Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Screenshot_20240211-082710.jpg


Hapa ndio tatizo lilipo huenda akiwa hewani atatumalizia simulizi yetu
 
EXTRA:
Kabla sijaendelea ningependa kidogo niwajuze kitu...Unajua watu hasa watoto wa mama hawaelewi baadhi ya vitu wanachukulia maisha poa hasa wakiwaona mabraza na madogo wa DOWNTOWN.
1:WEWE KAMA MPAKA LEO WAZAZI WAPO SHUKURU MUNGU
2:WEWE KAMA HUJAWAHI KUA TEJA SHUKURU MUNGU
3: WEWE KAMA HUJAWAHI KWENDA JELA SHUKURU MUNGU
4: WEWE KAMA HUJAWAHI KULALA NJAA SHUKURU MUNGU.
5: WEWE KAMA UNA AFYA NJEMA SHUKURU MUNGU.
6:WEWE KAMA UNA MKE MWELEWA SHUKURU MUNGU
7: WEWE KAMA UNA WATOTO SHUKURU MUNGU.
Watoto wa downtown hatukupenda kua wezi au majambazi au vibaka au matapeli...Hatukupenda kila siku kukinzana na vyombo vya sheria.hatukupenda kua wahalifu au makahaba au malaya na hatuna excuse yoyote ile.
Lakini maisha wewe yasikie kwa mwenzio omba yasikukute.
Hatukuzaliwa familia bora hivyo ilitubidi tupambane kuanzia kwenye kusoma mpaka kutafuta chaneli za kutoka.
Hatukutokea familia zenye uwezo au wazazi wetu kua na ajira rasmi....tulitokea maisha ya watu wa daraja la chini.
UNAJUA KWANINI????
1: TULIUZA NGADA.
2: TULIUZA SIGARA PORI.
3: TULIKUA MARIOO.
4: DADA ZETU KUA MAESCORT NA MAKAHABA NA MAPROSTUTE UGHAIBUNI.
5: WADOGO ZETU KUKATAA SHULE ILI KUSAKA MAHELA WAKITUIGA SISI.
6:WAZAZI WETU KUTUKOMAZA KABLA YA WAKATI.
7: NA WALIMU WETU WA SEKONDARI KUTUSUSA TUJIFUNDISHE WENYEWE NA TULIFAULU KIBISHI.
Maisha wakuu na yalitufanya tupambane na ni Mungu tu ndio ametuweka hai mpaka leo""TULIKUA WADOGO NA TULIHITAJI UPENDO NA UANGALIZI ILA JAMII ILITUTENGA MABRAZA WAKACHUKUA JUKUMU LA KUTULEA KIMTAA MPAKA TUNAKOMAA NA MAISHA.
HAKUNA KIONGOZI WA SERIKALI KUANZIA NGAZI YA KITAIFA MPAKA MTAA ALIYEWAHI KUTUPA SAPOTI YA VITENDO ZAIDI YA MANENO......NI MUNGU TU ALITUONEA HURUMA.
1: TUSHAKABA.
2:TUSHADHULUMU.
3:TUSHATAPELI.
4:TUSHANUSURIKA KUFA ILA HATUKUWAHI KUTAKA KUUA SABABU YA PESA""DAMU NZITO.
5:TULITOKA MBALI MPAKA HUKO MBALI HATUPAKUMBUKI TENA.
6: TUSHAJIKANA UTU WETU KATIKA HARAKATI KWA KUWEKA REHANI ROHO KWA DILI HATARI ZA KWENYE BLACK MARKET'S WORLDWIDE.
7:TUSHAPOTEZA HISIA ZA KUKASIRIKA AU KUSUSA AU KUNYONGONYEA.
Mtaani unaamka asubuhi baba anakuangalia na mama anakuangalia na wadogo zako wanakutazama.,....utafanyaje na umetokea maisha ya tabaka la chini????
THAT'S WHY WE BECOME FIRST DOPE NIGGA,S IN (EA) ENZI HIZO ZA MID 1980,S AND 1990,S...!!USIPOTOKA MAISHA YANAKUTOKEA WEWE
Mabraza walitufundisha roho ngumu.....ya kwamba dili halali fanyia mwangani na haramu fanyia gizani....Hata ulaya tulikataa kwenda bila mipango maana tulikua na ndoto kubwa kuliko uhalisia wenyewe...!!!
Kutokana na ndoto kubwa kuliko uhalisia kitaani tuliwapoteza hawa wana.....maisha ni kujaribu bahati nasibu ni kama kamari...kuna kula au uliwe...!!
RIP : NGUZO YOSSO A.K.A BOSS
RIP : ORIGINAL MUBANDA A.K.A NYERERE
RIP : JEBBY YOSSO A.K.A MTIKILA
RIP : MEDDY YOSSO A.K.A MTEMVU
RIP : MUNDENDE YOSSO A.K.A SOKOINE
RIP : KITWANA YOSSO A.K.A SALMINI
RIP : AFIZI YOSSO A.K.A KARUME
RIP : KIPEPE YOSSO A.K.A MALICHELA
RIP :MALI YA MUNGU A.K.A KAMBONA.
Watoto wa downtown tulipambana wenyewe hatukupambaniwa na hata nyumba za urithi hatukuhesabiwa sababu koo zetu za kiafrika tunazijua wenyewe.
Tofauti na sasa enzi hizo pamoja na tofauti zetu ugomvi kuibiana na kudhulumiana ila mwisho wa siku tulipeana chaneli.....za aina zote na kizazi chetu kilikua mfano wa kuigwa.. !!!Unajua watu wengi waga wanachukulia watoto wa downtown kama watoto wa kishua ila asilimia 80% ni watoto wa watanzania wenye kipato cha chini.Hivyo ukiona watoto wa downtown wamefanikiwa waheshimu""WAMEPAMBANA""
KATI YETU KUNA WALIOPO JELA MPAKA LEO KAMA AKINA...!!!
MUBABA 27yrs.....anatoka 2032
NONDO Life sentence
KIBAKULI SR Life sentence
BAKULE 17 years,,,anatoka 2026
Y2K 9 years anatoka mwaka huu 2024.....Hao wote wapo jela za ughaibuni na kuna wengine walishatoka kama akina
LUNYAMILA alikaa jela miaka 9
MEJA alikaa jela miaka 6
SHOKISHUGI alikaa jela miaka 4....na wengine weengi nimeshawasahau...wote walipata majanga katika kutafuta maisha
Maisha yanaenda kwa kasi na uzee unakuja ila kumbukumbu ni kama jana tu......enzi hizo watu wachache downtown....leo hii downtown pekee watu karibia laki nne wanaingia na kutoka city center kila baada ya masaa mawili.
Kwahiyo ukiona wazee wa downtown wana maisha yao basi wape heshima....mjini bila akili ya kiroho na kimwili hauwezi kufanikiwa kwa lolote na chochote.
MWISHO WA EXTRA
TUTAENDELEA NA SIMULIZI.....!!!
Mbona kama unanichanganya?
Story ya mabraza wa k.koo haijaisha tushahamia Congo?

