Scheme!!!
 
Kamtuhumu Kakoko kuwa anapindisha Ukweli lakini Kakoko huyohuyo katika ufafanuzi wake alimalizia kuwa waliwaandikia barua Wachina kutaka marekebisho sehemu ambazo wanaona hazijakaa sawa ili waje waweke mambo sawa ila hawakuwa wamejibu mpaka mda uo! Hatujui kwanini wachina kwao waliamua kupuuzia mapendekezo ya serikali!
Sijaelewa hapo uliposema "kamtuhumu", ambapo inaonesha someone else kamtuhumu huyo Kakoko! If so, huyo someone else ni nani?!

Au ulitaka kuandika "kumtuhumu", ukiwa na maana kwamba mimi namtuhumu Kakoko ambae kwa mujibu wa maelezo yako aliwaandikia Wachina?!

Kama NDIYO unavyomaanisha, hivi kabisa bado unaendelea kuamini yaliyokuwa yanasemwa na utawala uliopita?! Utawala ule ule ambao tuliambiwa hakuna corona, uchumi unapaa, pamoja na corona bado watalii wanaendelea kumiminika, n.k!!

Anyway, Mwakilishi wa kampuni iliyotaka kujenga hiyo bandari walikanusha vikali madai hayo ya Kakoko, na akasema wazi kwamba Kakoko anasambaza Fake News!!

Jinsi Mchina alivyokuwa ameongea lugha kali, ungemtarajia Kakoko atoke tena mbele kutoa ushahidi wa aliyosema ili kulinda image yake binafsi, na image ya TPA, lakini Kakoko akaufyata!!

The Citizen waliandika habari hiyo kwamba:-
Mr Mao said they have received no contract terms or an ultimatum from authorities regarding Bagamoyo Port, noting that they never dealt with Mr Kakoko to whom the reports were attributed.
Kisha wanamnukuu Mr. Mao
“The investor has not received any ultimatum in form of letter, notice or fax from the Government of Tanzania,” Mr Mao said adding: “The Investor is very disappointed to see fake information spread around, which not only damaged the ease of doing business environment of Tanzania, but also misguides the public and the top level officials of the government.”

The company’s response follows widely quoted reports by Mr Kakoko that the investor had been told to accept five revised conditions of the contract or leave. Mr Kakoko has been unavailable for comment since Friday on the turn of events.
Ilikuwaje Kakoko akakaa kimya pamoja na tuhuma mzito kama hizo?!
 
Nahisi nashindwa kukuelewa kwa sababu swali lako hufafanui vizuri!! Na kama ni kwa mazingira ya Tanzania, nchi za Magharibi, hususani US wamekuwa wakii-discredit BRI kwa kutumia hoja zifuatazo:-

1. BRI ni Debt Trap... kwamba, Mchina anataka kutumia mipesa yake kuzikopesha nchi mbalimbali duniani ili zikishindwa kulipa, Mchina azi-own hizo nchi; ikiwa ni pamoja na kutaka kuhodhi raslimali za nchi husika ili kufidia deni lao!

Ni kutokana na hilo, ndo maana Sri Lanka waliposhindwa kuiendesha Hambantota Port commercially, na hivyo kulazimika kuuza 70% ya hisa za Hambantota, kilichofuata hapo kutoka kwa nchi za magharibi ilikuwa "...si mnaona! Tuliwaambia"

Sasa kwa mazingira ya Tanzania kama unavyosema, unaweza kuhusisha mfano wa Hambantota Port na Bagamoyo Port endapo Bagamoyo Port itajengwa kwa mkopo, na kuiendesha sisi wenyewe!!

Sasa kama tutashindwa kuiendesha bandari kibiashara na hivyo kushindwa kulipa, si tunaweza kulazimika kumtafuta mwekezaji anayeweza kuiendesha profitably?! Hapo ndipo anapoweza kuingia Mchina, na kuamua kuiendesha Bagamoyo Port!

