Mabinti wanaomaliza vyuo na kurudi nyumbani wananyanyapaliwa sana na wazazi kuliko vijana wa kiume

Mmoja anafanya kazi ila still home wanaona kama "BADO HAITOSHI".... Yani mama mtu ana kitu moyoni anatamani akiseme lakini ndo ivo hawezi kukisema directly..
 
Wanateswaje?
Wananyanyaswaje?
Hakuna watu wanaojua kutia huruma kama hao wanaokaa nyumbani, hizo ni mbinu tu wanazitumia ili wasaidike kwenye mambo yao.
 
Inategemea na aina ya familia !! Mzazi anayejitambua hupenda kuona yaliyo mazuri kwa uzao wake !!
 
Ni uzembe was Hali ya juu ukamaliza chuo ukarudi nyumbani yaani UZEMBE MKUBWA SANA!!!

IWE KWA KIJANA WA KIUME AU KIKE DON'T GO BACK HOME!!

Ukifika mwaka was pili kafanye field za kimkakati huko unapoenda field Jenga urafiki na in service was pande hizo,chukua namba and keep in touch!!
Ukimaliza nenda kajitolee huku ukiomba KAZI in advance ikitokea pale pale,uwe ni teacher,uwe ninmwanasheria uwe nani just nenda kajitolee pale chapa kazi huku ukimuomba mungu aiseh utapata fungu lako!!!

Mi nilipomaliza chuo niliambiwa nirudi sijui Kuna kuvuna alizeti sijui vitu Gani,nikasema Kuna mchongo nafukuzia!!

Nikapiga mzigo was kutosha,Hadi naenda job nilikua kama na laki tisa za kuanzia life ongeza na za kujikimu 1.5 million nikapanga geto langu,Hadi seniors wakaniona mtamu kama mcharo vile!!

Yaani kitanda,sofa,jiko la gesi makapeti aiseh I was good those days!!hadi member mmoja akataka ni msajili!!!

DON'T GO BACK HOME!! DON'T I SAY!!!
 
Ndio ujikute unaona mbwa kama hao utajuta akijipata siku za mbeleni
 
Ndiyo maana baadhi wakisha maliza vyuo hawarudi makwao hata kama bado hawajapata ajira.

Wanaishi Kwa kudanga tu wapate Hela ya Kodi/Kula na simu Kali za kupostia Instagram lakini sio kurudi makwao.

Ni hatari Kwa kweli 🙌
 

Sijasoma post yako yote
Ila baadhi ya mabint huwa na matumizi ya hali ya juu sana wawapo vyuoni ukilinganisha na watoto wa kiume
Fikiria anatoka familia masikini lakini pamoja na kupata pengine 80% ya mkopo hawa wenzetu wakiwa vyuoni hujisahau na kujifananisha na watoto wa walamba asali. Sasa kwa kuwa familia (Masikini) inatumia uwezo wake wote hali inayopelekea kukopa na pengine kuuza mbuzi, kuku nk ili bint asome kwa raha...hii hufanya Familia imuone mzigo anapo rudi nyumbani baada ya masomo

Watoto wa kiume wengi wao, husoma tu kwa kuunga unga hata kama amepata mkopo wa 60% hivyo hata akimaliaza haonekani kuwa mzigo saaana...
 
Tabia zao ndizo Zina wafanya wazazi wawachukie, kama bint karudi nyumbani na tabia zake nzuri lazima ataishi vizuri, Mabinti wengi wakitoka chuo wakirudi nyumbani
Mkuu tabia zao za kutaka kuishi maisha ya chuo wakiwa Chini ya wazazi, yani wanataka wafanyiwe kazi zote za Nyumbani na wao kazi yao ni kutembea na kurudi muda wanao utaka.
 
Binti kamaliza chuo at 23-25, analala tu siku nzima ni kuchat tu hana analowaza, yupo ki slay queen hata vyombo tu ndani haoshi, lazima mzazi uone umebeba mzigo ndani, actually sio mabinti tu, hata vijana wa kiume wamekuwa namna hiyo hiyo, lazy affair, kula na kulala tu, hawawasikilizi wazazi wao. Usitegemee baba anayejitambua kukuangalia na kukuchekea.

Pamoja na hayo, umasikini wa kipato unachangia, huwezi kuona hayo kwenye familia za uchumi wa kati au juu.
 
Kuna binti nilikutana nae mrembo sana anatafuta kazi ,alikuwa ana stress nikaongea nae akaanza kulia ,nikamuacha alie kwanza
Nikamuuliza kwanin usirudi nyumbani kwenu Tabora mi nitakupa nauli ,hapa mwanza anaishi tu kwa wazazi wa rafiki yake,akasema bora akae tu kwa watu kuliko nyumbani ni shida sana akanisimuliza visa vya baba ake na mama yake wa kambo!
Ila wazazi tubadilike tufanye nyumbani iwe sehemu amani ya kwa watoto wetu warudi wanapotaka ilimradi wawe na adabu
 
True
 
Aisee umesema kwl kipindi jobless nilikuwa nambiwa nikaoshe mbwa baada ya kupata kazi cijawai osha mbwa..jmn tutafute hela
 
Umeandika upumbavu
 
Duh changamoto.
 
Wale waliotoka vijijini ndiyo huwa wanapata shida mara 2, maana kwanza atarudi nyumbani na kukuta age mate woote wameolewa, pia maisha ni ya tofauti na maisha waliyozoea mjini. Ndo maana ukifanya ka survey utagundua mabinti wengi wa vijijini wanaograduate huwa hawarudi makwao, ni either wanaenda kwa ndugu walio mijini au wanajibebesha kwa jamaa yeyote wafanye sogea tuishi✅
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…