#YNWA
 
Iseee! Patel kama ndo wenyewe hao mbona ulichukua pesa ndogo sana. Hapa code inazingatiwa maaana kuna vitu nikiconnect balaa.
Nikapata mchongo unatofautiana kidogo sana na huo basi muhindi akaruka hewani anatafuta mtu wa kusafirisha madini kutoka congo mpk tz hapo kumbuka wajomba zangu kitambo wako kwenye hizo mishe na ndio walioniunganisha na muhindi na wao wako Congo, kiufupi nilienda kwa lori sikupata shida mpk wakati wa kurudi mzigo ninao naambiwa kuwa makini madini huwa yana harufu. Basi nikajibebisha kwa dereva aliekua anarudi bongo ili yangu yaende bwana eee kadri nilivyokua naisogelea bongo shetani ananimbia utajiri huo unao toroka..... Sikua na simu lakini kila mji nilikua na maelekezo yake na kumbe kuna mtu sikuwa najua kama ananifatilia kila steps! Nafika mpkaani nikapanda bus mpka dar ile kufika tu wazee hawa hapa nikatoa mzigo nikapewa changu kwa usalama wangu sikwenda hotel walinitafutia night club asubuhi nikarudi zangu kwangu na maokoto kusubiri madili mengine. Umenikumbusha moja ya harakati zangu...... Siku nikipata muda ntaongeza manjonjo na viuongo kuficha id yangu nielezee vizuri. jf kuna watu wengi
NILICHUKUA HELA NDOGO KWA SABABU SIPENDI.....KUKAAA NA HELA NYINGI ZA WATU NI HATARI.....
MATAJIRI WATU WAZURI ILA SIO KWENYE HELA ZAO ZA BIASHARA......MNAWEZA KUUANA KISA HELA.
Nitakuchek DM sista usijali nikupe michongo.......
Bro wako nilikua chimbomoja linaitwa KAZIMBE......🤣🤣🤣🤣nimefirisika now.....dili zimekataa
 
Kaa pale , dah sisteri mpaka hapo ID yako wafiche wengine ila wewe ni dada angu hizo harakati zako zimekutambulisha vilivyo kwangu nakumanya vyema .