2. Military Bases... hii ndo hoja nyingine inayotumia na USA kwamba, lengo la Mchina kuwekeza kwenye bandari, na kuita hatua hiyo ni strictly business ni janja janja tu ya Mchina lakini lengo lake hasa ni kuweka military bases kwenye nchi husika at security risk!!

Kwa maana nyingine, anatuambia Mchina akijenga bandari pale Bagamoyo, halafu akawa anaiendesha yeye, hiyo ni one step ahead toward establishing military bases!!!

Sasa basi, kwangu hizo naziita propaganda tu kwa sababu, kimsingi wanachohofia US ni Mchina kusambaza ushawishi wake duniani! Ni kichekesho kusema Mchina anataka kuweka military bases wakati US wenyewe ndo wanaongoza kwa kuwa na military bases outside the United States!!

Si kwamba Mchina HANA nia ya kuweka hizo military bases... HELL NO!! Pale Djboouti kaweka military base pua na mdomo na military bases za US na France... sasa hiki ndicho wasichokitaka US na Washirika wake!!

Sasa njia pekee wanayoitumia US ni kutumia lugha itakayopendeza masikioni mwetu.... lugha kama "...hiyo mikopo ni debt trap" au "be careful, hiyo mikopo itahatarisha usalama wa nchi zenu" wakati US hao hao ndio wanaoongoza kudukua mawasiliano ya mataifa mengine, including mataifa ambayo ni washirika wake!

HOWEVER, hivi sasa ukifuatilia tayari wamegundua "threat card" imeshindwa kusaidia kwa sababu mataifa mengi zaidi yanaingia kwenye BRI. Ni kutokana na hilo, ndo maana nchi kama Ufaransa imeamua kutaka kurudisha mpira kwa kipa kama ilivyoandikwa kwenye website ya TV Station inayomilikiwa na serikali, yaani France24 kwamba:-



Hiyo ni kauli ya serikali, iliyoandikwa na media ya serikali husika; serikali hiyo hiyo "inayotutetea" dhidi ya Mchina!!!

Sasa, ni kweli wanatutahadhalisha dhidi ya China, au wanatutahadhalisha ili tutekeleze ajenda yao ya kupambana na na influence ya Mchina?

What about the United States?

Mchambuzi mmoja wa Kimarekani anaandika kwenye Jarida la Fortune kwamba:-

Kisha anaendelea:-


Nimemfuatilia huyo Mchambuzi, ana makala kwenye magazeti yote makubwa ya ughaibuni unayoyafahamu, lakini hapo kwenye RED anazungumza wazi ni namna gani Trump Administration imetumia miaka 4 kututahadhalisha ni namna BRI ilivyo Zimwi kwenye ngozi ya kondoo... na hapo ametumia neno SULLY!

Mchambuzi huyo anaendelea:-

Kisha anakumbusha kauli mbalimbali za viongozi wa Marekani katika kampeni yao ya ku-discredit BRI, kwamba:-

Nadhani jana niligusia suala la mataifa ya magharibi kuanza kuisaliti US kwenye kampeni zake dhidi ya BRI, na hapo juu Italy unaiona!! And it's a matter of time kabla washirika wake wengine hawajamsaliti kwa sababu ukweli mchungu ni kwamba, katika dunia ya leo unaweza kumkwepa Mmarekani lakini sio Mchina!!

Hapa chini jamaa anapigilia msumari:-

Sasa unaweza kuhoji tena in relation to Bandari ya Bagamoyo!!! Jibu la hilo lipo kwenye ufunguzi wa thread yangu kwamba:-

Kwamba, kwavile USA wanaiona BRI Threat kwa upande wao, basi tutarajie mengi mabaya yatasemwa yatakayotokana na miradi ya BRI!! Mengine ni ya kweli na mengine ni proganda!!

Wapiga propaganda wa magharibi wataandika hili na lile, na kisha miongoni mwetu tutayadaka bila kuyafanyia uchunguzi na kudadisi undani wake!!!

Na ukweli mchungu ni kwamba, ukaribu wa Tanzania na Uchina unaweza kuitisha zaidi US pengine kuliko possible investment ya nchi yoyote!!!

So, the question is: Kama kuna wapuuzi wanaosema watu aina yangu tumenunuliwa na Mchina, au tuna maslahu binafsi; what kama ni wao wenyewe ndio wamenunuliwa na hao Mabeberu ili kutishia watu wauogope mradi?!

And REMEMBER... hapa wala simaanishi kwamba ile framework agreement (sio MKATABA, ingawaje watu wanazugumzia mkataba) ni bora... LA HASHA, na ndo maana kwenye thread yangu nimeacha sehemu kwa ajili ya RECOMMENDATION!!

Binafsi, nina mengi ya kueleza kwenye financial aspects ya mradi kama vile jinsi ya ku-handle masuala ya kodi, na mambo mengine yenye maslahi kwetu, including muda wa ku-operate (from Build Operate Transfer Scheme)!!!

Hivi sasa naifanyia personal research Islamic Build Operate Transfer Scheme!!!
Ok Brother all the Best, kutokana na Elimu yako Mradi wa Bagamoyo port upo sawa au haupo sawa.


Na kwanini tusifanye on phases ili kupunguza risk cost
 
Sijaelewa hapo uliposema "kamtuhumu", ambapo inaonesha someone else kamtuhumu huyo Kakoko! If so, huyo someone else ni nani?!

Au ulitaka kuandika "kumtuhumu", ukiwa na maana kwamba mimi namtuhumu Kakoko ambae kwa mujibu wa maelezo yako aliwaandikia Wachina?!

Kama NDIYO unavyomaanisha, hivi kabisa bado unaendelea kuamini yaliyokuwa yanasemwa na utawala uliopita?! Utawala ule ule ambao tuliambiwa hakuna corona, uchumi unapaa, pamoja na corona bado watalii wanaendelea kumiminika, n.k!!

Anyway, Mwakilishi wa kampuni iliyotaka kujenga hiyo bandari walikanusha vikali madai hayo ya Kakoko, na akasema wazi kwamba Kakoko anasambaza Fake News!!

Jinsi Mchina alivyokuwa ameongea lugha kali, ungemtarajia Kakoko atoke tena mbele kutoa ushahidi wa aliyosema ili kulinda image yake binafsi, na image ya TPA, lakini Kakoko akaufyata!!

The Citizen waliandika habari hiyo kwamba:-

Kisha wanamnukuu Mr. Mao

Ilikuwaje Kakoko akakaa kimya pamoja na tuhuma mzito kama hizo?!
Unajua ni heri ungeandika kile kilichopo kwenye mkataba ulichokiona kuliko maneno ya Mchina kasema mchina kasema!! Embu tumia ubongo wako unafikiri ye anaweza kujisema vibaya? Weka ulichokiona kwenye mkataba habari za Mr. Mao alisema na aliandika kwa hasira achananazo hazina maana.
 
Unajua ni heri ungeandika kile kilichopo kwenye mkataba ulichokiona kuliko maneno ya Mchina kasema mchina kasema!! Embu tumia ubongo wako unafikiri ye anaweza kujisema vibaya? Weka ulichokiona kwenye mkataba habari za Mr. Mao alisema na aliandika kwa hasira achananazo hazina maana.
Duh! Nyie watu bhana... sijui huwa mnamsoma mtu na kumwelewa kabla hamjatoa hoja zenu, au huwa mnakurupuka tu! Hoja yako ilikuwa ni hii hapa:-
Kamtuhumu Kakoko kuwa anapindisha Ukweli lakini Kakoko huyohuyo katika ufafanuzi wake alimalizia kuwa waliwaandikia barua Wachina kutaka marekebisho sehemu ambazo wanaona hazijakaa sawa ili waje waweke mambo sawa ila hawakuwa wamejibu mpaka mda uo! Hatujui kwanini wachina kwao waliamua kupuuzia mapendekezo ya serikali!
Kwamba, ingawaje namtuhumu Kakoko lakini yeye alifafanua kwamba alimwandikia Mchina lakini Mchina hakujibu!!!