Wale wahindi wako walishanichezea mchezo mchafu ila alhamdulilah nilikuja kulala na dada yao .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
😂🤣🤣🤣🤣 mzee wa keko kama nakuona........nikitoka huku niliko nakuja kukupa dili.......mjanja mwezangu......HALINA HELA NYINGI ILA TUTASUKUMIZIA SIKU....
STAY LOW KEY.......
 
Mi sio dada ako bwana wwee! Nina uhuru wa kuongea hapa sababu hata mume wangu hajui
Vitu ambavyo nimewahi kufanya na sembuse familia yangu kaka kama wewe..... Sina kaka ujue, braza alizamia kitambo ujerumani mpaka sasa ivi namsubiri labda ipo siku ntamuona!!!.. Mi roho ngumu sina baba wala mama niliyopitia na uanaume wako hujawahi na hutawahi!. Hata humu jf member wawili tu ndo wananijua tena kupitia id tofauti na hii.
AU WEWE NDIO YULE DADA WA KITANZANIA NILIYEKUTANA NAE BEIRUT AKANISAIDIA NISIDAKWE NCHI YA WATU MAANA NILITELEKEZWA BAADA YA KUKUTANA NA WATU WENYE ROHO MBAYA SANA 2007.......ANA DILI ZA KUUZA SILAHA.....YAANI NI AGENT AFU KAPINDA BALAAA...
WATANZANIA WAMEPINDA SANA ILA WAPO LOW KEY......TOFAUTI NA WAKENYA KELELE NYINGI...!!
 
Natupia dili lilonipatia maokoto kizembe,
Basi 2016 niko zangu shoga angu akanipigia simu wee leo dada uko wapi? Fanya haraka kesho saa kumi uwe umefika kuna ramani huku. Basi nilifika kwa muda muafaka nikakutanishwa na boss.. Huyu bosi yeye ni dalali wa mabosi wenye pesa zao basi nikaelekezwa mchongo uko hivi unapewa pesa unaingia pori kununua mazao na kila mtu anapewa pesa kulingana na uaminifu wake na aliempeleka. Tulikua wengi wengine watu wazima kabisa kama kumi ivi! Basi baada ya mawaiza ya hapa na pale tukaanza kugawiwa pesa Yule shoga alipewa mil 100, mimi 50 wengine mpka mil 200 inategemea uzoefu! Hapo mnakubaliana bei kama gunia la mahindi ni laki moja bei mliyofungia basi ikipungua ni yako hakuna malipo rasmi ni akili yako tu! Mungu alivyomkubwa kama baada ya siku mbili jioni yake tunajiandaa tuanze safari ya pori boss alipigwa mzinga bonge la ajari aligongwa na roli kiufupi alitoka vipande vipande..... Huku wanachama tukaitana inakuaje tukimbie au?! Mtandao mkubwa tutakamatwa twende msibani tukasikilizie, basi mpaka msiba unaisha jamani hakuna alieuliza wala nn!! Wahuni wengine walienda kuchoma ofisi yake kupoteza ushahidi kabisa.
Yule shoga angu akaniambia hapa kila mtu njia yake ikipatikana ramani tutatafutana mie huyooooo mpaka Zanzibar, nikatoa kwanza 10ml ya kunipoza kula bata nikamsuprise shemeji yenu nikamtumia tiketi anifate,. Kufika full misifa babe mpambanaji wewe( kimoyoni laiti ungejua nyau wewewee)
Basi hiyo pesa niilipata bila stress wala kuvuja jasho kwa aina yoyote ile. Pesa iliobaki tulijenga kamjengo mkoani hukoo nikakaa kusubiri simu nyingne.
🤣🤣🤣🤣🤣 bas sista....nilidhani ww ndio yule dada wa kitanzania 2006 niliekutana nae Beirut.....nimevurugwa afu nina pasi ya kusafiria ya Burundi......wajanja wamenitapeli......Alinisaidia sana yule sista.....mpaka nafika nililotakiwa kufika.
🤣🤣😂😂Mm nishawahi kukaa na madini ya tanzanite ya thamani ya 460 Tz shilling ila sikua najua miaka mitatu na nusu wakati mwenye nayo yupo kifungoni.....baada ya yeye kupata msala huko singida.
Mpaka leo wale mabroo,,,,,huwambiii kitu kuhusu mm.
 
Fanya hivyo mwanangu , mie nakusubiria , japo kwasasa niko huku kwa akina mwaisa napambanisha
😂🤣🤣🤣🤣 mzee wa keko kama nakuona........nikitoka huku niliko nakuja kukupa dili.......mjanja mwezangu......HALINA HELA NYINGI ILA TUTASUKUMIZIA SIKU....
STAY LOW KEY.......
 
Back
Top Bottom