Now tell me: Kwahiyo unaamini hoja yako hiyo inaweza kujibiwa na mkataba na sio Mchina aliyeandikiwa na Kakoko, ambae nimekuonesha hapo kwamba Mchina kakanunusha na kumuita Kakoko ni mzushi?!

Hivi kuna ubaya hapo zaidi ya ule wa Kakoko kuitwa muongo na mwenyewe akakaa kimya?!

Sasa kama unaamini Mchina hawezi kujisema vibaya, how come Kakoko akakaa kimya pamoja na kusemwa vibaya?!

Halafu acheni hizi hoja nyepesi za kudai mikataba wakati tangu mzaliwe serikali haijawahi kuwaonesha hata mkataba wa ujenzi wa vyoo, lakini leo mnanidai mimi mkataba!! Huyo Kakoko mliwahi kumdai mkataba ili kujiridhisha ikiwa aliyowaambia yana ukweli, au mnatumia hoja ya mkataba kama defensive mechanism ya kukwepakujadili hoja!

Na hivi nilichokisema mimi kuhusu mradi ni maelezo ya Mchina, au ni maelezo yaliyotokana na matokeo ya utafiti?!
 
Ok Brother all the Best, kutokana na Elimu yako Mradi wa Bagamoyo port upo sawa au haupo sawa.
Kama hiyo "mradi upo sawa au hapana" unamaanisha "framework agreement(ambayo watu wanaita mkataba) ipo perfect, jibu ni VERY SIMPLE, katu haiwezi kuwa perfect, na kwahiyo majadiliano bado yanahitajika!!

Watu wanasaini framework agreement badala ya mkataba kwa sababu ya kutoa room ya majadiliano zaidi kabla ya mkataba kusainiwa rasmi!!

More often than not, hata huo mkataba hauwezi kuwa perfect, seuze framework agreement!!! Uzuri wa framework ndo huo, inakuwa hamjafikia tamati ya makubaliano!!

That having been said, ni LAZIMA framework agreement idadavulie kwa undani zaidi ili kabla hatujasaini mkataba, tuwe tayari tumezingatia maslahi mapana ya taifa! Lazima tuwe tumejua tupo tayari kuachia nini, na kutoachia nini; na ndo maana kwenye thread yangu hii, Post #8 nimeacha nafasi kwa kuandika "MAPENDEKEZO... Reserved For Later"!

Hapo nilikusudia niandike yale ninayoamini tukiya-demand kwenye mkataba basi mradi utakuwa na manufaa kwetu! Hapa panahitaji kujadili hadi unforeseen situations!!
Na kwanini tusifanye on phases ili kupunguza risk cost
Hata kwa sasa sio kwamba mradi utajengwa kwa mara moja... la hasha lakini hapo unaposema "...kwanini tusifanye" unamaanisha kwanini kwa ujumla wake tusijenge wenyewe kwa awamu, jibu ni kwamba inawezekana lakini ni suala linalohitaji mjadala!!

Kama kujenga wenyewe bandari ya kawaida tu, it's okay, lakini kama kujenga kama ile aliyokusudia Mchina, it's TOO RISKY coz' hatuna competitive and comparative advantages za kuweza kuendesha bandari kubwa kama hiyo!!
 
Hivi nyie watu huwa hamsikii mpaka damu iwatoke masikioni eeh? Tumeshasema miradi ya wizi wizi na ujanja ujanja iliishia wakati wa Kikwete, kuanzia Magu na kuendelea tunataka kila kitu wazi wazi. Wakati wa kutuchezea akili ulienda na kikwete. Tunataka miradi ya win win situation.
Btw, ardhi yetu ya bagamoyo na uhuru wetu vina thamani zaidi kuliko maisha ya huyo mtoto aliyekamatwa na sembe.
PLAIN BRAIN
 
SEHEMU YA TATU

Mchina Anataka Bandari Zingine Zisiendelezwe
.

Wenyewe mmeona kwenye hiyo tweet ya Moosa Mao, kwamba huo nao ni UZUSHI. Hivi kuna haja ya kuongeza hapo?

Ngoja niongeze, isije kuonekana Mchina anajikosha tu!

Hapa tufahamishane kwamba, suala la upanuzi wa Bandari ya Dar es salaam unaoendelea hivi sasa ni ushahidi tosha kwamba HUO NI UZUSHI.

Watu wengi wanadhani maboresho yanayoendelea Bandari ya Dar es salaam yameasisiwa na JPM… HELL NO!

HELL NO hata kama Wafuasi wa JPM wanataka kuaminisha watu kwamba ile ni kazi ya JPM kwa alama zote.

Ukweli ni kwamba, Mzee wa Msoga alipoingia madarakani, serikali yake iliandaa 4 BIG MASTER PLANS zilizolenga kuifikisha nchi kwenye uchumi wa kati by 2025. Master Plans hizo ni:-

Dar es salaam Metropolitan Development Project (DMDP)

DMDP ndiyo imezaa mazagazaga yote mnayoyaona Dar es salaam hii leo. Mazagazaga hayo ni pamoja na barabara, flyovers ambazo wafuasi wa JPM wana-force atukuzwe JPM kwa hilo, Mwendo Kasi, Ubungo Interchange, na Daraja la Salender.

Hadi JK anatoka madarakani, kazi kubwa ilikuwa imeshafanyika, na Wafadhili alishawapata!

Lau kama JK angeendelea kuwapo madarakani kwa miaka mingine 5, haya yote tunayoambiwa tumuimbe JPM kama shujaa, yangekuwa yamefanywa na JK mwenyewe.

  • Power System Master Plan (Mambo ya Umeme(.
  • Tanzania Intermodal & Rail Development Project (TIRP), na
  • Dar es salaam Maritime Gateway Project (DMGP).
DMGP iliasisiwa mwaka 2009 (au 2008), na kuanzia hapo zikaanza hatua za awali kama upembuzi yakinifu na kutafuta watoaji wa fedha za kugharamia mradi wa uboreshaji wa Bandari ya Dar es salaam.

Ukiingia tovuti ya TPA wanatoa dokezo kuhusu DMGP na kutaja wafadhilwanataja wafadhili hao kwamba:-


Baada ya hatua mbalimbali kukamilika, Septemba 2014 ikasainiwa MoU kama inavyoelezwa kwenye Project Appraisal Report ya Benki ya Dunia kwamba:-



Ripoti hiyo hapo juu ilitolewa wakati Benki ya Dunia walipoidhinisha Mkopo wa USD 345M hapo June 9, 2017 ili hatimae maboresho ya Bandari ya Dar es salaam yaanze rasmi!

Na kwa wenye uelewa wa mambo kama haya bila shaka watakuwa wamepata picha rasmi kwamba, isingewezekana JPM aliyeingia madarakani mwishoni kabisa mwa mwaka 2015, halafu miezi 18 baadae awe ameandaa mradi mkubwa kama wa uboreshaji wa bandari ya Dar es salaam, na kupewa pesa ndani ya huo muda.

Hapo hapo, Reuters October 27, 2014 inatukumbusha kwamba:-

DAR ES SALAAM (Reuters) - Construction of a Chinese-funded port and special economic zone in Tanzania worth at least $10 billion will start in July 2015, the president’s office said in a statement on Monday, for the first time setting a start date for the delayed initiative.

Sasa basi, kama serikali ilisaini MoU September 2014 ya kuboresha bandari ya Dar es salaam chini ya DSMGP, na mwezi mmoja baadae wanazungumzia suala la kuanza mradi wa Bandari ya Bagamoyo, huo ni ushahidi tosha kwamba habari za Mchina kukataza uendelezaji wa bandari zingine ni madai ya uongo na uzushi!

Na maelezo hayo moja kwa moja yanashabihiana na tweet ya Moosa Mao kwamba:-

View attachment 1765247
Uko very deep, informed and authoritative. Also your art of presentation is scholarly
 
Back
Top Bottom